Chilojnr
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 302
- 1,306
- Thread starter
- #521
NYEMO CHILONGANI
UCHAWI WA BILIONEA BAZOKA
0718069269
SEHEMU YA 30.
Maganza alitulia ofisini kwake huku kichwa chake kikiwa na mambo tele, bado alimfikiria Bazoka, mwanaume huyo alimsumbua kwa kuwa kulikuwa na mambo mengi yaliyokuwa yakimvuruga.
Kila alipokuwa akimfikiria, alikosa jibu, kuna wakati alianza kuhisi jamaa alikuwa mchawi lakini wazo hilo hakulitilia maanani kwa kuwa jamaa muonekano wake haukuwa kama wa kichawi hata kidogo.
Alihisi kulikuwa na jambo lililokuwa likiendelea nyuma ya pazia lakini pia hakuona kama kulikuwa na kitu, kichwa chake kilimwambia kulikuwa na jambo jingine lakini si hilo alilokuwa akilifikiria.
Alitulia, huku akiwa amezama kwenye mawazo ndipo akakumbuka kuhusu gari la Bazoka. Siku ya kwanza alipokwenda kufanya upelelezi wa kupotea kwa mtoto Yusufu, alikumbuka aliambiwa kuhusu gari ambalo halikuonekana, ilikuwa ni Noah Nyeupe.
Kengele ikagonga kichwani mwake, huyo Bazoka aliwahi kufika hapo kituo cha polisi akiwa na gari lake, akajitahidi kulikumbuka vilivyo, lilikuwa ni Noa Nyeupe kama alivyoambiwa.
Sasa hapo akaanza kupata picha kwamba inawezekana kabisa huyo Bazoka ndiye yule mwanaume aliyemteka Yusufu na baadaye kukutwa porini akiwa ameuawa kwa imani za kishirikina.
Alipokumbuka hilo, akatulia na kujipa makosa, aliwahi kusikia na kuona kwamba watoto wote waliokuwa na ulemavu wa ngozi walipokuwa wakitekwa, walipokuwa wakipatikana, miili haikuwa na viungo, watu walivitoa na kuondoka navyo, hiyo ilikuwa tofauti na Yusufu kwani alikutwa na viungo vyake vyote.
“Sasa mbona inanichanganya!” alijisemea.
“Ila acha nianze kudili na hii Noah, yaani moyo wangu unaniambia kwamba haya yote anayoyafanya ni Bazoka tu,” alijisemea, akiwa amemaliza kuwa kwenye hali hiyo, mara simu yake ya mezani ikaanza kuita, haraka sana akaichukua na kuipeleka sikioni.
“Halo!”
“Nakuhitaji ofisini,” ilisema sauti ya upande wa pili na kukata simu.
Sauti hiyo ilikuwa ni ya kamanda Masumbuko, aliijua auti yake na hivyo haraka sana akainuka na kwenda huko, alipofika ndani ya ofisi ya mkuu wake, akagonga mlango, akakaribishwa na kuingia ndani, macho yake yakatua kwa makamanda wengine wawili waliokaa kwenye viti vilivyokuwa humo, akapiga saluti.
“Kuna kazi nataka nikupe. Fuatilia mauaji ya mtu fulani,” alisema Kamanda Masumbuko.
“Mauaji gani mkuu?”
“Kuna mtu anaitwa Christopher, ama kwa jina jingine Bonge,” alijibu.
Maganza aliposikia majina hayo tu akashtuka na kumwangalia Masumbuko vilivyo, hayakuwa majina mageni masikioni mwake, aliwahi kuyasikia mahali au hata kufuatilia jambo kuhusu mtu huyo.
Hapo ndipo Masumbuko alipomwambia kwamba mwanaume aliyekuwa ameuawa alikuwa rafiki wa Bazoka, akakumbuka, alikuwa mmoja wa watu aliowahi kuwahoji baada ya kifo cha Sultani kutokea.
Sasa hapo kichwa chake kikachanganyikiwa zaidi, hapo kwa haraka sana akaanza kupata majibu ya kitu fulani, ni kweli alikuwa bize kumuhusisha Bazoka kwenye mauaji ya watu hao lakini inawezekana kulikuwa na watu walioamua kufanya mauaji kwa watu hao na huyo Bazoka naye alikuwa kwenye orodha hiyo.
