Hadithi

Husna Muba

JF-Expert Member
Jan 28, 2017
14,524
44,567
THE ISLAMIC WIFE

(Mke Muislamu)

Sehemu Ya 1

Mtunzi... MoonBoy

Simu No, +255714419487 WhatsApp

Inapoanzia Rasmi

NDUGU WASOMAJI WANGU... SIMULIZI HIII... HAITOKUWA NA VIPENGELE VIREFU, KAMA ILIVYO KATIKA SIMULIZI ZINGINE... HII ITAKUWA FUPI FUPI, KUNA SABABU ZILIZOPO NJE YA UWEZO WANGU NA NDIO MAANA IMEKUWA HIVYO..

HAYA TUANZENI RASMI HADITHI, SIMULIZI, STORY... AU VYOVYOTE UTAKAVYO IITA SAWA TU.....

SIMULIZI yetu inaanza Katika Chuo Binafsi ambacho ni chuo kikubwa sana kilichopo jijini Arusha,.. Wanafunzi walikuwa ni wengi sana na leo ni siku yao ya kupata likizo ndogo, yaani ule mwezi wa sita.. Mana kuna vyuo vingine hufunguliwa mwezi wa sita au saba lakini pia vipo vingine hufungwa miezi hio,.. Inategemea na utaratibu wa vyuo binafsi, yaani sio vyuo vya serikali...

Wanafunzi wengi sana walikuja kupokelewa na wazazi wao, walezi wao, au hata marafiki zao..

Nje ya geti la chuo hicho kulisimama magari makubwa makubwa, yaani sio malori, namaanisha magari ya thamani kubwa na mmoja wapo alikuwa ni Jamali aliokuja kumpokea mdogo wake,.. Gari aliokuja nayo ni gari aina ya VOGUE DISCOVERY V807
Gari yenye thamani kubwa sana duniani japo zipo zaidi ya hio lakini hizo ni babu kubwa na ukiona mmiliki wa gari hio usije kumdharau, sio tajiri wa mchezo mchezo,...

"aahhh dogo langu la faida.. Niambie sasa"
Alikuwa ni jamali aliomkumbatia mdogo wake wa kiume aitwae RAHIM, ukipenda unaweza kumwita RAM au RAMY... Ramy huyu ndio yule yule kijana tuliomzoe katika simulizi zilizopita na zinazokuja... Anaitwa Sharbiny Rashidy Kingazi, katika simulizi hii kutumia jina la Rahim,.. Ni mtoto wa kitajiri wacha mchezo, hata hiki chuo anachosoma hapa, ada yake ya mwezi mmoja tu unakula mpaka kufa kwako...

"niaje broo"
"nisalimie weweee, au kisa umepanda hewani tumelingana si ndio"
Aliongea jamali kumtaka rahim amsalimie mana ni kaka yake, na ni kweli wamelingana utafikiri wamezaliwa siku moja, kumbe wamepisha kama miaka 7 hivi au 8, basi rahim aliingiza begi lake la nguo kisha wakaondoka zao...

Walifika nyumbani kwao..... Hilo jumba lao sijui hata ulishawahi kuliona wapi, ni jumba haswa, yaani sio kijumba cha mchezo mchezo, yaani ni familia yenye pesa sana, ila kwa hasara zaidi ni kwamba hawaijui dini, wapo kama wapagani vile... Hua wao wanachojua ni pesa na starehe kwa kwenda mbele,... Geti lenyewe hakina mtu wa kufungua, bali kila mmoja kuna saa maalumu kaivaa hio ni spesho kwa familia hii,.. Na kama huna saa basi Utapiga kengele uje ufunguliwe, lakini kama una saa basi ni mwendo wa kuminya ukiwa humo humo ndani ya gari,..

Mama mzazi wa watoto hao alipomwona mtoto wake wa mwisho alimkimbilia sana na kumhag, (kukumbatiana)... Mama alifurahi sana kumwona mtoto wake,..
"weee ram umekonda mwanangu"
Aliongea mama yake ram au ramy.. Na wala ram hajakonda ila si unajua tu mambo ya akina mama, kupenda sana watoto wao wa kiume hata akinenepa atasema kakonda, ni upendo wa wazazi tu...

Basi waliingia ndani kisha akaandaliwa madiko diko ya maana, lakini ram alikuwa hatulii, moja haikai mbili haikai,....
"mamy, gari yangu ipo wapi pale mbona siioni"
Aliuliza ram, mana familia yote kila mmoja ana gari yake,
"baba yako kasafiri nayo.. Alafu wataka uende wapi na hujala"
Aliongea mama huku akimshika mkono kumzuia asitoke
"mama nimewamisi sana machizi wangu"
"kula kwanza"
"mama nitakula nikirudi"
Ram ni mtoto alielelewa katika mazingira ya kuachiwa sana kiasi cha kwamba ni yeye na starehe ni yeye na pesa... Hata mlango wa msikiti haujui toka kuzaliwa kwake,.. Hajui hata neno la Quran tukufu, yeye anajua starehe tu,..

Ram alitoka na gari ya baba yake, na kuelekea zake mjini kwa marafiki zake,... Aliwachukuwa washkaji zake kisha haoo, mwendo wa kwenda katika club kubwa kubwa zenye starehe za kila aina,.. Vinywaji alivyokuwa akivinunua, ni vinywaji vya gharama kubwa sana, usishangae ram kuacha milioni moja kwa masaa mawili tu... Walikunywa sana na kila mmoja aliondoka na mschana wake anaemjua...

Ram alirudi nyumbani usiku sana kama saa 6 hivi, kaingiza gari viziri na wakati huo alikuwa kalewa sana, mana kanywa vile vinywaji vya gharama kubwa ambavyo havileweshi sana kama utagusa gusa tu, lakini ukinywa nyingi hata kutembea utashindwa,..
"mamaaaa"
Ram aliita huku akishindwa hata kutoka kwenye mlango wa gari kwa kulewa,.. Mama yake alikuwa sebuleni hata kulala hajalala mana Mziwanda wake hajarudi,.. Japo ni tabia ya ram kila anapokuwa nyumbani kwa likizo hizi hua anakuwa mtu wa starehe sana na mama yake keshamzoea kihivyo yani,

"rahim mwanangu, leo umekunywa sana kwanini lakini"
Aliongea mama yake huku akimtoa katika gari
"mamaaa... Gambe (unywaji) la leo tamu mno"
"lakini umezidisha baba"
Mama akaanza kumkokota mtoto wake mpaka ndani,.. Na kwakuwa alikuwa kashiba alipotoka, basi mama hakuhangaika na kupika, japo wafanyakazi wapo wengi sana lakini kwa watoto wake hua anawapikia mwenyewe, eti haamini kama wanaweza kuwapikia watoto wake, hivyo anawapikia mwenyewe.... Ndani ya jengo hilo kuna wafanyakazi wengi sana na kila mtu ana kazi yake... Yaani watoto wa hii nyumba wakiamka tu ni wao na kula na starehe kwa wingi, hawana kazi wanajua hawa... Tena hapo ndani penyewe kuna kaunta utafikiri baa,.. Kama mtu una hamu ya wine basi unaingia kaunta na kujisevia... Na hapo kaunta hakuna Serengeti, hakuna Eagle, hakuna Safari, hakuna Kilimanjaro, Hakuna Tusker,.. Yaani hakuna kinywaji cha elfu 3 au 5...yaani hapo ni mwendo wa wine, wiski yaani vile vinywaji vinavyo anzia na bei ya shilingi laki moja na kuendelea

**************************************

Ikiwa ni siku ya ujumaa, iliotukuka umma ulishangaa kumwona shekhe fulani leo akiingia msikitini,.. Kila mtu alishangaa sana kwa kumwona shekhe aliovalia ki Nigeria,.. Wapo waliofurahia ujio wake lakini hakuna aliochukia ujio wake na wapo walioshangazwa na ujio wake...
"as Salaam Aleykum"
Aliwasalimia watu wote waliopo msikitini, tena alifika muda muafaka, katika swala ya Ijumaa mchana kweupee
"aahhh shekh rahim"
Aliitwa na imamu wa msikiti huo kisha akapewa nafasi ya kuswalisha ijumaa ya leo...
"naam mzee wangu"
"nina furaha sana kuwa na kijana mtiifu kama wewe.... Leo sijiskii vizuri hivyo nipo nyuma yako leo"
Aliongea imamu huyo huku rahim anajua maana ya kukaa nyuma yako, yaani kampa nafasi ya kuswalisha Al Ijumaa kareem,.. Huezi amini alikuwa ni rahim ndie mswalishaji wa Ijumaa ya leo,... Sasa hapa inakuwaje, mbona rahim tunaemjua sisi ni mtu wa starehe tu na hajui cha msikitini wala nini... Sasa mbona hapa anaonekana kuswalisha tena anaswalisha umati wa watu wasiopungua 300,... Sasa huyu ni rahim yupi na yule sharobaro mhuni ni rahim yupi?
 
THE ISLAMIC WIFE

(Mke Muislamu)

Sehemu Ya 2

Mtunzi... MoonBoy

Simu No, +255714419487 WhatsApp

Ilipoishia Jana →→↓↓

Ikiwa ni siku ya ujumaa, iliotukuka umma ulishangaa kumwona shekhe fulani leo akiingia msikitini,.. Kila mtu alishangaa sana kwa kumwona shekhe aliovalia ki Nigeria,.. Wapo waliofurahia ujio wake lakini hakuna aliochukia ujio wake na wapo walioshangazwa na ujio wake...
"as Salaam Aleykum"
Aliwasalimia watu wote waliopo msikitini, tena alifika muda muafaka, katika swala ya Ijumaa mchana kweupee
"aahhh shekh rahim"
Aliitwa na imamu wa msikiti huo kisha akapewa nafasi ya kuswalisha ijumaa ya leo...
"naam mzee wangu"
"nina furaha sana kuwa na kijana mtiifu kama wewe.... Leo sijiskii vizuri hivyo nipo nyuma yako leo"
Aliongea imamu huyo huku rahim anajua maana ya kukaa nyuma yako, yaani kampa nafasi ya kuswalisha Al Ijumaa kareem,.. Huezi amini alikuwa ni rahim ndie mswalishaji wa Ijumaa ya leo,... Sasa hapa inakuwaje, mbona rahim tunaemjua sisi ni mtu wa starehe tu na hajui cha msikitini wala nini... Sasa mbona hapa anaonekana kuswalisha tena anaswalisha umati wa watu wasiopungua 300,... Sasa huyu ni rahim yupi na yule sharobaro mhuni ni rahim yupi?

ENDELEA........

Kweli ram alikuwa ni kijana aliojawa na imani ya dini haswa,.. Kwani hata alipokuwa aki kim swala, ilikuwa inapendeza sana, kijana aliovalia kanzu yenye rangi bluu, kibarakashee chenye rangi ya bluu... Alipendeza sana,... Kama kawaida dakika chache tu mnamaliza swala ya Ijumaa,.. Baada ya swala, rahim alipongezwa sana mana ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuswalisha katika msikiti mkubwa sana uliopo mjini kati ila hatujui ni mji gani,.. Rahim alitoa mikono ya heshima kwa maostadhi wakubwa wakubwa huku akipongezwa sana, na wakati huo alikuwa akitoka nje kuwahi kitu fulani.. Lakini ile anafika tu nje, aliona mschana mweupe pee, kama malaika, mschana huyo alikuwa kapiga uchungi mzuri sana, nae alikuwa akitoka msikitini katika upande wa wanawake...
*************************************

"uuuuuuwiiiiiiiiiii... Mamaaaa"
Rahim alizinduka usingizini usiku wa manane, huku akiwa anahema juu juu, mama yake alikuja chumbani kwa rahim huku akiita
"rahim, mwanangu una nini"
Aliuliza mama yake
"mama... Huezi amini nimeota nipo msikitini, tena mbaya zaidi nilikuwa naswalisha watu zaidi ya 300 mama"
Aliongea hayo ram huku akisema MBAYA ZAIDI yaani badala ya kufurahi yeye anasema mbaya zaidi
"mwanangu, watakuwa ni wachawi hao.... Wewe huezi ota mambo kama hayo... Huo ni uchawi tu.. Pole sana mwanangu"
Yaani nyumba ya kishetani ni ya kishetani tu,... Yaani badala waone ni jambo jema eti wanasema ni uchawi huo...

Basi siku hio iliisha lakini ram bado anaiwazia ile ndoto ya kuingia ndani ya msikiti tena ameswalisha umati wa watu,... Lakini sasa kumbe yeye hawazii hilo, yeye anawaza mwisho wa ile ndoto kuna mwanamke kamuona.... Hicho ndicho anachokiwaza rahim....
"we vipi, mbona umetulia huku uwani peke yako"
Alikuwa ni kaka yake jamali, ndie alie muuliza
"broo, we acha tu.. Yaani kirudi shule jana tu... Wachawi wameshaanza kinifuata..."
"wachawi??...wachawi gani tena... Au ni yule mama nini?... Mi nakuambia yule mama balozi ni mchawi sana yule.. Alafu naskiaga anataka watoto wa mwisho mwisho tu"
Aliongea jamali huku akitaka hata kuamka na kumfuata huyo mama
"mi nadhani sio huyo mama"
"ndie tuuu"
"nimeota nipo ndani ya msikiti"
Jamali kusikia hivyo aliruka mpaka akadondoka hini
"unasemaje wewe"
"we acha tu broo... Tena mbaya zaidi nimeswalisha watu.. Nimevaa kanzu kubwaa"
"weweeeeeee.... Ahh Kudadeki kweli huo uchawi babu kubwa.. Yaani wewe uingie msikitini wewe... Hakiyamungu vile lazima siku hio mtu afe.. Au huo msikiti lazima uvunjike"
Aliongea jamali huku akicheza cheza kwa furaha ya ndoto ya rahim,...
Mara ghafla mama yao katokea pale walipo
"nyie kuna nini hapa mbona makelele tu"
Aliongea mama yao huku jamali akimjibu kuwa
"mama... Huyu balozi sasa ataniulia mdogo wangu.... Yaani mpaka kampeleka msikitini kweli"
Aliongea jamali huku kijasho Chembamba kikimtoka, kwa maneno ya kuikashifu dini yao,.....
"mi naona aende kwa bibi yake... Mana huyu balozi ataniulia mwanangu"
Mama nae aliingiza hofu kuhusu swala hilo,...
"ndio mama, kama vipi rahim aende akale likizo kwa bibi... Mana huyu balozi mimi nitamuua"
Aliongea jamali lakini ram yeye yupo kimya wala hana hata neno la kuongea, yeye anawaza tu yule mwanamke aliemuona wakati akitoka msikitini,...
"rahim mwanangu,... Si utaenda kwa bibi yako"
"mmmhhh huko kwa bibi kwani kuna uzuri gani"
"yaani ram mwanangu.. Bibi yako akuloge"
"sina maana hio... Wewe unajua tanga kulivyo, kumejaa wachawiii"
"sawa, lakini bibi yako ni mwenyeji wa kule, lazima watakuogopa... Afu kule kuna upepo mzuri.. Utainjoi."
Aliongea mama huyo huku ram akikubali kishingo upande,..
"kwanza kule ndio kwenu, nani anaweza kuloga mtu wa kijiji hicho hicho"
Mama rahim alizidi kumweleza mtoto wake juu ya safari hio
"sasa nitaenda na nini"
"si utachukuwa gari la baba yako hilo"
"aahhhh kila saa kuingia sheli, silipendi hilo gari mama"
"ataendesha kaka yako jamali"
"ina maana nakwenda na huyu bwege"
"aahhhh sasa mbona wamuita kaka yako bwege"
"huyu ni bwege huyu.. Hata kutongoza hajuagi"
Mama kuskia hivyo aliondoka zake mana ni vijimambo vya watoto wake hivyo haoni haja ya kuvisikiliza...

Baada ya siku kama mbili hivi rahim alipanga kila kitu hake, na jamali pia alifanya hivyo,.. Walipakia mabegi yao kuelekea mjini tanga,..
Lakini walipokua wakitoka nje ya geti, walikutana na gari ya kifahari hapo nje ya geti lao,... Alishuka mschana mrembo sana tena ni mtoto wa tajiri kama yeye alivyo,.. Na anamjua vizuri
"rahim Mambozako mpenzi wangu"
Alisalimia dada huyo lakini ram hakuwa na taimu nae
"poa"
"jamani rahim, toka urudi chuo, mpaka leo hujawahi hata kunipigia simu kwanini lakini"
Aliongea mdada huyo huku, akifikicha vidole vyake....
"oya ram... Si unasemeshwa huko"
Aliongea Jimmy huku akimtaka kutoa gari....
"aahhh achana nalo"
"heeeew rahim, yaani unaniambia mimi hivyo kweli.... Rahim mpenzi wangu"
"ebu toa gari tupite"
Lakini mdada huyo alionekana kuvaa saa apeho kwa ajili ya geti, hivyo ni mtu wa karibu wa familia hii,...
Ghafla mama katokea pale getini huku akisema
"ina maana bado hamjaondoka tu"
Aliongea mama huyo,....
"waaoooo mama mkwe.. Shkamoo"
"Marahaba mwanangu... Shakira hujambo"
"sijambo mama... Nilikuwa naongea na ram"
Aliongea Shakira kumaanisha ya kwamba, anamjali sana ram...
"okeee... Ila utammisi kweli ndani ya wiki hizi"
"kwanini mama nitammisi"
"hapo alipo anakwenda kwa bibi yake tanga"
"Whaaaat???.... Ram.. Yaani unaondoka hata kuniaga huniagi kwanini"
"ram alifunga kioo kwa dharau"
"ram jamani..... Mama mi lazima niende na ram... Siwezi kubaki mwenyewe hapa mjini"
Ohoooooo Shakira nae Anataka kwenda na mbaya zaidi ram hampendi dada huyo, sema kwa shinikizo la wazazi kutaka kuoana kwasababu wote ni matajiri, na hataki mwanamke kapuku..
"shakira mwanangu... Muache atarudi tu"
"hapana mama... Lazima nikaishi nae huko huko"
Ram kafungua kioo huku akisema

Je?.... Ram atasema nini kwa shakira?.... USIKOSE
 
THE ISLAMIC WIFE

(Mke Muislamu)

Sehemu Ya 3

Mtunzi... MoonBoy

Simu No, +255714419487 WhatsApp

Ilipoishia Jana →→↓↓

"ebu toa gari tupite"
Lakini mdada huyo alionekana kuvaa saa apeho kwa ajili ya geti, hivyo ni mtu wa karibu wa familia hii,...
Ghafla mama katokea pale getini huku akisema
"ina maana bado hamjaondoka tu"
Aliongea mama huyo,....
"waaoooo mama mkwe.. Shkamoo"
"Marahaba mwanangu... Shakira hujambo"
"sijambo mama... Nilikuwa naongea na ram"
Aliongea Shakira kumaanisha ya kwamba, anamjali sana ram...
"okeee... Ila utammisi kweli ndani ya wiki hizi"
"kwanini mama nitammisi"
"hapo alipo anakwenda kwa bibi yake tanga"
"Whaaaat???.... Ram.. Yaani unaondoka hata kuniaga huniagi kwanini"
"ram alifunga kioo kwa dharau"
"ram jamani..... Mama mi lazima niende na ram... Siwezi kubaki mwenyewe hapa mjini"
Ohoooooo Shakira nae Anataka kwenda na mbaya zaidi ram hampendi dada huyo, sema kwa shinikizo la wazazi kutaka kuoana kwasababu wote ni matajiri, na hataki mwanamke kapuku..
"shakira mwanangu... Muache atarudi tu"
"hapana mama... Lazima nikaishi nae huko huko"
Ram kafungua kioo huku akisema

ENDELEA.......

