The lost
JF-Expert Member
- Jul 3, 2017
- 2,695
- 8,209
Better were colonial days ndivyo navyoweza kusema. Wakati wa mateso ya kusulubiwa kwake Yesu Kristo alitamka maneno yenye tafakuri kubwa sana "KAMA WANAUTENDEA HIVI MTI MBICHI ITAKUWAJE KWA MTI MKAVU?" maneno haya yamebemba ujumbe mkubwa sana. Tangu utawala wa dola la Roma la kale mpaka wakati wa milki ya Brazantine watawala waliamini hawatakuja kuachia kiti cha utawala. Kama vile mtoto mdogo anavyoliacha ziwa la mama yake na kuanza maisha mapya ya kujilisha ndiyo hivyohivyo wakati ulifika wa mifumo mipya ya kidunia iliingia na falme zenye nguvu zilianguka. CCM wanaamini wao ndiyo wenye mamlaka ya kutawala nchi hii na yoyote anayejaribu kuwapinga atasakamwa ama mpaka kuuawa. Freeman Mbowe amejikuta katika matatizo kwa kile kinachotafsiriwa amejaribu kuwapokonya watawala tonge mdomoni. Mbowe amefitiniwa je ni wangapi miongoni wa wasio na sauti WANAFITINIWA?