Hadithi: Maisha yangu nyuma ya pazia jeusi

MAISHA YANGU NYUMA YA PAZIA JEUSI

SEHEMU YA 07

Ilipoishia….

“ Ingrid, hivi unadhani mimi si mwanadamu? Au unadhani mimi nafurahi kukuona una huzuni kwa ajili yangu? Hata mimi naumia pia, lakini ni bora maumivu haya unayoyapata sasa kuliko hayo ambayo utayapata baadae kwa kuwa na mimi. Umeamua kutangaza kuvunja urafiki wetu kwa jambo hili dogo, sawa. Lakini nakuomba utambue kuwa unanionea, haunitendei haki hata kidogo. Najua hatuwezi acha kuonana kila siku…lakini jaribu kufikiria mimi nitakuwa najisikiaje pale ambapo nitakuwa nakuona? Anyway… nipo tayari kukupa ukweli wangu wote nyuma ya maamuzi yangu siku yoyote ile ambapo utahitaji na kama ratiba yangu itaruhusu. Baada ya hapo unaweza kuendelea na msimamo wako wa kukata mahusiano na ukaribu wetu. Vinginevyo, nita’miss’ vitu vingi kutoka kwako rafiki yangu, Ingrid” sikutaka kumpa nafasi aijibu hoja hii,ilikata simu, nikaizima, nikalala.

Endelea…..

Asubuhi iliyofuata niliamka nikiwa na uchovu kwa kiasi fulani hivi. Nilichoamua kukifanya kwanza ni kufungua simu kisha nilitoka nje ili kufanya mambo mengine kama kuswaki na kuoga. Baada ya kukamilisha yote hayo nilirudi ndani na kukuta simu yangu kwenye kioo ikionyesha kuwa kulikuwa na jumbe mpya tatu za kawaida. Nilizifungua ili kujua ni nini kilikuwa kimeandikwa huko ndani na ni nani aliyekuwa amezituma.

Alikuwa ni Ingrid, ndiyo Ingrid. Msichana ambaye jana usiku alijiapiza kuwa hatowasiliana na mimi kamwe. Jumbe zote zilionyesha kuwa zilitumwa jana usiku. ujumbe wa kwanza ulisema ‘mbona umekata simu sasa’ ujumbe wa pili ulisema ‘barry, ndo umeamua kunizimia simu kabisa sio?’ na ya tatu ilisema ‘ipo siku utalipa kwa maumivu haya unayonisababishia’.

Nilisoma jumbe hizo huku nikiwa natabasamu, yaani mtu aliyekuwa aliyejiapiza kuwa ananichukia sana na pia hatonitafuta tena alikuwa ametuma jumbe tatu mfululizo. Lakini kiuhalisia hiyo ndiyo rangi halisi ya wanawake. Mwanamke anaweza kukwambia ndiyo ilhali akimaanisha hapana au anakwambia hapana ilhali anamaanisha ndiyo, mwanamke anaweza kukukasirikia usoni lakini moyoni anakufurahia au anaweza kuonyesha tabasamu usoni lakini moyoni anakuchukia pasi mfano. Hivyo ndivyo walivyo, kuna nyakati ni ngumu sana kutambua ni nini hasa kinaendelea ndani ya mioyo yao.

Hata hivyo jumbe zake zilinipa nguvu kwa kuwa nilikuwa nimebaki na hatua moja tu ya kukamilisha lengo langu la kumtoa Ingrid katika zone ya yeye kuwa mpenzi wangu na pia aendelee kuwa rafiki yangu. Nilijiona mshindi katika hili.

Japo alikuwa anakuja katika njia niliyokuwa naitaka lakini sikutaka kujibu jumbe zake kwani ule ulikuwa ni mchezo wa hisia na nilipaswa kuucheza kwa umahiri ili nishinde mechi katika dakika za awali kabisa. Nilimaliza kujiandaa kisha nikaenda zangu kazini kama kawaida. Baada ya kufika eneo langu la kazi nilianza kutekeleza majukumu ya kawaida ya kila siku. Ilipofika saa nne na dakika zake hivi niliona simu yangu ikiita…nikaangalia kwenye kioo, alikuwa ni Ingrid. Akili yangu ilivurugika ghafla maana nilijua ni lazima atakuja na malalamiko mengi kabisa. Nilitaka nisiipokee simu yake lakini nikaona kwamba kama nisipopokea nitaongeza matatizo hivyo ni heri niipokee tu.

Nilipokea simu kusikiliza huyu mwanamke alikuwa na mashitaka gani tena.

“hi barry, mzima wewe?” alisema akiwa na furaha hadi nikajiuliza kwani leo imekuwaje. Kwa jinsi tulivyoachana jana usiku sikutarajia kama angekuwa katika hali kama ile.

“mi mzima tu ndugu yangu” nilisema kwa sauti ya kuchangamka ili kwenda naye sawa ilhali kichwani nikiwa bado nawaza ni nini kimemfurahisha yeye asubuhi asubuhi.

“daaah, barry nina furaha sana leo, yaani we acha tu” alisema huku akionyesha ni kweli alikuwa na furaha. Hata mimi nilijikuta natabasamu kama zoba huku nikiwa sijui ni nini kinanifanya nitabasamu.

“hivyo ndo inavyotakiwa, siyo unakaa umenyong’nyea kama unadaiwa madeni, haya nimegee na mimi nifurahi basi rafiki yangu mwenyewe” niliongea kwa bashasha huku nikiongeza kicheko cha kinafki.

“leo matokeo yetu yamatoka, na nimefanya vizuri….yaani hadi siamini” alisema Ingrid akizidi kuidhihirisha furaha yake. Dooh kumbe ni mambo ya shule tena. Mimi shule niliitupaga mkono japokuwa nafsi haikuwa imependa, na nilikuwa natamani sana siku na mimi ningekuwa darasani na nifikie hatua kama yake lakini haikuwezekana.

Munkari ulishuka, japokuwa niliendelea kushikilia kiwango kilekile cha hisia nilichokuwa nacho mwanzo ili ingrid asinigundue kama kuna jambo kwa upande wangu halikuwa sawa. “safi sana ingrid, umepata division ngapi” nilimuuliza.

“one’ alijibu.

“hongera sana aisee, kumbe una miakili mingi hivi! kwa hiyo chuooo kileeeeeee, utakweda kusomea nini madame?”

“mi hata sielewi yaani, ila napenda sana sheria na mambo ya pesa pesa”

“sheria, unataka kuja kumfunga nani, mimi?” nilimtania.

“yaani wewe ndo utakuwa wa kwanza kabisa. Yaani jinsi unavyoninyanyasa mimi na hisia zangu siku nikipata safasi lazima uozee jela nakwambia” aliogea kwa utani lakini iliyokuwa na hisia za maumivu ndani yake.

“aisee, haina shida madame. Hata ukinihukumu kunyongwa mpaka kufa ni sawa tu maana sheria utakuwa nayo mikononi mwako” Nilikubaliana na mtazamo wake. Niliwahi kuambiwa kuwa ukitaka kumaliza migogoro isiyo ya lazima, kubaliana na kile mgomvi wako anakisema juu yako.

“barry, yaani nilianza kukuchukia lakini nimejikuta nashindwa, barry wewe ni mwanaume gani lakini?, unatongozwa na mwanamke unakataa?, na sijui hicho kitu unachotaka kuniambia kitakuwa na matokeo gani kwa upande wangu” aliongea kwa sauti ambayo nilikuwa nimeizoea, sauti ya mahaba yaliyojaa unyonge. Tayari tulikuwa tumesharudi kwenye uwanja wa nyumbani, uwanja uliojaa hisia za upendo na malalamiko.

“Ingrid, mimi nakujali kuliko unavyofikiria, na siku hiyo utajua tu kwa nini huwa nayasema yale ninayoyasema…..”

“si uniambie sasa hivi”

“Sasa hivi ni saa za kazi, pia ni story ndefu kidogo, so inahitaji muda pia”

“kwa hiyo ni lini?”

“nadhani jumapili hii, baada ya kutoka kanisani”

“mmmmh….haya sawa, maana hata kama nikipinga wewe ni kichwa ngumu, huwezi nielewa, sawa tu” wakati anayaongea hayo kuna mteja alifika pale akiwa anahitaji huduma, nikaamua kukatizo mazungumzo . “hapana ingridi, unanielewa vibaya, badae madame..niache nitimize wajibu kwanza” nikakata simu na kuendelea kumhudunia mteja. Niliendelea kufanya kazi yangu kwa moyo wote na ilipofika jioni nikaenda kukabidhi hesabu kwa bosi kama kawaida kisha nikarudi zangu geto. Siku zilizidi kusonga huku nikijaribu kujiweka mbali na Ingrid maana niligundua kuwa kadri nilivyokuwa najiweka karibu naye ndivyo alivyokuwa akipata matumaini ya kuwa huenda mimi na yeye tutakuwa pamoja.

