Haiti: Ndege yaanguka mtaa wenye watu wengi, yaua watu sita

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,455
4EQSHKAIHRM53JB5R66HZ2FYKM.jpg


Ndege ndogo imeanguka katika mtaa wenye watu wengi katika Jiji la Nchini Port-au-Prince Nchini Haiti, jana Aprili 20, 2022 na kuua watu sita akiwemo rubani wa ndege hiyo.

Ndege hiyo ilikuwa ikiruka kutoka Uwanja wa Ndege wa Port-au-Prince saa 9:44 Alasiri kuelekea katika Jiji lingine Nchini humo la Jacmel. Mamlaka za Usafiri wa Anga zimesema injini ilifeli na kusababisha ianguke saa 10:04 Jioni.

"Natoa pole kwa wafiwa na walioathiriwa kwa tukio hilo," aliandika Waziri Mkuu wa Haiti, Ariel Henry kupitia ukurasa wake wa Twitter

Meya wa Jiji ambapo ndege ilianguka, Jude Edouard Pierre amesema watu sita wamefariki, rubani akifariki wakati akiwa njiani kupelekwa hospitali.

Source: Usnews
 
Jamaa zangu wa air crash investigation watatupa majibu ya chanzo cha engine kufeli.
 
Si kila ajali hutolewa maelezo. Huangalia zile ajali ambazo zina manufaa
Hizo ninakili zetu sie wabongo wenzetu hawapo hivyo...lazima ufanye uchunguzi maana inaweza kuwa imesababishwa na design fault, ikimaanisha kwamba ndege zote za aina hiyo zinabidi zirekebishwe.

Sie wabongo tunajibu letu pendwa kwa kila ajali " mipango ya mungu"
 
Hizo ninakili zetu sie wabongo wenzetu hawapo hivyo...lazima ufanye uchunguzi maana inaweza kuwa imesababishwa na design fault, ikimaanisha kwamba ndege zote za aina hiyo zinabidi zirekebishwe.

Sie wabongo tunajibu letu pendwa kwa kila ajali " mipango ya mungu"
Wewe kweli mbumbumbu. Wenzenu hufanya uchunguzi? Akina Nani hao? Au unamaanisha Wazungu?

Kwa taarifa yako HAITI Ni Nchi ya Kisenge Sana kuliko hata Burundi na Somalia,Huwezi kuifananisha na Tanzania. Lile Bara ambapo wapo HAITI ilikuwa bahati mbaya Sana.
 
Hwenda Haiti kukawa sehemu ya tafiti na majaribio mengi ya nchi za magharibi....
 
Wewe kweli mbumbumbu. Wenzenu hufanya uchunguzi? Akina Nani hao? Au unamaanisha Wazungu?

Kwa taarifa yako HAITI Ni Nchi ya Kisenge Sana kuliko hata Burundi na Somalia,Huwezi kuifananisha na Tanzania. Lile Bara ambapo wapo HAITI ilikuwa bahati mbaya Sana.
Sasa unadhani nani atafanya uchunguzi kama sio wazungu?
Ndege zenyewe wanatengeneza wao so it only makes sense kwa wao kuhusika kwenye uchunguzi.
 


Ndege ndogo imeanguka katika mtaa wenye watu wengi katika Jiji la Nchini Port-au-Prince Nchini Haiti, jana Aprili 20, 2022 na kuua watu sita akiwemo rubani wa ndege hiyo.

Ndege hiyo ilikuwa ikiruka kutoka Uwanja wa Ndege wa Port-au-Prince saa 9:44 Alasiri kuelekea katika Jiji lingine Nchini humo la Jacmel. Mamlaka za Usafiri wa Anga zimesema injini ilifeli na kusababisha ianguke saa 10:04 Jioni.

"Natoa pole kwa wafiwa na walioathiriwa kwa tukio hilo," aliandika Waziri Mkuu wa Haiti, Ariel Henry kupitia ukurasa wake wa Twitter

Meya wa Jiji ambapo ndege ilianguka, Jude Edouard Pierre amesema watu sita wamefariki, rubani akifariki wakati akiwa njiani kupelekwa hospitali.

Source: Usnews
Haiti ni kanchi kenye majanga kila kukicha yani full majanga
 
Back
Top Bottom