JAMANI NDUGU WASOMAJI WANGU, KAMA KINA MAHALI UTAKUTA NENO ( SAM ) BASI UJUE LIMEKOSEWA TU, BALI NI ( RAM ).. KUNA SIMULIZI NYINGINE NAIANDIKA AMBAYO SHEBY AMETUMIA JINA LA SAM,.. HIVYO SAM NA RAM VINAENDANA,... KWAHIO UKIKUTA NENO SAM, HEBU LIFANYE KAMA VILE RAM... MANA LITAKUWA LIMEKOSEWA... SAM NI JINA LA KWENYE SIMULIZI NYINGINE SIO HIII... HII ANAKWENDA KWA JINA LA RAM.. NA SIO SAM

Unajua kuna itikadi za kifamilia zinakuwa kama zinataka kuendana,.. Mtoto wa masikini anapenda sana kuolewa na mtoto wa tajiri, lakini wazazi wa watoto wa kitajiri hawataki mtoto wao aoe au aolewe na mtoto wa kimaskini,.. Familia ya kitajiri hua inataka inataka muunganiko wa matajiri wenzake, yaani hataki masikini, hivyo Shakira nae ni mtoto wa mfanyabiashara mmoja maarufu sana jijini Arusha, hivyo kwao nae ni tajiri na hata wazazi wa rahim pia wametazamia mwanae amuoe Shakira, lakini kwakuwa mapenzi ni sawa na ndege anatua mti aupendae,... Kiukweli rahim hana mapenzi ya kweli kwa Shakira na licha ya hivyo, pia hajawahi hata kumuomba penzi lake, hivyo hana hisia nae kwasababu ni mschana wa kuchaguliwa tu, hajampenda yeye kama yeye,... Sasa shakira alipokuwa anang'ang'ania kwenda na rahim tanga,... Rahim akafungua kioo huku akisema
"nisikilize kwa makini we shakira.... Usije ukahisi mimi nakupenda, kaa ukijua sina hisia na wewe hata kidogo... Waambie wanaotaka nikuoe wakuoe wenyewe, mimi sina hisia na wewe... Achia mlango wa gari yangu na uondoke... Afu mazoea na wewe sitaki"
Mama yake rahim kasikia kila kitu alichokisema mtoto wake rahim
"we ram wewe... Unasemaje?.... Yaani unasubutu kuongea ujinga namna hio mbele yangu.... Shakira njoo mama, tutayamaliza tu"
Wakati huo shakira analia tu hana la kisema zaidi ya kulalamika tu
Rahim alipoona mama anazidi kutangaza Injili aliondoa gari kwa spidi kali,... Ndio safari ya tanga imeanza hio, kawaacha watu wengine wakiwa katika huzuni...
Mama yake ram akiwa katika hali ya kumbembeleza shakira aliopewa vigongo vyake muda sio mrefu,...

"lakini rahim, hujafanya fea pale,.. Mwanamke hua haambiwi ukweli"
Aliongea jamali ambae ni kaka yake na rahim,...
"amna lolote, mwanamke ukimficha ficha ndio anazidi kukusumbua,.. Mpe makavu live atuloe mbele uko"
"kiukweli imeniuma sana... Afu mtoto mwenyewe mkali vile unampa maneno hayo kweli"
"hata mbwa ni mkali weweee,... Sio yeye tu"
"ahhh... We kweli umelaaniwa"
"acha swaga zako basi broo"
Basi walikuwa wakiongea huku safari ikiendelea kwenda,... Walipitia supermarket na kununua zawadi nyingi sana kwa ajili ya bibi na babu kule kijijini,... Rahim alikuwa anafurahi sana mana hajawahi kwenda kula likizo tanga kwao, na leo ni kama mara ya pili au tatu, lakini mara zote hizo hakwenda kula likizo bali alikwenda kwenye misiba misiba tu...
"bibi anapenda chocolate utafiki katoto cha kike"
Aliongea ram huku akinunua chocolate za kutosha
"yule ni binti wa zamani wewee
Basi walikusanya bidhaa nyingi sana katika Mall mpya iliopo jijini Arusha iitwayo AIM MALL... Baada ya kujaza baadhi ya vitu katika VOGUE DISCOVERY V 807 ya baba yao,.. Safari ilianza rasmi ya kuelekea tanga, kama unavyojua umbali wa Arusha to Tanga ulivyo,... Iliwachukuwa masaa kadhaa huku wakibadilishana kuendesha,.. Walikuwa wawili tu katika gari hio,..

Baada ya masaa kadhaa walifika tanga mjini,.. Sasa wanashika njia ya kwenda katika mitaa yao,.. Ambako ndiko jengo lao la kitajiri lilipojengwa,
Mitaani watu ni kushangaa gari ilivyo new model, gari ya bei ghali zaidi duniani,.. Afu wanaendesha watoto wadogo tu,.. Bibi alipoona gari hio alijua ni mtoto wake mzee rashidi, yaani baba yao na akina rahim, lakini sivyo,.. Kumbe ni mijambazi yake ndio imevamia gari,... Sasa kama unavyojua maisha ya tanga, baiskeli nyingi sana, sasa katika pita pita wakati huo ram alikuwa anamwangalia bibi yake pale nje, mara ghafla kuna mtoto kapita mbele ya gari akiwa na baiskeli... Watu walishika vichwa tu... Ram alishuka haraka haraka na kumkomba yule mtoto aliokuwa akitokwa na damu nyingi sana kichwani,.. Ram alimpakia yule mtoto kisha wakamkimbiza hospitali..
"we ulikuwa unaangalia wapi... Ona sasa mtoto wa watu akifa je"
Alikuwa ni jamali aliokuwa akimfokea ram ambae ni mdogo wake,...
"broo huu sio wakati wa kulaumiana.. Mcheki dogo uyo asizime"
"aya yote umeyata wewe, ina mana humjui bibi mpaka uanze kumwangalia anavyokuja"
"tulia basi broo mbona injili nyingi ivo"
"sio ivo, tatizo lako ni msomi lakini hutaki kutumia akili zako kwenye vitu vya hatari kama hivi"
Jamali alikasirika sana kwa kitendo kilichotokea hapo...
Kwanza alipelekwa katika hospitali ya karibu na wao,.. Ili kupata huduma ya kwanza,.. Rahim kichwa chake kimechanganyikana yaani akileta utani anaweza kugonga mwingine tena mana alikuwa spidi sana ili kuweza kumwahisha kijana huyo..

Walipofika hospitali mara moja machela ililetwa, mtoto huyo akaingizwa katika chumba cha wagonjwa mahututi,.. Mana damu nyingi sana zilimtoka mtoto huyo na hata kutikisika alikuwa hatikisiki,... Akina rahim na kaka yake Jamali wakuwa katika mlango wa wodi hio huku wakiuzunguka kila mara,... Yaani hata kukaa hakukaliki,... Kuna viti lakini vilikuwa kama vina moto vile,... Baada ya kama nusu saa hivi mara dokta katoka huku akifungua kile kitambaa alichofunga puani,...
"dokta hali ya mgonjwa vipi"
Aliuliza rahim huku akiwa na wasiwasi juu ya mgonjwa wake,.. Kula likizo kumegeuka kula mateso ya moyo, mana kwa utajiri wao wanaweza kulizimisha swala hilo kama mtoto huyo atakufa... Lakini sasa roho ya mtu haiwezi kurudi... Wakati huo huo ndugu, wazazi ndio wanaingia... Ram ndio presha inazidi kumjia yani...
"dokta... Mgonjwa wangu anaendeleaje lakini"
Ram alirudia tena lakini dokta alikuwa mpole sana kwa hali isiojulikana...
"samahani sana kijana... Kiukweli tumejitahidi sana kadri ya uwezo wetu,... Lakini tumeshindwa kumtibu mgonjwa wako"
Ram machozi yalianza kumtoka huku akisema kuwa
"una maana gani dokta,... Eeehh mungu wangu siamini kama nimeua mtoto asiekuwa na hatia"
Sasa wale wazazi na ndugu waliokuja walikuwa hawajui kama hawa vijana ndio waliomgonga mtoto wao, sasa waliposikia tu ram akisema haamini kama kaua mtoto asiekuwa na hatia... Mama wa mtoto huyo nae kadondoka chini.... Machela nyingine ikaletwa kwa ajili ya mama....

Je? Nini kitaendelea??... Mtoto kafariki... Na vipi kuhusu mama aliedondoka nae???... USIKOSE
 
THE ISLAMIC WIFE

(Mke Muislamu)

Sehemu Ya 4

Mtunzi... MoonBoy

Simu No, +255714419487 WhatsApp

Ilipoishia Jana →→↓↓

Baada ya kama nusu saa hivi mara dokta katoka huku akifungua kile kitambaa alichofunga puani,...
"dokta hali ya mgonjwa vipi"
Aliuliza rahim huku akiwa na wasiwasi juu ya mgonjwa wake,.. Kula likizo kumegeuka kula mateso ya moyo, mana kwa utajiri wao wanaweza kulizimisha swala hilo kama mtoto huyo atakufa... Lakini sasa roho ya mtu haiwezi kurudi... Wakati huo huo ndugu, wazazi ndio wanaingia... Ram ndio presha inazidi kumjia yani...
"dokta... Mgonjwa wangu anaendeleaje lakini"
Ram alirudia tena lakini dokta alikuwa mpole sana kwa hali isiojulikana...
"samahani sana kijana... Kiukweli tumejitahidi sana kadri ya uwezo wetu,... Lakini tumeshindwa kumtibu mgonjwa wako"
Ram machozi yalianza kumtoka huku akisema kuwa
"una maana gani dokta,... Eeehh mungu wangu siamini kama nimeua mtoto asiekuwa na hatia"
Sasa wale wazazi na ndugu waliokuja walikuwa hawajui kama hawa vijana ndio waliomgonga mtoto wao, sasa waliposikia tu ram akisema haamini kama kaua mtoto asiekuwa na hatia... Mama wa mtoto huyo nae kadondoka chini.... Machela nyingine ikaletwa kwa ajili ya mama....

SONGA NAYO......

Rahim ni kijana mwenye roho ya huruma japo katawaliwa na mambo ya kidunia,.. Starehe ndio imemharibu rahim au familia yote wanaishi kistare tu, hawajui kama kuna mungu hawajui kama kuna kumswalia mtume Muhammad na Mwenyezi Mungu kwa ujumla, wao hawalijui hilo, dunia imewatawala kutokana na utajiri wao,... Rahim kila akirudi shule katika likizo ndogo yaani yeye hushinda kwenye maclub makubwa makubwa,.. Na wazazi wanalijua hilo, mana kuna siku familia yote inatoka auti, na hio ndio sababu mpaka watoto sasa hivi wanakuwa ni wachafu wa kupindukia, na yote haya yanasababishwa na wazazi wetu, katika hizi familia zenye unafuu wa maisha.... Wazazi tuwalee watoto wetu vizuri hata kama una uwezo kiasi gani, mlee mwanao vizuri

Sasa rahim akiwa hapo hospitali ndogo ndogo tu ya mtu binafsi,.. Dokta alitoka huku akiwa na huzuni kwa kiasi fulani na kumwambia rahim kuwa, wameshindwa kumtibu mtoto huyo..

"una maana gani dokta,... Eeehh mungu wangu siamini kama nimeua mtoto asiekuwa na hatia"
Sasa wale wazazi na ndugu waliokuja walikuwa hawajui kama hawa vijana ndio waliomgonga mtoto wao, sasa waliposikia tu ram akisema haamini kama kaua mtoto asiekuwa na hatia... Mama wa mtoto huyo nae kadondoka chini.... Machela nyingine ikaletwa kwa ajili ya mama

"dokta... Ina maana mumeshindwa kumponya huyo mtoto"
Aliongea rahim huku akilia haswa, mana hakutegemea kuua na pia hajawahi kuua,..
"lakini kijana.. Huyu mtoto bado hajafa.. Ni mzima tu"
"we dokta una akili wewe... Sasa mbona umesema mumeshindwa, una maana gani"
Wakati huo akiongea hayo kwa pembeni kuna jamaa mmoja ambae ni ostadhi,.. Na huyu jamaa ni kaka wa yule mtoto,.. Na yule mama aliozimia ni mama wa yule mtoto, halafu kuna kabinti kengine keupe pee ambako kwa sasa kapo na mama yake kule ndani baada ya kuzimia, nae huyo binti ni dada yake na huyo mtoto,..
"hapana kijana... Nilikuwa na maana ya kwamba, hospitali yetu imeshindwa kumtibu, hivyo naomba muende hospitali kuu ya mkoa wa tanga"
Rahim kusikia hivyo alitamani hata kuruka na huyo mtoto mpaka kwenye hio hospitali,... Sasa kabla hajauliza ni hospitali gani, yule binti katokea ili kumuita dokta,.. Wakati huo yule binti alikuwa analia ila machozi yake huezi kuyaona kwasababu kavaa kininja, mana ni mtoto wa Kiislamu,...
"hio hospitali inaitwa na ipo maeneo gani"
Rahim aliuliza huku binti akitaka kumuita dokta
"huyu mtoto mpeleke Bombo Hospital, kule atapata matibabu mazuri tu"
"Bombo Hospital ipo wapi hio hospitali"
Sasa kabla dokta hajajibu, yule binti kamshika rahim mkono huku akisema
"nitakupeleka kaka yangu, naomba mdogo wngu apone tu"
Sasa kile kitendo cha binti yule kumshika rahim... Rahim alisisimkwa na mwili wake kama vile kapigwa shoti,... Sasa ram kuona vile alimkwapua yule binti mkono ili asiushike tena
"niachie bwana... Na usinishike tena, una hadhi gani ya kunishika wewe"
Lakini sasa kumbe sio rahim peke yake aliosisimkwa, kumbe hata huyu binti pia alisisimkwa na mwili wake baada ya kumshika rahim... Binti alibaki kulia tu muda wote, mana rahim aliongea maneno machafu sana katika kinywa chake, na hapo hajitambui kuwa yeye ni nani, bali anajijua tu kuwa ana pesa nyingi za baba yake,.. Sasa yule ostadhi aliokuwa nyuma ya rahim, yeye akasema
"astah khafirullah"
Baada ya yale maneno ya rahim kumwambia mdogo wake kuwa hana hadhi ya kumshika, mana wao ni matajiri na hawa ni masikini tena masikini haswaa,...
"we nawe vipi huku nyuma yangu, au unaniloga nini na wewe"
Aliongea rahim baada ya kusikia ile Astah Khafirulah...
"Samahani ndugu yangu... Naomba tumtibu ndugu kipenzi... Samahani kama nimekuudhi ndugu yangu"
Yule ostadhi aliomba tu msamaha juu ya tukio hilo,.. Rahim ana roho ya huruma kidogo sana, lakini ana roho ya dharau mno,...
"Skia dokta, naomba unipeleke katika hio hospitali"
"hapana mimi siwezi kutoka hapa, mana ndio mkuu wa matibabu hapa"
"sasa nitapelekwa na nani"
"lakini kijana... Hawa ni ndugu wa huyo mtoto, kwanini wasikupeleke"
"wachawi hawa we huwaoni"
Yule ostadhi akaruadia tena yale maneno
"astah Khafirulah"
"we vipi jamaa... Tueshmiane bwana"
Rahim aliingia ndani na kumchukuw yule mtoto kisha akamueka pale ndani ya gari yao, wakati huo buti ya gari hio imejaa vitu vya kula kula tu.. Ndugu wa mtu huyo hawakupata hata nafasi ya kupanda katika gari hio kwasababu wanaonekana ni wachawi,... Rahim alichukuwa mtu mwingine ili aende nae huko hospitali

Baada ya nusu saa gari ilifika katika hospitali kuu ya mkoa wa Tanga, iitwayo BOMBO HOSPITAL, mtoto alipokelewa vizuri kisha akapatiwa matibabu mazuri tu,... Na wakati huo mama, kaka, dada, baba, wote walishafika hospitali hapo kwa ajili ya mtoto wao,.. Lakini sasa likaja swala la yule mtoto kuongezewa damu, japo hali yake sio mbaya kiafya,.. Lakini damu inahitajika
Ndugu walipimwa lakini nao damu zao zilikuwa ni chache mwilini, mana mtu anaetakiwa kutoa damu anatakiwa awe na damu nyingi, sasa kama ni chache afu ukatoa atajikuta nae anaingia kwenye matatizo,.. Damu iliomwagika ilikuwa ni nyingi sana, hivyo kunahitajika damu nyingi mno ili mtoto awe imara kama zamani,...
"aaahhh jamani... Tumewapima wote hamuda damu za kutosha... Lakini damu ya kuuza ipo"
Aliongea dokta huyo huku baba wa mtoto huyo akisema kuwa
"ni kiasi gani hio damu dokta"
Aliuliza baba mtu kisha dokta akajibu
"lita moja inauzwa shilingi milioni 3"
"mtume roho yangu... Yaani damu inauzwa kama nyumba.... Mungu wangu mwenetu atapona kweli"
Lakini kama nilivyokwambia kuwa rahim ana roho ya utu, ila kajawa na dharau na kebehi, kwa ajili ya pesa zao....
"dokta, naomba unipime mimi, kama itakuwa sawa utoe hata kama ni lita nne"
Aliongea rahim yule yule mwenye kiburi cha pesa, mpaka anaikashifu dini yake kwasababu ya pesa, na yote haya ni malezi ya wazazi.. Basi dokta alimchukua ram mpaka ndani na kuanza kumfanyia vipimo...
"jamani huyu kijana ana imani ya kuseidia watu"
Aliongea baba mtu, huku mama akidakia kuwa
"ni kweli.. Unajua mtu kujitolea damu sio kitu rahisi baba zena... Na hata kama kamgonga yeye, lakini haikuwa na lazima ya kutoa damu.. Lakini ona katoa.. Kiukweli ana malezi huyu mtoto"
Mama na baba hawakuweza kushuhudia dharau za rahim lakini walio ona ni kaka na dada,... baba na mama hawajui
"mama... Achana kabisa na huyo kijana,.. Dharau imelala hapo wacha kabisa... Zena alimshika tu mkono.. Huezi amini maneni alioyatoa huyu kijana.. Yanakera mno mama, nilitamani hata kulia"
Sasa huku chini ya miguu, zena alikuwa akimkanyaga kaka yake kuwa asiendelee kusema,... Mara ghafla rahim katoka na dokta,..
Familia ikanyanyuka ili kujua kinachoendelea,...
"dokta, mtoto wetu kapata tiba"
Mama aliuliza, huku baba mtu akitoa shukrani kwa kijana huyo japo hawajui kama wamefanikiwa
"aahhhh.... Mtoto wenu atapata damu, na tumefanya vipimo vyote kwa huyu kijana, na damu yake inaendana vizuri tu... Ila sasa"
Familia kusikia neno, ila sasa walianza kupatwa na wasiwasi juu ya kijana huyo...

