Babuu Rogger
JF-Expert Member
- Nov 16, 2011
- 1,529
- 1,114
Wana JF siku zote wanaume ni wabunifu sana. Siku hizi wanaume wanaopenda kuchukua wale wanawake ambao wanakuwa na makubaliano ya wakishamaliza majamboozi wanawalipa, sasa kinachofanyika mwanaume anamchukua mwanamke na kuanza kumpa kinywaji si unajua tena mambo yetu yale, sasa mambo yakishaanza kukolea anamtumia pesa 50,000/= au 100'000/= kwa njia ya m-pesa au tigo pesa pale pale walipo na sms inajibu pale pale kwamba mshiko umeingia na wakimaliza majamboozi atakwenda kuchukuwa atakakokwenda. Sasa mwanaume atatoka kama anakwenda toilet vile kisha anapiga huduma kwa wateja na kuwaomba wamrudishie pesa yake kwani amekosea namba aliyotuma, si unajua tena na jamaa walivyo fasta wanarudisha pesa kama ilivyo na ile msg ya kwa mwanamke inabakia kama ilivyo kwamba a/c yake ina mshiko. Sasa asubuhi wakati wameshamalizana mwanamke anatoka kwenda kuchukuwa mshiko wake na anakuta a/c haisomi na alishatoa huduma kwa ujasiri mkubwa. Hapo sasa ndipo huwa tunasema kweli akili ya mwanaume mwenyezi Mungu kaijenga.mchana mwema.