Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 152,886
- 453,430
SEHEMU YA 10
Alichokifanya ni kutafuta mazoea kwanza. Akajifanya anafika hapo mara kwa mara, azoeleke machoni kumbe upande wa pili alikuwa na mambo yake mengine.
Aisha hakujua mbinu za mwanaume huyo, alijua kwamba alipenda kufanya naye ngono kwa kuwa alijisikia kumbe kulikuwa na mengi yaliyokuwa yakiendelea nyuma ya pazia.
Kumpata nje na kwao ilikuwa ngumu hivyo alichokifanya ni kumuandaa kijana ambaye alimwambia angempelekea mwanamke wa kufanya naye mapenzi usiku kwa gharama zake.
“Yaani unilipie nifanye mapenzi na mwanamke?” aliuliza jamaa huyo huku akionekana kushtuka.
“Ndiyo! Hutaki nikamtafute mwingine?” aliuliza Massawe.
“Swali la kitoto sana hilo! Sasa kuna mwanaume anaweza kukataa mwanamke? Hebu mlete,” alisema kijana huyo.
Hakukuwa na tatizo, alichokifanya ni kuwasiliana na Aisha na kumwambia kwamba kulikuwa na mwanaume alihitaji kulala naye kwa malipo makubwa.
Kwa Aisha hakukuwa na tatizo, hayo yalikuwa maisha yake, aliyaendesha kwa kutumia mwili wake hivyo akakubaliana na Massawe na muda wa saa nne usiku akaondoka kwenda kuonana na mwanaume huyo katika Hoteli ya Zebra Lines iliyokuwa Kinondoni jijini Dar es Salaam.
“Nataka nilale na wewe mpaka asubuhi,” alisema kijana huyo huku akimwangalia Aisha.
“Hakuna shida. Uliambiwa malipo?”
“Hapana!”
“Elfu thelathini!”
“Haina shida!”
“Na chumba unalipia wewe!”
“Hakuna shida pia!” alisema kijana huyo aliyeonekana kuwa na uchu, kila alipomwangalia Aisha, jinsi alivyokuwa, mapaja yaliyonona, udenda ulikuwa ukimtoka.
Hakukuwa na muda wa kubaki hapo, moja kwa moja wakaingia hotelini, chumbani na kufanya starehe yao. Wakati walipokuwa wakiongea mpaka kwenda chumbani Massawe alikuwa akiwaangalia tu, alipoona wameondoka, haraka sana naye akaanza kuwahi nyumbani kwa Aisha.
Moyo wake ulikuwa na hamu ya kukutana na Bhoke, alichanganyikiwa, akili yake ilikuwa ikikifikiria kile kifua chake, alikitamani, katika maisha yake hakuwahi kufanya mapenzi na mwanamke aliyekuwa na kifua kama kile, hakujua ladha yake ilikuwaje hivyo ilikuwa ni lazima aijue kwa kwenda kufanya na huyo Bhoke.
Alichokifanya ni kutafuta mazoea kwanza. Akajifanya anafika hapo mara kwa mara, azoeleke machoni kumbe upande wa pili alikuwa na mambo yake mengine.
Aisha hakujua mbinu za mwanaume huyo, alijua kwamba alipenda kufanya naye ngono kwa kuwa alijisikia kumbe kulikuwa na mengi yaliyokuwa yakiendelea nyuma ya pazia.
Kumpata nje na kwao ilikuwa ngumu hivyo alichokifanya ni kumuandaa kijana ambaye alimwambia angempelekea mwanamke wa kufanya naye mapenzi usiku kwa gharama zake.
“Yaani unilipie nifanye mapenzi na mwanamke?” aliuliza jamaa huyo huku akionekana kushtuka.
“Ndiyo! Hutaki nikamtafute mwingine?” aliuliza Massawe.
“Swali la kitoto sana hilo! Sasa kuna mwanaume anaweza kukataa mwanamke? Hebu mlete,” alisema kijana huyo.
Hakukuwa na tatizo, alichokifanya ni kuwasiliana na Aisha na kumwambia kwamba kulikuwa na mwanaume alihitaji kulala naye kwa malipo makubwa.
Kwa Aisha hakukuwa na tatizo, hayo yalikuwa maisha yake, aliyaendesha kwa kutumia mwili wake hivyo akakubaliana na Massawe na muda wa saa nne usiku akaondoka kwenda kuonana na mwanaume huyo katika Hoteli ya Zebra Lines iliyokuwa Kinondoni jijini Dar es Salaam.
“Nataka nilale na wewe mpaka asubuhi,” alisema kijana huyo huku akimwangalia Aisha.
“Hakuna shida. Uliambiwa malipo?”
“Hapana!”
“Elfu thelathini!”
“Haina shida!”
“Na chumba unalipia wewe!”
“Hakuna shida pia!” alisema kijana huyo aliyeonekana kuwa na uchu, kila alipomwangalia Aisha, jinsi alivyokuwa, mapaja yaliyonona, udenda ulikuwa ukimtoka.
Hakukuwa na muda wa kubaki hapo, moja kwa moja wakaingia hotelini, chumbani na kufanya starehe yao. Wakati walipokuwa wakiongea mpaka kwenda chumbani Massawe alikuwa akiwaangalia tu, alipoona wameondoka, haraka sana naye akaanza kuwahi nyumbani kwa Aisha.
Moyo wake ulikuwa na hamu ya kukutana na Bhoke, alichanganyikiwa, akili yake ilikuwa ikikifikiria kile kifua chake, alikitamani, katika maisha yake hakuwahi kufanya mapenzi na mwanamke aliyekuwa na kifua kama kile, hakujua ladha yake ilikuwaje hivyo ilikuwa ni lazima aijue kwa kwenda kufanya na huyo Bhoke.