Je?... ILA SASA ina maana gani au anataka kusema nini huyo dokta??

ITAENDELEA...
 
THE ISLAMIC WIFE

(Mke Muislamu)

Sehemu Ya 5

Mtunzi... MoonBoy

Simu No, +255714419487 WhatsApp

Ilipoishia Jana →→↓↓

"ni kweli.. Unajua mtu kujitolea damu sio kitu rahisi baba zena... Na hata kama kamgonga yeye, lakini haikuwa na lazima ya kutoa damu.. Lakini ona katoa.. Kiukweli ana malezi huyu mtoto"
Mama na baba hawakuweza kushuhudia dharau za rahim lakini walio ona ni kaka na dada,... baba na mama hawajui
"mama... Achana kabisa na huyo kijana,.. Dharau imelala hapo wacha kabisa... Zena alimshika tu mkono.. Huezi amini maneni alioyatoa huyu kijana.. Yanakera mno mama, nilitamani hata kulia"
Sasa huku chini ya miguu, zena alikuwa akimkanyaga kaka yake kuwa asiendelee kusema,... Mara ghafla rahim katoka na dokta,..
Familia ikanyanyuka ili kujua kinachoendelea,...
"dokta, mtoto wetu kapata tiba"
Mama aliuliza, huku baba mtu akitoa shukrani kwa kijana huyo japo hawajui kama wamefanikiwa
"aahhhh.... Mtoto wenu atapata damu, na tumefanya vipimo vyote kwa huyu kijana, na damu yake inaendana vizuri tu... Ila sasa"
Familia kusikia neno, ila sasa walianza kupatwa na wasiwasi juu ya kijana huyo...

ENDELEA..........

Akina jamali na mdogo wake ambae ni rahim, watoto wa mzee rashidi, tajiri mkubwa sana jijini arusha,... Jamali alishamaliza chuo na sasa anafanya kazi kwenye kampuni ya baba yake, na rahim yeye bado yupo chuo mwaka wa mwisho huu, na sasa yupo likizi mkoani tanga ambako amezaliwa baba yake,... Lakini sasa akina jamali walipotoka arusha waliingia AIM MALL (Supermarket) wakanunua vitu vingi sana mpaka vinywaji vile vya bei ghali,... Kama vile waini, wiski, dorodo wisk, Angel,... Na kila kitu,.. Na walikuwa wakinywa katika gari, na ndio maana ajali ilitokea kwasababu walikunywa wakiwa ndani ya gari..

Sasa baada ya ndugu wazazi kupimwa, na kugundulika damu za wengine ni chache, na wengine ni damu za kizee, hususan baba na mama wana umri mkubwa hivyo huezi kutoa damu kumpa mtoto mdogo, mana ni damu za kizee hizo,

Baada ya wao kushindikana kutoa damu, rahim alijitolea kutoa damu, aliingia ndani ya wodi na kupimwa vizuri,... Dokta alitoka pamoja na rahim, wazazi wote na ndugu wakasimama ili kujua hali ya kupata damu kwa ajili ya mtoto wao,
"aahhhh.... Mtoto wenu atapata damu, na tumefanya vipimo vyote kwa huyu kijana, na damu yake inaendana vizuri tu... Ila sasa"
Familia kusikia neno, ila sasa walianza kupatwa na wasiwasi juu ya kijana huyo...
"dokta, una maana gani kusema Ila sasa"
Aliuliza mama yake zena, kisha dokta akamjibu kuwa
"huyu kijana, ana damu nyingi sana.. Lakini sasa, Damu yake ina kemikali za pombe,.. Amekunywa pombe muda sio mrefu.. Hivyo anapaswa kukaa masaa 48 mpaka kemikali hio iishe mwilini mwake ndipo tutoe damu"
Zena aliposkia rahim kanywa pombe, alitamani hata hio damu isitoke tena, mana anahisi mdogo wake ataambukizwa damu ya pombe....
"lakini dokta, sasa mtoto wangu itakuwaje, mana ni masaa mengi mno"
"aahhh mtoto hana tatizo, na ataweza kufikisha siku hizo... Lakini kikubwa zaidi ni huyu kijana asinywe pombe ndani ya siku hizo"
Jamali kuskia maneno hayo alishtuka sana, mana anamjua rahim hajawahi kupitisha hata siku moja bila kunywa hata grasi moja.. Mana hata kule shule, kuna ka Supermarket ka shule kwa ajili ya wanafunzi, na rahim alikuwa akiagiza wine kwa siri, hivyo hata kule ahule alikuwa anakunywa, na zilikuwa zikija kwa njia ya kuingiza bidhaa za Supermarket kwa ajili ya wanafunzi... Mana ni shule za Boding,...
"sasa dokta nadhani wataka kuniulia mdogo wangu"
Aliongea jamali huku akitaka kumchukuwa waondoke zao...
"broo subiri... Mimi nataka nihakikishe huyu mtoto anapona,.. Nipo tayari kuvumilia hayo masaa"
Aliongea rahim huku akiwafuata wazazi wa mtoto huyo...
"Samahanini sana wazazi wa huyu kijana... Mimi ndie niliemgonga mtoto wenu, na nitahakikisha mpaka anapona,. Kwahio nyinyi kazi yenu ni kuja kumjulia hali tu... Lakini kila kitu kuhusu matibabu nitalipia mimi"
Aliongea rahim kisha wakaingia kwenye gari,... Wazazi na ndugu waliingia katika wodi ili kumwangalia mtoto wao,.... Rahim alishalipa kila kitu hapo hospitali hivyo hakudaiwi kitu chochote kile...

Safari ya kwenda kwa bibi ndio imeanza upya, mana hapo walikuwa Bombo Hospital....
Ndani ya gari kumejaa vinywaji vile vya bei ghali mno, yaani ni vile vinywaji vya kitajiri, Rahim alikuwa akiviangalia tu huku akivitamani,... Bibi yao alikuwa nje ya nyumba akiwasubiria mana katika ile ajali bibi aliona hivyo wasiwasi ukamjia kuhusu wajukuu zake,... Jumba lao la hapo kijijini ni balaa,...
"nyie mu wazima jamani"
Bibi aliwauliza wajukuu zake kuwa wapo salama, wakati huo kuna mfanyakazi wa kike aliokuwa akiingiza vitu ndani pamoja na mapombe yale ya kitajiri, sio viserengeti vyenu vya elfu 2,... Mfanyakazi wa ndani alikuwa ni mschana mzuri sana lakini rahim hakuwa akiliona hilo, ni kumpelekesha kwa kwenda mbele,.. Rahim kitu cha kwanza alikimbilia kulala, ili kuweza kupumzisha akili yake, wakati huo jamali yupo sebuleni akitupia grass mbili tatu huku akitazama mpira katika tv..
"wewe mshenzi, humu sio baa"
Aliongea bibi huku jamali akicheka na kumjibu kuwa
"we bibi Weeeee, pesa ipo, kila kitu kipo, kwanini tusifurahi... Hebu njoo upate mbili tatu"
Jamali alikuwa akimtania bibi yake
"we, hivi huyo mtoto wa watu ni mzima?"
"bibi... Mtoto yupo salama, sema tabu kwa mjukuu wako"
"kafanya nini tena"
"kajitolea kutoa damu kwa yule mtoto, lakini alivyopimwa amegundulika kuwa ana kemikali ya pombe... Hivyo akae siku mbili bila kunywa pombe, kisha akatolewe damu"
"kwanini kafanya hivyo"
"kaamua mwenyewe"
Bibi yake rahim hakupenda rahim atoe damu,.... Kule chumbani rahimu kasikia maongezi yote, akaamua kutoka
"nasema hivi, hata kama nisingemgonga mimi, lakini damu ningetoa tu"
Aliongea rahim huku akija hapo sebuleni na kumkuta jamali akinywa wiski moja ya gharama sana...
"sasa broo baada unifariji ara nizifikishe hizo siku, afu ndio kwanzaa unanitamanisha"
"kwani nilikutuma utoe damu"
Yaani familia hii pombe kwa ni kama maji yaani hawalali bila kunywa, tena bora hata jamali kuliko rahim,... Basi yalikuwa ni maongezi ya kawaida tu lakini bibi hajapenda mjukuu wake atoe damu
"lakini rahim mjukuu wangu... Kwanini uendeshe gari na wakati imelewa... Afu huku kulewa kwanini huachi ingali bado ni mwanafunzi"
"bibi tulia nawewe, au chukuwa zamu yangu hizi siku mbili... Mana unaongeea"
"mshenzi wewe... Nitokeee hapa mlevi wewe"
Utani wa bibi kama tunavyoujua ulivyo,...

BAADA YA SIKU MBILI HIVI KUPITA

Na leo ndio ile siku ya rahim kwenda kutoa damu, lakini huezi amini rahim mpaka kaumwa kwa kukosa japo grass moja tu ya pombe, na mbaya zaidi toka aje hajawahi kwenda sehemu yeyote ile ya starehe zaidi ya kutembelea hospitali,...
"unaweza kulala na ulilax vizuri.. Yaani usijikaze"
Sauti ya dokta ikimuamuru rahim asijikaze mana akijikaza ataizuia damu kutoka,... Damu ya rahim ilikuwa ni safi kupita maelezo, mana ana siku 2 na masaa kadhaa hajapata hata gras moja ya wine,.. Shukrani zilitoka katika upande wa familia, licha ya kumgonga yeye, lakini jambo alilofanya ni jambo zito mno, rahim alitoka mpaka pale nje na kumkuta yule dada yake na yule mtoto,... Rahim hua hapendagi mwanamke aliefunika uso, yaani wale wanawake wanaovaa kininja ninja, alimwangalia sana huku moyoni mwake anasema kuwa
"anaonekana mtoto mdogo lakini mchawi"
Yaani rahim imani ya dini hana kabisa, lakini anajua kuwa kuna mungu, ila anazidharau dini mno,..
"As Salaam Aleykum Warahmatullah Wabarakatuh"
Alisalimia yule dada, huku akiwa kainamiana chini japo haonekani sura lakini anaona aibu...
"safi tu"
Rahim alishindwa kuitika jinsi inavyotakiwa na badala yake ameitika salamu ya kidunia,... Na hata hio yenyewe ameitika huku akiangalia pembeni kana kwamba hajapenda kusalimiwa.... Yaani hapendi wadada wa aina hio hata kidogo,...
"ivi ukivua huo mnguo wako utakufa"
Aliongea rahim huku akiwa kashikilia mkono pale kwenye alama aliotolewa damu,..
"haya ni mavazi ya heshima kwangu siwezi kuyavua"
"waaapi nyie mnaloga watu nyie"
"astah khafirulah... Usiseme hivyo we kaka"
"umesemaje.... Umentukana nini?"
"basi nisamehe, lakini sijakutukana"
Mara mama na baba walikuja na kumshukuru sana rahim kwa kutoa damu, mana bila yeye sijui ingekuwaje....
"Tunakushukuru sana kijana kwa msaada ulioufanya"
Wazazi wa zena waliingia tena kule ndani ili kuwa karibu na mtoto wao,.. Lakini sasa cha ajabu na cha kushangaza, yule mschana aitwae zena, dada yake na yule mtoto alikuwa analia lakini rahim hajui mana hakuwa akimwangalia katika macho japo kafunga kininja,.. Na pia muonekano wa zena inaonyesha dhahiri kuwa mtu huyo anamjua vizuri sana, na hatujui sababu ya kulia kwake,.....

Je? Zena analia nini??... Je? Yeye rahim wanajuana kivipi,..

USIKOSE
 
THE ISLAMIC WIFE

(Mke Muislamu)

Sehemu Ya 6

Mtunzi... MoonBoy

Simu No, +255714419487 WhatsApp

Ilipoishia Jana →→↓↓

"As Salaam Aleykum warahmatullah wabarakatuh"
Alisalimia yule dada, huku akiwa kainamiana chini japo haonekani sura lakini anaona aibu...
"safi tu"
Rahim alishindwa kuitika jinsi inavyotakiwa na badala yake ameitika salamu ya kidunia,... Na hata hio yenyewe ameitika huku akiangalia pembeni kana kwamba hajapenda kusalimiwa.... Yaani hapendi wadada wa aina hio hata kidogo,...
"ivi ukivua huo mnguo wako utakufa"
Aliongea rahim huku akiwa kashikilia mkono pale kwenye alama aliotolewa damu,..
"haya ni mavazi ya heshima kwangu siwezi kuyavua"
"waaapi nyie mnaloga watu nyie"
"astah khafirulah... Usiseme hivyo we kaka"
"umesemaje.... Umentukana nini?"
"basi nisamehe, lakini sijakutukana"
Mara mama na baba walikuja na kumshukuru sana rahim kwa kutoa damu, mana bila yeye sijui ingekuwaje....
"Tunakushukuru sana kijana kwa msaada ulioufanya"
Wazazi wa zena waliingia tena kule ndani ili kuwa karibu na mtoto wao,.. Lakini sasa cha ajabu na cha kushangaza, yule mschana aitwae zena, dada yake na yule mtoto alikuwa analia lakini rahim hajui mana hakuwa akimwangalia katika macho japo kafunga kininja,.. Na pia muonekano wa zena inaonyesha dhahiri kuwa mtu huyo anamjua vizuri sana, na hatujui sababu ya kulia kwake,.....

ENDELEA.........

Rahim ni kijana wa Kiislamu lakini hajui nini maana ya Uislamu,... Akiona mtu kavaa hijabu anamuona kama mchawi vile mana kavalia vazi jeusi mwanzo mwisho,.. Akiona mwanaume kavaa kanzu anamwona ni mchawi mwanzo mwisho.. Na hii yote inatokana na malezi ya wazazi wetu huko majumbani, mtoto haijui hata dini yeke, kisa kazaliwa kwenye kisima cha pesa basi hata salamu ya Kiislamu hajui hata kuitikia... Vijana tubadilikeni jamani, tumgeukieni mwenyezi Mungu, kwa Mungu sio kwa mzungu jamani.. Bila kifanya mema hapa duniani usije kitegemea utakuta pepo baada ya kifo chako.. Pepo yako ni hii hii unayoifanya hapa duniani, lakini moto wa jahanamu utaukuta ukiwa tayari kukuteketeza mana tayari umeshakula pepo yako toka duniani....

TUENDELEENI NA STORY

Wakati zena analia sana ila haonyeshi kama analia kutokana na uninja aliovaa, yaani kafunika mpaka uso mzima, kabakiza macho tu,.. Ghafla kaka yake kafika...
"ndugu yangu... Nakushukuru sana kwa kitendo ulichofanya, tunakuombea"
Sulesh ambaye ni kaka yake na zena alikuwa akitoa shukrani zake kwa rahim, lakini rahim kaangalia pembeni tena anatamani hata amtukane.. Mana ndio wachawi wake hao,...
"sawa"
Rahim aliitikia kishingo upande, na hata sulesh alijua kuwa kaitikiwa kwa dharau, lakini hakuwa na budi kutulia mana wao ni masikini na hawana lolote lile,.. Sasa sulesh kugeuka na kumwangalia mdogo wake, aligundua kuwa analia,.. Alimchukuwa ndugu yake na kwenda nae chemba
"zena, unalia nini sasa... Kama ni bakari atapona mana tayari keshawekewa damu"
Aliongea sulesh akidhani labda dada yake analia kwa ajili ya mdogo wake
"hapana kaka sulesh,... Naililia dini yangu jinsi inavyo kashifiwa na huyu kijana... Kiukweli sijapenda kwakweli"
Aliongea zena huku akizidi kulia kwa uchungu mno... Kumbe kilio chake ni kwa sababu ya rahim kuongea ujinga juu ya dini yake,...
"zena... Pesa inawapoteza watu wengi sana katika hii dunia... Tena bora ya huyu anajua kuna mungu ila haijui dini yake, na uzuri wa huyu hana roho ya kuuwa... Kuna wengine wanasema hakuna mungu,.. Mungu ni yeye na pesa zake... Huyu kijana ni malezi tu hayajamkaa vizuri.. Kalelewa na pesa na ndio mana hajui dini.. Hajui imani yeyote ile kuhusu dini"
Sulesh aliongea maneno hayo kwa uchungu wa hali ya juu sana,...

