kalaghesye
Member
- Jan 16, 2012
- 79
- 11
Hamjambo jamani? Niko katika kufanya utafiti kuhusu miundo ya taasisi na mambo yanayozingatiwa katika kuunda ORGANIZATION STRUCTURES ikiwemo Shughuli Mama (Core Function) na majukumu husika (Responsibilities). Hii ni katika kuangalia uzingatifu wa matumizi sahihi ya madaraka, mali za umma, ufanisi na uwajibikaji. Katika muda huu mfupi nimekutana na vituko vingi sana ikiwa ni pamoja na kuunda mifumo inayoyaongezea mashirika na nchi kwa ujumla matumizi yasiyo ya lazima na hatimaye kuliingizia Taifa hasara.
MOJA ni kuwa Idara huundwa ikiwa haina majukumu linganifu na shughuli mama ya shirika; Pili ni Idara huundwa ikiwa ina MKURUGENZI na MAMENEJA bila watu wa kuwa-manage! Baada ya kuuliza maswali kadhaa nikafikia kupata jibu lisilo la moja kwa moja kuwa kwenye mashirika ya Umma watu hutafuta njia mbalimbali kutengeneza mchongo kwa ajili ya maswahiba wao. Hii ni kwa sababu ukurugenzi/umeneja huendana na mshahara mkubwa, posho kubwa na safari za mara kwa mara za nje na ndani ya nchi. Hili si tatizo endapo kazi husika zingekuwepo (Job Description). Watu wamesahau kabisa kuwa hizi ni fedha za wavuja jasho.
Nina mifano kadhaa kuhusiana na hili .... katika mashirika niliyoyafanyia utafiti ni Mamlaka ya Bandari (TPA), Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Weights and Measures Agency (WMA), Shirika la Bima la Taifa (NIC), n.k.
Kwa mfano msharaha wa mwezi wa Mkurugenzi kwenye mashirika haya si chini ya Sh. 12,000,000/=, Meneja Shs. 8,000,000/=. Kuna shirika lina wakurugenzi Ishirini (20) na Mameneja zaidi ya Arobaini (40). Mh. Pinda anasema hakuna No More Posho huku wenzake wanatanuua miundo.
SWALI : Hivi Bodi za Wakurugenzi wa Mashirika ya Umma huwa zinaridhia miundo husika? Je, nini kuhusu Wizara Mama? Jamani tuzungumzie hili maana nchi inaumia. Mawaziri husika wa Mashirika tajwa Dr. Mwakyembe, Dr. Hussein Mwinyi, Dr. John Magufuli, Dr. Mgimwa mpo?
Dondoo za matokeo ya utafiti wangu zitakuwa wazi kadri muda unavyokwenda.
MOJA ni kuwa Idara huundwa ikiwa haina majukumu linganifu na shughuli mama ya shirika; Pili ni Idara huundwa ikiwa ina MKURUGENZI na MAMENEJA bila watu wa kuwa-manage! Baada ya kuuliza maswali kadhaa nikafikia kupata jibu lisilo la moja kwa moja kuwa kwenye mashirika ya Umma watu hutafuta njia mbalimbali kutengeneza mchongo kwa ajili ya maswahiba wao. Hii ni kwa sababu ukurugenzi/umeneja huendana na mshahara mkubwa, posho kubwa na safari za mara kwa mara za nje na ndani ya nchi. Hili si tatizo endapo kazi husika zingekuwepo (Job Description). Watu wamesahau kabisa kuwa hizi ni fedha za wavuja jasho.
Nina mifano kadhaa kuhusiana na hili .... katika mashirika niliyoyafanyia utafiti ni Mamlaka ya Bandari (TPA), Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Weights and Measures Agency (WMA), Shirika la Bima la Taifa (NIC), n.k.
Kwa mfano msharaha wa mwezi wa Mkurugenzi kwenye mashirika haya si chini ya Sh. 12,000,000/=, Meneja Shs. 8,000,000/=. Kuna shirika lina wakurugenzi Ishirini (20) na Mameneja zaidi ya Arobaini (40). Mh. Pinda anasema hakuna No More Posho huku wenzake wanatanuua miundo.
SWALI : Hivi Bodi za Wakurugenzi wa Mashirika ya Umma huwa zinaridhia miundo husika? Je, nini kuhusu Wizara Mama? Jamani tuzungumzie hili maana nchi inaumia. Mawaziri husika wa Mashirika tajwa Dr. Mwakyembe, Dr. Hussein Mwinyi, Dr. John Magufuli, Dr. Mgimwa mpo?
Dondoo za matokeo ya utafiti wangu zitakuwa wazi kadri muda unavyokwenda.