Haki za Raia anapokamatwa na Polisi: Je Dr. Ulimboka Alizijua?

Kichuguu

Platinum Member
Oct 11, 2006
15,293
18,873
JF ni darasa kubwa sana, miaka minne iliyopita, kuna mwanachama mmoja alitupa somo hapa kama ifuatavyo
  • Raia ana haki ya kumwomba askari ajitambulishe kwako.
    • Mwulize jina lake
    • Mwulize namba yake ya uaskari
  • Raia ana haki ya kujulishwa kwanini anatiliwa mashaka ama kukamatwa.
  • Raia ana haki ya kuwajulisha ndugu, jamaa ama sehemu anakofanyia kazi kwamba ama amekamatwa na polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
  • Raia ana haki ya kuomba na kupewa dhamana wakati akiwa kituo cha polisi ama Taasisi ya kuzuia rushwa.
    • Hutakiwi kutoa fedha kama dhamana uwapo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa, isipokuwa maelezo utakayoandika.
  • Raia ana haki ya kuwaeleza polisi ama Maafisa wa Kuzuia Rushwa kwamba lolote atakalosema linaweza kutumiwa kama ushahidi mahakamani, na asiburuzwe kuandika tu.
  • Raia ana haki ya kuomba Wakili wake awepo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa wakati anatoa maelezo yake.
  • Raia ana haki ya kuyasoma kabla ya kutia sahihi yake.
  • Raia ana haki ya kudai risiti ya orodha ya vitu vyake/fedha zake alizozitoa ama kukabidhi kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
  • Raia kama ni mwanamke ana haki ya kupekuliwa na polisi wa kike, na iwapo hakuna polisi mwanamke, basi mwanamke yeyote na vile vile kwa mwanamume.
  • Raia ana haki ya kufikishwa mahakamani katika muda usiozidi saa 24 tangu alipokamatwa na kufikishwa kituo cha polisi.

(1) Je kuna yeyte kati yetu amewahi kufikiria ku-exercise rights zake mbele ya polisi?

(2) Ilikuwaje Dr. Ulimboka alikubali kukamatwa na polisi bila kuzingatia haki zake hizo? hasa zile tatu za kwanza? Inawezekana hakuwa anazijua; tujitahidi tujifunze mambo mengine yaliyok nje ya taaluma zetu, hasa sheria.

(3) Inawezekana alikuwa anazijua lakini hakuwa na nafasi ya kuzi-exercise kwa vile askari walimfuata wakiwa wamemshikia bunduki, lakini je iwapo askari wakikushikia bunduki mbele ya watu ukanyamaza unategemea mtakapokuwa peke yenu watakuwa na huruma kwako? Kwa marekani kuna kitu kinaitwa miranda rights, ambazo kwa Tanzania usipojibu swali la polisi utapata kipigo kikali sana hasa iwapo utakuwa peke yako pamoja na askari hao. Salama yako mbele ya askari wa Tanzania ni kuhakikisha kuwa una shaidi mwingine independent.
 
sidhani kama walikuja kama wana usalama,nahisi walimwendea kama watu wanaohitaji mazungumzo ya faragha na Dr. Ull. Ndio maana baadhi ya mabandiko yanaonyesha kuwa ni watu ambao alikua anawasiliana nao mara kwa mara wakijitambusha kama maafisa wa serikali. Hata ikija kufahamika kwamba Dr.ull kuna uzembe aliufanya,hauwezi kuhalalisha unyama aliofanyiwa.!!!
 
sidhani kama walikuja kama wana usalama,nahisi walimwendea kama watu wanaohitaji mazungumzo ya faragha na Dr. Ull. Ndio maana baadhi ya mabandiko yanaonyesha kuwa ni watu ambao alikua anawasiliana nao mara kwa mara wakijitambusha kama maafisa wa serikali. Hata ikija kufahamika kwamba Dr.ull kuna uzembe aliufanya,hauwezi kuhalalisha unyama aliofanyiwa.!!!

Siyo kwamba ninahalalisha kilichotokea; mambo alifyofanyiwa Dr ulimboka ni ya kinyaman na ya aibu sana kwa taifa. Nilichofanya hapa ni kukumbusha tena kuwa tujitahidi kuwa makini tunapochukuliwa na watu tusiowafahamu kwa kisingizio kuwa ni wana usalama. Sheria za kutulinda katika mazingira hayo zipo kama ilivyobainishwa hapo.
 
Siyo kwamba ninahalalisha kilichotokea; mambo alifyofanyiwa Dr ulimboka ni ya kinyaman na ya aibu sana kwa taifa. Nilichofanya hapa ni kukumbusha tena kuwa tujitahidi kuwa makini tunapochukuliwa na watu tusiowafahamu kwa kisingizio kuwa ni wana usalama. Sheria za kutulinda katika mazingira hayo zipo kama ilivyobainishwa hapo.
Hakuna haki inayofuatwa wala itakayokusaidia vyombo vya usalama viapofanya udhalimu. Hizo haki ulizoorodhesha zinauhusiano gani na Dr Ulimboka na yaliyomkuta? Hakukuwa na muda kwani aliposimama kutaka kuondoka alifuatwa akapigwa na kuburuzwa kuelekea kwenye gari ambalo halikua na number ambamo aliteswa na baada ya kupoteza fahamu na wao kuamini kwamba kafa alitupwa porini. Hayo mambo ya number sijui jina utamuuliza nani?
 
Hivyi unapo bakwa na vibaka labda wewe ni mwanaume au mwanake haki zako ni zipi? Kuna familia moja jirani yangu walivamiwa na vibaka usiku, familia ile ni ya watu 7 wale vibaka wakamkamata baba na mama mwenye nyumba wakawafunga kwa kamba mikono na miguu, kisha wakawaamsha watoto, mtoto wa kwanza wakiume mwenye miaka 16 wapili wa kike mwenye miaka 14, na hao wengine wadogo wa dogo miaka 12 kwenda chini. Wale vibaka wakawalawiti wazazi wao na kumlala mama yao, kisha wakamlazimisha yule mtoto wa kwanza kulawiti baba na kumlala mama yake kwa amri na kibano kikali kisha wakamchukua yule wa kike na kutokomea nae kusiko julikana hadi aliporudi asubuhi akiwa amebakwa ile mbaya, je? Baada ya tukio hili unafikiri familia hii itafanyaje, na tayari mambo haya yamefanyika mbele ya watoto wote na mkubwa wao kawala uroda wazazi wake?
 
Ulimboka hakukamatwa alitekwa kimafia so hizo taratibu za kipolisi hazikufuatwa! Ila naqchojiuliza hao aliokuwa nao wakaona anaburuzwa kwa nguvu na palikuwa ni baa kwa nn hawakumsaidia mwenzao na kuomba msaada kwa raia wengine ili ijulikane anakamatwa kivipi??
 
Tatizo ni kwa hao polisi na vyombo vingine vya usalama ,Je wao wanazifuata sheria hizo au sheria za wao kumkamata mtu wanazifuata ?
 
Kumbuka kuwa, kuna tofauti kati ya kukamatwa na kutekwa. Yule alitekwa, kwa maana ya kwamba walimchukua kwa mabavu. Unapotekwa hata kama unazijua haki zako huwezi kuwa nafasi ya kujitetea.
 
Hivi mtu amekufunga kitambaa usoni hicho kitambulisho utakisomaje? Hebu tujuze mleta mada.
 
Mazingira ya kukamatwa kwake hayakuruhusu hayo uliyotaja yafuatwe. Lakini kilichotekea ni dhahiri kuwa alitekwa na watu wa usalama kwa nia ya kummaliza.
 
Huyu mleta Uzi ni mlevi aende zake kwa mama muuza akazimue badala ya kuleta utumbo hapa jamvini
Mkuu.... hapana. Mwanzisha mada ni mtu makini sana, labda wengine ni wageni hapa jamvini hamjamfahamu. Nadhani inatosha kujibu kwa staha kuwa Dr Ulimboka alitekwa na sio kama alikamatwa. Lakini bado kuna kitu cha kujifunza hapa.
Kwenye hali ya mgomo unaohusishwa kundi la watu wengi, viongozi wasiwe warahisi kukubali vikao visivyo rasmi na watu wasio rasmi, japo haindoi kwa asilimia mia moja hatari ya kutekwa.
 
JF ni darasa kubwa sana, miaka minne iliyopita, kuna mwanachama mmoja alitupa somo hapa kama ifuatavyo


(1) Je kuna yeyte kati yetu amewahi kufikiria ku-exercise rights zake mbele ya polisi?