Hatimaye siku ikafika, sikutaka kwenda kanisani. Niliamka asubuhi nikafanya usafi na nikaendelea kujiandalia kifungua kinywa. Nilifanya hayo huku nikiperuzi kwenye mtandao wa jamiiforums. Jamiforums ilikuwa ni sehemu ambayo nilikuwa naitumia kama sehemu ya kuniondolea msongo wa mawazo. Si kwamba nilikuwa naperuzi tu kama mgeni bali nilikuwa mwanachama kabisa, nilikuwa natumia jina la ‘Jiwe la gizani’. Japo sikuwa na muda mrefu sana tangu nijiunge jf lakini nilikuwa nimeanza kuwa maarufu kutokana na nyuzi zangu zenye story zilizojaa ucheshi. Watu wengi walikuwa wakivutiwa nazo. Japo kile nilichokuwa nakiandika hakikuwa na uhalisia katika maisha yangu lakini nilikuwa nafurahi kwa sababu nilichukulia kama sehemu ya burudani kwangu na kwa wasomaji wengine. Wakati naperuzi katika uzi wa picha za vituko, simu yangu iliita. Alikuwa ni ingrid,…nikapokea.

“mambo barry” alinisalimia

“ni gud madame, lete habari..”

“safi, twende kanisani” alisema Ingrid

“leo mimi sijisikii kwenda” ilimjibu

“kwa nini?”

“jana nilichoka sana so nimeamka na uchovu” nilidanganya.

“mh, haya. Kwa hiyo leo nitatembea peke yangu?” aliiuliza kwa sauti yeye deko la kike.

“kaniombee tu madame” sikumjibu swali lake ila nilimwambia hivyo hili ahitimishe maongezi yake.

“unakumbuka leo ndiyo siku uliyoniahidi kuwa utaniambia kwa kina kuhusu ile ishu”

“yeah, nakumbuka vyema kabisa”

“saa ngapi sasa?”

“ukitoka kanisani”

“usije ukaondoka sasa maana wewe akili yako unaijua mwenyewe”

“nani kakwambia tunakuja kuongelea nyumbani? Tunatakiwa kutoka nje ya hapa, mazingira ya hapa si rafiki kabisa”

“mmmmh!..... hivi unadhani kupata ruhusa kutoka kwa baba ni jambo rahisi,?”

“kama ikishindikana basi”

“mmmh una roho mbaya wewe, ok ngoja nitajaribu. Ni wapi huko tutaenda?” aliuliza.

“nadhani itakuwa vizuri kama tutaenda sehemu iliyotulia kama ufukweni hivi”

“kuna fukwe nyingi sana lakini” alisema Ingrid. Nilimtajia ufukwe ambao niliona unafaa kwa kuzingatia umbali kutoka eneo tuliloishi. “mhh..haya, niombee nipate ruhusa” alisema Ingrid. Nikamhakikishia kuwa nitafanya hivyo kisha tukaagana na kukata simu.

Baada ya kukata simu, simu yangu ilinirudisha kwenye ukurasa wa jamiiforums ambao nilikuwa naupitia kabla ya simu ya Ingrid kuingia lakini niliamua kutokuendelea kuperuzi kwa kuwa akili yangu ilitekwa na jambo jingine. Nilifikiria kile ambacho ningeenda kumwambia Ingrid. Nikajikuta mnyonge ghafla. Lilikuwa ni jambo ambalo nilikuwa sipendi kabisa kulisimulia ila nililazimika kutokana na jinsi Ingrid alivyokuwa, alikuwa ni king’aganizi mno. Hivyo kwa wakati huo hiyo ndiyo ilikuwa ndiyo njia pekee ya mimi kujinasua kwake. Niliamini kama angekisikia kisa hicho angenielewa na kuniacha huru.

Hali ya kulifikiria tukio hili ilisababisha nifungue begi na kutoa bahasha ambayo ndiyo ilikuwa ni kielelezo na kumbukumbu pekee niliyokuwa nayo kuhusu tukio lile. Nikaifunngua nikavitoa vilivyokuwamo, nikavitandaza chini sakafuni kisha nikawa naviangalia. Jinsi nilivyokuwa naviangalia ndivyo nilizidi kuchochea hisia za maumivu na majuto ambayo yaliweka kambi ndani yangu kwa muda mrefu. Hisia hizi zilikuja kwa nguvu kubwa kiasi nilishindwa kuyazuia machozi. Kuna msemo kuwa kila mtu ana sehemu ya udhaifu wake, na ule ndiyo ulikuwa udhaifu wangu. Mara zote nilijikuta mnyonge sana mbele ya tukio lile.

Nilifumba macho huku nikiendelea kuyahisi machozi yakiwa yanatiririka taratibu kwenye mashavu yangu. Kisha taratibu nikaanza kuona taswira ya msichana ikiwa katika hali iliyofifia. Kadri muda ilivyozidi kwenda taswira ile ilianza kuonekana dhahiri kiasi cha kuweza kumtambua, alikuwa ni Jennifer. Jennifer alionekana akibubujikwa na machozi zaidi yangu mimi huku akionyesha ishara za kunilalamikia.

“damn, what the f..” niliongea kwa sauti kubwa huku nikirusha mikono. Na kwa kuwa niliongea kwa sauti kubwa sana nilijistukia na nikaamua nisiimalizie sentensi hiyo. Nilikuwa nahema kwa sauti kubwa sana. Nilijifuta machozi huku nikivurudisha vile vitu kwenye bahasha na kisha nikairudishia bahasha kwenye begi.

Niliendelea kuandaa kifungua kinywa huku nikiwa siko sawa kihisia.

Masaa yakasonga, asubuhi ikaondoka kinyonge huku ikiukaribisha mchana. Jua likawaka na joto likazidi kuongezeka. Siku hiyo sikujisikia kabisa kujiandalia chakula cha mchana hivyo nikatoka kwenda kwa mama’ntilie ambaye nilikuwa nakwenda kila mara kama ikitokea siku hiyo sijisikii kupika. Na kwa kuwa muda ulikuwa umeenda hivyo niliamua kuunganisha safari kwamba nikitoka hapo niunganishe moja kwa moja kwenda kwenye eneo la miadi.

Nilipomaliza kula nilichukua usafiri wa umma nikasogea eneo la miadi yangu na Ingrid. Nikashuka nikatembea kwa miguu hadi nilipofika eneo rasmi tulilokubaliana. Muda wote huu nilikuwa nawasiliana na Ingrid kwa njia ujumbe mfupi. Aliniambia kuwa baba yake alimruhusu lakini kwa masharti ya kuwa awe amefika nyumbani kabla ya saa moja usiku. Pia aliniambia kuwa alipata ruhusa hiyo kwa kumdanganya baba yake kuwa anaenda kumtembelea rafiki yake na akanisisitiza kuwa muda uzingatiwe. Nikamhakikishia kuwa mambo yatakuwa sawa.

Nilikaa kumsubiri huku nikiangalia madhari ya ufukwe, niliwatazama watu waliokuja na wapenzi wao kujivinjari. Kuna walikuwa wanacheza michezo ya kimahaba, kuna waliokuwa wamekaa huku wakiongea, ilimradi kila mtu alijaribu kumuonyesha ni kwa jinsi gani anampenda na kumjali mwenzi wake. Lakini kwangu ilikuwa ni kinyume, yaani wakati watu wengine wanawaleta watu wao kuja kuimarisha mapenzi yao, mimi nilikuwa nimemwita Ingrid pale kuja kuliua penzi lake changa alilokuwa nalo juu yangu. Kweli binadamu tunafanana lakini hatupo sawa. Nilitembea huku mikono nikiwa nimeitumbukiza kwenye mifuko ya suruali huku masikio yangu yakiwa yanaburudishwa na sauti za mawimbi ya maji yaliyokuwa yakipiga kwenye ufuo. Bahari iliniburudisha kiasi chake ikizingatiwa kuwa mimi nilikulia maeneo ya kanda ya kati ambako kulikuwa na mazingira ya ukame hivyo kuona eneo kubwa la ardhi lililojazwa maji halikuwa jambo nililoweza kulishuhudia. Macho yangu yalizoea kuona madimbwi na mabwawa madogo madogo.