"dogo, tayari umeshamaliza haja yako ya kutoa damu,... Twende tukatoe loku, mana una siku mbili hujagusa kitu"
Jamali alimchukuwa mdogo wake na kupanda katika gari yao ya kifahari,.

BAADA YA WIKI MOJA KUPITA

Rahim akiwa zake nyumbani time za jioni hivi,.. Alikuwa akichati na rafiki zake katika mtandao kwa kitumia laptop,.. Huku simu kubwaa iko kwa pembeni,.. Rahim alikuwa nje ya nyumba kabisa, na jamali alikuwa ndani anaangalia tv,... Sasa rahim akiwa anafurahi kichati Instagram na friends zake tena wakiwa online LIVE CHAT,... Ghafla aliona mschana mzuri akipita mbele yake,... Yaani sio kwenye kompyuta, bali amepita mbele ya macho yake pale alipokaa... Lakini sasa mschana huyo ni wale wale wanaovaa mahijabu, sema huyu kaachia uso, yaani hajafunika uso wote, kafunga ushungi wa kawaida tu
Rahim alikuwa akimtolea macho mno, alikuwa ni mschana mzuri sana mithili ya malaika,...
"we vipi... Ushapenda nini"
Alikuwa ni kaka yake jamali, ndio kamshtua kwa maneno hayo
"broo hiki kitoto ni kizuri sio mchezo ndugu yangu"
"sasa wewe na yeye wapi na wapi"
"kivipi"
"wale si unasemaga ni wachawi kwako, iweje leo awe mzuri"
"mmmmhhh ni kweli... Lakini duuu"
Rahim alibaki kumsindikiza kwa macho tu huku akitamani hata kuwa nae kimapenzi,..
Lakini sasa mschana huyo kumbe alikuwa na rafiki yake anafuata kwa nyuma, waliachana kwa dakika kadhaa tu...

"zena mbona umeniacha sasa"
Aliongea yule rafiki yake huku akihema kwa kukimbia
"nilijia huji sasa hivi.."
"afu mbona imefungua kitambaa cha usoni"
Alimuuliza rafiki yake mbona alifungua kitambaa cha usoni mbacho hicho kitambaa ndicho kinacho unganika na kingine ili kufunika uso wote kasoro macho tu.. Lakini sasa huyu mschana aitwae zena ndio yule yule mwenye mdogo wake aliogongwa na gari, yaani mdogo wake sulesh, au dada yake Bakari,.....
"nina maana yangu tu"
"ok sawa... Ila zena... Mbona yule kaka alikuwa anakuangalia mpaka unapotelea hapa"
"mmmhh nani huyo"
"si yule alikuwa kakaa pale kashika kompyuta ndogo"
"yule mkaka wa kidunia"
"ndio... "
"mmmhhh atajua mwenyewe"
Basi hayo yalikuwa ni maongezi yao baina ya fadhila na zena, watu hawa ni marafiki wa karibu sana, na wanaishi kama ndugu....

Siku ya pili tena, rahim alitega muda kama ule ule, ili yule dada aongew nae hata kama ni mchawi,.. Mwenyewe anasema tanga kuna wachawi wazuri sana,... Na rahim hajui kama huyo ndio yule zena aliokuwa nae kule hospitali, mana zena alipokuwa hospitali alifunika uso wote kasoro macho, sasa jana alivyopita, kaachia uso wake ukaonekana, na hapo rahim ndipo alipomuona,... Ghafla akamuona yule ragiki yake zena aitwae fadhila,... Rahim Alimwita fadhila na fadhila hakukataa mana wahenga walisema, usikatae wito bali kataa neno...
"As Salaam Aleykum Warahmatullah wabarakatuh"
Fadhila alimsalimia rahim huku akimpa mkono uliofunikwa na hijabu, ikiwa na maana kuwa asigusane na mwanaume ngozi kwa ngozi mana hapo alipo ana uzu (usafi wa roho)
"safi tu"
Rahim hajui hata kuitikia salamu hio, mana hakuwa akiipenda...
"hali yako"
"nzuri tu... Aahhh Samahani dada.. Eti yule rafiki yako leo hapiti hapa"
Aliuliza rahim huku akinyoosha vidole kwa ishara ya vitendo
"rafiki yangu nani mbona hata simkumbuki"
"mweupe hivi"
"aaahhhh zena"
"mmmhhh nadhani atakuwa huyo"
"leo hajaingia madrasa... Anaumwa"
"madrasa ndio nini.... Na anaumwa nini, mbona jana kapita mzima tu"
"heeeeee we kaka, hata madrasa hujui.... Ok, madrasa ni darasa la kiislamu linalofundisha maadili ya dini, linafundisha Quran tukufu, linafundisha mambo mengi sana juu ya dini yetu ya Kiislamu"
Rahim hapo hata haelewi kitu, anabaki hewani hewani tu
"ok anaumwa na nini"
"ni malaria ya ghafla tu yalimuanza jana"
"hospitali gani"
"hapo kwa MOHAJI HOSPITAL"
Rahim alitamani kwenda hata jioni hio hio,... Lakini wamewekewa torati ya kuto toka usiku...
"tafadhali, naomba kesho unipeleke"
Aliongea rahim... Lakini fadhila alionekana kujigonga kwa rahim, ila hakupenda kusema,....

Kweli zena alikuwa mgonjwa na fadhila leo alikwenda hospitali kumwona rafiki yake, ikiwa ni mida ya saa moja hivi, yupo nae katika kitanda cha wagonjwa...
"As Salaam Aleykum Warahmatullah wabarakatuh"
"Waleykhu Msalam Warahmatullah wabarakatuh... Hali yakl fadhila"
"salama tu... Sjui wewe huku waendeleaje"
"aahhh tunamshukuru mwenyezi Mungu kwa kuendelea kunipa pumzi yake"
"hata mimi nashukuru kukuona ukiwa hai.... Ila nina ujumbe wako zena"
"ujumbe... Ujumbe gani tena fadhila"
"yule kijana wa jana nimekutana nae leo"
"Enheee... Kasemaje"
"nimemwambia unaumwa... Akatamani hata kuja leo leo lakini kasema nimlete kesho"
"sasa kwanini usimlete"
Aliongea zena huku akitamani hata aje
"lakini zena... Yote tisa, kumi yule kijana anaonekana kakupenda wewe"
"mmmhhh fadhila Usiseme hivyo.. Yule ni mtu wa kidunia siwezi kuwa nae... Afu yule ni kama shetani... Yaani nimekosa kupata mume mwenye imani kama yangu mpaka nimfuate yule... Siwezi"
"sasa mbona unatamani aje"
"ivi unajua kuwa yule ndie aliemgonga mdogo wangu"
"unasemaje...."
"ndio yeye... Afu yeye ndio kamwongezea damu mwenyewe.. Yule kijana ni mtu wa starehe sana, ni mdogo lakini anakunywa pombe.. Simtaki... Kama ni kuniona tu aje lakini kama ni mambo hayo asije"
"mmmhh Afadhali... Mana nilijua unampenda"
Aliongea fadhila na kumshtua zena
"kwanini useme hivyo fadhila"
"mimi... Nitafanya mpango nimbadilishe,... Kiukweli ni kijana mzuri kwa sura.. Ila tabia yake nitairekebisha tu"
Zena alishangaa kusikia hivyo
"sasa wewe umrekebishe ili iweje"
"nampenda... Natamani awe mume wangu"
"fadhilaaaaaaaaaaaaaaaaaa"
"nini?"
Zena aliita kwa hasira huku akilia kana kwamba maneno ya fadhila yamemgusa vilivyo....

Je?... Kwanini zena analia... Na je? Alioyasema Fadhila kamaanisha kweli au karopoka tu

ITAENDELEA...
 
THE ISLAMIC WIFE

(Mke Muislamu)

Sehemu Ya 7

Mtunzi... MoonBoy

Simu No, +255714419487 WhatsApp

Ilipoishia Jana →→↓↓

"lakini zena... Yote tisa, kumi yule kijana anaonekana kakupenda wewe"
"mmmhhh fadhila Usiseme hivyo.. Yule ni mtu wa kidunia siwezi kuwa nae... Afu yule ni kama shetani... Yaani nimekosa kupata mume mwenye imani kama yangu mpaka nimfuate yule... Siwezi"
"sasa mbona unatamani aje"
"ivi unajua kuwa yule ndie aliemgonga mdogo wangu"
"unasemaje...."
"ndio yeye... Afu yeye ndio kamwongezea damu mwenyewe.. Yule kijana ni mtu wa starehe sana, ni mdogo lakini anakunywa pombe.. Simtaki... Kama ni kuniona tu aje lakini kama ni mambo hayo asije"
"mmmhh Afadhali... Mana nilijua unampenda"
Aliongea fadhila na kumshtua zena
"kwanini useme hivyo fadhila"
"mimi... Nitafanya mpango nimbadilishe,... Kiukweli ni kijana mzuri kwa sura.. Ila tabia yake nitairekebisha tu"
Zena alishangaa kusikia hivyo
"sasa wewe umrekebishe ili iweje"
"nampenda... Natamani awe mume wangu"
"fadhilaaaaaaaaaaaaaaaaaa"
"nini?"
Zena aliita kwa hasira huku akilia kana kwamba maneno ya fadhila yamemgusa vilivyo....

ENDELEA.........

Mapenzi ni jambo lingine, haijalishi dini wala kabila, damu zikishaendana tu yaani hakuna atakaezuia swala hilo, huezi kuamini kuwa zena na imani yake dhabiti ya dini ya kiislamu lakini katokea kumpenda rahim,.. Ila sasa kitu ambacho hakipendi kwa rahim ni ile tabia yake,... Ana tabia mbaya ya kuikashifu dini yaani pesa zao anaona ndio kila kitu

"sasa wewe umrekebishe ili iweje"
"nampenda... Natamani awe mume wangu"
"fadhilaaaaaaaaaaaaaaaaaa"
"nini?"
Zena aliita kwa hasira huku akilia kana kwamba maneno ya fadhila yamemgusa vilivyo,
"skia fadhila.... Hata mimi nina moyo wa kupenda, lakini tabia ya yule mtu, hata baba na mama hawatonielewa japo kumsaidia mdogo wangu ila sio swala la kuwa nae
"zena... Mimi simpendi... Nilitaka kujua tu kama kweli unampenda... Nimeshajua"
Fadhila kumbe hakumaanisha kweli kama anampenda, lakini moyoni mwake, kweli anampenda ila hataki kumuudhi rafiki yake...
"Ufyuuuuuu... Basi mlete hata anijulie hali"
"lakini zena... Kwanini umempenda yule kijana"
Fadhila alimuuliza zena kwnini kamapenda na wakati ni mvulana wa starehe tu,.. Anakunywa pombe, ni mtu wa wanawake tuuu
"fadhila.... Kabla ya kukutana na mtu huyu... Hii sura Nilishawahi kuiota akiwa kama mume wangu mtarajiwa... Lakini ndoto ile, niliota akiwa ni Muislamu mzuri tu.. Yaani alikuwa kaishika dini vilivyo... Lakini sasa nimekuja kishangaa ni mtu wa tofauti kabisa yani... Na mbaya zaidi kuna siku nilimshika mkono, kwa nia ya kumuomba nimpeleke Bombo Hospital... Lakini kitendo cha kumgusa tu, nilosisimka mwili mzima.. Na hata yeye pia ilikuwa hivyo mana alinisukima kana kwamba hakuupenda msisimko ule... Toka siku ile kaingia moyoni kakaa.. Lakini matendo yake sasa siyapendi hata kidogo.. Mtu mwenyewe unaambiwa hawezi kukaa hata siku moja bila kunywa hizo wine zao"
Zena aliongea sana, mpaka anatamani kulia
"sasa kwanini ulimpenda"
"mimi sijui"

Kesho yake mida ya mchana hivi rahim akiwa nyumbani kwao yeye na kaka yake
"broo yule mtoto niliomuona juzi.... Kiukweli ni mkali mno"
Mara bibi yake kasikia maneno ya rahim
"wewe mjinga sana,.. Ulizani kina wahuni kama huko mjini kwenu... Huku uwe na adabu na wasichana wa watu"
"bibi vunga basiiii"
"nivunge nini"
"mtoto mkali yule"
"mkali amekuwa mbwa"
Rahim alikuwa akiongea na bibi yake kwa utani,....

"skia bibi... Huyu mjukuu wako ana dharau za pesa.... Huezi amini Waislamu wa watu eti anasema ni wachawi, ivi ana akili kweli huyu? Afu mbaya zaidi eti kaona binti wa Kiislamu afu anasema ni mkali... Mjinga sana huyu"
"heeeeeeee unasema anawaita nani?... Hivi we mtoto pesa zitakupeleka wapi?... Kwanini huiheshimu dini yako"
Rahim kuona bibi anaongea sana aliondoka zake,... Kachukuwa gari kisha akawa anaelekea zake mjini.. Lakini ghafla fadhila katokea,
"enheee we mdada"
Aliita rahim wakati huo fadhila kavalia nguo za kawaida tu
Fadhila aliingia katika gari mana anakumbuka jana alimwahidi kumpeleka hospitali ambako zena kalazwa... Fadhila mwenyewe haamini kama kapanda kqenye hio gari, na anatamani sana awepo katika hii familia, lakini atawezaje?.. Gari ilitua mbele ya hospitali, kisha rahim akaingia ndani kwa kuelekezwa na fadhila kuwa ni wodi namba fulani... Rahim hajui lolote la kubisha Hodi hajui... Aliingia tu bila hata hodi
"heeeeeee mbona umeingia kama chooni"
Aliongea zena, tena bila kumuogopa mana alishadokezewa na fadhila kuwa rahim atakuwa anakupenda.. Hivyo ana uhakika hawezi kimfanya lolote,
"kwani una nini"
Ubaya wa rahim ana dharau sana yaani hataki umseme jambo limguse
"basi yaishe"
Rahim alikuwa ana Tabasamu tu, mana kumkuta zena akiwa kavalia mavazi ya kawaida, yaani sio hijabu bali alivalia gauni lake refu suruali ndefu, kisha kufunika nywele zake kwa ushungi... Alikuwa ni mzuri mithili ya malaika,....
"kumbe unapendeza kiasi hiki"
Na hapo rahim bado hajajua kuwa huyo ni yule zena waliokuwa wote katika ile hospitali ya bombo,.. Mana yule alifunika sura yote na kubakiza macho tu,...
"tayari umeshaniona unaweza kwenda"
Alionhea zena, lakini rahim ndio kwanza kakaa....
"unakaaje bila ruksa yangu... Baba na mama wakikukuta hapa.. Naomba uondoke"
Zena alizidi kuwa mkali zaidi
"mwanamke mzuri kama wewe... Kuwa mkali haipendezi, tena ukali wako ni bora iwe kwa mwanamke mwenzio... Ila sio mwanaume"
Aliongea rahim huku akikaa vizuri,

"tatizo lako wewe una tabia mbaya... Wewe ni mtoto wa Kiislamu, unatakiwa ufuate misingi ya dini.. Lakini kwa pesa ulizo nazo unaikashifu dini yako kwa kuwaita watu ni wachawi... Nani alikuambia Quran inahusishwa na hayo mambo.. Wewe ni Muislamu,.. Sisi sio wachawi.. Zile ni nguo za heshima kwa wanawake,.. Kiukweli unapata dhambi kubwa sana kutuita wachawi, kisa tumejifunga vitambaa vya uso.. Hakika hata hizo pesa zako utaziacha hapa hapa.. Hata hilo gari lako hutoenda nalo... Unakosea sana kuita watu ni wachawi... Nani alishawahi kukuloga wewe,.. Kwanini unajibebea mizigo ya dhambi ambayo haikuhusu....... Nasema sitaki kukuona, naomba utoke nje"

Zena aliongea mpaka analia,.. Sasa hapa ndio tunajua kweli zena anampenda rahim, ila sasa tabia yake,.. Rahim ni sharobaro mpenda starehe sana, ana dharau za kutupa..
"yaani kulia kwako tu ni uzuri tosha"
Aliongea rahim kisha akamuita dokta
"dokta.. Huyu mgonjwa anadaiwa"
"ndio... Lakini sio kubwa sana"
Mara zena kasema kuwa
"usilipe kiasi chochote kile... Mana haina maana kusaidia mtu wakati mungu wako humheshim.....pesa zako sii chochote mbele za Mungu.. Tutalipa wenyewe"
Rahim, alikasirika sana mana hua hapendi kuambiwa ukweli juu ya maisha yake... Kweli rahim hakulipa ile pesa, alitoka... Lakini ghafla anakutana na baba yake zena na mama yake zena... Mbaya zaidi mpaka yule mtoto aliomgonga, mbaya zaidi na sulesh ambae ni kaka yake zena.... Sasa rahim anajiuliza, hawa wanamfuata nani tena huku..
"shkamoni"
"Marahaba ujambo"
"sijambo... Mama vp kuna nini huku"
"ni yule mtoto wangu wa kike... Kalazwa toka juzi"
Wakati huo baba mtu kaingia ndani lakini bila ya salamu au kumjulia hali mtoto wake... Kaanza kuuliza
"yule kijana kafata nini huku ndani"
Mzee alimuuliza mtoto wake wa kike
"alikuja kuniona tu"
"nimesema hivi, sitaki tena kumuona huyu mtu... Kama keshatoa msaada kwa mdogo wako inatosha, lakini sio kwako tena... Naona unataka kinivunjia heshima yangu kwa bwana hamisi"
"hapana baba"
"sasa kesho... Nakwenda kwa bwana hamisi kuchukuwa ng'ombe wa kwanza.... Sasa ole wako"
"babaaaaaaaa"
"nini...."
"basi sawa tu"
Zena alianza kulia kwa uchungu huku mzee akitoka kwa hasira... Alimkuta rahim anaongea na mama hapo nje
"we kijana... Naomba ukae mbali na binti yangu.... Usinitishe na pesa zako sawa... Binti yangu ana mchumba wake huyo... Maswala ya kumfata fata utakiona cha moto"

Je?... Rahim atamjibu nini mzee huyo.. Au atamfanya nini??.. USIKOSE

ITAENDELEA...
 