Marafiki zake waliuawa, kwake haikumuingia akilini kwamba ni Bazoka ndiye aliyefanya mauaji hayo, kwa mara ya kwanza akaanza kukubaliana na Bazoka kwamba kulikuwa na mtu mwingine aliyekuwa akiyafanya hayo yote lakini si yeye.
Hayo yote yalifikiriwa kichwani mwake ndani ya sekunde chache tu, Masumbuko akampa faili kuhusu mauaji ya mwanaume huyo na kurudi nalo ofisini mwake, akalifungua na kuanza kulifuatilia.
Kilichoandikwa humo kikaanza kumtia hofu, alisoma maelezo vizuri na kugundua kwamba mtu aliyefanya mauaji alikuwa mwanamke ambaye baada ya tukio hilo hakuonekana tena.
Mauaji yake yalikuwa sawa na yale ya Sultani, naye aliuawa na mwanamke nyumbani kwake, ila huyo Bonge aliuawa akiwa ofisini mwake. Akachanganyikiwa mno, hakutaka kubaki ofisini, haraka sana akaondoka na kuelekea huko ofisini, alitaka kuliona eneo la tukio.
Alipofika huko, alikuta ofisi ikiwa imefungwa ila tayari alipewa ufunguo kwa lengo la kuingia na kuanza kuchunguza. Aliangalia mpangilio wa ofisi huku mikononi akiwa na glove kwa ajili ya kuacha kila kitu kama kilivyokuwa bila kuweka alama yoyote ile ya vidole vyake.
“Maiti yake ilikutwa hapa, ilikuwa imelala bila shaka,” alijisemea huku akikiangalia kitu, kwenye meza kulikuwa na alama fulani nyekundu, alihisi zilikuwa damu.
“Mwanamke alikaa wapi? Labda kwenye kiti hiki,” alijiuliza na kujijibu.
“Inawezekana ndani kulikuwa wawili tu? Hapana! Ndiyo! Hapana! Ndiyo! Inawezekana kabisa. Sasa baada ya kufanya haya mauaji mwanamke alikimbilia wapi?” alijiuliza huku akiangalia dirisha la vioo tupu, lilikuwa limefungwa vilivyo.
“Hakuweza kupitia dirishani kwa sababu bado lilikuwa limefungwa, kama angepitia hapa basi dirisha lingekuwa wazi,” alijisemea.
“Hebu subiri!” alisema.
Haraka sana akachukua simu yake na kumpigia mtu alikuwa karibu na ofisi yake na kumwambia akaagalie ofisini kwake, kwenye lile faili ambapo kulikuwa na namba ya simu ya dada wa mapokezi.
Haraka sana hilo likafanywa na mwanaume aliyekuwa upande wa pili na baada ya dakika kadhaa, akatumiwa namba ya msichana huyo, haraka sana akaipigia, akaanza kuzungumza naye.
“Nataka nikuone hapa ofisini, hakikisha ndani ya nusu saa uwe umefika,” alimwambia baada ya kuitambulisha.
Baada ya kuzungumza naye, akatulia humo ofisini huku akiendelea kufuatilia kwa karibu na kujaribu kufikiri ni kitu gani kilichokuwa kimetokea. Baada ya dakika ishirini, msichana huyo akafika ofisini hapo na kuanza kuzungumza naye.
Alimuhadithia kila kitu kilichokuwa kimetokea, namna bosi wake alivyofika ofisini hapo na kuzungumza naye, alipoingia ndani na msichana huyo kutokea, naye akaingia.
“Halafu?” aliuliza.
“Baada ya dakika kadhaa, rafiki yake akafika ofisini hapa,” alimwambia.
“Rafiki yupi?”
“Bazoka!”
“Bazoka?” aliuliza huku akiwa na mshtuko kwa mbali.
“Ndiyo!”
“Alifika huku huyo msichana akiwa ndani?”
“NdiyO!”
“Halafu ikawaje?”
“Aliingia na kuongea naye kidogo, hakukaa sana, akatoka, aliniambia anamuacha bosi wake akizungumza na huyo msichana halafu yeye angerudi kwani hakujua kama alikuwa na mgeni,” alimwambia.
“Sawa. Bazoka alivyoondoka, una uhakika msichana huyo aliendelea kubaki humo ndani?” alimuuliza kana kwamba yule msichana alijigeuza Bazoka na kuondoka.
“Ndiyo kwani niliendelea kusikia vicheko vyao ndani ya ofisi!”
“Sawa. Endelea.”
Baada ya lisaa hivi, Bazoka akarudi!”
“Lengo la kurudi?”
“Aliniambia alimuachia uhuru bosi ili afanye yake!”
“Yapi?”
“Kufanya mapenzi na msichana huyo, hivyo aliporudi, tulikuwa tunaongea kwa utani kwamba bado wanaendelea kufanya kwani kulikuwa kimya kabisa,” alisema.
“Sasa nyie mlijuaje kama amekufa?”
“Bazoka alichoka kusubiri, akaamua kuingia ndani! Ndipo alipoikuta hiyo maiti na kuniita,” alijibu.
“Kwa hiyo Bazoka ndiye aliyegundua maiti ya bosi wako?” aliuliza.
“Ndiyo!”
Kwa kipindi hicho kama kulikuwa na watu waliokuwa wamechanganyikiwa kwa matukio mengi yaliyokuwa yakitokea, basi yeye alikuwa wa kwanza. Alitamani kumuhusisha BAzoka kwenye jambo hilo lakini kwa jinsi msichana yule alivyokuwa amesimulia, hakuona ni wapi mwanaume huyo alipokuwa amehusika.
Yeye mwenyewe inaonyesha kabisa hakuwa amejua kilichokuwa kimetokea, aliingia na kukuta maiti, sasa kama kweli alitakiwa kumuhusisha ilikuwa ni lazima kuwa na sababu mahali ama hata uwalakini wa kumuingiza kwenye tukio hilo.
Alipanga kumpigia simu Bazoka na kwenda kuzungumza naye, alihisi inawezekana kabisa akawa anafahamu kilichokuwa kimetokea kwa ukaribu lakini hofu yake ilikuwa moja kwamba asingepata ushirikiano kutoka kwake kwa kuwa alimsumbua sana.
“Kwenye hii kesi acha nifuatilie taratibu,” alijisemea, alihitaji kufanya uchunguzi wa mauaji hayo kimyakimya kabisa, ikiwezekana amfahamu msichana huyo kwanza.
Je, nini kitaendelea?
Tukutane Jumanne mahali hapa.
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
UCHAWI WA BILIONEA BAZOKA
0718069269
SEHEMU YA 30.
Maganza alitulia ofisini kwake huku kichwa chake kikiwa na mambo tele, bado alimfikiria Bazoka, mwanaume huyo alimsumbua kwa kuwa kulikuwa na mambo mengi yaliyokuwa yakimvuruga.
Kila alipokuwa akimfikiria, alikosa jibu, kuna wakati alianza kuhisi jamaa alikuwa mchawi lakini wazo hilo hakulitilia maanani kwa kuwa jamaa muonekano wake haukuwa kama wa kichawi hata kidogo.
Alihisi kulikuwa na jambo lililokuwa likiendelea nyuma ya pazia lakini pia hakuona kama kulikuwa na kitu, kichwa chake kilimwambia kulikuwa na jambo jingine lakini si hilo alilokuwa akilifikiria.
Alitulia, huku akiwa amezama kwenye mawazo ndipo akakumbuka kuhusu gari la Bazoka. Siku ya kwanza alipokwenda kufanya upelelezi wa kupotea kwa mtoto Yusufu, alikumbuka aliambiwa kuhusu gari ambalo halikuonekana, ilikuwa ni Noah Nyeupe.
Kengele ikagonga kichwani mwake, huyo Bazoka aliwahi kufika hapo kituo cha polisi akiwa na gari lake, akajitahidi kulikumbuka vilivyo, lilikuwa ni Noa Nyeupe kama alivyoambiwa.
Sasa hapo akaanza kupata picha kwamba inawezekana kabisa huyo Bazoka ndiye yule mwanaume aliyemteka Yusufu na baadaye kukutwa porini akiwa ameuawa kwa imani za kishirikina.
Alipokumbuka hilo, akatulia na kujipa makosa, aliwahi kusikia na kuona kwamba watoto wote waliokuwa na ulemavu wa ngozi walipokuwa wakitekwa, walipokuwa wakipatikana, miili haikuwa na viungo, watu walivitoa na kuondoka navyo, hiyo ilikuwa tofauti na Yusufu kwani alikutwa na viungo vyake vyote.
“Sasa mbona inanichanganya!” alijisemea.
“Ila acha nianze kudili na hii Noah, yaani moyo wangu unaniambia kwamba haya yote anayoyafanya ni Bazoka tu,” alijisemea, akiwa amemaliza kuwa kwenye hali hiyo, mara simu yake ya mezani ikaanza kuita, haraka sana akaichukua na kuipeleka sikioni.
“Halo!”
“Nakuhitaji ofisini,” ilisema sauti ya upande wa pili na kukata simu.
Sauti hiyo ilikuwa ni ya kamanda Masumbuko, aliijua auti yake na hivyo haraka sana akainuka na kwenda huko, alipofika ndani ya ofisi ya mkuu wake, akagonga mlango, akakaribishwa na kuingia ndani, macho yake yakatua kwa makamanda wengine wawili waliokaa kwenye viti vilivyokuwa humo, akapiga saluti.
“Kuna kazi nataka nikupe. Fuatilia mauaji ya mtu fulani,” alisema Kamanda Masumbuko.
“Mauaji gani mkuu?”
“Kuna mtu anaitwa Christopher, ama kwa jina jingine Bonge,” alijibu.
Maganza aliposikia majina hayo tu akashtuka na kumwangalia Masumbuko vilivyo, hayakuwa majina mageni masikioni mwake, aliwahi kuyasikia mahali au hata kufuatilia jambo kuhusu mtu huyo.
Hapo ndipo Masumbuko alipomwambia kwamba mwanaume aliyekuwa ameuawa alikuwa rafiki wa Bazoka, akakumbuka, alikuwa mmoja wa watu aliowahi kuwahoji baada ya kifo cha Sultani kutokea.
Sasa hapo kichwa chake kikachanganyikiwa zaidi, hapo kwa haraka sana akaanza kupata majibu ya kitu fulani, ni kweli alikuwa bize kumuhusisha Bazoka kwenye mauaji ya watu hao lakini inawezekana kulikuwa na watu walioamua kufanya mauaji kwa watu hao na huyo Bazoka naye alikuwa kwenye orodha hiyo.
Marafiki zake waliuawa, kwake haikumuingia akilini kwamba ni Bazoka ndiye aliyefanya mauaji hayo, kwa mara ya kwanza akaanza kukubaliana na Bazoka kwamba kulikuwa na mtu mwingine aliyekuwa akiyafanya hayo yote lakini si yeye.
Hayo yote yalifikiriwa kichwani mwake ndani ya sekunde chache tu, Masumbuko akampa faili kuhusu mauaji ya mwanaume huyo na kurudi nalo ofisini mwake, akalifungua na kuanza kulifuatilia.
Kilichoandikwa humo kikaanza kumtia hofu, alisoma maelezo vizuri na kugundua kwamba mtu aliyefanya mauaji alikuwa mwanamke ambaye baada ya tukio hilo hakuonekana tena.
Mauaji yake yalikuwa sawa na yale ya Sultani, naye aliuawa na mwanamke nyumbani kwake, ila huyo Bonge aliuawa akiwa ofisini mwake. Akachanganyikiwa mno, hakutaka kubaki ofisini, haraka sana akaondoka na kuelekea huko ofisini, alitaka kuliona eneo la tukio.
Alipofika huko, alikuta ofisi ikiwa imefungwa ila tayari alipewa ufunguo kwa lengo la kuingia na kuanza kuchunguza. Aliangalia mpangilio wa ofisi huku mikononi akiwa na glove kwa ajili ya kuacha kila kitu kama kilivyokuwa bila kuweka alama yoyote ile ya vidole vyake.
“Maiti yake ilikutwa hapa, ilikuwa imelala bila shaka,” alijisemea huku akikiangalia kitu, kwenye meza kulikuwa na alama fulani nyekundu, alihisi zilikuwa damu.
“Mwanamke alikaa wapi? Labda kwenye kiti hiki,” alijiuliza na kujijibu.
“Inawezekana ndani kulikuwa wawili tu? Hapana! Ndiyo! Hapana! Ndiyo! Inawezekana kabisa. Sasa baada ya kufanya haya mauaji mwanamke alikimbilia wapi?” alijiuliza huku akiangalia dirisha la vioo tupu, lilikuwa limefungwa vilivyo.
“Hakuweza kupitia dirishani kwa sababu bado lilikuwa limefungwa, kama angepitia hapa basi dirisha lingekuwa wazi,” alijisemea.
“Hebu subiri!” alisema.
Haraka sana akachukua simu yake na kumpigia mtu alikuwa karibu na ofisi yake na kumwambia akaagalie ofisini kwake, kwenye lile faili ambapo kulikuwa na namba ya simu ya dada wa mapokezi.
Haraka sana hilo likafanywa na mwanaume aliyekuwa upande wa pili na baada ya dakika kadhaa, akatumiwa namba ya msichana huyo, haraka sana akaipigia, akaanza kuzungumza naye.
“Nataka nikuone hapa ofisini, hakikisha ndani ya nusu saa uwe umefika,” alimwambia baada ya kuitambulisha.
Baada ya kuzungumza naye, akatulia humo ofisini huku akiendelea kufuatilia kwa karibu na kujaribu kufikiri ni kitu gani kilichokuwa kimetokea. Baada ya dakika ishirini, msichana huyo akafika ofisini hapo na kuanza kuzungumza naye.
Alimuhadithia kila kitu kilichokuwa kimetokea, namna bosi wake alivyofika ofisini hapo na kuzungumza naye, alipoingia ndani na msichana huyo kutokea, naye akaingia.
“Halafu?” aliuliza.
“Baada ya dakika kadhaa, rafiki yake akafika ofisini hapa,” alimwambia.
“Rafiki yupi?”
“Bazoka!”
“Bazoka?” aliuliza huku akiwa na mshtuko kwa mbali.
“Ndiyo!”
“Alifika huku huyo msichana akiwa ndani?”
“NdiyO!”
“Halafu ikawaje?”
“Aliingia na kuongea naye kidogo, hakukaa sana, akatoka, aliniambia anamuacha bosi wake akizungumza na huyo msichana halafu yeye angerudi kwani hakujua kama alikuwa na mgeni,” alimwambia.
“Sawa. Bazoka alivyoondoka, una uhakika msichana huyo aliendelea kubaki humo ndani?” alimuuliza kana kwamba yule msichana alijigeuza Bazoka na kuondoka.
“Ndiyo kwani niliendelea kusikia vicheko vyao ndani ya ofisi!”
“Sawa. Endelea.”
Baada ya lisaa hivi, Bazoka akarudi!”
“Lengo la kurudi?”
“Aliniambia alimuachia uhuru bosi ili afanye yake!”
“Yapi?”
“Kufanya mapenzi na msichana huyo, hivyo aliporudi, tulikuwa tunaongea kwa utani kwamba bado wanaendelea kufanya kwani kulikuwa kimya kabisa,” alisema.
“Sasa nyie mlijuaje kama amekufa?”
“Bazoka alichoka kusubiri, akaamua kuingia ndani! Ndipo alipoikuta hiyo maiti na kuniita,” alijibu.
“Kwa hiyo Bazoka ndiye aliyegundua maiti ya bosi wako?” aliuliza.
“Ndiyo!”
Kwa kipindi hicho kama kulikuwa na watu waliokuwa wamechanganyikiwa kwa matukio mengi yaliyokuwa yakitokea, basi yeye alikuwa wa kwanza. Alitamani kumuhusisha BAzoka kwenye jambo hilo lakini kwa jinsi msichana yule alivyokuwa amesimulia, hakuona ni wapi mwanaume huyo alipokuwa amehusika.
Yeye mwenyewe inaonyesha kabisa hakuwa amejua kilichokuwa kimetokea, aliingia na kukuta maiti, sasa kama kweli alitakiwa kumuhusisha ilikuwa ni lazima kuwa na sababu mahali ama hata uwalakini wa kumuingiza kwenye tukio hilo.
Alipanga kumpigia simu Bazoka na kwenda kuzungumza naye, alihisi inawezekana kabisa akawa anafahamu kilichokuwa kimetokea kwa ukaribu lakini hofu yake ilikuwa moja kwamba asingepata ushirikiano kutoka kwake kwa kuwa alimsumbua sana.
“Kwenye hii kesi acha nifuatilie taratibu,” alijisemea, alihitaji kufanya uchunguzi wa mauaji hayo kimyakimya kabisa, ikiwezekana amfahamu msichana huyo kwanza.
Je, nini kitaendelea?
Tukutane Jumanne mahali hapa.
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app