Ilikuwa na saa tisa na dakika zake hivi wakati Ingrid aliponipigia na kuniambia kuwa alikuwa amefika eneo ambalo tulitakiwa tuonane. Nilimuelekeza mahali ambapo nilikuwepo, dakika kadhaa baadaye alifika mahali nilipokuwepo. Alikuwa amevalia vyema kiasi cha kuongeza mvuto wake ambao nilizoea kuuona kila siku. Alivalia gauni la urefu wa saizi ya magoti lenye rangi nyekundu, rangi inayotafririwa kuwa ni rangi ya upendo japo kua wakati rangi hii huashiria uovu. Hii ni kwa sababu upendo na chuki, vyote kwa pamoja hutembea katika damu. Urefu wa gauni lake ulifanya miguu yake iliyojaa vyema kuonekana dhahiri kabisa, watoto wa mjini huiita miguu ya bia. Miguuni alivalia viatu vyepesi visivyo na visigino virefu vilevyokuwa na rangi nyeusi. Nywele alizisuka kwa mtindo ambao hadi sasa sijawahi kuufahamu, labda ni kwa sababu mimi siyo mfuatiliaji sana wa mambo ya urembo kwa wanawake. Kwa ujumla, Ingrid alikuwa ni mwanamke wa ndoto kwa wanaume wengi. Ingrid alikiwa amekamilika katika mwonekano wake na mitazamo yake.

Alinisalimia, nikapokea salamu yake nikiwa na uso wa furaha sana. Bila kusubiri maongezi zaidi nilimshika mkono na kumpeleka mahali ambapo nilipachagua kwa ajili ya sisi kukaa. Palikuwa ni mbali na bugudha za watu waliokuwa wanaogelea na kufanya mambo mengine ya starehe. Niliamua kufanya matendo ya kirafiki ili kuhakikisha kuwa Ingrid hajisikii vibaya. Tulifika mahali tulipokuwa tunaelekea, tukakaa kwenye mchanga safi wa ufukwe. Ingrid alikaa upande wa wangu wa kushoto akaweka mikono yake juu ya mikono yangu kisha akaegesha kichwa chake kwenye bega langu. Nami nikanyanyua mkono wangu wa kushoto kisha nikauzungusha mabegani mwake kama sehemu ya kumuunga mkono. Sasa tulikuwa ni muungano haswa. Hisia zetu ziliunganika na kutengeneza hisia moja, hisia ya penzi lililojaa mtanziko. Niliamua kuvunja ukimya kabla ya yeye hajafanya hivyo.

“Ingrid” nilimwita

“sema babaa” aliitika huku akiniangalia usoni. Sauti aliyoitumia kutamka hiyo setensi fupi ilinifanya nipoteze kumbukumbu ya kile nilichokuwa nataka kukisema. Nilikaa kimya kwa muda huku nikijaribu kuvuta kumbukumbu ya nini nilitaka kukisema. Baada ya sekunde kadhaa, nilikumbuka na nikaendelea kuongea.

“mara zote umekuwa ukiniona mimi ni mtu nisiyejali hisia zako, ama nakufanyia makusudi kwa kuwa najua kuwa unanipenda mimi sana. Si kweli, leo nataka kukupa kisa kilichonikuta na kufanya niwe mgumu kukubaliana na wewe. Nadhani tukishatoka hapa utakuwa unaelewa ni kwa nini nakuwa mzito sana kukualiana na wewe.” Niliongea huku mkono wangu wa kushoto ukitambaa taratibu katika bega la Ingrid hali iliyofanya Ingrid azidi kutulia.

“barry, nipo hapa kukusikiliza. Lakini nadhani wajua ni jinsi gani ninavyokupenda” aliongea huku akiupapasa mikono yangu.

“najua, najua Ingrid. Ndiyo maana nimekuita hapa ili nikushirikishe jambo hili kubwa sana katika maisha yagu” niliongea huku macho yangu yakiwa yanaangalia mawimbi ya bahari. Niliendelea kuangalia upande wa bahari, nikazidi kuangalia mawimbi yalivyokuwa yakitembea kwa kasi kuja na kurudi. Nilifanya yote haya ili kuvuta kumbukumbu zote za tukio zima ili nisisahau hata tukio moja. Nilipanga kumwambia kila kitu.

Baada ya kuwa na hakika kuwa nilikuwa nakumbuka kila kitu nikaanza kusimulia.

Miaka sita iliyopita..

Itaendelea…..
 
MAISHA YANGU NYUMA YA PAZIA JEUSI

SEHEMU YA 07

Ilipoishia….

“ Ingrid, hivi unadhani mimi si mwanadamu? Au unadhani mimi nafurahi kukuona una huzuni kwa ajili yangu? Hata mimi naumia pia, lakini ni bora maumivu haya unayoyapata sasa kuliko hayo ambayo utayapata baadae kwa kuwa na mimi. Umeamua kutangaza kuvunja urafiki wetu kwa jambo hili dogo, sawa. Lakini nakuomba utambue kuwa unanionea, haunitendei haki hata kidogo. Najua hatuwezi acha kuonana kila siku…lakini jaribu kufikiria mimi nitakuwa najisikiaje pale ambapo nitakuwa nakuona? Anyway… nipo tayari kukupa ukweli wangu wote nyuma ya maamuzi yangu siku yoyote ile ambapo utahitaji na kama ratiba yangu itaruhusu. Baada ya hapo unaweza kuendelea na msimamo wako wa kukata mahusiano na ukaribu wetu. Vinginevyo, nita’miss’ vitu vingi kutoka kwako rafiki yangu, Ingrid” sikutaka kumpa nafasi aijibu hoja hii,ilikata simu, nikaizima, nikalala.

Endelea…..

Asubuhi iliyofuata niliamka nikiwa na uchovu kwa kiasi fulani hivi. Nilichoamua kukifanya kwanza ni kufungua simu kisha nilitoka nje ili kufanya mambo mengine kama kuswaki na kuoga. Baada ya kukamilisha yote hayo nilirudi ndani na kukuta simu yangu kwenye kioo ikionyesha kuwa kulikuwa na jumbe mpya tatu za kawaida. Nilizifungua ili kujua ni nini kilikuwa kimeandikwa huko ndani na ni nani aliyekuwa amezituma.

Alikuwa ni Ingrid, ndiyo Ingrid. Msichana ambaye jana usiku alijiapiza kuwa hatowasiliana na mimi kamwe. Jumbe zote zilionyesha kuwa zilitumwa jana usiku. ujumbe wa kwanza ulisema ‘mbona umekata simu sasa’ ujumbe wa pili ulisema ‘barry, ndo umeamua kunizimia simu kabisa sio?’ na ya tatu ilisema ‘ipo siku utalipa kwa maumivu haya unayonisababishia’.

Nilisoma jumbe hizo huku nikiwa natabasamu, yaani mtu aliyekuwa aliyejiapiza kuwa ananichukia sana na pia hatonitafuta tena alikuwa ametuma jumbe tatu mfululizo. Lakini kiuhalisia hiyo ndiyo rangi halisi ya wanawake. Mwanamke anaweza kukwambia ndiyo ilhali akimaanisha hapana au anakwambia hapana ilhali anamaanisha ndiyo, mwanamke anaweza kukukasirikia usoni lakini moyoni anakufurahia au anaweza kuonyesha tabasamu usoni lakini moyoni anakuchukia pasi mfano. Hivyo ndivyo walivyo, kuna nyakati ni ngumu sana kutambua ni nini hasa kinaendelea ndani ya mioyo yao.

Hata hivyo jumbe zake zilinipa nguvu kwa kuwa nilikuwa nimebaki na hatua moja tu ya kukamilisha lengo langu la kumtoa Ingrid katika zone ya yeye kuwa mpenzi wangu na pia aendelee kuwa rafiki yangu. Nilijiona mshindi katika hili.

Japo alikuwa anakuja katika njia niliyokuwa naitaka lakini sikutaka kujibu jumbe zake kwani ule ulikuwa ni mchezo wa hisia na nilipaswa kuucheza kwa umahiri ili nishinde mechi katika dakika za awali kabisa. Nilimaliza kujiandaa kisha nikaenda zangu kazini kama kawaida. Baada ya kufika eneo langu la kazi nilianza kutekeleza majukumu ya kawaida ya kila siku. Ilipofika saa nne na dakika zake hivi niliona simu yangu ikiita…nikaangalia kwenye kioo, alikuwa ni Ingrid. Akili yangu ilivurugika ghafla maana nilijua ni lazima atakuja na malalamiko mengi kabisa. Nilitaka nisiipokee simu yake lakini nikaona kwamba kama nisipopokea nitaongeza matatizo hivyo ni heri niipokee tu.

Nilipokea simu kusikiliza huyu mwanamke alikuwa na mashitaka gani tena.

“hi barry, mzima wewe?” alisema akiwa na furaha hadi nikajiuliza kwani leo imekuwaje. Kwa jinsi tulivyoachana jana usiku sikutarajia kama angekuwa katika hali kama ile.

“mi mzima tu ndugu yangu” nilisema kwa sauti ya kuchangamka ili kwenda naye sawa ilhali kichwani nikiwa bado nawaza ni nini kimemfurahisha yeye asubuhi asubuhi.