THE ISLAMIC WIFE

(Mke Muislamu)

Sehemu Ya 8

Mtunzi... MoonBoy

Simu No, +255714419487 WhatsApp

Ilipoishia Jana →→↓↓

Kweli rahim hakulipa ile pesa, alitoka... Lakini ghafla anakutana na baba yake zena na mama yake zena... Mbaya zaidi mpaka yule mtoto aliomgonga, mbaya zaidi na sulesh ambae ni kaka yake zena.... Sasa rahim anajiuliza, hawa wanamfuata nani tena huku..
"shkamoni"
"Marahaba ujambo"
"sijambo... Mama vp kuna nini huku"
"ni yule mtoto wangu wa kike... Kalazwa toka juzi"
Wakati huo baba mtu kaingia ndani lakini bila ya salamu au kumjulia hali mtoto wake... Kaanza kuuliza
"yule kijana kafata nini huku ndani"
Mzee alimuuliza mtoto wake wa kike
"alikuja kuniona tu"
"nimesema hivi, sitaki tena kumuona huyu mtu... Kama keshatoa msaada kwa mdogo wako inatosha, lakini sio kwako tena... Naona unataka kinivunjia heshima yangu kwa bwana hamisi"
"hapana baba"
"sasa kesho... Nakwenda kwa bwana hamisi kuchukuwa ng'ombe wa kwanza.... Sasa ole wako"
"babaaaaaaaa"
"nini...."
"basi sawa tu"
Zena alianza kulia kwa uchungu huku mzee akitoka kwa hasira... Alimkuta rahim anaongea na mama hapo nje
"we kijana... Naomba ukae mbali na binti yangu.... Usinitishe na pesa zako sawa... Binti yangu ana mchumba wake huyo... Maswala ya kumfata fata utakiona cha moto"

ENDELEA.......

Mzee Mvungi aliwaka moto alikuwa hana utani kabisa na mtoto wake, na kama unavyojua wazazi wa kijijini hua wanapenda kuwachagulia watoto wao wachumba wa kiwaoa,.. Kumbe hata zena ni mmoja wapo, na mzee unaambiwa anataka ng'ombe saba, kama mahari kwa mtoto wake, familia moja imekubali kulipia ng'ombe sana na leo mzee anakwenda kuchukuwa ng'ombe mmoja...

Sasa kumbe mzee hakufurahiwa na rahim kabisa, na licha ya baba, hata mama pia hakumfurahia rahim, hata pale wakati Bakari anaumwa, walikuwa hawataki kompleni na huyu kijana,.. Na aliosababisha watulie alikiwa ni sulesh,... Mana hata damu hawakuitaka na hawakuwa na shida nayo,... Na siku ile ilikuwa hivi

"baba, mtoto anaumwa na huyo ndie aliemgonga, acha presha mtoto apone mzee"
Sulesh alimwambia baba yake siku hio aliotaka kuamsha tempa, kwahio hata zile shukrani zilikuwa ni za kuzuga tu
"huyu kijana mchafu sana atawezaje kutoa damu kwa mtoto wangu... Hebu ona ana kemikali za pombe katika damu hio je itakuwaje kuhusu mtoto wangu.."
"baba, kama ingelikuwa haifai, hata dokta angesema kuwa haifai... Lakini kwakuwa inafaa ndio mana akapewa siku kadhaa asinywe pombe"

Sulesh alimtuliza baba yake huku mama nae akiwa hataki pia... Yaani hii familia imejawa na imani ya dini, hivyo hawakupenda rahim atoe damu kwa mtoto huyo licha ya kwamba yeye ndie alimgonga.... Wazee walikubali kishingo upande tu..

Sasa leo kwenye ugonjwa wa zena rahim kakutana na mzee Mvungi
"we kijana... Naomba ukae mbali na binti yangu.... Usinitishe na pesa zako sawa... Binti yangu ana mchumba wake huyo... Maswala ya kumfata fata utakiona cha moto"
Rahim aligeuka kwa hasira huku akijiandaa kumjibu,.. Lakini kabla hajafanya hivyo alimwona zena katika dirisha akimwambia kwa vitendo kuwa asithubutu kufanya au kuongea lolote lile,.. Rahim alibakia kutulia tu, huku akiondoka zake kwa hasira, na hapo alikuja na fadhila,... Fadhila kasikia kila kitu,...

Rahim hakukata tamaa alihakikisha tu mpaka zena anapona vizuri, na leo ilikuwa ni siku ya zena kutoka hospitali, rahim kapata nafasi hata ya kutoka nae nje ya hospitali...
Na wakati huo zena alikuwa kavaa NIKABU anaonekana macho tu,.. Rahim hapendi hilo vazi lakini kwa maneno aliopewa na zena pale hospitali kuwa pesa zako magari yako, nyumba zako, utaziacha hapa hapa,...
"we ram, si upande gari sasa"
Aliongea jamali huku akifungua mlango,
"wacha mgonjwa anyooshe miguu"
Aliongea rahim, huku wakitembea pamoja... Lakini wakati huo zena hapendi kuwa sambamba na rahim, kwasababu mavazi yake, hayakuwa sahihi kutembea na zena..
"ivi we kijana, unaweza kuniacha nielekee nyumba mwenyewe"
Aliongea zena, na wakati huo fadhila yupo nyuma kama mita 20 hivi, ili kiwapa nafasi,..
"kwanini"
"mavazi yako hayastahili kutembea na mimi"
"ok... Sawa nitakuacha"
Zena anampenda rahim yaani ghafla tu alijikuta tu anampenda vile alivyo, lakini sasa hataki kuwa na mahusiano ya kificho, anataka wajulikane kwa wazazi na wazazi wenyewe ndio hao wameshaanza kumchukia rahim, we ulifikiri nini kitatokea hapo....

Sasa wakiwa wanaendelea kutembea taratibu,...
"ndugu zangu seidia.... Nisaidieni"
Alikua ni omba omba aliokuwa kakaa pembezumwa barabara, na alikuwa hana mikono pia miguu, na mbaya zaidi hata kuona kwake ni kwa shida, kwasababu ya umri wake kuwa mkibwa, yaani ni mzee....
"we vipi... Unaniomba pesa kwani kanipa baba ako.... Ntakutia teke la mbavu"
Rahim aliongea hivyo huku kweli akitaka kifanya hivyo kwa kumpiga yule kilema wa watu, tena alikuwa ni mzee sana,...
Zena alimzuia asifanye kile alichokifanya, afu zena kumbe alimpitisha makusudi sehemu hio,...
Zena hakumsemesha kitu,.. Mzee wa watu katulia kimya huku akilia kwa umasikini aliokuwa nao, hana mikono hana miguu, lakini rahim kashindwa kumsaidia, tena mbaya zaidi kampa na vitisho vya kutaka kumpiga mateke ya mbavu... Zena ilimuuma sana lakini hakusema kitu alimwacha tu

Baada ya siku kadhaa kupita,.. Rahim akiwa nyumbani kwao,..
"ivi bibi... Eti yule binti ana mchumba yule"
Rahim alimuuliza bibi yake,... Lakini jamali akamjibu
"wewe umesha ambiwa kuwa ana mchumba sasa yanini ung'ang'anie.. Ujinga uo"
Mara bibi kaingilia kati,...
"ngoja... Licha ya kuwa na mchumba,.. Huyu ni kichaa sana huyu... Wewe na usharobaro wako huu ulitegemea utampata mschana kama yule... Watoto wa tanga wana imani ya dini.. Sasa wewe hivi ulivyo.. Kweli we ni mjinga kama alivyosema kaka ako"
Bibi na jamali walikuwa wakiongea maneno makali sana ya kukatisha tamaa
"lakini bibi.. Unaependa ni moyo au mavazi"
Aliuliza rahim
"na uliona wapi mavazi bila vitendo... Haya mavazi na vitendo vyako, kuna tofauti"
"aahhhhhh broo, achana na bibi twenzetu club sisi"
Aliongea rahim huku bibi akisema kuwa
"umeona eeee..... Sasa yule ni mtu wa club yule... We ulifikiri utampata kwa staili hio"
"kwani si atamfuata mtu wake"
Jamali na rahim walichukuana haoo mpaka club, waliagiza wanavyojua wao mana pesa iko,...

Wakati wanarudi, walikutana na zena na rafiki yake fadhila,...
"zena... We zena wewe"
Rahim aliita huku akimfuata mana walikuwa wanatembea kwa miguu, hua rahim hapendelei gari mara kwa mara,...
"we, we, we,.. Ishia hapo hapo.. Yaani usinisogelee"
"kwanini sasa"
"we hujioni ulivyo... Tena staki mazoea na wewe"
Aliongea zena kisha akaondoka zake.. Lakini fadhila yeye hakuondoka alibaki na rahim,.. Unajua hata fadhila anampenda rahim, lakini anamuogopa zena, mana zena anampenda kupita maelezo,... Sema tabia ya rahim ni mbaya mno, na zena haipendi... Sasa zena baada ya kuona fadhila haji,.. Ilibidi arudi taratibu mana kakata kona kadhaa hivi lakini fadhila Haji...
Wakati huo fadhila ndio anaongea,...

************************************

"rahim... Kwani wewe unampenda zena"
Fadhila alimuuliza rahim wakati huo zena anachungulia tu mahali,...
"kiukweli nampenda kwasababu ni mzuri, natamani kuwa nae"
"sio.. Umuoe"
"aahhhh wakuoa atakuwa mimi bwana"
"sasa kwanini unahangaika na mtu ambae hakupendi.... Kwasababu mimi juzi nilimwambia kuwa rahim yule mjukuu wa bibi mzungu anaonekana anakupenda... Alichonijibu siwezi kuamini kwakweli"
"kakujibu nini......"
Fadhila anaharibu kila kitu kwa zena,
"kwanza.... Zena ana mume.. Alafu alishawahi kutoa mimba tatu, usimuone vile, kamrudia mungu hivi karibuni tu lakini alikuwa kama wewe"
"we muongo.."
"ninao ushahidi wote??.... Ila usije kupaniki"
"sawa.. Ebu Niambie"

Je?... Nini kitaendelea???... Zena ana mume kweli... Zena katoa mimba kweli?... Zena alikuwa mhuni kweli??

ITAENDELEA...
 
THE ISLAMIC WIFE

(Mke Muislamu)

Sehemu Ya 9

Mtunzi... MoonBoy

Simu No, +255714419487 WhatsApp

Ilipoishia Jana →→↓↓

Aliongea zena kisha akaondoka zake.. Lakini fadhila yeye hakuondoka alibaki na rahim,.. Unajua hata fadhila anampenda rahim, lakini anamuogopa zena, mana zena anampenda kupita maelezo,... Sema tabia ya rahim ni mbaya mno, na zena haipendi... Sasa zena baada ya kuona fadhila haji,.. Ilibidi arudi taratibu mana kakata kona kadhaa hivi lakini fadhila Haji...
Wakati huo fadhila ndio anaongea,...

************************************

"rahim... Kwani wewe unampenda zena"
Fadhila alimuuliza rahim wakati huo zena anachungulia tu mahali,...
"kiukweli nampenda kwasababu ni mzuri, natamani kuwa nae"
"sio.. Umuoe"
"aahhhh wakuoa atakuwa mimi bwana"
"sasa kwanini unahangaika na mtu ambae hakupendi.... Kwasababu mimi juzi nilimwambia kuwa rahim yule mjukuu wa bibi mzungu anaonekana anakupenda... Alichonijibu siwezi kuamini kwakweli"
"kakujibu nini......"
Fadhila anaharibu kila kitu kwa zena,
"kwanza.... Zena ana mume.. Alafu alishawahi kutoa mimba tatu, usimuone vile, kamrudia mungu hivi karibuni tu lakini alikuwa kama wewe"
"we muongo.."
"ninao ushahidi wote.... Ila usije kupaniki"
"sawa.. Ebu Niambie"

ENDELEA........

Fadhila alionekana kuongea maneno ya kumchafulia zena, mana rahim anampenda sana zena... Yaani anampenda mno toka alipomwona basi anatamani kuwa nae kama mpenzi wake,... Lakini pia sio rahim tu, bali hata zena katokea kumpenda rahim, lakini tatizo la rahim, ni hio tabia yake ambayo zena hatamani kuiona kwa rahim....

"we muongo..."
"ninao ushahidi wote... Ila usije kupaniki"
"sawa.. Ebu niambie"
Rahim alikaa tayari kwa kusikiliza umbea wa fadhila kuwa zena alishawahi kutoa mimba tatu, na alikuwa mhuni kama rahim alivyo kwa sasa

************************************

Lakini sasa kumbe hayo yalikuwa ni mawazo ya zena pale alipokuwa anachungulia baada ya kuona fadhila haji, sasa ndipo alipohisi kuwa fadhila huenda anaongea hayo maneno,... Sasa kama zena kayawaza hayo basi ni kweli,..
"fadhila anaongea nini na yule kijana"
Aliongea zena kimoyomoyo kama vile anajiuliza mwenyewe,...

Wakati huo huku fadhila alikuwa akimwambia rahim kuwa
"sikiliza rahimu, hapa ulipo umelewa wewe, huezi kuongea nae hata kidogo"
Aliongea fadhila huku nae akitaka kuondoka,...
"kwani sasa hivi mtarudi tena huku"
"hapana, ndio tumetoka madrasa sasa hivi"
"sasa nitamuonaje"
"labda uende dukani kwao"
Aliongea fadhila, huku nae akipiga hatua za kuondoka....
"sawa"
Ghafla jamali katokea huku akicheka
"tatizo mdogo wangu unajisumbua sana, hawa watoto wa watu wa Kiislamu unataka kuwafanya nini... Hawa si wachawi wako hawa"
Aliongea jamali na hapo walipo walikuwa wameshapata moja moto moja baridi,...
"ah ah broo, usiseme hivyo bwana"
"heeeeeeee.... We si ndio uliokuwa unasema ni wachawi na nguo zao"
"ndio, lakini sio zena"
Waliongea kisha wakaingia zao ndani, rahim kwa sasa kidogo kapunguza kuikashifu dini... Toka alivyopewa darasa kule hospitali mpaka sasa hataki tena kusema wachawi,...

Kesho yake mida ya mchana hivi, alimwita hadija ambae ndio mfanyakazi wa ndani hapo kwao,...
"dija"
"abee kaka"
Rahim alimwita kwa upole, mana hua anamnyanyasaga sana dija au hadija, maskini hadija wa watu kaja kwa heshima anajua lazima apewe kazi ya ajabu ajabu tu...
"abee kaka"
Alifika dija huku akiwa kachuchumaa
"hapana, kaa kwenye kochi"
Hadija alishangaa sana mana rahim ni dikteta mzuri sana,... Sasa leo anashangaa anaambiwa akae kwenye kochi..
"asante kaka"
Aliongea hadija mtoto mpole, tena nae alikuwa anapenda sana kufunga ushungi, lakini rahim alipokuja tu hapo nyumbani, akamkataza kufunga ushungu, na akamwambia endapo ataendelea kufunga ushungi angemfukuza kazi,... Na hata dija alikuwa yeye na madrasa hawaachani lakini aliacha kwasababu ya rahim....
"Samahani sana dada angu"
Rahim leo kamuomba msamaha dija, mpaka dija alitaka kuanguka kutoka sofani,... Mana rahim hajawahi kumpumzisha dija yaani ni tabu tupu kisa wana hela,..
"lakini kaka, hujanifanyia chochote kibaya"
"hapana dija... Vipo nilivyokufanyia... Nimekunyanyasa sana, sikupi raha ndani ya nyumba... Na uzuri wako huo lakini sikuwa nikiuona"
Dija alibaki kutabasamu tu,.. Unajua ukiwa mfanyakazi afu boss anakusifia vizuri lazima uachie Tabasamu mwanana..
"lakini kaka mbona mimi nilishakusamehe tu"
Wakati huo jamali alikuwa hayupo
"sasa, kuna kitu nataka nikuombe"
Dija ndio akajua kumbe misamaha yote hii kumbe kuna kitu anataka kuniomba,....
"sawa kaka"
"sasa sikia... Nataka uende kwa akina zena,... Ukamwambie jioni tukutane"
"mmmhhhhh kakaaa....."
Dija aliguna, mana swaga za zena na swaga za rahim, ni tofauti kabisa, yaani hawaendani hata kidogo.. Na dija aliguna kwasababu anajua tu rahim anataka kumchezea mtoto wa watu...
"unaguna nini sasa"
"hapana kaka... Sawa naenda sasa hivi"
Dija alitoka kichwa wazi lakini rahim alimuita na kumwambia afunge ushungi,... Dija alizidi kushangaa, rahim kabadirika kwa kiasi kikubwa sana,... Basi dija aliondoka huku akifunga kitambaa chake kichwani,..

