tindikalikali
JF-Expert Member
- Jan 14, 2011
- 4,855
- 1,117
Huyu ni msichana ambaye nilianza kumfatilia toka mwaka 2009 mwanzoni. Mwanzo aliniambia anihitaji, nilipojitahidi kumbembeleza aliniambi kwamba hakuna kitu anakichukia kama mapenzi japo hakunipa sababu zake. Muda ulienda na nilijitahidi kuweka ukaribu naye, huku nikiendelea kumuaminisha kwamba nampenda. Siku zilienda mbele na katika hali ya kutaka kunirudisha nyuma, akaniambia kwamba "ana mtu", kitu ambacho hakikuwepo lakini yeye alisisitiza hivyo. Ulipita muda bila kuwasiliana naye{alikuwa shuleni}, baada ya kumaliza form 6 mwaka huu alinitafuta, na tukaanza kuwasiliana tena. Lakini kila nilipoongelea suala la mapenzi, aligeuka mbogo japo alianza kuhitaji kujua habari zangu. Kuna siku baada ya kumshawishi sana alijibu " I dont luv 2 be urs", sms hiyo ilinifanya nimchunie, lakini baada ya wiki 2 aliniuliza "mbona kimya", nilimjibu kwamba "napenda sana kuwa karibu na wewe ila siwezi kuendelea kujiumiza", hapo naye akakaa kimya. Usiku wa kuamkia leo nimeongea naye kwa kina kama masaa 3, ndipo akanithibitishia kwamba hajawahi kuwa na mpenzi na wala hafikirii, nikamuuliza plan zake, akasema nimwambie kwanza za kwangu, nilimweleza ndipo naye akanambia kwamba ataingia kwenye mahusiano pale tu atakapokuwa na elimu+kazi yake. Alisisitiza sana niheshimu malengo yake. Kwa kifupi tumeelewana lakini hatujakubaliana. Nipo njia panda, je anaweza kuwa wangu na kunipenda?, na nahitaji ushauri wenu jinsi ya kumtoa katika hofu alizonazo.