“daaah, barry nina furaha sana leo, yaani we acha tu” alisema huku akionyesha ni kweli alikuwa na furaha. Hata mimi nilijikuta natabasamu kama zoba huku nikiwa sijui ni nini kinanifanya nitabasamu.

“hivyo ndo inavyotakiwa, siyo unakaa umenyong’nyea kama unadaiwa madeni, haya nimegee na mimi nifurahi basi rafiki yangu mwenyewe” niliongea kwa bashasha huku nikiongeza kicheko cha kinafki.

“leo matokeo yetu yamatoka, na nimefanya vizuri….yaani hadi siamini” alisema Ingrid akizidi kuidhihirisha furaha yake. Dooh kumbe ni mambo ya shule tena. Mimi shule niliitupaga mkono japokuwa nafsi haikuwa imependa, na nilikuwa natamani sana siku na mimi ningekuwa darasani na nifikie hatua kama yake lakini haikuwezekana.

Munkari ulishuka, japokuwa niliendelea kushikilia kiwango kilekile cha hisia nilichokuwa nacho mwanzo ili ingrid asinigundue kama kuna jambo kwa upande wangu halikuwa sawa. “safi sana ingrid, umepata division ngapi” nilimuuliza.

“one’ alijibu.

“hongera sana aisee, kumbe una miakili mingi hivi! kwa hiyo chuooo kileeeeeee, utakweda kusomea nini madame?”

“mi hata sielewi yaani, ila napenda sana sheria na mambo ya pesa pesa”

“sheria, unataka kuja kumfunga nani, mimi?” nilimtania.

“yaani wewe ndo utakuwa wa kwanza kabisa. Yaani jinsi unavyoninyanyasa mimi na hisia zangu siku nikipata safasi lazima uozee jela nakwambia” aliogea kwa utani lakini iliyokuwa na hisia za maumivu ndani yake.

“aisee, haina shida madame. Hata ukinihukumu kunyongwa mpaka kufa ni sawa tu maana sheria utakuwa nayo mikononi mwako” Nilikubaliana na mtazamo wake. Niliwahi kuambiwa kuwa ukitaka kumaliza migogoro isiyo ya lazima, kubaliana na kile mgomvi wako anakisema juu yako.

“barry, yaani nilianza kukuchukia lakini nimejikuta nashindwa, barry wewe ni mwanaume gani lakini?, unatongozwa na mwanamke unakataa?, na sijui hicho kitu unachotaka kuniambia kitakuwa na matokeo gani kwa upande wangu” aliongea kwa sauti ambayo nilikuwa nimeizoea, sauti ya mahaba yaliyojaa unyonge. Tayari tulikuwa tumesharudi kwenye uwanja wa nyumbani, uwanja uliojaa hisia za upendo na malalamiko.

“Ingrid, mimi nakujali kuliko unavyofikiria, na siku hiyo utajua tu kwa nini huwa nayasema yale ninayoyasema…..”

“si uniambie sasa hivi”

“Sasa hivi ni saa za kazi, pia ni story ndefu kidogo, so inahitaji muda pia”

“kwa hiyo ni lini?”

“nadhani jumapili hii, baada ya kutoka kanisani”

“mmmmh….haya sawa, maana hata kama nikipinga wewe ni kichwa ngumu, huwezi nielewa, sawa tu” wakati anayaongea hayo kuna mteja alifika pale akiwa anahitaji huduma, nikaamua kukatizo mazungumzo . “hapana ingridi, unanielewa vibaya, badae madame..niache nitimize wajibu kwanza” nikakata simu na kuendelea kumhudunia mteja. Niliendelea kufanya kazi yangu kwa moyo wote na ilipofika jioni nikaenda kukabidhi hesabu kwa bosi kama kawaida kisha nikarudi zangu geto. Siku zilizidi kusonga huku nikijaribu kujiweka mbali na Ingrid maana niligundua kuwa kadri nilivyokuwa najiweka karibu naye ndivyo alivyokuwa akipata matumaini ya kuwa huenda mimi na yeye tutakuwa pamoja.

Hatimaye siku ikafika, sikutaka kwenda kanisani. Niliamka asubuhi nikafanya usafi na nikaendelea kujiandalia kifungua kinywa. Nilifanya hayo huku nikiperuzi kwenye mtandao wa jamiiforums. Jamiforums ilikuwa ni sehemu ambayo nilikuwa naitumia kama sehemu ya kuniondolea msongo wa mawazo. Si kwamba nilikuwa naperuzi tu kama mgeni bali nilikuwa mwanachama kabisa, nilikuwa natumia jina la ‘Jiwe la gizani’. Japo sikuwa na muda mrefu sana tangu nijiunge jf lakini nilikuwa nimeanza kuwa maarufu kutokana na nyuzi zangu zenye story zilizojaa ucheshi. Watu wengi walikuwa wakivutiwa nazo. Japo kile nilichokuwa nakiandika hakikuwa na uhalisia katika maisha yangu lakini nilikuwa nafurahi kwa sababu nilichukulia kama sehemu ya burudani kwangu na kwa wasomaji wengine. Wakati naperuzi katika uzi wa picha za vituko, simu yangu iliita. Alikuwa ni ingrid,…nikapokea.

“mambo barry” alinisalimia

“ni gud madame, lete habari..”

“safi, twende kanisani” alisema Ingrid

“leo mimi sijisikii kwenda” ilimjibu

“kwa nini?”

“jana nilichoka sana so nimeamka na uchovu” nilidanganya.

“mh, haya. Kwa hiyo leo nitatembea peke yangu?” aliiuliza kwa sauti yeye deko la kike.

“kaniombee tu madame” sikumjibu swali lake ila nilimwambia hivyo hili ahitimishe maongezi yake.

“unakumbuka leo ndiyo siku uliyoniahidi kuwa utaniambia kwa kina kuhusu ile ishu”

“yeah, nakumbuka vyema kabisa”

“saa ngapi sasa?”

“ukitoka kanisani”

“usije ukaondoka sasa maana wewe akili yako unaijua mwenyewe”

“nani kakwambia tunakuja kuongelea nyumbani? Tunatakiwa kutoka nje ya hapa, mazingira ya hapa si rafiki kabisa”

“mmmmh!..... hivi unadhani kupata ruhusa kutoka kwa baba ni jambo rahisi,?”

“kama ikishindikana basi”

“mmmh una roho mbaya wewe, ok ngoja nitajaribu. Ni wapi huko tutaenda?” aliuliza.

“nadhani itakuwa vizuri kama tutaenda sehemu iliyotulia kama ufukweni hivi”

“kuna fukwe nyingi sana lakini” alisema Ingrid. Nilimtajia ufukwe ambao niliona unafaa kwa kuzingatia umbali kutoka eneo tuliloishi. “mhh..haya, niombee nipate ruhusa” alisema Ingrid. Nikamhakikishia kuwa nitafanya hivyo kisha tukaagana na kukata simu.

Baada ya kukata simu, simu yangu ilinirudisha kwenye ukurasa wa jamiiforums ambao nilikuwa naupitia kabla ya simu ya Ingrid kuingia lakini niliamua kutokuendelea kuperuzi kwa kuwa akili yangu ilitekwa na jambo jingine. Nilifikiria kile ambacho ningeenda kumwambia Ingrid. Nikajikuta mnyonge ghafla. Lilikuwa ni jambo ambalo nilikuwa sipendi kabisa kulisimulia ila nililazimika kutokana na jinsi Ingrid alivyokuwa, alikuwa ni king’aganizi mno. Hivyo kwa wakati huo hiyo ndiyo ilikuwa ndiyo njia pekee ya mimi kujinasua kwake. Niliamini kama angekisikia kisa hicho angenielewa na kuniacha huru.

Hali ya kulifikiria tukio hili ilisababisha nifungue begi na kutoa bahasha ambayo ndiyo ilikuwa ni kielelezo na kumbukumbu pekee niliyokuwa nayo kuhusu tukio lile. Nikaifunngua nikavitoa vilivyokuwamo, nikavitandaza chini sakafuni kisha nikawa naviangalia. Jinsi nilivyokuwa naviangalia ndivyo nilizidi kuchochea hisia za maumivu na majuto ambayo yaliweka kambi ndani yangu kwa muda mrefu. Hisia hizi zilikuja kwa nguvu kubwa kiasi nilishindwa kuyazuia machozi. Kuna msemo kuwa kila mtu ana sehemu ya udhaifu wake, na ule ndiyo ulikuwa udhaifu wangu. Mara zote nilijikuta mnyonge sana mbele ya tukio lile.

Nilifumba macho huku nikiendelea kuyahisi machozi yakiwa yanatiririka taratibu kwenye mashavu yangu. Kisha taratibu nikaanza kuona taswira ya msichana ikiwa katika hali iliyofifia. Kadri muda ilivyozidi kwenda taswira ile ilianza kuonekana dhahiri kiasi cha kuweza kumtambua, alikuwa ni Jennifer. Jennifer alionekana akibubujikwa na machozi zaidi yangu mimi huku akionyesha ishara za kunilalamikia.

