Wenyewe wanajiita ".......club kubwa.........club yenye uweledi wa hali ya juu.........club yenye hela......"Leo nimesikia audio ikitembea mitandaoni inayodaiwa kuwa imerekodiwa na Manara akimtuhumu kwa mambo mengi Barbara.Inaonekana hawa watu wana mgogoro wa mda mrefu na hawawezi kufanya kazi tena pamoja. Wewe kama mwanasoka unadhani nini kifanyike? Au ni madhara ya Mo kujimilikisha timu kifamilia?🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Kwenye audio hyo Manara kaenda mbali zaidi na kumtishia Barabara sijui Barnaba sorry Barbana,duuh Barbara kwamba ataiacha timu kama alivyoikuta.Sasa hapo sijui nani anaondoka nani anabaki.
Povu ruksa nina nguo chafu hapa.
Najaribu kuapload audio husika hapa inazingua
=====
Afisa Habari wa Simba Haji Manara ameamua kumtolea uvivu Mtendaji Mkuu wa Klabu hiyo Barbara Gonzalez.
Haji anadai Mtendaji huyo amekuwa akimuandama sana na kumnyima raha muda wote toka ameshika majukumu hayo.
View attachment 1862918
Manara ameshajisahau kwamba yeye pale Simba au Nje ya Simba Hana lolote..Kupiga domo kila mtu anaweza....Kusema kwa Boss wako we Nani huo ni uswahili....Taasisi ina miiko na taratibu zake...Huwezi kumwambia Boss wako Koma..Na ndio mana sisi Watanzania hatuwezi kufanya kazi tuka excell vizuri kwenye international Level..Manara uswahili unamdanganya.. manara hana uwezo wa kumtoa simba babra wala mo.. ila babra na mo wana uwezo wa kumtoa simba manara..
Mwenye pesa sio mwenzako.. hao kina chama na konde boy unawaona sababu ya kina babra na mo hapo.. hizo robo fainali za klabu bingwa unaziona sabab ya kina babra na mo.
Je manara ana uwezo wa kulipa mshahara hata wa zimbwe tu?
Hivi ni Jukwaa lipi huwa unachangia vitu vya maana?Write your reply...Barbara na MO waondoke, watuachie Manara wetu
Mwenyekiti ana PhD.Mchukueni na manara awe msemaji wenu
Tatzo shule hamna kichwaniDah huyu Manara akikasirika huwa anakosa busara sana, Hakupaswa kumuongelea mkuu wake wa kazi hivi.
Nilimuona alivyomporomoshea maneno yule mtangazaji wa Clouds kwenye press yake na waandishi wa habari kabla ya game ya Yanga nikamtoa thamani.
Leo hii Haji hata kama umesingiziwa kitu, sio maadili mema kufanya hivi alichofanya. Mkuu wako wa kazi ana haki ya kukuonya iwapo amehisi umekosea, ila wewe wa chini yake hupashwi kumdindia na kumuwekea kibesi hivi, badala yake angepeleka haya malalamiko kwa viongozi wakubwa na sio kumwaga mboga hadharani.
Fala SanaAsalamareku mtanzania Karibu tena kwenye show za vpl kwenye mtanange mgumu ni dabi kubwa uwenda Africa mashiriki na kati waweza iita simba derby Wana lunyasi kati ya Haji sande manara vs Barbara Gonzalez uwezekano wa mvua kunyesha ni asilimia 40 timu zimekwisha kuingia uwanja huku mwamunzi wa kati ni bodi ya simba na mwamunzi wa kulia assistant refaree mshabiki na wanachama wa simba mwamunzi wa kushoto ni moooo energy zikiwa zimebaki sekunde kadhaa mtanange kuanza na refa anampa idhini kuanza Haji naaam kipyanga kimeshasikika na show imeanza Haji Haji na mpira Haji anasakama lango la Barbara, haji anaachia shuti nje kidogo ya kumi na 8 unakwenda nje kidogo ya lango wakati huo huo mwamzi wa pembeni MO akinyoosha kibendera kumaanisha ni offside lkn inaonekana sande alikuwa akifanya dribbling kutokea langoni kwake wacha tuone marudio ya picha kama tutanufaika nayo kutoka kwa lupanda HD mtumbad kwako John samweli, ilikuwa semi voly ambapo manara alikunjuka shuti kali na kwenda nje kidogo ya mringoti mitatu
Aggregate inasoma sifuri bin sifuri Usiyotarajia yanaweza kutokea dabi haina mwenyewe anachua Sasa Barbara barabara na mpira oooh sande kalabwa bonge la tobo mpka mwamzi wa kati anachekelea Barbara anakunjuka shuti kali ninagonga mtambaa wa panya na kurudi ndani anainasa tena barabara anacheza pasi fupi fupi nje ya kumi na nane lengo ni kumvuta adui asogee nje ya lango barabara anapigia kibao kataa kwenda kwa winga yake manara anakimbia kwa speed kwenda kudhibit na kuchukua mpira mwamunzi wa pembeni kibendera kipoo juu huku Barbara akiwa chini anagaagaa kwa maumivu wacha tuone picha za marudio, ohoo mwamunzi wa pembeni MO kaenda yombo na kumpa faida Barbara ikiwa si haki yake ohoo hahaha Barbara analia kwa uchungu pale chini lengo ni kumhadaa mwamzi wa kati manara anaonywa kwa mdomo akiambiwa Mara ya pili Sitakusamehe huku manara akijiuliza kwa kosa gani nilofanya na mpira ni dakika ya 43
Refaree anamaliza mpira bila ya nyongeza yeyote Sande anatoka huku akifoka kwa kutoridhishwa na maamuzi ya waamuzi naam timu zinakwenda kupumzika kujianda na dkika 45 zingine za kipindi cha pili mimi baki kwenye runinga yako na Mimi ni Baraka Hudson mpenja sauti ya radi mtafasiri wa dakika hizi 90 nikiwa na John samweli
Huyo Kitenge ndo kavujisha hii clip?
Kwa hiyo ni kiwewe cha kupigwa kimoja pale mkapa?😂 Mkuu amini maneno yangu alaf caption this 25/7/2021 Simba 3-1 Yanga baada ya hapo hutasikia hiyo ishu tena na manara ataendelea Kama kawaida
Yeye mwenyewe analipwa jiwe saba bila mkataba ndio ataweza kumlipa mtu kweli?Manara uswahili unamdanganya, Manara hana uwezo wa kumtoa simba Babra wala Mo.. ila Babra na Mo wana uwezo wa kumtoa Simba Manara..
Mwenye pesa sio mwenzako.. hao kina chama na konde boy unawaona sababu ya kina babra na Mo hapo.. hizo robo fainali za klabu bingwa unaziona sababu ya kina Barbara na Mo.
Je Manara ana uwezo wa kulipa mshahara hata wa Zimbwe tu?