Haikuwa uamuzi sahihi kusitisha ajira hata kwa Walemavu, hili kundi linataabika sana mtaani

Natafuta matibabu

JF-Expert Member
Aug 1, 2020
262
301
Suala la ajira limekuwa ni kilio kwa makundi yote katika jamii hasa wenye vipato vya chini ikiwemo wenye ulemavu wa aina mbalimbali na wasio na ulemavu pindi wanapohitimu elimu zao ama ngazi ya cheti hadi shahada hasa katika utawala huu wa serikali ya awamu ya tano.

Tumesikia kauli mbalimbali hasa za wale tuliowapa dhamana ya kutuongoza kutusihi tujiajiri bila kuzingatia hizo kauli zinahusu makundi ya aina gani ya jamii(wenye mitaji au wasio na mitaji, wenye ulemavu au wasio na ulemavu).

Kati ya haya makundi, kundi linaloathirika sana ni hili kundi la walemavu wasio na mitaji na serikali ipo kimya bila kuwaajiri.

Nimefikiria sana hii serikali ilipositisha kuajiri wale wanaohitimu masomo yao katika ngazi mbalimbali za kielimu kama ilivyokuwa desturi katika awamu iliyopita, huu uamuzi ulizingatia uwepo wa hili kundi la walemavu kweli? Hivi wanajua hili kundi linavyonyanyasika mtaani? Vyama vya kutetea Walemavu navyo kimya(mara mwisho niliwasikia wanapongeza taratibu za uchaguzi mwaka jana)

Sijajua Sheria inasemaje kuhusu ajira kwa walemavu, hata kama ajira zilisitishwa kwa namna moja ama nyingine ili kupisha mambo mengine kufanyika, hili kundi la walemavu lisingesitishiwa ajira kutokana na uhitaji wake wa kujikwamua katika maisha ya kila siku. Haipendezi mlemavu kajitahidi kapata elimu nzuri ama ngazi ya astashahada stashahada au shahada halafu anarudi mtaani anakuwa mzigo tena ukilinganisha na asiye mlemavu.

Serikali toeni ajira kwa walemavu wenye sifa na uwezo wa kazi kulingana na taaluma zao.
 
Mkuu sisi wattu wenye ulemavu hakika tunapata changamoto sana. Bora hata umelisemea. Fikiria mtu asiyeona anajitahidi anamaliza shahada yake anarudi kukaa nyumbani.
Inasikitisha sana, ivi sheria inasemaje kuhusu hili suala la ajira kwa walemavu hata kama haifuatwi.

Hili kundi haitakiwi kusahaulika kiasi hiki hata kama mambo mengi makubwa yanatekelezwa
 
Lakini neno ulemavu ni vile ww unavyojiposition...kama ni mlemavu wa viungo
je akili nayo ina ulemavu?
Mie nadhan kama akili haina ulemavu basi huna haja kucomplain serikali...anza ww serikali ije kukupush
Tuchukulie mfano hawa walemavu wasioona.

Sawa atakuwa na akili timamu lakini tatizo ni kutoona ambalo litakuwa changamoto katika kutumia akili yake ili aweze kufanya mambo kadhaa. Watu kama hawa wanahitaji msaada.
 
Hatuna pa kupanza sauti tunabaki kuugulia maumivu kimya kimya
Inabidi kuyazoea maumivu, na ndio kwanza hajamaliza hata nusu mwaka toka ameapishwa, akimaliza miaka miwili raia wa hali ya chini watachakaa chaka chaka kama tambala bovu. Ikipita miaka mitano hatutazamani usoni raia halafu watarudi kwenye majukwaa na kuomba kura tena.

Halafu shida zipo kwa wananchi wa chini tu, kama vi catoon mbele ya walioridhika, so sio tatizo kwao, wao hawajui nini maana ya kukosa mlo wala njaa, hawajui nini maana ya kukosa ajira, hawajui nini maana ya kukosa hata vocha, wala kutembea kwa miguu mpaka chupi kuchana mapaja, wao account za benki zinasoma mamillioni kila mwisho wa mwezi (Jumlisha posho, mafuta ya gari, kiinua mgongo, posho za kufanya kazi nje ya sehemu ya ajira, posho za safari n.k) VX zinapaki nje ya milango yao kwa kugonga meza bungeni na kusifia utumbo. Maisha mazuri.

Kipi utakachoongea wewe halafu wao wakuelewe? Haiwezekani kuelewana kwasababu ni level mbili tofauti za kimaisha.

Kumbuka, wabunge wa kupita bila kupingwa wameshaanza kuomba bunge lisibadili katiba yote libadili kipengele tu cha "MIHULA YA URAIS IONGEZWE".

Na kuna maandamano ya kutengenezwa kwa raia yapo njiani ili Rais aongezewe muda wa kutawala, ikiwezekana nchi itawaliwe "KIFALME" au awe "RAIS WA MAISHA" kama Yoweri Kaguta Museven.

#Nchi hii bila katiba mpya yenye kuwawekea mipaka viongozi na kuwawajibisha ni kazi bure, raia wa chini watapigwa vid**e kila kona ya mwili mpaka machoni.
 
Inabidi kuyazoea maumivu, maana wabunge wa kupita bila kupingwa wameshaanza kuomba bunge lisibadili katiba yote libadili kipengele tu cha "MIHULA YA URAIS IONGEZWE".

Na kuna maandamano ya kutengenezwa kwa raia yapo njiani ili Rais aongezewe muda wa kutawala, ikiwezekana nchi itawaliwe "KIFALME" au awe "RAIS WA MAISHA" kama Yoweri Kaguta Museven.
Kuwa Rais wa Maisha sio tatizo endapo haki za kila mmoja zikizingatiwa.

Kama anataka kuwa Rais wa maisha ili atukandamize hilo hapana
 
Back
Top Bottom