Wakati huo huku kwa akina zena, zena akiwa dukani akiuza bidhaa ndogo ndogo kama sehemu ya kujipatia riziki yake japo hana majukumu yeyote yale lakini kapewa kamtaji na baba yake hivyo kafungua kiduka cha bidhaa za kawaida tu...
Mara alimuona rafiki yake dija,
"heeeeee dija... Ulikuwa wapi wewe, siku hizi hata madrasa sikuoni kabisaa"
Aliongea zena baada ya kumuona dija, mana wanajuana vizuri sana
"we acha tu zena.... As Salaam Aleykum warahmatullah wabarakatuh"
"Waleykhu msalam warahmatullah wabarakatuh.. Haya vipi hali yako"
"aahh tunamshukuru mwenyezi Mungu anasaidia"
"haya za wapi saa hizi mida ya kuswali hii"
Zena alimuuliza hadija kuwa saa tisa hii anakwenda wapi na mida ya kuswali mana hata zena wakati huo alikuwa akitandika mswala (mkeka spesho wa kuswalia) ili aswali swala ya alasiri...
"we acha tu zena... Huu mguu ni wako huu"
Aliongea hadija huku akikaribishwa vizuri ndani
"enhee haya karibu tuswali kwanza.. Kisha tuendelee na maongezi yaliokuleta"
Basi zena na hadija waliswali hapo hapo mana mida ulishafika... Na kuswali ni popote pale kikubwa uwe na uzu (usafi wa mwili)..
Baada ya kumaliza kuswali walipiga dua ya kumaliza ibada yao.. Dija alimisi sana vipengele vya kuswali, mana toka rahim aje, hajawahi kutoka nyumbani... Japo ni mfanyakazi tu

"enheee niambie dija... Umesema mguu huo ni wangu"
"ndio zena.... Kuna ujumbe nimekuletea kwako toka kwa kaka rahim"
"heeeee yule si mtoto kwako yule, sa kwanini awe anakutuma"
"najua sana, kale ni katoto sana kwangu... Yaani nalingana na kaka yake yule jamali, lakini rahim hanieshim tena ndio kwanza ananipeleka puta, nafanya mpaka kazi ambazo hazina ulazima"
"mmmhhh pole sana... Najua ni haki yako mana ndio kazi yako"

"sasa zena... Rahim kaniambia leo mkutane"
"we, usiongee kwa sauti hivyo... Wazazi watasikia"
"sawa, lakini ujumbe ndio huo alionipa"
"hapana... Mwambie siwezi kukutana kafiri"
Aliongea zena huku roho ikimuuma kweli
"hapana zena... Hayo sio maneno ya kumwambia, nipe jibu zuri nikamjibu, yule ni boss wangu lazima nitoe maneno ya heshima hata kama ni mtoto kwangu"
"sikiliza dija... Yule mkaka hata mimi pia nimejikuta tu nampenda... Yaani sio yeye tu,... Huezi amini madrasa kwetu kuna wavulana wengi sana, tena wenye hekima mbele za mungu na kwa wazazi wao... Lakini sijawahi kumpenda kijana wowote kati yao.. Nilishangaa sana kwanini nilijikuta nampenda yule... Tena nampenda sana tatizo ni tabia yake"

"enheee hapo hapo... Yaani hapo ndipo unapoongea pointi ya msingi sana.... Sasa yule sio wa kumjibu hivyo,... Kikubwa wewe mkubalie tu"
"dija wewe ivi nitaanzaje kumwambia nakupenda, vile alivyo mhuni, eti mimi mtoto wa Kiislamu nimelelewa na wazazi wangu wote... Leo nikamtaamkie nampenda... Haaaaaa labda abadilike"
Aliongea zena huku akitaka kuamka kwa hasira
"sasa we ulifikiri atabadilikaje bila kuwepo na mtu wa kumwambia?"
"hata wewe pia unaweza kumwambia abadilike"
"hapana... Mimi siwezi, ila wewe unaweza"
"kivipi sasa"
"sikia... Wewe mkubalie.. Halafu kaa nae chini kama mpenzi wako.. Mpe maneno makali, mi naamini atabadilika tu... Hebu ona... Toka aje mimi sijawahi kuja madrasa, toka aje mimi sijawahi kufunga ushungi, lakini leo kunituma kwako kaniruhusu kuvaa ushungi.. Yaani mpaka nimeshangaa jambo hili"
Sasa zena akakumbuka kuna siku alimpa vigongo vyake kule hospitali alipokuja kumwona,..
"sawa... Ila nenda kamwambie kuwa asije akiwa kalewa...."
"sawa... Unajua zena mi nataka uwe wifi yangu, afu unaliinga"
"sio hivyo dija... Tatizo kaka enu sjui kalelewa vipi yani"
"sasa wewe ndio unatakiwa uwe mama yake.. Mana anaonekana kakuja moyoni mwake we acha tu"
"kweli akibadilika,... Mimi sina tabu mana moyo wangu umetua pale ila tabia yake sasa ndio mbaya"
Zena aliongea huku akimtoa dija kama kumsindikiza
"sasa tabia hio wa kuikomesha ni wewe"
Basi dija aliondoka zake kisha zena akarudi dukani kwao na kuendelea na mauzo kama kawaida,...

Wakati huo hadija kafika nyumbani na kumkuta rahim anaangalia miziki kwenye TV, na alikuwa akiifurahia kweli miziki ya Bongofleva.... Ghafla hadija kaingia huku akicheka Cheka, rahim akahisi tu mambo yatakuwa mazuri huko
"Enheee dada dija kuna nini"
Heeeeee leo hadija kaitwa dada, haamini yaa saa hadi saa rahim anazifi kubadilika... Na hapo hajakunywa wiski zake wala wine, yaani toka alipokunywa jana ndio mpaka sasa hivi...
"mambo safi tu... Ila.. Kasema kuwa, ili mkutane, hutakiwi kunywa pombe, hataki unywe pombe kuanzia leo"
Hadija kaongeza chumvi, yeye kaambiwa akija aje akiwa hajalewa lakini hadija kaongeza chumvi kuwa, kuanzia leo asinywe pombe... Saa ngapi rahim hajaamka kwa hasira
"ati nini... Anikataze pombe akiwa kama nani.. Yeye ni nani yangu"
Sasa hadija kuona rahim kawa mkali, ikabidi anyooshe maelezo vizuri
"ah ah, kasema hivi ukienda hio jioni usilewe, hajasema uache pombe"
"sasa mbona ulisema, kasema niache kunywa pombe"
"nilikosea kaka"
Sasa kumbe jamali alikuwa ndani keshakuja, kusikia kila kitu
"haaaaaaaa... Sasa itakuaje"
Rahim aliongea hivyo huku akishika kichwa, kana kwamba ni kitu kigumu sana kwake
"kwani huezi kukaa hata siku moja bila kunywa kaka"
"kazi yako imeshaisha nenda kaendelee na kazi zingine"
Rahim alimuamuru hadija akaendelee na kazi.... Sasa dija alipoingia chumbani kwake alimkuta jamali,....
Kumbe jamali na hadija wana mahusiano,m ya kimapenzi wanapenda mno...
"we jamali umekuja saa ngapi huku"
"muda sio mrefu.. We ulikuwa wapi"
"nilipeleka ujumbe kwa zena... Sasa zena kaniambia nimwambie rahim aende wakakutane akiwa hajalewa"
Jamali alicheka sana kusikia hivyo, mana anamjua sana mdogo wake alivyo
"sasa unacheka nini baby"
"hadija.."
"abeee"
"unamjua bubu alivyo"
"ndio... Bubu si mtu ambae hawezi kuongea"
"sasa... Rahim asipokunywa pombe.. Yaani kuongea jambo kama hilo hawezi kamwe... Yaani hata mwanamke awe mzuri vipi... Kwanza hatoweza kumsalimia.. Cha pili anakuwa kainamiana kama kondoo.. Yaani asipokunywa anatia huruma huyo, we umuone hivyo... Hatokaa kwenda bila kunywa, hilo sahau, mana atakwenda kumchekea tu kama chizi"
"ivi unasema kweli jamali??"
"bila shaka huo ndio ukweli.... Na kama huyo mwanamke anampenda mdogo wangu... Basi nenda kamwambie kuwa amruhusu anywe hata glasi moja tu ya wine... Bila hivyo wataishia kusimama tu hapo walipokutana"

Je?... Itakuwaje??... Zena anaweza kumruhusu rahim anywe hata glasi moja ili atongozwe...

ITAENDELEA......
 
THE ISLAMIC WIFE

(Mke Muislamu)

Sehemu Ya 10

Mtunzi... MoonBoy

Simu No, +255714419487 WhatsApp

Ilipoishia Jana →→↓↓

Kumbe jamali na hadija wana mahusiano,m ya kimapenzi wanapenda mno...
"we jamali umekuja saa ngapi huku"
"muda sio mrefu.. We ulikuwa wapi"
"nilipeleka ujumbe kwa zena... Sasa zena kaniambia nimwambie rahim aende wakakutane akiwa hajalewa"
Jamali alicheka sana kusikia hivyo, mana anamjua sana mdogo wake alivyo
"sasa unacheka nini baby"
"hadija.."
"abeee"
"unamjua bubu alivyo"
"ndio... Bubu si mtu ambae hawezi kuongea"
"sasa... Rahim asipokunywa pombe.. Yaani kuongea jambo kama hilo hawezi kamwe... Yaani hata mwanamke awe mzuri vipi... Kwanza hatoweza kumsalimia.. Cha pili anakuwa kainamiana kama kondoo.. Yaani asipokunywa anatia huruma huyo, we umuone hivyo... Hatokaa kwenda bila kunywa, hilo sahau, mana atakwenda kumchekea tu kama chizi"
"ivi unasema kweli jamali??"
"bila shaka huo ndio ukweli.... Na kama huyo mwanamke anampenda mdogo wangu... Basi nenda kamwambie kuwa amruhusu anywe hata glasi moja tu ya wine... Bila hivyo wataishia kusimama tu hapo walipokutana"

ENDELEA........

Katika dunia wanaume tupo tofauti kabisa hususan katika upande wa kuongea na wanawake kwa nijia tofauti kabisa,... Kweli wapo watu hawajui hata kuongea na mwanamke mpaka azingue kichwa chake, sasa kumbe rahim ana tatizo hilo, ujanja wake woote, kumbe asipolewa anakuwa kama kondoo.... Dija alifikisha ujumbe kwa zena, na zena hakuwa na hiana, mana kaambiwa kama kweli unampenda basi wewe ndio ufanye kazi ya kumbadirisha... Heeee atabadirisha wote lakini sio rahim,....

Wakati huo rahim anaumiza kichwa itakuwaje asipopata hata grasi moja ya wiski, ili mdomo uwe mwepesi wa kuongea,... Wakati rahim akiendelea kuumiza kichwa ghafla simu yake inaita, kuangalia jina alikuwa ni baba yake
"haloo dady, shkamoo"
Alimsalimia baba yake huku akiwa na shauku ya kukutana na zena...
"Marahaba ujambo...... Sasa rahim, hebu nenda hapo bandari ya Tanga kuna jenereta limefika ulipelekea sehemu husika"
Aliongea baba yake, mana akina rahim wanadili na mambo ya usafirishaji wa mizigo au bidhaa za watu, hivyo kuna mzigo kutoka china unatakiwa kufika kwa wenyewe na kwakuwa rahim na jamali wapo tanga, basi ni rahisi kulifikisha kwa wahusika mana baba yao yupo kenya kuna biashara kaifuatilia....
"sawa dady"
Basi rahim alikubali kufanya kazi hio, na hapo hapo akawa anakwenda chumbani kwa kaka yake ambae ni jamali,... Lakini kabla hajaenda huko, alisikia sauti ya kiume kutoka chumbani kwa dija,... Saa ngapi rahim hajachungulia, alikuta kaka yake ananing'inia tu...
Rahim alikuwa hajui kama dija na jamali kumbe wana mahusiano ya kimapenzi,... Ikabidi atumie simu kumpigia... Alimweleza jinsi alivyoambiwa na baba yake,.. Lakini kwa utamu wa mapenzi jamali alikataa kwenda,.. Rahim hakutaka kupoteza muda, alichukuwa gari kisha akatembea mbele kuelekea bandarini,.. Ikiwa ni time ya saa kumi hibi za jioni, rahim anafika bandarini kila mtu anamshangaa mtoto mdogo afu ni tajiri, lakini hawajui kama ni mtoto wa mzee Rashidy, mana gari alioingia nayo hapo, ni kichefuchefu kwa matajiri wengine walioko hapo bandarini,....
Meli ilioleta mzigo ikiwa ndio kwanza inatia nanga,... Haraka haraka anapewa Documents za jenereta hilo ili kleni ianze kazi yake ya kulishusha,

"boss, clan ipo tayari, sasa gari ya kutolea hapa mpaka msikitini litakuwa wapi"
Rahim kusikia linakwenda msikitini, aliomba karatasi ya malipo
"unasema ni jenereta la wapi?"
"ni la msikitini boss"
"limeshalipiwa"
"aahhhh hapana ila litalipiwa mpaka likifika sehemu husika"
"ebu lete karatasi ya charging"
Akapewa karatasi ambayo ni Way Bill ya malipo,...
"khaaaaaa.... Mbona wamechajiwa pesa ndogo hivi?... Nani kachaji hii mashine"
"mzew wako"
"hapana.... Hii pesa ni ndogo sana, haliwezi kitoka china mpaka hapa.. Afu lilipiwe milioni mia moja tu?... Haiwezekani"
Rahim alimpigia baba yake simu, wakati huo mashine inashushwa kuingia katika gari
"Eeenn haloo dady... Mbona hii mashine imesafirishwa kwa gharama ndogo hivi"
"rahim.. Hio ni mashine ya msikitini"
"lakini dady... Kwani kuna siku tulishawahi kula au kulala msikitini"
Rahim alikuwa hajui kama kuna cha nyumba ya ibada wala nink, yaani yeye anachotaka ni hela tu,... Hajuagi neno msaada, hajui neno kutoa sadaka, yaani yeye yupo yupo tu
"ok.. Ebu we fanya hilo unalohisi ni sawa"
"eew hilo ndio jibu sasa.... Huu mzigo ni wa milioni 200 huu.... "
"ok... Sawa.. Afu waambie hao vijana wakupatie pesa ya mwezi mzima.. Kisha uipeleke benki"
"sawa"

Sasa kule kwa pembeni kuna watu waliokuwa wakishangaa ni mtu gani huyu asiejua mambo ya dini, hajui hana jambo la kutoa sadaka kwa watu,...
"huyu ni tajiri gani tena... Ama kweli wahenga walisema kuwa tajiri ni ngumu kuingia kwenye tundu la sindano...... Eti rehema huyu ni nani"
Ni wanawake fulani waliokuwa nao wamejitanda Kiislamu wamevalia nikabu zao saafi Kabisa,
"huyu si mtoto wa mzee rashidi.."
"mzew Rashidy huyu huyu mwenye hio meli iliosimama hapo"
"ndio... Huyu ndio mtoto wake wa pekee"
Aliongea mwanamke huyo kuwa rahim ni mtoto wa pekee kwenye hio familia, hawajui kama kuna jamali,..
"lakini mbona baba yake mkarimu sana kuliko mtoto... Hebu ona mashine inakwenda kufanyia kazi za ibada, lakini yeye halijui hilo"
"sikili shamy,...huyu mtoto naskia amelelewa vibaya mno, yaani ana dharau huyo"
"mmmhhh au labda atazikwa na pesa zao"

Watu walikuwa hawaamini kwa kitendo anachokifanya rahim,.. Rahim alichukuwa kitabu cha kuandikia way bill kisha akaandika upya kuwa inatakiwa ilipiwe milioni mia mbili na sio milioni mia moja kama ilivyoandikwa awali..
"alafu hashim... Mzee kaniagiza unipatie pesa za transport za mwezi mzima"
"sawa boss"
Hashim alikimbia haraka mpaka ndani ya meli hio ya mzee Rashidy,... Kweli akina rahim ni matajiri haswa lakini pesa zao hazina faida kwa jamii, tena ndio kwanza mtoto mtu ananyanyasa walala hoi...
Begi la pesa lilitolewa utafikiri kuna nguo humo nfani, kumbe ni pesa zote
"boss... Hizi hapa"
"sasa unanipa nibebe mimi au? Peleka kwenye gari huko"
Aliongea rahim, yaani rahim yupo kidikteta zaidi, na hakuna wakumsemesha mana yeye ndio mbadala wa baba yake, au kaka yake jamali,...
"boss, huezi kuzihakikisha tu"
"ivi we hashim una akili kweli wewe... Yaani begi lote hilo mimi niliesabu, huo muda anao nani... Peleka begi ndani ya gari.. We niambie ni kiasi gani"
"ni bilioni 7 pointi 4"
"sasa bilioni saba, naanzaje kizihesabu kw mkono.... Safari za maji zinakupunguza akili wewe"
Basi hashim aliingiza begi hilo la pesa ambazo zimepatikana kwa njia ya usafirishaji wa mizigo au bidhaa mbali mbali za watu... Hivyo hizo ni ingizo la mwezi mmoja kwenye meli hio moja... Bado kwenye magari makubwa yanayosambaa mikoani na nje ya nchi... Bado hizo sheli walizonazo.. Bado wana supermarket mbili... Arusha na Dar es Salaam,.. Lakini sasa pesa zao zinajaa tu benki hazina hata faida, na mtu mbaya zaidi ni rahim anaetaka pesa zijae tu benki... Unaambiwa kwa Tanzania mzee Rashidy ndio anaongoza kwa pesa, lakini hatangazwi na wala hajulikani... Basi rahim aliondoka na mashine hio kuelekea sehemu husika

Sasa huku kwenye makutano kati ya zena na rahim.... Maskini ya mungu zena yupo chini ya mti akimsubiri rahim aje, wakati huo ni mida ya saa 12 za jioni zena alikuwa anakwenda madrasa,... Sasa akaona akutane na rahim kisha aondoke,.. Lakini kakaa weee, haoni mtu,.. Mpaka zena akachoka kukaa, ikabidi aondoke lakini alikuwa kakasirika mno, na wala hataki kuskia jambo la rahim tena,..
Sasa zena alipofika mbele alikutana na dija anatoka dukani
"we dija wewe... "
"heeeee zenaaa... Pole rafiki yangu, najua utakuwa umemsubiri eti eeeh"
"sana tu yaani, yaani mpaka nimechoka"
"mwenzangu weee... Kilichomfanya asije ni kwamba... Kumbe asipolewa hajui hata kuongea yaani ni kama bubu unaambiwa"
"heeeee, yaani asipolewa hawezi kuongea"
"yaani sio kuwa hawezi kuongea... Yaani namaanisha ukikutana nae naskia atainamisha tu kichwa chini kama kondoo"
"mmmhhhhh, basi.. Na mimi kukutana na mlevi Kiukweli siwezi, tena mwambie anikome kabisaa"
"heeeeeee zenaaa... Yamekuwa hayo tena"
"lakini dija... We si unajua ukali wa wazazi wangu wewe... Hivi leo niwe na mahusiano na yule kaka yenu, itakuwaje, si nitauwawa mimi..."
"basi humpendi kala etu"
"dija Usiseme hivyo,.. Nampenda sana tu, lakini tabia yake hakuna mtu anaipenda Kiukweli"
"mmmhhh we haya bwana.. Kwaheri, lakini kaa ukijua wakumbadirisha mi wewe na sii mwingine... Na kama unampenda mruhu ukutane nae hata kama kalewa, akutaamkie tu anakupenda we mkubalie.. Kitakachofuata hapo ni kumkataza yale yasio faa"
Aliongea hadija kuwa zena akubali tu akutane nae hata kama kalewa kikubwa yu ni mataamshi yakamilike
Zena hakumjibu kitu aliweka juzuu zake katika begi, mana alikuwa akijisomea pale alipokuwa akimsubiri rahim...

