Haiti ni kielelezo cha ujinga wa Mwafrika

Despite the Haitian victory, France refused to recognize the newly independent country's sovereignty until 1825, in exchange for 150 million gold francs. This fee, demanded as retribution for the "lost property,"—slaves, land, equipment etc.—of the former colonialists, was later reduced to 90 million. Haiti agreed to pay the price to lift a crippling embargo imposed by France, Britain, and the United States— but to do so, the Haitian government had to take out high interest loans. The debt was not repaid in full until 1947.[19]
 
Kuna watu wanadhani kama wakiendesha utawala wa kubinya haki za raia na uonevu kwa wananchi kadri watakavyo basi maendeleo wanayofikiri wananchi wanapaswa kuwa nayo yatakuja na wananchi watafurahi.

Huko America ipo nchi inaitwa Haiti ambayo raia wake kwa zaidi ya 90% ni Waafrica wenzetu weusi. Kwa kipindi kirefu cha uhuru wake wa miaka zaidi 200 (Haiti imepata uhuru mwaka 1804, January 1) ikiwa ni nchi ya pili kuwa huru katika America baada ya USA iliyoitangulia kwa miaka 28 tu.

Pamoja na miaka mingi ya uhuru Haiti ni moja ya nchi masikini kabisa duniani. Ikiwa ndiyo kinara wa umasikini huko America. Hii yote imesababishwa na aina ya siasa ambazo wananchi wa Haiti wamejikuta wakikabilina nazo ambazo kwa kiasi kikubwa zinaendana na siasa za sasa za serikali ya Magufuli.

Haiti ni nchi yenye demokrasia ya maneno huku serikali ikiwa busy kubinya uhuru wa raia na kufanya mambo inavyopenda na siyo kadri raia wa nchi hiyo wanavyotaka. Lakini kwa sababu raia hawana cha kufanya imebidi waishi katika hali hiyo ambayo imewasababishia umasikini na unyonge kwa miaka 214.

America walipopata uhuru walichagua kuwa na siasa ya kistaarabu yenye kuheshimu haki za raia na uhuru wa kujieleza. Haiti wao ilikuwa kinyume chake na matokeo yake leo hii nchi hizi mbili za mwanzo kupata uhuru huko America moja wanaishi kama peponi (USA) na wengine wapo jehanum(Haiti)

Yanayotokea hapa nchini leo yananifanya nione kabisa nchi yetu imeamua kupita njia waliyopita/wanayopita Haiti. Kufail kwa Haiti imekuwa ni reference ya ujinga wa mtu mweusi. Kwamba hata ipite miaka mingapi hatuwezi kuendesha nchi ikaweza kuendelea.

Nawasihi viongozi wetu wabadilike na wakubali ukweli kuwa Watanzania siyo ng'ombe ambao wanaweza kuwaburuza kadri watakavyo. Waone umuhimu wa kuheshimu haki za raia na haki ya kuwa na mawazo tofauti. Mambo ya kusema mtu akiandamana ataenda msimulia baba yake au kuwa mtu akiandamana hata chumbani kwake watamkamata ni tabia za ki-Haiti na kama wataendelea hivyo basi wajue hata miaka 200 itapita na hakuna maendeleo yatakayokuwepo kama ilivyo Haiti.

Viongozi wetu waone aibu kusema uongo hadharani kama yule aliyesema wanaoandaa maandamano wanandaa risasi wajipige ili kuchafua sura ya nchi. Hata kama sisi Waafrica hususani Watanzania ni wajinga lakini tusioneshe ujinga wetu hadharani kama alivyofanya yule waziri wetu leo pale Singida. Waziri yule ni Dr. anapoamua kusema uongo hadharani kama alivyosema leo basi ajaribu hata kuufanya ili uonekane ni uongo uliotolewa na mtu mwenye PhD na siyo anaongopa kama kilaza wa darasa la nne.
kwa uongozi uliopo hawana exposure tusitegemee maendeleo yoyote zaidi ya kutawala kwa vitisho na kugandamiza demokrasia
 
Real, Unafahamu historia ya Haiti mkuu, Kama unaongelea kile kisiwa cha makazi ya watumwa waliochoka basi mleta uzi nina kupinga nenda google au Wikipedia soma vizuri The Haitian development and its reform utajua kwanini Haiti ni maskini
Mkuu tumegee unachokifahami
 
Mwigulu mchemba ni kielelezo kwamba mwanasiasa akiwa siasani kuwa phd holder sio jambo la maana sana. Unaweza kutema mashudu kadri utakavyo ili mradi magufuli anafurahia.
 
Haiti ipo kwenye ukanda wa majanga. Kila ikijaribu kujiinua inaangushwa ama na matetemeko au vimbuka.
 
Kasome historia ya Singapore na nchi nyingine zote zilizo katika kile kijulikanacho kama 4 Asian Tigers ujue njia zilizopitia kutoka kuwa mataifa fukara hadi kuwa mataifa tajiri...tatizo la mwafrika sio kumpa uhuru, ni kumbadili utamaduni wake completely (Culture, attitude and mentality)


zetu zitabadilika lini.
kuna kitu kinachoweza kuleta hayo zaidi ya elimu?
 
Hakuna nchi yenye utawala wa kibabe ambayo imefanikiwa kuwafanya wananchi wake kuwa na maendeleo.

Mifano mizuri linganisha Taifa la China lenye udikteta na tawala huru kama Taiwan, Hong Kong na nchi kama Singapore na Japan.

Mpaka leo nchi ya China kwa kipimo cha maendeleo ya raia, ni duni sana.


Mkuu...Singapore imetoka kuwa nchi fukara ya ulimwengu wa tatu hadi kuwa nchi tajiri ya ulimwengu wa kwanza ikiwa chini ya utawala wa miaka 30 wa waziri mkuu mmoja Lee Kuan Yew aliyeongoza nchi kwa mkono wa chuma. Kasome historia ya Singapore chini ya Lee Kuan Yew then utaona namna ya kubadili nchi na utamaduni wa raia.

Kimsingi nchi zilizoendelea haraka Asia maarufu kama 4 Asian Tigers (Singapore, South Korea, Taiwan na HongKong) zote ziliendelea kwa haraka chini ya ubinyaji mkubwa sana wa uhuru, zilipopata maendeleo makubwa zikaanza kuachia uhuru wa raia taratibu....

Hiyo China yenyewe imeanza kupata mwelekeo wa kimaendeleo ama kujenga misingi ya kimaendeleo wakati wa Mao Tse Tung katika kile kijulikanacho kama The time of Cultural revolution kuanzia miaka ya 1960, ni katika kipindi ambacho china ilipitia mkono wa chuma ajabu na mamilioni ya watu kufa kwa njaa...

Tangu kuisha vita vya pili vya dunia, ni nchi moja tu iliyotoka kwenye umaskini kwenda kwenye utajiri kwa kupitia demokrasia safi na uhuru wa kila mwananchi, nchi hiyo ni Poland....!!!
 
Back
Top Bottom