Mwanamageuko
JF-Expert Member
- Oct 31, 2010
- 8,602
- 5,569
Hivi hamjajiuliza hivi mheshimiwa sana bwana SK kwanini amebakiwa na habari moja tu kila wiki toka uchaguzi uishe?
Hivi bado hamjajiuliza mtu huyohuyo aliyekuwa akianika ufisadi mpaka akamwagiwa tindikali (kwa mujibu wa madai yake, maana yawezekana ulikuwa mpango wake mwenyewe katika kuosha nyota - kawaida huwa siwaamini wachonganishi na wasiopenda amani - huo ni muono wangu mniwie radhi.)
Pia hatujuzwi hata na magazeti yake kesi ile ilikwishaje!!! badala yake hataki tumhoji hayo anatuletea mapya (naogopa sana kuyaita utumbo kwa maana yanauza kuliko mambo yaliyo muhimu kwa taifa).
SK ni miongoni waandishi habari ambao wamepata kuheshimika, na kwa namna ya uandishi wao ulivyo ukisifiwa, walifikia kilele na kuonekana mashujaa. Leo hii wamejaa majungu baada ya kuona magazeti yao yanafilisika, (yapo baadhi yako taabani hata mishahara inakaribia kushindikana, waandishi wao wanaishi kwa kudra za Mungu) Hivyo basi katika njia mbadala ya kujikimu alianza na CUF sijui walimshinda nguvu sasa AMEHAMIA RASMI CHADEMA kwa kupitia MLANGO WA NYUMA.
Sitoshangaa kesho akienda NCCR na TLP ili mradi aone ni chama kipi kina nguvu
AMKENI MUUJUE UKWELI!
Hivi bado hamjajiuliza mtu huyohuyo aliyekuwa akianika ufisadi mpaka akamwagiwa tindikali (kwa mujibu wa madai yake, maana yawezekana ulikuwa mpango wake mwenyewe katika kuosha nyota - kawaida huwa siwaamini wachonganishi na wasiopenda amani - huo ni muono wangu mniwie radhi.)
Pia hatujuzwi hata na magazeti yake kesi ile ilikwishaje!!! badala yake hataki tumhoji hayo anatuletea mapya (naogopa sana kuyaita utumbo kwa maana yanauza kuliko mambo yaliyo muhimu kwa taifa).
SK ni miongoni waandishi habari ambao wamepata kuheshimika, na kwa namna ya uandishi wao ulivyo ukisifiwa, walifikia kilele na kuonekana mashujaa. Leo hii wamejaa majungu baada ya kuona magazeti yao yanafilisika, (yapo baadhi yako taabani hata mishahara inakaribia kushindikana, waandishi wao wanaishi kwa kudra za Mungu) Hivyo basi katika njia mbadala ya kujikimu alianza na CUF sijui walimshinda nguvu sasa AMEHAMIA RASMI CHADEMA kwa kupitia MLANGO WA NYUMA.
Sitoshangaa kesho akienda NCCR na TLP ili mradi aone ni chama kipi kina nguvu
AMKENI MUUJUE UKWELI!