Jamaa mswahili sana atambue Simba ni kubwa kuliko yeye aondoke tu atuachie club yetu
 
  • Thanks
Reactions: mmh
Leo nimesikia audio ikitembea mitandaoni inayodaiwa kuwa imerekodiwa na Manara akimtuhumu kwa mambo mengi Barbara.Inaonekana hawa watu wana mgogoro wa mda mrefu na hawawezi kufanya kazi tena pamoja. Wewe kama mwanasoka unadhani nini kifanyike? Au ni madhara ya Mo kujimilikisha timu kifamilia?🤣🤣🤣🤣🤣🤣

Kwenye audio hyo Manara kaenda mbali zaidi na kumtishia Barabara sijui Barnaba sorry Barbana,duuh Barbara kwamba ataiacha timu kama alivyoikuta.Sasa hapo sijui nani anaondoka nani anabaki.

Povu ruksa nina nguo chafu hapa.


Najaribu kuapload audio husika hapa inazingua

=====

Afisa Habari wa Simba Haji Manara ameamua kumtolea uvivu Mtendaji Mkuu wa Klabu hiyo Barbara Gonzalez.

Haji anadai Mtendaji huyo amekuwa akimuandama sana na kumnyima raha muda wote toka ameshika majukumu hayo.

View attachment 1862918
Wenyewe wanajiita ".......club kubwa.........club yenye uweledi wa hali ya juu.........club yenye hela......"

Sasa club yenye hela msemaji wao leo karopoka analipwa mshahara mia saba, ila akiwa kwenye press anavyotuna, ngano yenye amira inasubiri ,".......sisi tuna hela....😀😀😀😀😀😀😀😀"

Hapo sasa ndipo mnapoona IQ ya Manara, kwa club yenye uweledi jambo kama hili lisingefika kwenye social networks kwani linashusha hadhi ya club na uongozi mzima unaonekana hauna maana na ni wakipuuzi.

Sasa Manara naona anachambana na BEST WAKE Barbara, anashindana na mtoto wa kike.......ngojea tuangalie show dada CEO naye anaandaa MNYUKLIA WAKE.
 
Manara uswahili unamdanganya.. manara hana uwezo wa kumtoa simba babra wala mo.. ila babra na mo wana uwezo wa kumtoa simba manara..

Mwenye pesa sio mwenzako.. hao kina chama na konde boy unawaona sababu ya kina babra na mo hapo.. hizo robo fainali za klabu bingwa unaziona sabab ya kina babra na mo.

Je manara ana uwezo wa kulipa mshahara hata wa zimbwe tu?
Manara ameshajisahau kwamba yeye pale Simba au Nje ya Simba Hana lolote..Kupiga domo kila mtu anaweza....Kusema kwa Boss wako we Nani huo ni uswahili....Taasisi ina miiko na taratibu zake...Huwezi kumwambia Boss wako Koma..Na ndio mana sisi Watanzania hatuwezi kufanya kazi tuka excell vizuri kwenye international Level..

ujinga Kama Huu wa mipasho unakufanya wewe Haji utoe picha pana ya vijana wengi wa kitanzania...Nakuambia Haji Bila Simba wewe Ni Zero tena Minus Zero ..Sio lolote. SIMBA inakubeba wewe mana ni Taasisi wewe huna lolote...

NAWASHAURI simba baada ya Hii mfukuzeni Kazi huyu jamaa...Mpira sio ujinga ujinga wala sio siasa eti ukifukuzwa Chadema utaenda CCM....

MPIRA Ni tofauti sana. HUYU kajiona mkubwa kuliko Simba..Mfukuzeni Hana lolote..Kwanza Msemaji ndio nini???

Kule Al ahly mnamjua msemaji wao?? Je hawajachukua Ubingwa wa Afrika?? Kocha ndio anaongea kitalaamu sio bla bla...

Fukuza huyu mtu kazi mkimuacha mmeua team na atajiona mungu.
 
Haji Manara ni mshamba sana japo kila siku anajisifia kazaliwa kariakoo. Hajui taratibu za taasisi zinavyofanya kazi badala yake analeta uswahili kwenye mambo ya msingi kabisa. Ukiwa mfanyakazi wa taasisi yoyote ukizinguana na mwajiri au bosi wako mnamalizana huko huko ndani ya hiyo taasisi na mkishindwana mnaenda mahakama ya kazi mpaka mahakama ya rufaa huko. Sasa yeye anabwata bwata tu mitandaoni na kutisha watu huku anaomba huruma ya mashabiki aibu kubwa kwake kwa mtu anayejifanya mjuaji wa kila kitu.

Kwanza huyu ndiye afisa habari wa hovyo kabisa kuwahi kutokeaTanzania kwa sababu kila siku yeye ndiye anayeongoza kutukana na kutishia waandishi wa habari anaowaalika mwenyewe na wala huwa hajui kuwa anaharibu "brand" ya Simba na makampuni anayoyawakilisha kama balozi wa hayo makampuni. Pili muda wote yeye ni kuizungumizia na kuitukana Yanga wakati yeye kaajiriwa na Simba. Haji ni sawa tu yule shabiki wa Yanga aliyeibatiza jina la utopolo nawashangaa sana Simba kumpa hicho cheo na kumuacha nacho mpaka leo eti afisa habari wa timu. "Anyway" bodi ya Simba na Mo ndio wakulaumiwa jini wamelifuga wenyewe acha liwatafune kwani walitakiwa wawe wameshamfukuza siku nyingi sana.

Simba ni kubwa kuliko Haji Manara, Mo, Barbra, Kaduguda, Try Again na wengineo wote. Viongozi, wafadhili na wawekezaji wote watapita lakini Simba itadumu milele kwa hiyo mtu yoyote asijifanye eti yeye ni muhimu sana pale Simba.
 
Dah huyu Manara akikasirika huwa anakosa busara sana, Hakupaswa kumuongelea mkuu wake wa kazi hivi.

Nilimuona alivyomporomoshea maneno yule mtangazaji wa Clouds kwenye press yake na waandishi wa habari kabla ya game ya Yanga nikamtoa thamani.

Leo hii Haji hata kama umesingiziwa kitu, sio maadili mema kufanya hivi alichofanya. Mkuu wako wa kazi ana haki ya kukuonya iwapo amehisi umekosea, ila wewe wa chini yake hupashwi kumdindia na kumuwekea kibesi hivi, badala yake angepeleka haya malalamiko kwa viongozi wakubwa na sio kumwaga mboga hadharani.
 
Dah huyu Manara akikasirika huwa anakosa busara sana, Hakupaswa kumuongelea mkuu wake wa kazi hivi.

Nilimuona alivyomporomoshea maneno yule mtangazaji wa Clouds kwenye press yake na waandishi wa habari kabla ya game ya Yanga nikamtoa thamani.

Leo hii Haji hata kama umesingiziwa kitu, sio maadili mema kufanya hivi alichofanya. Mkuu wako wa kazi ana haki ya kukuonya iwapo amehisi umekosea, ila wewe wa chini yake hupashwi kumdindia na kumuwekea kibesi hivi, badala yake angepeleka haya malalamiko kwa viongozi wakubwa na sio kumwaga mboga hadharani.
Tatzo shule hamna kichwani
 
Asalamareku mtanzania Karibu tena kwenye show za vpl kwenye mtanange mgumu ni dabi kubwa uwenda Africa mashiriki na kati waweza iita simba derby Wana lunyasi kati ya Haji sande manara vs Barbara Gonzalez uwezekano wa mvua kunyesha ni asilimia 40 timu zimekwisha kuingia uwanja huku mwamunzi wa kati ni bodi ya simba na mwamunzi wa kulia assistant refaree mshabiki na wanachama wa simba mwamunzi wa kushoto ni moooo energy zikiwa zimebaki sekunde kadhaa mtanange kuanza na refa anampa idhini kuanza Haji naaam kipyanga kimeshasikika na show imeanza Haji Haji na mpira Haji anasakama lango la Barbara, haji anaachia shuti nje kidogo ya kumi na 8 unakwenda nje kidogo ya lango wakati huo huo mwamzi wa pembeni MO akinyoosha kibendera kumaanisha ni offside lkn inaonekana sande alikuwa akifanya dribbling kutokea langoni kwake wacha tuone marudio ya picha kama tutanufaika nayo kutoka kwa lupanda HD mtumbad kwako John samweli, ilikuwa semi voly ambapo manara alikunjuka shuti kali na kwenda nje kidogo ya mringoti mitatu

Aggregate inasoma sifuri bin sifuri Usiyotarajia yanaweza kutokea dabi haina mwenyewe anachua Sasa Barbara barabara na mpira oooh sande kalabwa bonge la tobo mpka mwamzi wa kati anachekelea Barbara anakunjuka shuti kali ninagonga mtambaa wa panya na kurudi ndani anainasa tena barabara anacheza pasi fupi fupi nje ya kumi na nane lengo ni kumvuta adui asogee nje ya lango barabara anapigia kibao kataa kwenda kwa winga yake manara anakimbia kwa speed kwenda kudhibit na kuchukua mpira mwamunzi wa pembeni kibendera kipoo juu huku Barbara akiwa chini anagaagaa kwa maumivu wacha tuone picha za marudio, ohoo mwamunzi wa pembeni MO kaenda yombo na kumpa faida Barbara ikiwa si haki yake ohoo hahaha Barbara analia kwa uchungu pale chini lengo ni kumhadaa mwamzi wa kati manara anaonywa kwa mdomo akiambiwa Mara ya pili Sitakusamehe huku manara akijiuliza kwa kosa gani nilofanya na mpira ni dakika ya 43

Refaree anamaliza mpira bila ya nyongeza yeyote Sande anatoka huku akifoka kwa kutoridhishwa na maamuzi ya waamuzi naam timu zinakwenda kupumzika kujianda na dkika 45 zingine za kipindi cha pili mimi baki kwenye runinga yako na Mimi ni Baraka Hudson mpenja sauti ya radi mtafasiri wa dakika hizi 90 nikiwa na John samweli
Fala Sana
 
Ila simba nao wajinga sana, tangu lini afisa habari wa Coca cola akawa ambasador wa Pepsi?

Yaani Haji ni afisa habari wa Simba, ambayo ina dhaminiwa na bidhaa za Metl, hapo hapo ni balozi wa bidhaa za Asasi na GSM washindani wa Metl.

Haji ameitumia simba kupata umaarufu, kisha akautumia huo umaarufu kutangaza bidhaa za kampuni mshindani wa wadhamini wa simba......
 
Manara uswahili unamdanganya, Manara hana uwezo wa kumtoa simba Babra wala Mo.. ila Babra na Mo wana uwezo wa kumtoa Simba Manara..

Mwenye pesa sio mwenzako.. hao kina chama na konde boy unawaona sababu ya kina babra na Mo hapo.. hizo robo fainali za klabu bingwa unaziona sababu ya kina Barbara na Mo.

Je Manara ana uwezo wa kulipa mshahara hata wa Zimbwe tu?
Yeye mwenyewe analipwa jiwe saba bila mkataba ndio ataweza kumlipa mtu kweli?
 
6324C7F7-BD11-418E-BFD1-8E5618686176.jpeg

Oscar Oscar kama angekuwa ni Simba. Angekuwa anasubiri simu sasa hivi?
 
Back
Top Bottom