My Soulmate Episode 1
Produced by EquatorStory Specials
Stela :”Nickson uko wapi jamani ?? Mpaka sasa umechelewa sana.”. Ilikuwa ni sauti ya stela akimngojea mpenzi wake Nickson alie kuwa njiani akitokea kazini .
Nickson:”Nimekuona mpenzi hapo ulipo nakuja jamani.”. Nickson alisogea taratibu kumfikia mpenzi wake aliekuwa akimngojea na jazba taratibu ilianza kupanda kisa mpenzi wake amechelewa.
Nickson:”Mambo mpenzi?”.
Stela :”Mxxheeewww ”.
Nickson: “Jamani mpenzi nisamehe bure tu jamani ni kazi.”
Stela:”Aaah kazi gani bhana..???.” Stela aliuliza kwa hasira akianza kuhisi mpenziwe hamchukuliii serious.
Stela:”Haiwezekani tuuupange huu mtoko karibu mwezi mzima alafu uchelewe!. Baby kweli unanipenda???.” Stela alitamani kuondoka akasimama kwa hasira.
Stela:”Nenda kalale na hiyo kazi yako kama unaipenda hivyo. Maaana wewe unatumia matope ama ubongo?. Mimi si nimeondoka kazini mapema sana yani we bado hata ndo unatoka sasa. So hujapitia nyumbani kuoga ushaaanza kunukia jasho.”Nickson akamshika mkono kwa nguvu na Stela akaaanza kumpiga vikofi kwenye mkono aliemshikia Nickson ili asiondoke .
Nickson: “Baby am sorry nakupenda wewe lakini bila hiii kazi sidhani kama tungekua hapa. Baby ni dakika 20 tu jamani. Tafadhali nisamehe sitorudia mpenzi.”Stela akaaanza akakumbuka aliwahi kumwambia Nickson kipindi hicho “Mapenzi hayaliki”.
Stela:”Sawa nimekusamehe lakini usirudie tena. Lakini baby….”Stela aliamua kumsamehe na wakaaanza maongezi yao .
Nickson: “Stela sema mama!..”.
Stela:”Baby kweli wewe tunapanga mtoko unanpangia na kitu cha kula mimi si mpenzi wako natakiwa nile kitu nachotaka bhana.”Stela alisema huku akiwa na ka uchungu.
Nickson :”Baby..”.Stela akamkatisha.
Stela:”Subiri sijamaliza kuongea ”. Nickson alikaa kimya akimsikilizia mpenzi wake .
Nickson :”Sawa mama zungumza ”.Nickson aliamua kuwa mpole na kuwa msikivu kwa sababu ana amini kwamba katika mahusiano lazima kuwe na usikivu pale mmoja wapo anapotaka kuzungumza .Nickson alikaaa na kuweka mkono wake wa kuume kidevuni huku akikuna taratibu ndevu zake mbili tatu.
Stela : “Huwezi ukaniambia ety pamoja na kusubiri huu mtoko mweeeezi mzima unaniambia bajeti yako ni 10,000 tu?”.
Nickson : “Mama ..”. Stela alimsimamisha hapo kabla hajafika mbali .
Stela:”Eeeeeh nishakwambia uache kuniiita Mama unanizeeesha bhana.”
Nickson:”Am sorry baby. Unajua nataka uwe mama watoto wangu tena nataka motto wa kwanza aitwe Rose kama ni wa kiume ataitwa Samuell”.
Stela:”Nickson am serious na swali langu.”Stela alioneka akianza kunyanyua nyusi ya kulia na kupindisha shingo kidogo kama anavyofanyaga akiwa na hasira au akiwa serious na jambo.
Nickson :”Sawa Ma… I mean sawa Baby stela…. Nakujibu “.
Stela : “Enheee…..”. Stela alikaaa chonjo kusikilizia jibu huku akisogeza nywele zake za rasta zijulikanazo kama yeboyebo na kucha zake alizongezea za bandia za rangi ya nyekundu ili zisi mghasi .