Sasa kumbe ile mashine au jenereta linapokwenda ndio hapo hapo anapokwenda kisomea au kiswalia zena,.. Wakati huo zena wapo rosheni ya juu, mana ndio upande wa wanawake, na chini ni wanaume.. Ulikuwa ni msikiti mkubwa sana mkoani Tanga, na ndio ulioagiza jenereta kutoka china,.. Kweli palikuwa na mshekhe wakubwa, mawalii wakubwa wakubwa... Mamufti wale wenye makarama yao, Waislamu wazito wazito hivi waliokuwa wakilisubiria jenereta hilo

Mashekhe hao walimkaribisha rahim kwa furaha, wakizani ni. Mtu mwema kumbe ni kishetani cha duniani,..
"As Salaam Aleykum warahmatullah wabarakatuh"
Walimsalimia rahim karibia mashekhe wote... Tena huku akipewa na mikono ya baraka,...
"safi tu, mambozenu"
Heeeeeeee mashekhe walishangaa huyu ni kijana wa wapi, tena ni Muislamu lakini hata kuitikia salamu ya Kiislamu hajui,.. Tena mabaya zaidi anawaambia MMBOZENU? Mashehe walipiga astah khafirulah wote, lakini rahim haelewi kitu, Wakati huo zena anaona chini lakini hajui kama ni rahim, waumi walikuwa wakifurahi kwa jenereta hilo kufika, mana umeme unapozimika hua wanakosa mawaidha mazuri yatolewayo na Mashehe wao,.. Sasa rahim akawapa ile karatasi ya malipo, Mashehe walishangaa kuona kiasi cha malipo kimekuwa kikubwa zaidi,
"shekhe jumaa, mbona milioni mia mbili badala ya mia moja"
Mmoja wa mashekhe alimuuliza shekhe mwenzie, na wakati huo sasa kumbe hata baba yake na zena nae ni mmoja wa mashekhe hao... Alipomuona ni huyo kijana, aliona hapa ipo shuhuli pevu,...
"huyo kijana ni mshenzi sana.. Yaani hapa hio mashine haitoshuka bila hio pesa kutolewa"
Aliongea baba yake zena, aliokuwa kavalia kanzu yake saafi na kibaraka shehe,..
"kwani we unamjua huyu kijana"
Wakati huo rahim yeye yupo kwenye gari yake anasikiliza muziki wa Bongofleva, tena kwa sauti bila kujali kuwa hapo ni msikitini,.. Palitakiwa kuwa na heshima,..
"ndio... Tena ndio aliowahi kunigongea mtoto wangu yule mdogo... Afu mbaya zaidi nikaanza kumuona analeta ukaribu na binti yangu"
"mmhhhhh sasa hii pesa mbona ni kubwa,.. Pesa yenyewe tumeichangisha ndani ya miezi 6 ikapatikana hio milioni mia moja.. Haya hii mia moja ilio ongezeka hapa tunaitoa wapi"
Mara rahim katoka ndani ya gari,
"jamani vipi... Nipatieni pesa mchukuwe mzigo wenu... Mimi nikajua mnazihesabu kumbe mnang'aa macho tu"
Baba yake zena alikuwa anatikisa kichwa tu, kana kwamba anayoyafanya huyu kijana, hata shetani hafanyi hivyo,... Sasa kule juu zena keshamjua kuwa ni rahim,.. Huezi amini zena alikuwa analia, mana rahim hajui umuhimu wa mashine hio,..
"zena, ivi unajua kuwa rahim anakupenda sana"
Aliongea fadhila huku akitaka kumshawishi akatoe neno pale chini

Wakati huo mashekhe wanarudisha karatasi ya malipo, ikiwa na maana ya kwamba wameshindwa kulipia hizo gharama, japo na pesa yenyewe ya kulinunua imechangishwa ndani ya miaka mitano, na bado hawajamaliza kulilipia jenereta hilo, mana ni yale majenereta makubwa ambayo umeme ukikatika linajiwasha wenyewe,.. Majenereta yanayotakiwa kukaa katika hospitali zote, nyumba za ibada iwe kanisani au msikitini,... Rahim alimwamuru dereva ageuze gari waondoke zao,.. Wakati huo fadhila bado anazidi kumshawishi zena, akajaribu kumkubalia huenda akaliacha
"fadhila... Baba yule pale chini, nitawezaje kufanya hivyo... Na istoshe rahim hakosi bunduki yule,.. Akiniua je?.. Hapana bora waondoke tu, kwanza simtaki tena"
Aliongea zena kwa uchungu huku machozi yakimtoka kwa wingi sana,.. Na Wao walikuwa wakiangalia kwa chini, yaani akina zena wapo rosheni ya juu, sasa wanaangalia chini... Kweli rahim mtoto wa Kiislamu aliokosa utu, anadiriki kugeuza gari lake na gari ilioleta jenereta igeuze waondoke nalo mpaka watakapolilipia waje walichukiwe,... Kama unavyojua vilio vya wamama wanaoijua dini,...
Sasa hapo hapo madrasa ya wanawake, pia mama yake zena yupo, mana hio ni familia ya Kiislamu, hivyo wote wanajua wajibu wao juu ya kujua maandishi ya Mwenyezi Mungu,... Fadhila alimkimbilia mama yake zena kule kwa wamama...
"mama zena... Mshauri zena aende akamzuie yule kijana"
"weeeee weee, unataka mwanangu aingie matatizoni... Yule mtoto nimesikia sifa zake ni mbaya"
"mama... Kumbuka jenereta lina umuhimu sana hapa msikitini... Kwanini asifanye hivi"
Aliongea fadhila na wakati wamama wanalalamika kweli kwa kitendo cha rahim kukosa hata ile staha ya ubinaadamu,...
"sasa zena ni nani yake mpaka aweze kumzuia"
"rahim, anampenda sana mwanao, yaani anampenda mno"
"ati unasemaje wewe.... Yaani mwanangu apendwe na yule kafiri, tena kanigongea mtoto wangu kamtia kovu la maisha"
Sasa fadhila kugeuka nyuma, hamuoni zena....

Wakati huo huku chini magari ndio yanaondoka,... Ghafla mzee mvungi au baba yake na zena, anashangaa kumwona zena akiwa kasimama katikati ya barabara... Tena huku gari zikiwa na mqendo mzuri tu... Mzee alitamani kupaa mpaka pale,... Zena kapiga moyo konde, na rahim akisimama tu basi lazima kieleweke, lakini asiposimama basi mashine itakwenda na jinsi ya kuipata hakina, labda wajichange tena kwa mwezi 6 kama ilivyo ya awali.. Sasa mama ndio nae anashangaa kumuona zena kasimama katikati ya barabara, eti anazuia hizo gari zisiondoke... Sasa hapo kinachoangaliwa ni upendo bali sii kingine....

Je? Nini kitaendelea?..... Zena atafanikiwa kumzuia rahim??... Na je Rahim atakubali kuacha jenereta bila pesa???..... USIKOSE

ITAENDELEA...
 
THE ISLAMIC WIFE

(Mke Muislamu)

Sehemu Ya 11

Mtunzi... MoonBoy

Simu No, +255714419487 WhatsApp

Ilipoishia Jana →→↓↓

"weeeee weee, unataka mwanangu aingie matatizoni... Yule mtoto nimesikia sifa zake ni mbaya"
"mama... Kumbuka jenereta lina umuhimu sana hapa msikitini... Kwanini asifanye hivi"
Aliongea fadhila na wakati wamama wanalalamika kweli kwa kitendo cha rahim kukosa hata ile staha ya ubinaadamu,...
"sasa zena ni nani yake mpaka aweze kumzuia"
"rahim, anampenda sana mwanao, yaani anampenda mno"
"ati unasemaje wewe.... Yaani mwanangu apendwe na yule kafiri, tena kanigongea mtoto wangu kamtia kovu la maisha"
Sasa fadhila kugeuka nyuma, hamuoni zena....

Wakati huo huku chini magari ndio yanaondoka,... Ghafla mzee mvungi au baba yake na zena, anashangaa kumwona zena akiwa kasimama katikati ya barabara... Tena huku gari zikiwa na mqendo mzuri tu... Mzee alitamani kupaa mpaka pale,... Zena kapiga moyo konde, na rahim akisimama tu basi lazima kieleweke, lakini asiposimama basi mashine itakwenda na jinsi ya kuipata hakina, labda wajichange tena kwa mwezi 6 kama ilivyo ya awali.. Sasa mama ndio nae anashangaa kumuona zena kasimama katikati ya barabara, eti anazuia hizo gari zisiondoke... Sasa hapo kinachoangaliwa ni upendo bali sii kingine....

ENDELEA.........

Sasa tunataka tujue zena alikubali vp kwenda kufanya tukio lile, na wakati alibembelezwa na fadhila lakini akakataa katu katu,.. Sasa kama unakumbuka saa ile fadhila anakwenda kwa mama yake na zena kumwambia amwambie mwanae akajaribu kuzuia jenereta lisiondoke, mana anachokifanya yule kijana sio kitu kizuri katika nyumba ya ibada kama hio, ni mtu gani asiojua dini.. Sasa fadhila alipoondoka, kuna wamama watatu wenye heshima zao na wao walikuwepo madrasa hapo wakijifunza mambo mbalimbali ya qur-aan.. Walimsogelea zena huku wakimwambia kuwa
"tumesikia kuwa yule kijana anakupenda sana, na sisi ni watu wa zamani.. Na kidini hairuhusiwi mwanamke wa Kiislamu kuolewa au kiwa na mahusiano na mwanaume kafiri... Yule kijana ni dhahiri kuwa ana imani ya kikafiri yule... Lakini kama nawe unampenda na yeye anakupenda,... Basi jaribu kufanya hili zoezi, na ukifanikiwa, basi kuna uwezekano mkubwa huyu kijana kutulia... Tunakuomba mtoto wetu yule ni shetani tu anampitia, hebu jaribu upendo wako"
Aliongea mama mmoja mwenye busara zake,...
"ni kweli,.. Kama mtu ana uwezo wa kubadirika basi basi hakuna tatizo katika dini"
Aliongea mama mwingine mwenye busara zaidi
"sisi kama watu wazima tutakuwa nawe bega kwa bega lakini kile kifaa kisiondoke hapa msikitini, hata Mwenyezi Mungu atakufungulia milango ya baraka juu yak"
Huyu ni mama mwingine kana kwamba wote watatu jambo lao ni moja

"mama zangu, kweli natamani kufanya hivyo, lakini wazazi wangu... Hawataki niwe na huyu kijana"
"sisi tupo juu yako... Swala hili tuachie sisi"
Zena akiwaangalia wale wamama ni watu wazima na hekima zao, afu msikiti mkubwa sana yaani tanga yote, msikitini mkubwa zaidi kuliko yote tanga nzima ni huo, ambao una kila kitu ndani yake... Kina madrasa ya watoto, kuna madrasa ya watu wazima, na pia kina madrasa ya bijana wakubwa kama akina rahim, kuna ukumbi wa kufungishia ndoa za Kiislamu, kuna sehemu kubwa sana za kuswalia,... Yaani ni jengo kubwa sana na linahitaji kifaa kama hicho kwa nia ya kutokatiza mawaidha au wakati wa kuswali pindi umeme unapokuwa umekatika.... Zena kweli aliwasikia na kunyanyuka, alikuwa juu ya ghorofa lakini alishuka na kwenda kusimama katika kati ya barabara, huku juu fadhila anageuka hamuoni zena,... Mama nae hamuoni mwanae, wote sasa wakawa macho chini kuangalia kile anachokifanya zena,.. Sasa huku chini baba mtu kaona mtoto wake anachokifanya, mzee mvungi hataki utani na familia yake,... Alinyanyuka katika kiti na kutaka kwenda kimzuia, lakini hawa mashekhe wengine, wanajua upendo ulivyo, kwahio walimzuia kwanza shekhe mvungi ili waone matokea juu ya mtoto wa kike.... Na hapo kinachoangaliwa ni upendo na sii kingine

Rahim kweli alisimamisha gari yake, mana yeye ndio alikuwa mbele na lori lenye mashine lipo nyuma yake akiliongoza,...
"we unataka kufa mbele za watu"
Zena kuskia hivyo aliogopa mno, lakini akajikaza tu, mana mpaka kitendo cha kusimama ni dhahiri kuwa anamuheshim sana zena, mana uwezekano wa kumkwepa ulikuwepo mkubwa sana lakini rahim hakutaka kumkwepa...
"bora uniue kuliko kuondoka na kitu kitakachoweza kusaidia umati wa watu.... Hebu angalia watu wote hao, wanatamani uache hilo jenereta, lakini kwa ulivyo na roho mbaya kqeli unaondoka nalo.. Huna hata aibu rahim, wewe ni Muislamu wa nchi gani wewe,... Kwani pesa ni kitu gani"
Wakati huo zena akiyaongea hayo mama kule juu anatetemeka kwa woga, mana ni familia ambayo haina kitu lakini anakwenda kuongea maneno makali mbele ya mtu mwenye kitu, ni kuji risk maisha... Lakini sasa kumbe alichokisema jamali kuwa rahim asipolewa na kukutana na mtu ampendae hua haongei,... Sasa zena akawa anasubiri jibu,... Lakini kabla ya kujibiwa akakumbuka maneno ya dija kuwa
"mmmhhh zena... Kumbe rahim asipolewa anakuwa kama kondoo mbele ya mwanamke anaempenda"
Alipokumbuka hilo, zena alisogea karibu na rahim kisha akamshika mkono, rahim kumbe kweli anampenda zena, japo hatujui kama ana nia gani kati ya kuoa au kichezea tu,...
"rahim.... Kama unanipenda kweli, utaiacha hii mashine... Lakini kama hunipendi basi ondoka nayo"
Zena Aliongea hivyo kwa ujasiri huku akiamini kuwa hapa hakuna lolote,..
"Samahani kaka, naomba mshushe hio mashine"
Aliongea zena, lakini wale watu walishindwa kifanya hivuo mana wanasubiri kauli kutoka kwa boss,..
"rahim, waamuru basi watu wako"
Rahim alinyoosha tu kidole juu kisha akaonyeshea chini, maana yake jenereta lishushwe.... Waumini wote hawaamini, huezi amini hata zena alikuwa analia kwa furaha,..
"rahim,... Naomba jioni tukutane kama ulivyotaka.... Lakini Please nakuomba ukija usije ukiwa imelewa sana, kidogo tu inatosha ili tu uongew na mimi.... Ahsante kwa kinielewa"
Zena alimruhusu rahim aje akiwa kashtua kidogo, mana kama atakuja akiwa hajashtua basi hakuna atakacho ongea, yaani hata neno nakupenda kwake ni zito,.. Na hii watoto wa matajiri ndivyo walivyo asilimia chache kutongoza hawajui, wanajivunia pesa zao tu,... Sasa sehemu ambayo haitumii pesa, wanapata shida mno....
Na zena kumruhusu ashtue haina maana anywe kila siku No, bali alimwambia ashtue ili aweze kumtaamkia hata hio nakupenda tu inatosha, mana asipokunywa hatoweza kuitaamka... Na rahim anakuwa domo zege mbele ya mwanamke anaempenda lakini kwa mwanamke ambae hana hisia nae,.. Doooohhh utasemwa wewe mpaka ukimbie... Zena aliondoka na kwenda kwenye ile mashine, wasichana wenzake walimpongeza, wamama walikuwa wakilia kwa furaha ya mashine hio, mana waliichangia kwa miaka kadhaa iliyopita mpaka pesa ya kununulia ikapatikana,... Na hapo bado haijaisha kulipwa sema wachina nao sjui waliona huruma kwa kuwauzia kwa pesa nusu...

Mzee mvungi haamini kama mtoto wake ndio sababu ya mashine hio kubaki, tena sasa uzuri zaidi hata ile milioni mia moja ilioandikwa na baba yake haijachukuliwa, maana yake ni kwamba imesafirishwa bure mapaka hapo, lakini ni kwa nguvu za zena,..

Akina rahim na timu yake ya kwenye meli waliondoka zao, ila rahim yeye alielekea benki kuweka maingizo ya meli,... Mashine imeletwa na ndege mpaka mahali fulani ndio ikapakiwa kwenye meli mpaka Tanzania,.... Wakati huo sasa huku madrasa mama mtu anafuta jasho utafikiri ni yeye ndio kafanya ile kazi,..
"mama zena,.. Kweli pale kuna upendo wa hali ya juu... Kikubwa ni kwamba mwacheni mtoto wenu afanya atalo"
"hapana mama salma,.. Yule kijana hawezi kuwa na mtoto wangu.. Sitaki"
Zena akisikia hivyo anatamani hata kulia
"hapana mama zena... Yule kijana kuna uwezekano mkubwa kubadirika.. Kikubwa mtoto wako ajitambue tu yupo katika hali gani"
"sawa, lakini yule kijana sio Mtu eti"
"hio kazi mwachie mtoto wako... Kikubwa tu we mpe ruksa"
Mama yake zena hakujibu chochote kile na hata kule chini mzee katuliza mzuka baada ya mashine kubaki kwa nguvu za mtoto wake, rahim kweli ni ibilisi sio mchezo....

Ikiwa ni mida ya saa mbili kasoro usiku, rahm akiwa nyumbani kwao, na wakati huo alikuwa anachapa grasi za kutosha, na kuambiwa ashtue tu, ili akataamke tu kuwa anampenda, mana mwanamke kuanza kumwambia mwanaume kuwa anampenda, ni jambo gumu sana kwao, na pia sio maadili ya mtanzania kwa mwanamke kumtaamkia mwanaume kuwa anampenda,... Lakini zena anampenda kweli sema tabia za rahim sio nzuri...
"bibi, eti mjukuu wako anakunywa ili akakutane na mwanamke"
Jamali aliongea hayo kana kwamba anamkandia rahim,
"hata huyo mwanamke mwenyewe hana akili, kama ni mimi sikutani na mlevi"
"bibi, afu huezi amini ni yule mdada mweupe pale mtaa wapili"
"nani huyo.."
"kuna kabinti keupe kanapita pata hapa nje"
"au ni yule mtoto wa mzee mvungi"
"atakuwa ndio huyo.. Anapenda kuvaa nikabu hivi"
"sasa yule binti na huyu mwehu wapi na wapi"
"nashangaa mimi"
Jamali na bibi yake walikuwa wanamsema rahim
"sasa wewe, na huo usharobaro wako na mtoto wa watu mshika dini... Unataka kumpotosha au... Hebu ona huona huo mkofia aliovaa..."
"bibi, kila siku mi namuambia huyu mjukuu wako, haendani na yule binti hataki kusikia"
Wakati huo rahim yeye anaongeza vigrasi vya wiski, wakati aliambiwa ashtue tu lakini anakunywa grasi za kutosha...
Alipomaliza wala hakuongea na mtu, huyoo, tena hatumii gari wala nini, mguu wake, na wakati huo vinywaji bado havijamkolea vizuri katika mwili, mana kabigonga sasa hivi tu...
Kweli alipofika mahali chini ya mti alimkuta zena akiwa kasimama... Mtoto kanyooka kila kona tukiongelea uzuri ndio kabisaa hatusemi kitu...
"umevaa zile nguo zako tena.. Sa ntakuonaje"
Aliongea rahim, na wakati huo sasa pombe imeanza kukolea ukilinganisha na vile alivyotembea, ndio kabisaa imempa joto
"rahim... Mi sijakwambia unywe hivyo"
"kwani kuna shida gani"
"usiniguse... We ongea hapo hapo"
"lakini si uliniambia wewe au hukumbuki"
"rahim... Niamnie basi mi niende"
"sa mbona uko mbali ivo"
Zena hakuwa na hamu tena ya kukutana nae mana hakumwambia alewe hivi, sasa kaja kalewa sana, kana kwamba mpaka zena anaona kero,...
"kwani wataka nini kwangu"
Aliongea zena japo anajua kile anachokitaka rahim,
"zena, ivi ni mwanaume gani utakaempata na anaekupenda kama mimi... Kiukweli nilikuwa nachukia sana watu wanaovaa mavazi ya kufunika macho... Lakini toka nikutane na wewe nimeona ni kawaida tu... Zena??... Nakupenda eti"
Zena alisikia kwa masikio yake akitaamkiwa kuwa anapendwa,... Tabasamu zito lilimjia zena,.. Unajua kuambiwa unapendwa sio jambo dogo eti
"rahim... Nimekuelewa viziri tu... Na sio wewe tu, hata mimi Pia nakupenda... Lakini sasa kwa tabia yako ya kwenda baa, mi siwezi kuwa na wewe"
"zenaaaa.... Mi nanywea nyumbani"
"sasa sikia.... Kama kweli wewe unanipe..... "
Sasa kabla zena hajamalizaa kuongea, alishangaa kumwona baba yake akiwa nyuma ya rahim,... Sasa rahim yeye hajui na kule kulewa ndio kabisaa haelewi,... Zena katulia tu wala hasemi,
"yaani umevua mpaka nikabu kwa ajili ya huyu mtu....."
Aliongea mzee mvungi na hapo rahim ndio akajua kumbe nyuma yake kuna mtu,...
"aaahhhh dingi.. Mambo Vipi"
Rahim aliita na kumsalimia mzee huyo, wakati huo zena anamkataza rahim asiongee lolote,..
"ngoja niongee na baba mkwe"
Wakati huo rahim pombe ndio zimemzidi kichwa
"ivi mwanangu... Katika kutafuta kwako koote, umemuona huyu"
Aliongea mzee huku rahim akidakia juu kwa juu
"aahhhhh mzee, kwani mimi sio mtu?"

Je? Mzee atafanya nini hapo???... Na je? Vp kuhusu zena,???? USIKOSE

ITAENDELEA...
 
THE ISLAMIC WIFE

(Mke Muislamu)

Sehemu Ya 12

Mtunzi... MoonBoy

Simu No, +255714419487 WhatsApp

Ilipoishia Jana →→↓↓

"zena, ivi ni mwanaume gani utakaempata na anaekupenda kama mimi... Kiukweli nilikuwa nachukia sana watu wanaovaa mavazi ya kufunika macho... Lakini toka nikutane na wewe nimeona ni kawaida tu... Zena??... Nakupenda eti"
Zena alisikia kwa masikio yake akitaamkiwa kuwa anapendwa,... Tabasamu zito lilimjia zena,.. Unajua kuambiwa unapendwa sio jambo dogo eti
"rahim... Nimekuelewa viziri tu... Na sio wewe tu, hata mimi Pia nakupenda... Lakini sasa kwa tabia yako ya kwenda baa, mi siwezi kuwa na wewe"
"zenaaaa.... Mi nanywea nyumbani"
"sasa sikia.... Kama kweli wewe unanipe..... "
Sasa kabla zena hajamalizaa kuongea, alishangaa kumwona baba yake akiwa nyuma ya rahim,... Sasa rahim yeye hajui na kule kulewa ndio kabisaa haelewi,... Zena katulia tu wala hasemi,
"yaani umevua mpaka nikabu kwa ajili ya huyu mtu....."
Aliongea mzee mvungi na hapo rahim ndio akajua kumbe nyuma yake kuna mtu,...
"aaahhhh dingi.. Mambo Vipi"
Rahim aliita na kumsalimia mzee huyo, wakati huo zena anamkataza rahim asiongee lolote,..
"ngoja niongee na baba mkwe"
Wakati huo rahim pombe ndio zimemzidi kichwa
"ivi mwanangu... Katika kutafuta kwako koote, umemuona huyu"
Aliongea mzee huku rahim akidakia juu kwa juu
"aahhhhh mzee, kwani mimi sio mtu?"

ENDELEA........

Hakuna kitu kibaya kama ulevi, kwasababu ulevi hua hautambui umuhimu wa mtu aliopo mbele yako, kila mtu kwako ni sawa tu, sasa rahim kasimama na baba mkwe lakini anamuona kama mshikaji mwenzie tu, na hata majibu anayomjibu sio ya heshima kama inavyotakiwa,...
"wewe kijana mbona ni mdogo sana lakini mambo yako ni ya kikafiri tu"
Aliongea mzee mvungi, huku rahim anatikisika tu kwa ukali wa kinywaji alichokunywa,..
"mzee, pesa.... Kuna kitu kinashinda pesa hapa duniani"
Mzee aliona kusimama na huyu mtu ni sawa na kumsapoti tu
"sikiliza we kijana.... Sitaki ufuate mtoto wangu, sema nimepunguza hasira kwa kile ulichokifanya kule msikitini japo ni kwa nguvu ya mwanangu, lakini... Sitaki tena nikuone nae"
"ah ah, mzee kwani tatizo nini... Hela au?"
"siuzi mtu"
"mi nataka kuoa eti"
Zena kuskia rahim kataamka neno nataka kuoa, alishangaa, mana walevi au masharobaro hua hawaoagi,..
"kwa hali hii utamuoa nani.. Pumbavu wewe"
"aahhh mzee ume mind sio"
"kwenda zako... Zena... Sitaki kukuona na huyu mtu..."
Zena hakujibu chochote kwa baba yake,... Rahim aliachwa peke yake pale chini ya mti, lakini ukweli keshauongea kwa zena, na zena keshajua kuwa anapendwa na rahim tena sana tu,... Sasa ile anataka kuondoka ghafla anakutana na fadhila nae alikuwa anatoka zake dukani, mana fadhila na zena hawapo mbali sana, fadhila alisharudi nyumbani na kubadili mavazi yake, na fadhila yeye ni mtoto wa Kiislamu lakini yeye malezi aliopewa ni malezi ya kawaida tu, yaani ni kama rahim, sema tu kidogo fadhila anaifuata dini, na fadhila yeye anawajua wanaume haswa,.. Wakati huo rahim kaachwa peke yake na fadhila yeye alikuwa akipita tu, na hakutegemea kumkuta ram maeneo yale,...
"heeeee rahim mambo"
Wakati huo rahim pombe imezidi kumkolea kichwani mana pombe za matajiri hua hazipandi haraka, ikiwa na maana kuwa kama mtu huyo kainywea mjini, hivyo kitendo ha kutoka mjini kwenda kwake, kinawezekana hata kama anaendesha gari, hio sio kiroba wakati huo huo uko tilalila, sasa rahim huezi amini yani na ile pombe hata kusimama vizuri sio kivile, mana kanywa grasi nyingi sana,..
"powa kwani we nani"
Aliongea kwa sauti ya ulevi huku akipiga hatua moja mbele, hatua mbali nyuma, kana kwamba hapo haendi mtu,...
"jamani ni mimi fadhila"
"fadhila yupi Uyooooo"
"mmmhhhh afu rahim umelewa wewe"
"we unamjua aliolewaaaaaaa"
Rahim alipomaliza tu kuongea alizidiwa na kuanguka chini,.... Mpaka hapo hakujua kilichoendelea

Kesho yake asubuhi rahim anaamka nyumbani kwao,.. Alikuwa akijivuta sana afu kidogo kawa mwepesi lakini alikuwa kachoka mno,.. Ilikuwa ni mida ya saa nne hivi za asubuhi,..
"vp broo"
Alimsalimia kaka yake aliokuwa anaangalia tv huku akinywa chai
"poa niaje"
"freshi tu......daahhh sjui leo wachawi wamenilimisha leo"
"wapi hao.... Hao wavaa kanzu na nikabu au?"
Aliongea jamali mana rahim wachawi wake hua ni Waislamu, yaani Muislamu kwake ndio mchawi... Kweli pesa ina dharau sana...
"ah ah, broo sijasema kuwa Waislamu ndio wamenilimisha, afu ilo swala naomba life, mana ukisema wachawi ni hao, basi hata zena wangu ni mchawi"
Sasa rahim aliposema zena,... Jamali kuna tukio kalikumbuka
"ahahahahaha kumbe yule aliokuleta jana ndio zena"
"nani kanleta jana??...mimi si nilikuja mwenyewe"
"we bwege nini... Si uliletwa hapa na mdada maji ya kunde hivi sjui mweupe mi sijui.. Kakuleta hapa saa saba za usiku"
"saaa saba???.... We umeota wewe.. Siamini kumbe hata wewe unaotaga"
Rahim alikataa kuwa jana aliletwa na mtu, tena mwanamke...
"aahhhhh niache bwana nikaoge"
Sasa alipokuwa anakatiza kona kwenda kuoga, alikutana na dija nae anatoka kuoga, si unajua wadada wakitoka kuoga wanakuwaje,.. Rahim katoa macho, macho nayo hayajatosheka, ikahamishiwa kwenye ubongo, ubongo nao haujatosheka, ikahamishiwa kwenye damu, damu nayo haijatosheka ikapeleka kule chini, kule chini nako hakujatulia,... Na hapo ndio rahim anagundua kiungo chake kilikuwa kikiuma baada ya kusachi network,...
"sasa ram, unamwangalia dija humjui"
Jamali aliongea kwa hasira mana dija na jamali wana mahusiano ya kimapenzi hivyo rahim alipokuwa anamwangalia dija, jamali alichukia sana kana kwamba labda rahim alimtamani...
"Samahani broo... Ila mbona kiungo changu kinauma"
"sasa unamwambia nani... Jana ulipokuja saa saba hapa afu unasema kiungo chako kinauma"
"broo, mi sijafanya kitu jana... Afu jointi zote zinaniuma"
"nennda zako kaoge uko, afu hujaoga kabisa jana"
Rahim aliingia zake bafuni lakini kweli anajihisi kuchoka, japo kaka yake anamwambia jana kuletwa saa saba za usiku,... Na hata kama kaletwa muda huo kwani kuna ulazima viungo vyake vijiskie kuchoka
Sasa alipoingia bafuni alivuta kumbukumbu ya jana, lakini kila akivuta inaishia pale pale zena alipo ondoka na baba yake, kwahio hakumbuki kuwa, baada ya hapo alikutana na fadhila,...
"au zena alirudi nini... Mbona broo anakazania nililetwa na mwanamke"
Rahim alijiuliza na asipate jibu sahihi,
"huyu broo atakuwa sio mzima huyu.... Lakini sasa mbona nimechoka utafikiri nililala na mwanamke?"
Rahim alijikuta hata kuoga anachelewa kwa kuwaza maumivu ya viungo vyake, na maumivu hayo ni dhahiri kuwa jana alikuwa na mwanamke
"ahahahahhahahah... Zena mjanja sana, yaani kajifanya kaondoka afu karudi... Mmhhh lakini kanikwangua mno"
Rahim alipata jibu kuwa ni zena ndie alie mpeleka nyumbani, lakini sisi wasomaji tunajua mtu wa mwisho kukutana na rahim ni fadhila, hivyo kama anahisi kitendo kama hicho basi ni fadhila
Rahim alimaliza kuoga, kisha akarudi mezani kupata chai,.. Wakati huo inakwenda saa sita mchana, lakini wao ndio wanakunywa chai,... Ghafla simu ya rahim iliita,... Kuangalia jina alikuwa ni mama yake mzazi
"haloo mamy, shkamoo"
"Marahaba ujambo"
"sijambo mama vp uko chuga"
"safi tu... Naona umekuwa kimya sana hakumbuki kama kuna kurudi shule"
"aaaaa mamy, mbona bado wiki nzima, acha nile bata kwanza"
"sasa utajiandaa vipi jamani"
"mamy, nitakuja baada ya siku hizi hizi"
"sawa, ila hakikisha unakuja hapa siku mbili kabla ya kwenda shule sawa"
"sawa mamy"
Simu ilikata huku rahim akikasirika mno,...
"uyu mza nae"
Aliongea rahim huku akiitupa simu kochini...
"kwani vipi dogo"
"ah maza uyo"
"kasemaje kwani"
"anataka nirudi home eti mambo ya shule shule aahhh"
"utaki sasa au?..."
"aahhh bado bado"
"lakini ukumbuke ni mwaka wako wa mwisho huu, tena unakwenda kumalizia tu"
"najua... Au nawe wanikandia nini"
"kunywa chai ujue swaga zingine"
Basi rahim alikaa kitako na kugonga chai, baada ya kumaliza kunywa chai.. Alitamani sana kukutana na zena, ila kwa mida hio ya mchana hawezi kumpata mana yupo nyumbani, mida yake mizuri ni ile ya jioni wakati akienda madrasa, au akirudi madrasa, hua ndio mida mizuri ya kukutana nae,... Sasa rahim anapajua vizuri nyumbani kwa akina zena, basi akawa anatembea zake kwa mguu taratibu,.. Alipofika alipiga jicho kule kwao, kwa bahati nzuri zena alikuwepo dukani, mana hapo hapo kuna kaduka hivi na zena anapenda kuuza yeye, ila ikifika jioni anakwenda zake madrasa, ila kuswali hua anaswalia hapo hapo dukani,... Sasa rahim anatafuta gia ya kuendea pale dukani ili amuulize kwanini jana kaenda kulala nae wakati akiwa kalewa, hilo tu ndio swali kwake,... Sasa rahim akakaza moyo mpaka pale dukani, na hapo alikuwa hajalewa, na duka hilo lipo hapo hapo nyumbani, hivyo mzee akitoka tu atamuona rahim,...
"mambo zena"
"sema As salama Aleykum warahmatullah wabarakatuh"
"mmmhhhhhh hio ndefu sitoweza kuitaamka"
"afu umekujaje sa hii wazazi wangu wapo"
Rahim mwanamke akishakuwa wake hua kuongea anaweza lakini ni kwa upole utafikiri kondoo,..
"kuna kitu nataka nikuulize zena... Kizuri sana ila sijui kwanini umenivizia nikiwa nimelewa"
"nimefanya nini"
Sasa wakati huo huo fadhila nae anatokea nae alikuwa anakuja kwa zena, lakini alipomwona rahim pale dirishani, alibana mahali, na alikuwa akisikia yaliokuwa yakiongelewa na rahim....
"mmmhhh eti unajifanya hujui... Jana ulinifanyia nini... Mpaka saa saba za usiku"
Sasa zena yeye anashangaa maneno ya rahim,... Lakini sasa kule kwa fadhila nae alikuwa anajiuliza kuwa
"khaaa... Ina maana rahim hakumbuki tukio la jana??.... Safi sana.... Wacha amwambie ili zena akasirike na waachane..... Rahim. Lazima awe wangu"

Je?.. Nini kitaendelea??...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom