Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,293
- 18,873
JF ni darasa kubwa sana, miaka minne iliyopita, kuna mwanachama mmoja alitupa somo hapa kama ifuatavyo
(1) Je kuna yeyte kati yetu amewahi kufikiria ku-exercise rights zake mbele ya polisi?
(2) Ilikuwaje Dr. Ulimboka alikubali kukamatwa na polisi bila kuzingatia haki zake hizo? hasa zile tatu za kwanza? Inawezekana hakuwa anazijua; tujitahidi tujifunze mambo mengine yaliyok nje ya taaluma zetu, hasa sheria.
(3) Inawezekana alikuwa anazijua lakini hakuwa na nafasi ya kuzi-exercise kwa vile askari walimfuata wakiwa wamemshikia bunduki, lakini je iwapo askari wakikushikia bunduki mbele ya watu ukanyamaza unategemea mtakapokuwa peke yenu watakuwa na huruma kwako? Kwa marekani kuna kitu kinaitwa miranda rights, ambazo kwa Tanzania usipojibu swali la polisi utapata kipigo kikali sana hasa iwapo utakuwa peke yako pamoja na askari hao. Salama yako mbele ya askari wa Tanzania ni kuhakikisha kuwa una shaidi mwingine independent.
- Raia ana haki ya kumwomba askari ajitambulishe kwako.
- Mwulize jina lake
- Mwulize namba yake ya uaskari
- Raia ana haki ya kujulishwa kwanini anatiliwa mashaka ama kukamatwa.
- Raia ana haki ya kuwajulisha ndugu, jamaa ama sehemu anakofanyia kazi kwamba ama amekamatwa na polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
- Raia ana haki ya kuomba na kupewa dhamana wakati akiwa kituo cha polisi ama Taasisi ya kuzuia rushwa.
- Hutakiwi kutoa fedha kama dhamana uwapo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa, isipokuwa maelezo utakayoandika.
- Raia ana haki ya kuwaeleza polisi ama Maafisa wa Kuzuia Rushwa kwamba lolote atakalosema linaweza kutumiwa kama ushahidi mahakamani, na asiburuzwe kuandika tu.
- Raia ana haki ya kuomba Wakili wake awepo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa wakati anatoa maelezo yake.
- Raia ana haki ya kuyasoma kabla ya kutia sahihi yake.
- Raia ana haki ya kudai risiti ya orodha ya vitu vyake/fedha zake alizozitoa ama kukabidhi kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
- Raia kama ni mwanamke ana haki ya kupekuliwa na polisi wa kike, na iwapo hakuna polisi mwanamke, basi mwanamke yeyote na vile vile kwa mwanamume.
- Raia ana haki ya kufikishwa mahakamani katika muda usiozidi saa 24 tangu alipokamatwa na kufikishwa kituo cha polisi.
(1) Je kuna yeyte kati yetu amewahi kufikiria ku-exercise rights zake mbele ya polisi?
(2) Ilikuwaje Dr. Ulimboka alikubali kukamatwa na polisi bila kuzingatia haki zake hizo? hasa zile tatu za kwanza? Inawezekana hakuwa anazijua; tujitahidi tujifunze mambo mengine yaliyok nje ya taaluma zetu, hasa sheria.
(3) Inawezekana alikuwa anazijua lakini hakuwa na nafasi ya kuzi-exercise kwa vile askari walimfuata wakiwa wamemshikia bunduki, lakini je iwapo askari wakikushikia bunduki mbele ya watu ukanyamaza unategemea mtakapokuwa peke yenu watakuwa na huruma kwako? Kwa marekani kuna kitu kinaitwa miranda rights, ambazo kwa Tanzania usipojibu swali la polisi utapata kipigo kikali sana hasa iwapo utakuwa peke yako pamoja na askari hao. Salama yako mbele ya askari wa Tanzania ni kuhakikisha kuwa una shaidi mwingine independent.