Nickson:”Baby unajua mimi nina majukumu na laki na nusu nimetoka kwa ajili ya project.”.Stela akamkatisha hapo hapo .
Stela :”Tena ishia hapo hapo.” Mara wakasikia sauti ya mtu mwingine kutazama ni waiter wa pale hoteli waliopo ijulikana nayo kama “Mwambao hotel” iliopo upande wa pili kutazamana na Stand ya ma bus “Dar express”.
Waiter:”Jamani za jioni Kwema hapa!?”.Waiter aliuliza kwa sauti ya upole na kwa sauti ya ukarimu.
Nickson & Stela: ”Salama tu.” Wote waliiitikia kwa pamoja kama waliambizana kujibu hivyo.
Waiter:”Niwahudumie nini joini ya leo?”.
Nickson : “Kuku nusu kiasi gani?”. Nickson aliuliza akimwangalia waiter kwa makini asikie bei chapu apige hesabu ya fasta .
Waiter:”Ni 6000”. Waiter alijibu lakini akaongezea . “Kwa sasa kuku zimeisha ndugu labda kama hamtojali mchukue nyama choma nusu 5,000”.Nickson moyoni akajisemea kumbee bora hata bajeti itaaenda sawa sawia.
Nickson:”Sawa naomba hiyo hiyo”. Akamgeukia Stela na kumuambia. “Baby utakula na nini? “
Stela : “Na chipsi tu”. Stela alisema hivyo akizungusha macho maaana anajua ingekua mtu mwingine angeagiza nyama kilo na ndizi kama tano. Ili apate na ya kumbebea mdogo wake aliemwacha (Yunis) nyumbani.
Nickson:”Na mimi naomba na chipsi .” Alisema huku ana piga mahesabu yake “chipsi 2x2000 =4000 na nyama choma 5000 so inakuwa 9000 na soda moja 10,000 yake imeisha.”.Nickson akamgeukia mpenzi wake .
Nickson:”Baby unakunywa na soda gani?”.Alimuliza mpenzi wake kwa upendo na ujasiri kuwa bado yupo ndani ya bajet ya 10,000.
Stela : “Na grand malta.” Stela alijibu akiangalia upande mwingine wa hoteli ile ilokuwa bize kweli na ma bus yakishusha watu kutoka sehemu mbali mbali.Nickson moyoni alistuka kidogo akajisemea “Kiiiiibo na grand tena?”. Nickson akamwai waiter wakati stela akiangalia ma Bus “Mwambie haipo..” alisema kwa mdomo bila kutoa sauti.
Waiter:”Samahani Grand malta zimeisha”. Nickson akadakia fasta .
Nickson:”Leta na supa leta tu si ndio beby?. “alimuliza stela akiwa na confidence hawezi kataaa ndo soda aliokunywa walipo enda uzunguni park mara ya mwisho .
Stela :”Ndio na supa-leta ya moto tafadhali”.Stela alijibu akiwa hajui kuwa hana namna .
Waiter:”Sawa chipsi mbili na nyama choma na supa leta. Kaka utakunywa nini?”. Waiter alitaka kujua Nickson atakunywa nini.
Nickson:”Ah mi nina hii tayari”. Aliwahi kumwonesha soda ya takeaway alie kuja nayo .Sawa waiter akaondoka na kuwaacha wakiendelea mazungumzo yao.Nickson alitumia hizi sekunde kadhaaa akimwangalia mpenzi wake alivyo. Stela hyo siku alikua amevaaa suruali ya jeans inayombana nakuonesha umbo lake kiasi flani cha kuvutia . Alikua kavaa t-shirt ambayo Nickson alimpa kama zawadi imeandika na maaandishi kwa nyuma ikisema “ExonGraphics” ambalo ndo jina la kampuni ambalo Nickson anatarajia kufungua hivi punde.
Nickson:”Enhee mpenzi ulikua unasemaje?”. Stela alimgeukia taratibu akiwa anaonekana kuwa alizama kwenye kukuru-kakara za pale stand inayo tazamana na hotel waliiopo.
Stela:”Nataka ugali maharage”. Alijibu hapo wakaaanza kucheka yeye pamoja na Nickson wakikumbuka kipindi kile ambacho Stela alimjibu Nickson wakati huo bado mahusiano yao hayaja anza alikua akimtesa tu na vituko vya stela vya hapa na pale.
Stela:”Baby lakini kweli mi nakushauri uachane na hiyo project bora ufanye biashara nyingine kama kuchukua nguo kwenye soko la maimoria uje uuuze nipe hata mimi nitakuuzia. Pia ntakusaidia kuchagua.”
Nickson:”Lakini baby mimi nikipata Camera moja tu inanitosha kutoka katika maisha haya ”.Nickson alisema akiwa na matumaini.
Stela :”Kwani Camera kiasi gani?”. Aliuliza akitaka kujua yamkini ata weza kumpa ushauri.
Nickson : “Camera nzuri laki saba na lenzi laki tatu. “. Stela alianza tena kupandisha nyusi ya kulia akaweka nywele tena vizuri akanyoosha mkono kumuashiria Nickson aaache kuongea.
Stela : ”Sawa na umechanga sh ngapi mpaka sasa!? ”. Stela aliuliza huku amesogeza kichwa mbele na sikio linamtazamia Nickson asikie jibu kwa makini.
Nickson:”Ndo nimetoa laki na nusu sai….”. Stela akamkatisha.
Stela:”Baby iyo hela nyingine utapata wapi?”.
Nickson : “Ntajichanga tu Baby namwamini Mungu ”.Stela akawa ana guna mhhh mhhhh.
Stela: ”Sawa iyo hela yote uka nunue Camera uanze kutafuta wa kuwapiga picha na Studio huna na Laptop yako yenyewe ndo hyo……. ”. Stela ali kuwa kimya kidogo
Stela :” Baby kuwa mjanja umesoma mpaka umemaliza chuo umemaliza huezi kufanya vitu vya kijinga hivyo”.
Nickson : “Hayaaa sasa ushaaanza..”Nickson alijua tu wataaanza kugombana kisa mipango yake.
Stela : “Nishaanza nini? Afu nishakuambia usinikatishe nikiongea.”Stela aliendelea tu kuongea kama ana rap nyimbo anayoipenda.
Nickson: “Sasa mpenzi sikia nikuambie kitu mimi ntakupa hela uongeze na yako tuanze biashara”.
Stela : “Nickson mimi nitawezaje kutoa hela hapo na unajua dhahiri ya mimi ni secretary wa pale Matumizi Company ya Yule Mmasai Vicent Mbekure ”Stela alikua anaongea kudhibitisha hela ndogo alionayo .
Nickson:”Sawa Baby mimi nitafanya kukupa ”.Nickson sio wa maneno mengi sana na alijua mpenzi wake anataka kumwambia kitu gani.
Stela : “Sawa mimi ntaenda maimoria mwenyewe ukinipa ”. Mara waiter akaja
Waiter: ”Jamani chakula chenu kiko tayari. Munaweza kwenda kunawa pale mkihitaji waiter alisema hivyo akinyoshea mkono bomba la kunawia. “Jamani karibuni na mu enjoy.”
Nickson wakasimama wakaenda kunawa kama walivyoshauriwa wakala kwa kucheka kulishana hapa na pale. Mara wachokozane. Walipo maliza Nickson alilipa bill iliyo kuja kama alivyotegemea na kupigia mahesabu . Nickson akampa mpenzi wake nauli na pia akaanza kutembea kwa miguu kuelekea ghetto kwake.
Stela : “Baby kwaheri! Nimeshiba” . Alimwita Nickson aliokuwa ameanza kutafuta njia ya kwenda nyumbani kwake . Nickson akageuka aka mpulizia busu la hewani mpenziwe.
Itaendelea….
Produced by EquatorStory Specials
Stela :”Nickson uko wapi jamani ?? Mpaka sasa umechelewa sana.”. Ilikuwa ni sauti ya stela akimngojea mpenzi wake Nickson alie kuwa njiani akitokea kazini .
Nickson:”Nimekuona mpenzi hapo ulipo nakuja jamani.”. Nickson alisogea taratibu kumfikia mpenzi wake aliekuwa akimngojea na jazba taratibu ilianza kupanda kisa mpenzi wake amechelewa.
Nickson:”Mambo mpenzi?”.
Stela :”Mxxheeewww ”.
Nickson: “Jamani mpenzi nisamehe bure tu jamani ni kazi.”
Stela:”Aaah kazi gani bhana..???.” Stela aliuliza kwa hasira akianza kuhisi mpenziwe hamchukuliii serious.
Stela:”Haiwezekani tuuupange huu mtoko karibu mwezi mzima alafu uchelewe!. Baby kweli unanipenda???.” Stela alitamani kuondoka akasimama kwa hasira.
Stela:”Nenda kalale na hiyo kazi yako kama unaipenda hivyo. Maaana wewe unatumia matope ama ubongo?. Mimi si nimeondoka kazini mapema sana yani we bado hata ndo unatoka sasa. So hujapitia nyumbani kuoga ushaaanza kunukia jasho.”Nickson akamshika mkono kwa nguvu na Stela akaaanza kumpiga vikofi kwenye mkono aliemshikia Nickson ili asiondoke .
Nickson: “Baby am sorry nakupenda wewe lakini bila hiii kazi sidhani kama tungekua hapa. Baby ni dakika 20 tu jamani. Tafadhali nisamehe sitorudia mpenzi.”Stela akaaanza akakumbuka aliwahi kumwambia Nickson kipindi hicho “Mapenzi hayaliki”.
Stela:”Sawa nimekusamehe lakini usirudie tena. Lakini baby….”Stela aliamua kumsamehe na wakaaanza maongezi yao .
Nickson: “Stela sema mama!..”.
Stela:”Baby kweli wewe tunapanga mtoko unanpangia na kitu cha kula mimi si mpenzi wako natakiwa nile kitu nachotaka bhana.”Stela alisema huku akiwa na ka uchungu.
Nickson :”Baby..”.Stela akamkatisha.
Stela:”Subiri sijamaliza kuongea ”. Nickson alikaa kimya akimsikilizia mpenzi wake .
Nickson :”Sawa mama zungumza ”.Nickson aliamua kuwa mpole na kuwa msikivu kwa sababu ana amini kwamba katika mahusiano lazima kuwe na usikivu pale mmoja wapo anapotaka kuzungumza .Nickson alikaaa na kuweka mkono wake wa kuume kidevuni huku akikuna taratibu ndevu zake mbili tatu.
Stela : “Huwezi ukaniambia ety pamoja na kusubiri huu mtoko mweeeezi mzima unaniambia bajeti yako ni 10,000 tu?”.
Nickson : “Mama ..”. Stela alimsimamisha hapo kabla hajafika mbali .
Stela:”Eeeeeh nishakwambia uache kuniiita Mama unanizeeesha bhana.”
Nickson:”Am sorry baby. Unajua nataka uwe mama watoto wangu tena nataka motto wa kwanza aitwe Rose kama ni wa kiume ataitwa Samuell”.
Stela:”Nickson am serious na swali langu.”Stela alioneka akianza kunyanyua nyusi ya kulia na kupindisha shingo kidogo kama anavyofanyaga akiwa na hasira au akiwa serious na jambo.
Nickson :”Sawa Ma… I mean sawa Baby stela…. Nakujibu “.
Stela : “Enheee…..”. Stela alikaaa chonjo kusikilizia jibu huku akisogeza nywele zake za rasta zijulikanazo kama yeboyebo na kucha zake alizongezea za bandia za rangi ya nyekundu ili zisi mghasi .
Nickson:”Baby unajua mimi nina majukumu na laki na nusu nimetoka kwa ajili ya project.”.Stela akamkatisha hapo hapo .
Stela :”Tena ishia hapo hapo.” Mara wakasikia sauti ya mtu mwingine kutazama ni waiter wa pale hoteli waliopo ijulikana nayo kama “Mwambao hotel” iliopo upande wa pili kutazamana na Stand ya ma bus “Dar express”.
Waiter:”Jamani za jioni Kwema hapa!?”.Waiter aliuliza kwa sauti ya upole na kwa sauti ya ukarimu.
Nickson & Stela: ”Salama tu.” Wote waliiitikia kwa pamoja kama waliambizana kujibu hivyo.
Waiter:”Niwahudumie nini joini ya leo?”.
Nickson : “Kuku nusu kiasi gani?”. Nickson aliuliza akimwangalia waiter kwa makini asikie bei chapu apige hesabu ya fasta .
Waiter:”Ni 6000”. Waiter alijibu lakini akaongezea . “Kwa sasa kuku zimeisha ndugu labda kama hamtojali mchukue nyama choma nusu 5,000”.Nickson moyoni akajisemea kumbee bora hata bajeti itaaenda sawa sawia.
Nickson:”Sawa naomba hiyo hiyo”. Akamgeukia Stela na kumuambia. “Baby utakula na nini? “
Stela : “Na chipsi tu”. Stela alisema hivyo akizungusha macho maaana anajua ingekua mtu mwingine angeagiza nyama kilo na ndizi kama tano. Ili apate na ya kumbebea mdogo wake aliemwacha (Yunis) nyumbani.
Nickson:”Na mimi naomba na chipsi .” Alisema huku ana piga mahesabu yake “chipsi 2x2000 =4000 na nyama choma 5000 so inakuwa 9000 na soda moja 10,000 yake imeisha.”.Nickson akamgeukia mpenzi wake .
Nickson:”Baby unakunywa na soda gani?”.Alimuliza mpenzi wake kwa upendo na ujasiri kuwa bado yupo ndani ya bajet ya 10,000.
Stela : “Na grand malta.” Stela alijibu akiangalia upande mwingine wa hoteli ile ilokuwa bize kweli na ma bus yakishusha watu kutoka sehemu mbali mbali.Nickson moyoni alistuka kidogo akajisemea “Kiiiiibo na grand tena?”. Nickson akamwai waiter wakati stela akiangalia ma Bus “Mwambie haipo..” alisema kwa mdomo bila kutoa sauti.
Waiter:”Samahani Grand malta zimeisha”. Nickson akadakia fasta .
Nickson:”Leta na supa leta tu si ndio beby?. “alimuliza stela akiwa na confidence hawezi kataaa ndo soda aliokunywa walipo enda uzunguni park mara ya mwisho .
Stela :”Ndio na supa-leta ya moto tafadhali”.Stela alijibu akiwa hajui kuwa hana namna .
Waiter:”Sawa chipsi mbili na nyama choma na supa leta. Kaka utakunywa nini?”. Waiter alitaka kujua Nickson atakunywa nini.
Nickson:”Ah mi nina hii tayari”. Aliwahi kumwonesha soda ya takeaway alie kuja nayo .Sawa waiter akaondoka na kuwaacha wakiendelea mazungumzo yao.Nickson alitumia hizi sekunde kadhaaa akimwangalia mpenzi wake alivyo. Stela hyo siku alikua amevaaa suruali ya jeans inayombana nakuonesha umbo lake kiasi flani cha kuvutia . Alikua kavaa t-shirt ambayo Nickson alimpa kama zawadi imeandika na maaandishi kwa nyuma ikisema “ExonGraphics” ambalo ndo jina la kampuni ambalo Nickson anatarajia kufungua hivi punde.
Nickson:”Enhee mpenzi ulikua unasemaje?”. Stela alimgeukia taratibu akiwa anaonekana kuwa alizama kwenye kukuru-kakara za pale stand inayo tazamana na hotel waliiopo.
Stela:”Nataka ugali maharage”. Alijibu hapo wakaaanza kucheka yeye pamoja na Nickson wakikumbuka kipindi kile ambacho Stela alimjibu Nickson wakati huo bado mahusiano yao hayaja anza alikua akimtesa tu na vituko vya stela vya hapa na pale.
Stela:”Baby lakini kweli mi nakushauri uachane na hiyo project bora ufanye biashara nyingine kama kuchukua nguo kwenye soko la maimoria uje uuuze nipe hata mimi nitakuuzia. Pia ntakusaidia kuchagua.”
Nickson:”Lakini baby mimi nikipata Camera moja tu inanitosha kutoka katika maisha haya ”.Nickson alisema akiwa na matumaini.
Stela :”Kwani Camera kiasi gani?”. Aliuliza akitaka kujua yamkini ata weza kumpa ushauri.
Nickson : “Camera nzuri laki saba na lenzi laki tatu. “. Stela alianza tena kupandisha nyusi ya kulia akaweka nywele tena vizuri akanyoosha mkono kumuashiria Nickson aaache kuongea.
Stela : ”Sawa na umechanga sh ngapi mpaka sasa!? ”. Stela aliuliza huku amesogeza kichwa mbele na sikio linamtazamia Nickson asikie jibu kwa makini.
Nickson:”Ndo nimetoa laki na nusu sai….”. Stela akamkatisha.
Stela:”Baby iyo hela nyingine utapata wapi?”.
Nickson : “Ntajichanga tu Baby namwamini Mungu ”.Stela akawa ana guna mhhh mhhhh.
Stela: ”Sawa iyo hela yote uka nunue Camera uanze kutafuta wa kuwapiga picha na Studio huna na Laptop yako yenyewe ndo hyo……. ”. Stela ali kuwa kimya kidogo
Stela :” Baby kuwa mjanja umesoma mpaka umemaliza chuo umemaliza huezi kufanya vitu vya kijinga hivyo”.
Nickson : “Hayaaa sasa ushaaanza..”Nickson alijua tu wataaanza kugombana kisa mipango yake.
Stela : “Nishaanza nini? Afu nishakuambia usinikatishe nikiongea.”Stela aliendelea tu kuongea kama ana rap nyimbo anayoipenda.
Nickson: “Sasa mpenzi sikia nikuambie kitu mimi ntakupa hela uongeze na yako tuanze biashara”.
Stela : “Nickson mimi nitawezaje kutoa hela hapo na unajua dhahiri ya mimi ni secretary wa pale Matumizi Company ya Yule Mmasai Vicent Mbekure ”Stela alikua anaongea kudhibitisha hela ndogo alionayo .
Nickson:”Sawa Baby mimi nitafanya kukupa ”.Nickson sio wa maneno mengi sana na alijua mpenzi wake anataka kumwambia kitu gani.
Stela : “Sawa mimi ntaenda maimoria mwenyewe ukinipa ”. Mara waiter akaja
Waiter: ”Jamani chakula chenu kiko tayari. Munaweza kwenda kunawa pale mkihitaji waiter alisema hivyo akinyoshea mkono bomba la kunawia. “Jamani karibuni na mu enjoy.”
Nickson wakasimama wakaenda kunawa kama walivyoshauriwa wakala kwa kucheka kulishana hapa na pale. Mara wachokozane. Walipo maliza Nickson alilipa bill iliyo kuja kama alivyotegemea na kupigia mahesabu . Nickson akampa mpenzi wake nauli na pia akaanza kutembea kwa miguu kuelekea ghetto kwake.
Stela : “Baby kwaheri! Nimeshiba” . Alimwita Nickson aliokuwa ameanza kutafuta njia ya kwenda nyumbani kwake . Nickson akageuka aka mpulizia busu la hewani mpenziwe.
Itaendelea….