(2) Ilikuwaje Dr. Ulimboka alikubali kukamatwa na polisi bila kuzingatia haki zake hizo? hasa zile tatu za kwanza? Inawezekana hakuwa anazijua; tujitahidi tujifunze mambo mengine yaliyok nje ya taaluma zetu, hasa sheria.

(3) Inawezekana alikuwa anazijua lakini hakuwa na nafasi ya kuzi-exercise kwa vile askari walimfuata wakiwa wamemshikia bunduki, lakini je iwapo askari wakikushikia bunduki mbele ya watu ukanyamaza unategemea mtakapokuwa peke yenu watakuwa na huruma kwako? Kwa marekani kuna kitu kinaitwa miranda rights, ambazo kwa Tanzania usipojibu swali la polisi utapata kipigo kikali sana hasa iwapo utakuwa peke yako pamoja na askari hao. Salama yako mbele ya askari wa Tanzania ni kuhakikisha kuwa una shaidi mwingine independent.

Mimi nafikiri wale aliokuwa nao walikuwa wanaijua issue yenyewe. Hata huyo rafiki yake alihusishwa kwenye dill. Itakuwaje uko na mtu akamatwe halafu usifuatilie anapelekwa wapi wala usihangaike kumwekea dhamana?
 
Mi nadhani siku raia wa Tanzania atakapopata haki zake mbele ya polisi wa kitanzania, hata jina la Tanzania litakuwa limebadilika na kuitwa vinginevyo. Kwa Tanzania raia ywyote anayetuhumiwa anakuwa amehukumiwa kuwa mkosaji mpaka mahakama itakapotengua na kusema vinginevyo. Labda kama una hela, unaweza kupata haki hata ya kuua ukisimamiwa na polisi wa Tanzania. Siwaamini mapolisi hata kama watavaa mapambo ya almasi usoni na kichwani. Nimekumbana nao mara nyingi kwa mambo ya kuchomekea, mpaka ukiwaonyesha kwamba unao uwezekano wa kufikisha mambo yao kwa mkuu kuliko wao ndio angalau wanalegeza kamba. Kipigo na mateso ndio ustaarabu waliosomea mapolisi wetu, usiombe ukutane nao kwenye anga zao, ukitoka salama nenda kamshukuru Mungu wa dini yako.
 
Huyu mleta Uzi ni mlevi aende zake kwa mama muuza akazimue badala ya kuleta utumbo hapa jamvini
Iwapo katika post hiyo umeona ni ulevi basi wewe binafsi una upungufu mkubwa sana wa akili, yaani akili yako haijakomaa kuweza kutambua mambo yanayojadiliwa na watu wengin. Katika kiswahili tuna methali inasema jambo usilolijua ni sawa na usiku wa giza; kwako wewe post hiyo inaonekana ni usiku wa kiza kikubwa sana, yaani huoni kitu. Kwa akili yako hiyo, nakushauri usiwe unachangia post usizozifahamu; kwa vile umejiunga juzi tu, basi tulia uwe unasoma na kufuatiliwa watu wenye wakili wanavyojadiliana mambo hadi akili yako itakapokomaa vya kutosha.
 
Mazingira ya kukamatwa kwake hayakuruhusu hayo uliyotaja yafuatwe. Lakini kilichotekea ni dhahiri kuwa alitekwa na watu wa usalama kwa nia ya kummaliza.

Kama kweli alitekwa akavutwa kwa nguvu, ilikuwaje rafiki yake na wale wengine aliokuwa nao hawakufuatilia mara moja kuona anapelekwa wapi. Taarifa nilizosoma ni kuwa alitolewa pale kwa ahadi ya kupelekwa central kuhojiwa, na ndiyo maana rafiki zake walimfuata huko central kwa nia ya kumdhamini. Waliomchukua walikuwa na bunduki wakijitambulisha kuwa ni askari.
 
huyu jamaa haelewi tofauti ya kukamatwa na kutekwa achana nae wenda hadi yamkute ndo atajua maana halisi ya kutekwa
 
Kichuguu,

..Je, raia wana haki ya kukataa[right to remain silent] kutoa maelezo kwa vyombo vya dola??
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom