GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,544
- 108,871
Katika hali isiyokuwa ya kawaida kabisa leo Jumatano tarehe 8 Mwezi April 2020 alipokuwa akizungumza katika Kipindi bora cha Michezo cha Mchana chaa Kipenga Extra kinachorushwa na Redio bora kabisa ya Kiswahili Afrika Mashariki ya East Africa Radio Msemaji wa Klabu Kubwa, bora na iliyobarikiwa na Mwenyezi Mungu kwa Kuchukua Mataji na kuweka Rekodi nzuri Barani Afrika ya Simba Sports Club Haji Sunday Manara ameamua Kumtolea Uvivu aliyekuwa Msemaji wa Klabu yenye ' Nuksi ' duniani ya Yanga SC sasa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mheshimiwa Jerry Muro.
Swali la Mtangazaji Goza Chuma kwenda Kwake Haji Manara.....
" Una maoni gani juu ya hawa Wasemaji wenzako hasa wa Wapinzani wako wakubwa Yanga SC? "
Jibu lililochafua hali ya hewa la Haji Manara kwa Mtangazaji Goza Chuma.....
" Ni Wasemaji wazuri na bahati nzuri wote kuanzia Nugaz, Bumbuli na hata huyu Jimmy Kindoki ni Marafiki zangu na sina Uadui nao ila huwa tunaamua tu Kucharurana ili Kunogesha Mpira wetu ila kuna aliyewahi kuwa Msemaji wao Jerry Muro sasa ni Mkuu wa Wilaya ya Arumeru alivuka mipaka na hivi karibuni kabla ya Mechi yetu nao waliyotufunga alikuwa akizunguka katika Media mbalimbali Kunitukana, Kunishambulia huku akinidhalilisha mno.
Sasa nilichokifanya baada ya Kumsikia nilimuandika Meseji na hata nyie Watangazaji mkiitaa mwambieni awaonyeshe nikimuonya kuwa kama Jerry Muro ataendelea Kunishambulia Binafsi kwa kutoka nje ya mambo yetu ya Mpira wa Simba na Yanga nitaenda Kutoa SIRI yake moja Kubwa ambayo nina uhakika itaisimamisha Tanzania na hata dunia kwa muda na ambayo inaweza hata kufanya ang'olewe ( atumbuliwe ) haraka katika huo Wadhifa wake.
Na kwa Kujiamini Kwangu zaidi Mimi Haji Manara hata hiyo Siri nilimuandikia katika hiyo hiyo Meseji. Na nina uhakika DC Jerry Muro hatonyanyua tena Mdomo wake Kunishambulia kwani amekutana na Mtoto wa Mjini kweli kweli ila niliamua tu Kumstahi. Ole wake anishambulie tena katika Redio na Runinga nitafunguka kila Kitu Kudadadeki "
GENTAMYCINE nimekuwa nikijiuliza ni kwanini siku hizi DC Jerry Muro kapoa na kapotea sana Masikioni mwa Watu na hasa katika Media za Tanzania kumbe jibu ni kwamba sasa hivi anawaza endapo Siku akikosea tu au akijisahau na kwa bahati mbaya akamshambulia tena Adui (Hasimu) wake Haji Manara basi Betrii itachomolewa rasmi na ataanikwa vibaya hadi atatafuta Mapori ya Kujificha.
Shikamoo Haji Sunday Manara a.k.a DE LA BOSS na pole sana DC Jerry Muro umekutana na Mtoto wa Mjini aliyetukuka hasa.
Swali la Mtangazaji Goza Chuma kwenda Kwake Haji Manara.....
" Una maoni gani juu ya hawa Wasemaji wenzako hasa wa Wapinzani wako wakubwa Yanga SC? "
Jibu lililochafua hali ya hewa la Haji Manara kwa Mtangazaji Goza Chuma.....
" Ni Wasemaji wazuri na bahati nzuri wote kuanzia Nugaz, Bumbuli na hata huyu Jimmy Kindoki ni Marafiki zangu na sina Uadui nao ila huwa tunaamua tu Kucharurana ili Kunogesha Mpira wetu ila kuna aliyewahi kuwa Msemaji wao Jerry Muro sasa ni Mkuu wa Wilaya ya Arumeru alivuka mipaka na hivi karibuni kabla ya Mechi yetu nao waliyotufunga alikuwa akizunguka katika Media mbalimbali Kunitukana, Kunishambulia huku akinidhalilisha mno.
Sasa nilichokifanya baada ya Kumsikia nilimuandika Meseji na hata nyie Watangazaji mkiitaa mwambieni awaonyeshe nikimuonya kuwa kama Jerry Muro ataendelea Kunishambulia Binafsi kwa kutoka nje ya mambo yetu ya Mpira wa Simba na Yanga nitaenda Kutoa SIRI yake moja Kubwa ambayo nina uhakika itaisimamisha Tanzania na hata dunia kwa muda na ambayo inaweza hata kufanya ang'olewe ( atumbuliwe ) haraka katika huo Wadhifa wake.
Na kwa Kujiamini Kwangu zaidi Mimi Haji Manara hata hiyo Siri nilimuandikia katika hiyo hiyo Meseji. Na nina uhakika DC Jerry Muro hatonyanyua tena Mdomo wake Kunishambulia kwani amekutana na Mtoto wa Mjini kweli kweli ila niliamua tu Kumstahi. Ole wake anishambulie tena katika Redio na Runinga nitafunguka kila Kitu Kudadadeki "
GENTAMYCINE nimekuwa nikijiuliza ni kwanini siku hizi DC Jerry Muro kapoa na kapotea sana Masikioni mwa Watu na hasa katika Media za Tanzania kumbe jibu ni kwamba sasa hivi anawaza endapo Siku akikosea tu au akijisahau na kwa bahati mbaya akamshambulia tena Adui (Hasimu) wake Haji Manara basi Betrii itachomolewa rasmi na ataanikwa vibaya hadi atatafuta Mapori ya Kujificha.
Shikamoo Haji Sunday Manara a.k.a DE LA BOSS na pole sana DC Jerry Muro umekutana na Mtoto wa Mjini aliyetukuka hasa.