Haitakuwa busara kuiuza au kuivunja Ikulu ya Dar es Salaam

mandokwa

JF-Expert Member
Jun 5, 2013
620
865
Wakuu hali zenu,
Najua mnajua kwamba tunakaribia kuhamia dodoma. Na baadhi ya vyanzo vya habari vinasema tukihama yale majengo ya serikali magogoni na mawizara tutayauza. Hili ndilo limenifanya niandike angalau kuweka mawazo yangu sawa.

Nashauri majengo ya Ikulu yabaki na tuyafanye makumbusho ambayo vizazi vyetu vitaendelea kujifunza historia endelevu ya taifa letu. Kwanza itaingiza kipato lakini pia itatoa fursa ya kulinda mandhari na heshima ya kitaifa. Nashukuru nimewahi kuishi uingereza na ufaransa kwa muda flan. wenzetu majengo kama haya huyahifadhi na kuyapa thamani zaidi. Tuweke uhai ndani ya majengo haya kwa kuonesha matukio gani au historia gani zilifanyika kwamfano rais gani alipenda kukaa na kufanya nini wapi? mikataba kadhaa ilisainiwa wapi au tukio gani lilifanyika wapi. ni muhimu, hatuhami nchi tunabadili makazi hakuna haja ya kuuza au kuvunja maana wapo ambao mawazo yao mafupi sana.

Msiweke mkuu wa mkoa mle kwani haya majengo hadhi na gharama zake ni kubwa sana. Mkuu wa mkoa aendelee kuishi anakoishi sasa. mnaweza kuweka ikawa ni ikulu ndogo ya raisi na ikatunzwa pia sio mbaya sana. Majengo ya wizara nakadhalika yakodishwe na sio kuuza. ukiuza unapata pesa once unatumia kujenga kolomije na zinaisha. ukiwekeza kwenye mambo mengine utaendelea kupata pango na umiliki wako utaendelea. tusiwe na mawazo ya kuharibu tu. tujifunze kwa wenzetu.

Nawasilisha kwa wenye akili walione,

Nangu mandokwa

 
Hhh jamaa ni raisi wa ujenzi sio wa uchumi kila siku ye habari zake ni barabara na majengo tu maswala ya uchumi kwake hayajui

Ukitaka kuamini simamisha msafara wake alafu msikilize habari zake anazoongea utamsikia anaongea kujenga na kubomoa tu hhhhh
 
Hivi hati ya kiwanja bado ina jina la malkia? Kuna tetesi kuna kigogo aliikopea bank.
 
Huu mchezo wa kuweja ukulu ndogo au ofisi ndogo Dar utafanya watu wasihamie Dodoma. Ofisi ndogo na ikulu ndogo itakuwa na mvuto kama Nyumba ndogo vile! Piga bei ikulu fasta ili wahusika wasije kubadili mawazo huko mbeleni! Dr Kisha keshapata mabilioni yake tayari, itapendeza akiuziwa hiyo ikulu!
 
Wakuu hali zenu,
Najua mnajua kwamba tunakaribia kuhamia dodoma. Na baadhi ya vyanzo vya habari vinasema tukihama yale majengo ya serikali magogoni na mawizara tutayauza. Hili ndilo limenifanya niandike angalau kuweka mawazo yangu sawa.

Nashauri majengo ya Ikulu yabaki na tuyafanye makumbusho ambayo vizazi vyetu vitaendelea kujifunza historia endelevu ya taifa letu. Kwanza itaingiza kipato lakini pia itatoa fursa ya kulinda mandhari na heshima ya kitaifa. Nashukuru nimewahi kuishi uingereza na ufaransa kwa muda flan. wenzetu majengo kama haya huyahifadhi na kuyapa thamani zaidi. Tuweke uhai ndani ya majengo haya kwa kuonesha matukio gani au historia gani zilifanyika kwamfano rais gani alipenda kukaa na kufanya nini wapi? mikataba kadhaa ilisainiwa wapi au tukio gani lilifanyika wapi. ni muhimu, hatuhami nchi tunabadili makazi hakuna haja ya kuuza au kuvunja maana wapo ambao mawazo yao mafupi sana.

Msiweke mkuu wa mkoa mle kwani haya majengo hadhi na gharama zake ni kubwa sana. Mkuu wa mkoa aendelee kuishi anakoishi sasa. mnaweza kuweka ikawa ni ikulu ndogo ya raisi na ikatunzwa pia sio mbaya sana. Majengo ya wizara nakadhalika yakodishwe na sio kuuza. ukiuza unapata pesa once unatumia kujenga kolomije na zinaisha. ukiwekeza kwenye mambo mengine utaendelea kupata pango na umiliki wako utaendelea. tusiwe na mawazo ya kuharibu tu. tujifunze kwa wenzetu.

Nawasilisha kwa wenye akili walione,

Nangu mandokwa
Wapingishwe chadema hapo !
 
hatuhami nchi tunabadili makazi hakuna haja ya kuuza au kuvunja maana wapo ambao mawazo yao mafupi sana.
Unayajua roho ya uharibifu? Ikikuvaa wewe ni kuvunja tu, Hata isipofanya vunja wewe vitavunjika vyenyewe. Hili Pepo linasingiziwa tu kuwa eti ni expansion joint
Msiweke mkuu wa mkoa mle kwani haya majengo hadhi na gharama zake ni kubwa sana. Mkuu wa mkoa aendelee kuishi anakoishi sasa. mnaweza kuweka ikawa ni ikulu ndogo ya raisi na ikatunzwa pia sio mbaya sana. Majengo ya wizara nakadhalika yakodishwe na sio kuuza. ukiuza unapata pesa once unatumia kujenga kolomije na zinaisha. ukiwekeza kwenye mambo mengine utaendelea kupata pango na umiliki wako utaendelea. tusiwe na mawazo ya kuharibu tu. tujifunze kwa wenzetu.

Nawasilisha kwa wenye akili walione,

Nangu mandokwa
Hapa umeeleweka vyema.
 
13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom