Haki itendeke kwa waliomuua Padre Evarist na Waliochoma moto makanisa - Zanzibar

Abraham Lincolnn

JF-Expert Member
Apr 12, 2018
2,499
4,207
Tunaomba serikali iliangalie swala hili mara ya pili na ukweli ujulikane kwani ni wazi kuwa haki haijatendeka kwa Padri aliyeuwawa huko Zanzibar.

Ni muda mrefu sasa umepita na serikali zote zipo kimya wala hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa wala yeyote aliyefikishwa katika vyombo vya sheria.Hakika damu ya Padre huyu haitawaacha salama.

Kuna makanisa yalichomwa moto,Je wahusika ni kina nani? Walikuwa na lengo gani? Kiongozi/Viongozi wao ni kona nani? Matokea ya uchunguzi yanasemaje? Hatua gani zimechukuliwa?

Sio kwa ubaya,Ila naamini Ingekuwa ni waislam Sheikh wao ameuawa au misikiti kuchomwa moto basi wangeitisha maandamano na pasingekalika lakini kwakuwa wakristu mafundisho yao yanasema akupigae kofi upande mmoja mgeuzie jingine basi tunadhulumiwa nafsi zetu.

Tunaomba haki kwa padre Evarist na makanisa yaliyochomwa moto Zanzibar.Baadhi watahusisha hili na kufunguliwa kwa viongozi wa UAMSHO,Sawa tunakubali kuwa UAMSHO hawahusiki basi tunaomba kuelezwa wahusika ni nani?.Hakika hili chozi halitawaacha salama na tutazidi kupiga kelele hadi haki itakapotendeka.
 
Mimi ni mkatoliki pure lakini majuzi tu ziliungua shule zaidi ya 10 za kiislamu ndani ya utawala wa magufuli lakini mpaka Leo hakuna mtu ambaye alishakamatwa!

Wengine wanasema inawezekana ni wao kwa wao na mimi nauliza kwanini kama ni wao kwa wao tusiwe sisi kwa sisi?

Sisi hatuwezi kufanyiana uhuni? Wakristo wangapi wametishiwa kuuwawa utawala uliopita na wengine Wachungaji na mapadri kuambiwa sio RAIA wa Tanzania.?

Ingekuwa ni utawala huu watu wangepiga kelele na kuusisha uislamu na uhuni?

Ndugu zangu hakuna dini duniani inayomtambua Mungu inayoweza kuhusishwa na upuuzi kama huo wala inaweza kufanya uhuni kama huo.

Ujambazi unafanywa na mkiristo na sio ukiristo pia ujambazi unafanywa na muislamu ila sio uislamu.

Tuache siasa kwenye kila jambo huwezi ukausisha kifo cha MTU na yeye kuwa dini fulani hata kama aliuwawa na muislamu ila sio uislamu.

Na unapo mkamata mtu uwe na ushahidi wa kutosha kumshitaki na sio kumkamata wakati ushahidi hauna miaka 9 mpumbavu unakuwa ni wewe.
 
Uamsho wamekaa gerezani miaka 7 serikali wameshindwa kuthibitisha mashtaka dhidi yao leo wameachiwa huru mnaanza ngonjera mlitaka wakae huko bila tuhuma dhidi yao kuthibitishwa hadi lini? Kama mna ushahidi si mngepeleka ili wahukumiwe kunyongwa.
Who narrated that? Don't be so emotional,buddy!
 
Mimi ni mkatoriki pure lakini majuzi tu ziliungua shule zaidi ya 10 za kiislamu ndani ya utawala wa magufuli lakini mpaka Leo hakuna mtu ambaye alishakamatwa?....
Kumbuka zimechomwa shule za bakwata tu, siyo za madhehebu mengine ya kiislam, sasa subiri baada ya hawa masheh kutoka uone kama zitaendelea kuchomwa
 
Serikali ya kiislamu na kizanzibari jombaa

Usitegemee hatua kali kuchukuliwa dhidi ya mwislamu ama mzanzibari
 
Kwa hiyo unataka kusema wakristo wenyewe ndo walichoma makanisa na kuua padre?
 
Kama kuua hao wakatoliki wameua Sana miaka ya nyuma na pengine hata leo kwaminajili ya kuuneza Ukristo!

Na hakuna hatua ngumu zilizochukuliwa zaidi ya wao kuomba msamaha!

Kwahio Kama ilivyo falsafa yao ukipigwa upande huu usirudishe Bali geuka upigwe na upande mwingine ili yule akupigae asiwe na la kukupigia tena.
 
Nchi hii Wakristo hawana haki. Akiwa mkiristo anakua labeled individually lakini akifa Muislam anakua labeled Kama muislam na kifo hicho huhesabika Kama shambulio dhidi ya Uislam.

Ben SANANE, Azory Gwanda na mauaji ya Fr Evarist ni mifano hai. Wangekuwa Waislam ungeona Moto wake. Ifike mahala wote tuwe na thamani sawa na mauti ya kila mmoja ibebe uzito sawa.
 
Huu ubaguzi wa dini usipodhibitiwa hali itakuja kuwa mbaya leo wakristo wanawachukia waislamu waziwazi kwa kuwaita magaidi bila uthibitisho wowote ila wanaitwa magaidi kwa sababu ya uislamu wao tu
Youtube haiko mbali

Ka-search mihadhala ya JUMUKI

Ndo utajua kuwa hawaonewi

Serikali ya Samia imeongozwa na udini katika kuwaachia

Shame to her
 
Kwa hiyo unataka kusema wakristo wenyewe ndo walichoma makanisa na kuua padre?
Nadhani hajasema hivyo ila amekufungulia uwanja mpana wakutafakari.hebu rejea lile tukio la arusha kulipuliwa bomu kanisani,hivi unajua akaekamatwa ktk tukio lile baada yawatu kumuona wakati arusha bomu lamko? Je unakumbuka alikuwa wa dini gani?
 
Back
Top Bottom