“damn, what the f..” niliongea kwa sauti kubwa huku nikirusha mikono. Na kwa kuwa niliongea kwa sauti kubwa sana nilijistukia na nikaamua nisiimalizie sentensi hiyo. Nilikuwa nahema kwa sauti kubwa sana. Nilijifuta machozi huku nikivurudisha vile vitu kwenye bahasha na kisha nikairudishia bahasha kwenye begi.

Niliendelea kuandaa kifungua kinywa huku nikiwa siko sawa kihisia.

Masaa yakasonga, asubuhi ikaondoka kinyonge huku ikiukaribisha mchana. Jua likawaka na joto likazidi kuongezeka. Siku hiyo sikujisikia kabisa kujiandalia chakula cha mchana hivyo nikatoka kwenda kwa mama’ntilie ambaye nilikuwa nakwenda kila mara kama ikitokea siku hiyo sijisikii kupika. Na kwa kuwa muda ulikuwa umeenda hivyo niliamua kuunganisha safari kwamba nikitoka hapo niunganishe moja kwa moja kwenda kwenye eneo la miadi.

Nilipomaliza kula nilichukua usafiri wa umma nikasogea eneo la miadi yangu na Ingrid. Nikashuka nikatembea kwa miguu hadi nilipofika eneo rasmi tulilokubaliana. Muda wote huu nilikuwa nawasiliana na Ingrid kwa njia ujumbe mfupi. Aliniambia kuwa baba yake alimruhusu lakini kwa masharti ya kuwa awe amefika nyumbani kabla ya saa moja usiku. Pia aliniambia kuwa alipata ruhusa hiyo kwa kumdanganya baba yake kuwa anaenda kumtembelea rafiki yake na akanisisitiza kuwa muda uzingatiwe. Nikamhakikishia kuwa mambo yatakuwa sawa.

Nilikaa kumsubiri huku nikiangalia madhari ya ufukwe, niliwatazama watu waliokuja na wapenzi wao kujivinjari. Kuna walikuwa wanacheza michezo ya kimahaba, kuna waliokuwa wamekaa huku wakiongea, ilimradi kila mtu alijaribu kumuonyesha ni kwa jinsi gani anampenda na kumjali mwenzi wake. Lakini kwangu ilikuwa ni kinyume, yaani wakati watu wengine wanawaleta watu wao kuja kuimarisha mapenzi yao, mimi nilikuwa nimemwita Ingrid pale kuja kuliua penzi lake changa alilokuwa nalo juu yangu. Kweli binadamu tunafanana lakini hatupo sawa. Nilitembea huku mikono nikiwa nimeitumbukiza kwenye mifuko ya suruali huku masikio yangu yakiwa yanaburudishwa na sauti za mawimbi ya maji yaliyokuwa yakipiga kwenye ufuo. Bahari iliniburudisha kiasi chake ikizingatiwa kuwa mimi nilikulia maeneo ya kanda ya kati ambako kulikuwa na mazingira ya ukame hivyo kuona eneo kubwa la ardhi lililojazwa maji halikuwa jambo nililoweza kulishuhudia. Macho yangu yalizoea kuona madimbwi na mabwawa madogo madogo.

Ilikuwa na saa tisa na dakika zake hivi wakati Ingrid aliponipigia na kuniambia kuwa alikuwa amefika eneo ambalo tulitakiwa tuonane. Nilimuelekeza mahali ambapo nilikuwepo, dakika kadhaa baadaye alifika mahali nilipokuwepo. Alikuwa amevalia vyema kiasi cha kuongeza mvuto wake ambao nilizoea kuuona kila siku. Alivalia gauni la urefu wa saizi ya magoti lenye rangi nyekundu, rangi inayotafririwa kuwa ni rangi ya upendo japo kua wakati rangi hii huashiria uovu. Hii ni kwa sababu upendo na chuki, vyote kwa pamoja hutembea katika damu. Urefu wa gauni lake ulifanya miguu yake iliyojaa vyema kuonekana dhahiri kabisa, watoto wa mjini huiita miguu ya bia. Miguuni alivalia viatu vyepesi visivyo na visigino virefu vilevyokuwa na rangi nyeusi. Nywele alizisuka kwa mtindo ambao hadi sasa sijawahi kuufahamu, labda ni kwa sababu mimi siyo mfuatiliaji sana wa mambo ya urembo kwa wanawake. Kwa ujumla, Ingrid alikuwa ni mwanamke wa ndoto kwa wanaume wengi. Ingrid alikiwa amekamilika katika mwonekano wake na mitazamo yake.

Alinisalimia, nikapokea salamu yake nikiwa na uso wa furaha sana. Bila kusubiri maongezi zaidi nilimshika mkono na kumpeleka mahali ambapo nilipachagua kwa ajili ya sisi kukaa. Palikuwa ni mbali na bugudha za watu waliokuwa wanaogelea na kufanya mambo mengine ya starehe. Niliamua kufanya matendo ya kirafiki ili kuhakikisha kuwa Ingrid hajisikii vibaya. Tulifika mahali tulipokuwa tunaelekea, tukakaa kwenye mchanga safi wa ufukwe. Ingrid alikaa upande wa wangu wa kushoto akaweka mikono yake juu ya mikono yangu kisha akaegesha kichwa chake kwenye bega langu. Nami nikanyanyua mkono wangu wa kushoto kisha nikauzungusha mabegani mwake kama sehemu ya kumuunga mkono. Sasa tulikuwa ni muungano haswa. Hisia zetu ziliunganika na kutengeneza hisia moja, hisia ya penzi lililojaa mtanziko. Niliamua kuvunja ukimya kabla ya yeye hajafanya hivyo.

“Ingrid” nilimwita

“sema babaa” aliitika huku akiniangalia usoni. Sauti aliyoitumia kutamka hiyo setensi fupi ilinifanya nipoteze kumbukumbu ya kile nilichokuwa nataka kukisema. Nilikaa kimya kwa muda huku nikijaribu kuvuta kumbukumbu ya nini nilitaka kukisema. Baada ya sekunde kadhaa, nilikumbuka na nikaendelea kuongea.

“mara zote umekuwa ukiniona mimi ni mtu nisiyejali hisia zako, ama nakufanyia makusudi kwa kuwa najua kuwa unanipenda mimi sana. Si kweli, leo nataka kukupa kisa kilichonikuta na kufanya niwe mgumu kukubaliana na wewe. Nadhani tukishatoka hapa utakuwa unaelewa ni kwa nini nakuwa mzito sana kukualiana na wewe.” Niliongea huku mkono wangu wa kushoto ukitambaa taratibu katika bega la Ingrid hali iliyofanya Ingrid azidi kutulia.

“barry, nipo hapa kukusikiliza. Lakini nadhani wajua ni jinsi gani ninavyokupenda” aliongea huku akiupapasa mikono yangu.

“najua, najua Ingrid. Ndiyo maana nimekuita hapa ili nikushirikishe jambo hili kubwa sana katika maisha yagu” niliongea huku macho yangu yakiwa yanaangalia mawimbi ya bahari. Niliendelea kuangalia upande wa bahari, nikazidi kuangalia mawimbi yalivyokuwa yakitembea kwa kasi kuja na kurudi. Nilifanya yote haya ili kuvuta kumbukumbu zote za tukio zima ili nisisahau hata tukio moja. Nilipanga kumwambia kila kitu.

Baada ya kuwa na hakika kuwa nilikuwa nakumbuka kila kitu nikaanza kusimulia.

Miaka sita iliyopita..

Itaendelea…..
Nakuzibgatia sana mkuu, bonge moja la story.
 
MAISHA YANGU NYUMA YA PAZIA JEUSI

SEHEMU YA 07

Ilipoishia….

“ Ingrid, hivi unadhani mimi si mwanadamu? Au unadhani mimi nafurahi kukuona una huzuni kwa ajili yangu? Hata mimi naumia pia, lakini ni bora maumivu haya unayoyapata sasa kuliko hayo ambayo utayapata baadae kwa kuwa na mimi. Umeamua kutangaza kuvunja urafiki wetu kwa jambo hili dogo, sawa. Lakini nakuomba utambue kuwa unanionea, haunitendei haki hata kidogo. Najua hatuwezi acha kuonana kila siku…lakini jaribu kufikiria mimi nitakuwa najisikiaje pale ambapo nitakuwa nakuona? Anyway… nipo tayari kukupa ukweli wangu wote nyuma ya maamuzi yangu siku yoyote ile ambapo utahitaji na kama ratiba yangu itaruhusu. Baada ya hapo unaweza kuendelea na msimamo wako wa kukata mahusiano na ukaribu wetu. Vinginevyo, nita’miss’ vitu vingi kutoka kwako rafiki yangu, Ingrid” sikutaka kumpa nafasi aijibu hoja hii,ilikata simu, nikaizima, nikalala.

Endelea…..

Asubuhi iliyofuata niliamka nikiwa na uchovu kwa kiasi fulani hivi. Nilichoamua kukifanya kwanza ni kufungua simu kisha nilitoka nje ili kufanya mambo mengine kama kuswaki na kuoga. Baada ya kukamilisha yote hayo nilirudi ndani na kukuta simu yangu kwenye kioo ikionyesha kuwa kulikuwa na jumbe mpya tatu za kawaida. Nilizifungua ili kujua ni nini kilikuwa kimeandikwa huko ndani na ni nani aliyekuwa amezituma.

Alikuwa ni Ingrid, ndiyo Ingrid. Msichana ambaye jana usiku alijiapiza kuwa hatowasiliana na mimi kamwe. Jumbe zote zilionyesha kuwa zilitumwa jana usiku. ujumbe wa kwanza ulisema ‘mbona umekata simu sasa’ ujumbe wa pili ulisema ‘barry, ndo umeamua kunizimia simu kabisa sio?’ na ya tatu ilisema ‘ipo siku utalipa kwa maumivu haya unayonisababishia’.

Nilisoma jumbe hizo huku nikiwa natabasamu, yaani mtu aliyekuwa aliyejiapiza kuwa ananichukia sana na pia hatonitafuta tena alikuwa ametuma jumbe tatu mfululizo. Lakini kiuhalisia hiyo ndiyo rangi halisi ya wanawake. Mwanamke anaweza kukwambia ndiyo ilhali akimaanisha hapana au anakwambia hapana ilhali anamaanisha ndiyo, mwanamke anaweza kukukasirikia usoni lakini moyoni anakufurahia au anaweza kuonyesha tabasamu usoni lakini moyoni anakuchukia pasi mfano. Hivyo ndivyo walivyo, kuna nyakati ni ngumu sana kutambua ni nini hasa kinaendelea ndani ya mioyo yao.

Hata hivyo jumbe zake zilinipa nguvu kwa kuwa nilikuwa nimebaki na hatua moja tu ya kukamilisha lengo langu la kumtoa Ingrid katika zone ya yeye kuwa mpenzi wangu na pia aendelee kuwa rafiki yangu. Nilijiona mshindi katika hili.

Japo alikuwa anakuja katika njia niliyokuwa naitaka lakini sikutaka kujibu jumbe zake kwani ule ulikuwa ni mchezo wa hisia na nilipaswa kuucheza kwa umahiri ili nishinde mechi katika dakika za awali kabisa. Nilimaliza kujiandaa kisha nikaenda zangu kazini kama kawaida. Baada ya kufika eneo langu la kazi nilianza kutekeleza majukumu ya kawaida ya kila siku. Ilipofika saa nne na dakika zake hivi niliona simu yangu ikiita…nikaangalia kwenye kioo, alikuwa ni Ingrid. Akili yangu ilivurugika ghafla maana nilijua ni lazima atakuja na malalamiko mengi kabisa. Nilitaka nisiipokee simu yake lakini nikaona kwamba kama nisipopokea nitaongeza matatizo hivyo ni heri niipokee tu.

Nilipokea simu kusikiliza huyu mwanamke alikuwa na mashitaka gani tena.

“hi barry, mzima wewe?” alisema akiwa na furaha hadi nikajiuliza kwani leo imekuwaje. Kwa jinsi tulivyoachana jana usiku sikutarajia kama angekuwa katika hali kama ile.

“mi mzima tu ndugu yangu” nilisema kwa sauti ya kuchangamka ili kwenda naye sawa ilhali kichwani nikiwa bado nawaza ni nini kimemfurahisha yeye asubuhi asubuhi.

“daaah, barry nina furaha sana leo, yaani we acha tu” alisema huku akionyesha ni kweli alikuwa na furaha. Hata mimi nilijikuta natabasamu kama zoba huku nikiwa sijui ni nini kinanifanya nitabasamu.

“hivyo ndo inavyotakiwa, siyo unakaa umenyong’nyea kama unadaiwa madeni, haya nimegee na mimi nifurahi basi rafiki yangu mwenyewe” niliongea kwa bashasha huku nikiongeza kicheko cha kinafki.

“leo matokeo yetu yamatoka, na nimefanya vizuri….yaani hadi siamini” alisema Ingrid akizidi kuidhihirisha furaha yake. Dooh kumbe ni mambo ya shule tena. Mimi shule niliitupaga mkono japokuwa nafsi haikuwa imependa, na nilikuwa natamani sana siku na mimi ningekuwa darasani na nifikie hatua kama yake lakini haikuwezekana.

Munkari ulishuka, japokuwa niliendelea kushikilia kiwango kilekile cha hisia nilichokuwa nacho mwanzo ili ingrid asinigundue kama kuna jambo kwa upande wangu halikuwa sawa. “safi sana ingrid, umepata division ngapi” nilimuuliza.

“one’ alijibu.

“hongera sana aisee, kumbe una miakili mingi hivi! kwa hiyo chuooo kileeeeeee, utakweda kusomea nini madame?”

“mi hata sielewi yaani, ila napenda sana sheria na mambo ya pesa pesa”

“sheria, unataka kuja kumfunga nani, mimi?” nilimtania.

“yaani wewe ndo utakuwa wa kwanza kabisa. Yaani jinsi unavyoninyanyasa mimi na hisia zangu siku nikipata safasi lazima uozee jela nakwambia” aliogea kwa utani lakini iliyokuwa na hisia za maumivu ndani yake.

“aisee, haina shida madame. Hata ukinihukumu kunyongwa mpaka kufa ni sawa tu maana sheria utakuwa nayo mikononi mwako” Nilikubaliana na mtazamo wake. Niliwahi kuambiwa kuwa ukitaka kumaliza migogoro isiyo ya lazima, kubaliana na kile mgomvi wako anakisema juu yako.

“barry, yaani nilianza kukuchukia lakini nimejikuta nashindwa, barry wewe ni mwanaume gani lakini?, unatongozwa na mwanamke unakataa?, na sijui hicho kitu unachotaka kuniambia kitakuwa na matokeo gani kwa upande wangu” aliongea kwa sauti ambayo nilikuwa nimeizoea, sauti ya mahaba yaliyojaa unyonge. Tayari tulikuwa tumesharudi kwenye uwanja wa nyumbani, uwanja uliojaa hisia za upendo na malalamiko.

“Ingrid, mimi nakujali kuliko unavyofikiria, na siku hiyo utajua tu kwa nini huwa nayasema yale ninayoyasema…..”

“si uniambie sasa hivi”

“Sasa hivi ni saa za kazi, pia ni story ndefu kidogo, so inahitaji muda pia”

“kwa hiyo ni lini?”

“nadhani jumapili hii, baada ya kutoka kanisani”

“mmmmh….haya sawa, maana hata kama nikipinga wewe ni kichwa ngumu, huwezi nielewa, sawa tu” wakati anayaongea hayo kuna mteja alifika pale akiwa anahitaji huduma, nikaamua kukatizo mazungumzo . “hapana ingridi, unanielewa vibaya, badae madame..niache nitimize wajibu kwanza” nikakata simu na kuendelea kumhudunia mteja. Niliendelea kufanya kazi yangu kwa moyo wote na ilipofika jioni nikaenda kukabidhi hesabu kwa bosi kama kawaida kisha nikarudi zangu geto. Siku zilizidi kusonga huku nikijaribu kujiweka mbali na Ingrid maana niligundua kuwa kadri nilivyokuwa najiweka karibu naye ndivyo alivyokuwa akipata matumaini ya kuwa huenda mimi na yeye tutakuwa pamoja.

Hatimaye siku ikafika, sikutaka kwenda kanisani. Niliamka asubuhi nikafanya usafi na nikaendelea kujiandalia kifungua kinywa. Nilifanya hayo huku nikiperuzi kwenye mtandao wa jamiiforums. Jamiforums ilikuwa ni sehemu ambayo nilikuwa naitumia kama sehemu ya kuniondolea msongo wa mawazo. Si kwamba nilikuwa naperuzi tu kama mgeni bali nilikuwa mwanachama kabisa, nilikuwa natumia jina la ‘Jiwe la gizani’. Japo sikuwa na muda mrefu sana tangu nijiunge jf lakini nilikuwa nimeanza kuwa maarufu kutokana na nyuzi zangu zenye story zilizojaa ucheshi. Watu wengi walikuwa wakivutiwa nazo. Japo kile nilichokuwa nakiandika hakikuwa na uhalisia katika maisha yangu lakini nilikuwa nafurahi kwa sababu nilichukulia kama sehemu ya burudani kwangu na kwa wasomaji wengine. Wakati naperuzi katika uzi wa picha za vituko, simu yangu iliita. Alikuwa ni ingrid,…nikapokea.

“mambo barry” alinisalimia

“ni gud madame, lete habari..”

“safi, twende kanisani” alisema Ingrid

“leo mimi sijisikii kwenda” ilimjibu

“kwa nini?”

“jana nilichoka sana so nimeamka na uchovu” nilidanganya.

“mh, haya. Kwa hiyo leo nitatembea peke yangu?” aliiuliza kwa sauti yeye deko la kike.

“kaniombee tu madame” sikumjibu swali lake ila nilimwambia hivyo hili ahitimishe maongezi yake.

“unakumbuka leo ndiyo siku uliyoniahidi kuwa utaniambia kwa kina kuhusu ile ishu”

“yeah, nakumbuka vyema kabisa”

“saa ngapi sasa?”

“ukitoka kanisani”

“usije ukaondoka sasa maana wewe akili yako unaijua mwenyewe”

“nani kakwambia tunakuja kuongelea nyumbani? Tunatakiwa kutoka nje ya hapa, mazingira ya hapa si rafiki kabisa”

“mmmmh!..... hivi unadhani kupata ruhusa kutoka kwa baba ni jambo rahisi,?”

“kama ikishindikana basi”

“mmmh una roho mbaya wewe, ok ngoja nitajaribu. Ni wapi huko tutaenda?” aliuliza.

“nadhani itakuwa vizuri kama tutaenda sehemu iliyotulia kama ufukweni hivi”

“kuna fukwe nyingi sana lakini” alisema Ingrid. Nilimtajia ufukwe ambao niliona unafaa kwa kuzingatia umbali kutoka eneo tuliloishi. “mhh..haya, niombee nipate ruhusa” alisema Ingrid. Nikamhakikishia kuwa nitafanya hivyo kisha tukaagana na kukata simu.

Baada ya kukata simu, simu yangu ilinirudisha kwenye ukurasa wa jamiiforums ambao nilikuwa naupitia kabla ya simu ya Ingrid kuingia lakini niliamua kutokuendelea kuperuzi kwa kuwa akili yangu ilitekwa na jambo jingine. Nilifikiria kile ambacho ningeenda kumwambia Ingrid. Nikajikuta mnyonge ghafla. Lilikuwa ni jambo ambalo nilikuwa sipendi kabisa kulisimulia ila nililazimika kutokana na jinsi Ingrid alivyokuwa, alikuwa ni king’aganizi mno. Hivyo kwa wakati huo hiyo ndiyo ilikuwa ndiyo njia pekee ya mimi kujinasua kwake. Niliamini kama angekisikia kisa hicho angenielewa na kuniacha huru.

Hali ya kulifikiria tukio hili ilisababisha nifungue begi na kutoa bahasha ambayo ndiyo ilikuwa ni kielelezo na kumbukumbu pekee niliyokuwa nayo kuhusu tukio lile. Nikaifunngua nikavitoa vilivyokuwamo, nikavitandaza chini sakafuni kisha nikawa naviangalia. Jinsi nilivyokuwa naviangalia ndivyo nilizidi kuchochea hisia za maumivu na majuto ambayo yaliweka kambi ndani yangu kwa muda mrefu. Hisia hizi zilikuja kwa nguvu kubwa kiasi nilishindwa kuyazuia machozi. Kuna msemo kuwa kila mtu ana sehemu ya udhaifu wake, na ule ndiyo ulikuwa udhaifu wangu. Mara zote nilijikuta mnyonge sana mbele ya tukio lile.

Nilifumba macho huku nikiendelea kuyahisi machozi yakiwa yanatiririka taratibu kwenye mashavu yangu. Kisha taratibu nikaanza kuona taswira ya msichana ikiwa katika hali iliyofifia. Kadri muda ilivyozidi kwenda taswira ile ilianza kuonekana dhahiri kiasi cha kuweza kumtambua, alikuwa ni Jennifer. Jennifer alionekana akibubujikwa na machozi zaidi yangu mimi huku akionyesha ishara za kunilalamikia.

“damn, what the f..” niliongea kwa sauti kubwa huku nikirusha mikono. Na kwa kuwa niliongea kwa sauti kubwa sana nilijistukia na nikaamua nisiimalizie sentensi hiyo. Nilikuwa nahema kwa sauti kubwa sana. Nilijifuta machozi huku nikivurudisha vile vitu kwenye bahasha na kisha nikairudishia bahasha kwenye begi.

Niliendelea kuandaa kifungua kinywa huku nikiwa siko sawa kihisia.

Masaa yakasonga, asubuhi ikaondoka kinyonge huku ikiukaribisha mchana. Jua likawaka na joto likazidi kuongezeka. Siku hiyo sikujisikia kabisa kujiandalia chakula cha mchana hivyo nikatoka kwenda kwa mama’ntilie ambaye nilikuwa nakwenda kila mara kama ikitokea siku hiyo sijisikii kupika. Na kwa kuwa muda ulikuwa umeenda hivyo niliamua kuunganisha safari kwamba nikitoka hapo niunganishe moja kwa moja kwenda kwenye eneo la miadi.

Nilipomaliza kula nilichukua usafiri wa umma nikasogea eneo la miadi yangu na Ingrid. Nikashuka nikatembea kwa miguu hadi nilipofika eneo rasmi tulilokubaliana. Muda wote huu nilikuwa nawasiliana na Ingrid kwa njia ujumbe mfupi. Aliniambia kuwa baba yake alimruhusu lakini kwa masharti ya kuwa awe amefika nyumbani kabla ya saa moja usiku. Pia aliniambia kuwa alipata ruhusa hiyo kwa kumdanganya baba yake kuwa anaenda kumtembelea rafiki yake na akanisisitiza kuwa muda uzingatiwe. Nikamhakikishia kuwa mambo yatakuwa sawa.

Nilikaa kumsubiri huku nikiangalia madhari ya ufukwe, niliwatazama watu waliokuja na wapenzi wao kujivinjari. Kuna walikuwa wanacheza michezo ya kimahaba, kuna waliokuwa wamekaa huku wakiongea, ilimradi kila mtu alijaribu kumuonyesha ni kwa jinsi gani anampenda na kumjali mwenzi wake. Lakini kwangu ilikuwa ni kinyume, yaani wakati watu wengine wanawaleta watu wao kuja kuimarisha mapenzi yao, mimi nilikuwa nimemwita Ingrid pale kuja kuliua penzi lake changa alilokuwa nalo juu yangu. Kweli binadamu tunafanana lakini hatupo sawa. Nilitembea huku mikono nikiwa nimeitumbukiza kwenye mifuko ya suruali huku masikio yangu yakiwa yanaburudishwa na sauti za mawimbi ya maji yaliyokuwa yakipiga kwenye ufuo. Bahari iliniburudisha kiasi chake ikizingatiwa kuwa mimi nilikulia maeneo ya kanda ya kati ambako kulikuwa na mazingira ya ukame hivyo kuona eneo kubwa la ardhi lililojazwa maji halikuwa jambo nililoweza kulishuhudia. Macho yangu yalizoea kuona madimbwi na mabwawa madogo madogo.

Ilikuwa na saa tisa na dakika zake hivi wakati Ingrid aliponipigia na kuniambia kuwa alikuwa amefika eneo ambalo tulitakiwa tuonane. Nilimuelekeza mahali ambapo nilikuwepo, dakika kadhaa baadaye alifika mahali nilipokuwepo. Alikuwa amevalia vyema kiasi cha kuongeza mvuto wake ambao nilizoea kuuona kila siku. Alivalia gauni la urefu wa saizi ya magoti lenye rangi nyekundu, rangi inayotafririwa kuwa ni rangi ya upendo japo kua wakati rangi hii huashiria uovu. Hii ni kwa sababu upendo na chuki, vyote kwa pamoja hutembea katika damu. Urefu wa gauni lake ulifanya miguu yake iliyojaa vyema kuonekana dhahiri kabisa, watoto wa mjini huiita miguu ya bia. Miguuni alivalia viatu vyepesi visivyo na visigino virefu vilevyokuwa na rangi nyeusi. Nywele alizisuka kwa mtindo ambao hadi sasa sijawahi kuufahamu, labda ni kwa sababu mimi siyo mfuatiliaji sana wa mambo ya urembo kwa wanawake. Kwa ujumla, Ingrid alikuwa ni mwanamke wa ndoto kwa wanaume wengi. Ingrid alikiwa amekamilika katika mwonekano wake na mitazamo yake.

Alinisalimia, nikapokea salamu yake nikiwa na uso wa furaha sana. Bila kusubiri maongezi zaidi nilimshika mkono na kumpeleka mahali ambapo nilipachagua kwa ajili ya sisi kukaa. Palikuwa ni mbali na bugudha za watu waliokuwa wanaogelea na kufanya mambo mengine ya starehe. Niliamua kufanya matendo ya kirafiki ili kuhakikisha kuwa Ingrid hajisikii vibaya. Tulifika mahali tulipokuwa tunaelekea, tukakaa kwenye mchanga safi wa ufukwe. Ingrid alikaa upande wa wangu wa kushoto akaweka mikono yake juu ya mikono yangu kisha akaegesha kichwa chake kwenye bega langu. Nami nikanyanyua mkono wangu wa kushoto kisha nikauzungusha mabegani mwake kama sehemu ya kumuunga mkono. Sasa tulikuwa ni muungano haswa. Hisia zetu ziliunganika na kutengeneza hisia moja, hisia ya penzi lililojaa mtanziko. Niliamua kuvunja ukimya kabla ya yeye hajafanya hivyo.

“Ingrid” nilimwita

“sema babaa” aliitika huku akiniangalia usoni. Sauti aliyoitumia kutamka hiyo setensi fupi ilinifanya nipoteze kumbukumbu ya kile nilichokuwa nataka kukisema. Nilikaa kimya kwa muda huku nikijaribu kuvuta kumbukumbu ya nini nilitaka kukisema. Baada ya sekunde kadhaa, nilikumbuka na nikaendelea kuongea.

“mara zote umekuwa ukiniona mimi ni mtu nisiyejali hisia zako, ama nakufanyia makusudi kwa kuwa najua kuwa unanipenda mimi sana. Si kweli, leo nataka kukupa kisa kilichonikuta na kufanya niwe mgumu kukubaliana na wewe. Nadhani tukishatoka hapa utakuwa unaelewa ni kwa nini nakuwa mzito sana kukualiana na wewe.” Niliongea huku mkono wangu wa kushoto ukitambaa taratibu katika bega la Ingrid hali iliyofanya Ingrid azidi kutulia.

“barry, nipo hapa kukusikiliza. Lakini nadhani wajua ni jinsi gani ninavyokupenda” aliongea huku akiupapasa mikono yangu.

“najua, najua Ingrid. Ndiyo maana nimekuita hapa ili nikushirikishe jambo hili kubwa sana katika maisha yagu” niliongea huku macho yangu yakiwa yanaangalia mawimbi ya bahari. Niliendelea kuangalia upande wa bahari, nikazidi kuangalia mawimbi yalivyokuwa yakitembea kwa kasi kuja na kurudi. Nilifanya yote haya ili kuvuta kumbukumbu zote za tukio zima ili nisisahau hata tukio moja. Nilipanga kumwambia kila kitu.

Baada ya kuwa na hakika kuwa nilikuwa nakumbuka kila kitu nikaanza kusimulia.

Miaka sita iliyopita..

Itaendelea…..
Filimbi imepulizwa sasa mchezo uanze vyema.
Tuko pamoja sana mkuu.
 
MAISHA YANGU NYUMA YA PAZIA JEUSI

SEHEMU YA 08

Ilipoishia....

“barry, nipo hapa kukusikiliza. Lakini nadhani wajua ni jinsi gani ninavyokupenda” aliongea huku akiupapasa mikono yangu.

“najua, najua Ingrid. Ndiyo maana nimekuita hapa ili nikushirikishe jambo hili kubwa sana katika maisha yagu” niliongea huku macho yangu yakiwa yanaangalia mawimbi ya bahari. Niliendelea kuangalia upande wa bahari, nikazidi kuangalia mawimbi yalivyokuwa yakitembea kwa kasi kuja na kurudi. Nilifanya yote haya ili kuvuta kumbukumbu zote za tukio zima ili nisisahau hata tukio moja. Nilipanga kumwambia kila kitu.

Baada ya kuwa na hakika kuwa nilikuwa nakumbuka kila kitu nikaanza kusimulia.

Miaka sita iliyopita..

Endelea....

Baada ya kufaulu elimu yangu ya msingi nilipangiwa kusoma shule moja ya upili ambayo ilikuwa jirani na kijiji tulichokuwa tunaishi. Nilienda kuanza masomo yangu hapo lakini ilipofika mwezi wa saba kwa sababu ambazo baba yangu aliziona, aliamua kunihamisha shule na kunipeleka shule nyingine iliyokuwa mbali kidogo na eneo lile. Sababu zilizomfanya baba anihamishe ni kwamba alipenda nichanganyike na watu wapya kwa sababu watu wanafunzi wengi niliokuwa nasoma nao kwenye shule ile wengi wao walikuwa ni wale tuliosoma wote shule ya msingi. Kwa hiyo alitaka nipanue wigo ili kufahamiana na watu wengi zaidi kwa kupata changamoto kwa watu tofauti, kitu ambacho hata mimi nilikubaliana nacho. Lakini kitu kingine kizuri zaidi ilikuwa ni kwamba ningweza kuonana na Denis, rafiki yangu ambaye yeye alihamia shule hiyo katika miezi ya mwanzoni kabisa.

Taratibu za kuhamia shule hiyo mpya zilianza. Nilishona sare na kununuliwa mahitaji mengine ambayo yalikuwa yanahitajika. Shule huyo ilikuwa ni ya bweni kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita. Kwa kidato cha kwanza hadi cha nne ilikuwa ni ya mchanganyiko; wavulana na wasichana. Kwa kidato cha tano na cha sita walikuwa ni wavulana pekee.

Ilikuwa ni siku ya jumamosi nilipokafika shuleni hapo kuripoti. Taratibu za malipo zilifanyika kila kitu kikawa kimekamilika. Baada ya hapo nilichukuliwa na wanafunzi wenzangu walioagizwa na mwalimu kunipeleka katika bweni nililokuwa nimepangiwa. Walinisaidia kubeba begi langu na sanduku langu la chuma kama ilivyo jadi ya watu wa nchi hii, ukarimu kwa wageni. Wakati tukiwa tunaenda na wanafunzi hao ambao nao walionekana walikuwa ni kidato cha kwanza kwa kuwa walikuwa ni wadogo wadogo kuliko hata mimi, walikuwa wakinipa maneno ya ukaribisho huku wakiniuliza baadhi ya vitu kama jina langu na sehemu niliyokuwa natoka. Na mimi niliwajibu kadri walivyokuwa wanauliza pia nao walijitambulisha majina yao, mmoja aliitwa Ibrahim na mwingine Jackson. Tulifika katika bweni nililokuwa nimepangiwa, lilikuwa ni bweni la mkwawa chumba nanba 6. Baada ya kufika katika mlango wa chumba namba 6 Jackson alipiga hodi na akaruhusiwa. Tukaingia, tulikuta wanafunzi wakiwa ndani huku wakiendelea na shughuli zao kulikoambatana na stori za hapa na pale lakini walitulia kidogo baada ya sisi kuingia.

“oooi, inakuwaje” Jackson alisalimia

“poa poa” baadhi waliitikia kwa kupishana kidogo.

“mambo vipi?” nami pia nilisalimia

“poa poa” baadhi waliitikia huku wakigeuza shingo zao kuniangalia.

“mbona mabegi, matranka vipi ni mgeni?” mmoja aliuliza.

“ndiyo bwana, room leader yupo wapi?” Jackson aliuliza.

“halafu we Jackson acha dharau, ina maana hadi leo hujajuaga kuwa mimi ndo room leader humu ndani?” alidakia mmoja iliyekuwa kwenye deka ya juu katika moja ya vitanda vilivyokuwemo ndani ya kile chumba. Kauli iliyosababisha kuzuka kwa vicheko na maneno mengi ya utani.

Licha ya yote hayo walinikaribisha vizuri na nikaonyeshwa kitanda ambacho ningekuwa nakitumia. Niliwashukuru sana. Wanachumba wenzangu wapya nao walianza kuniuliza maswali kama waliyokuwa wakiniuliza Ibrahim na mwenzake Jackson nami nikawajibu. Baada ya hapo Ibrahim na Jackson waliondoka.

Nikaonyeshewa mahali pakuweka vitu vyangu kama sanduku na begi. Nilishauriwa kuwa begi la madaftari ni vizuri kama nitakuwa naweka kitandani kwangu. Kiukweli nilikuwa mgeni wa maisha ya shule za bweni. Lakini nilijipa moyo kuwa nitazoea tu, tena ndani ya muda mfupi. Pia nilihitaji kuonana na Denis, maana alikiwa ndiye rafiki yangu pekee niliyekuwa naye shuleni hapo kwa wakati ule. Niliamua kumuuliza mmoja ya wanachumba wenzangu.

“Denis….Denis” alisema huku akifinya jicho moja huku akiwa ameamgalia juu ili kuvuta kumbukumbu vizuri. “aaaaah nimeshampata. Si ni mweusi mnene mnene kidogo?” aliniuliza

“ndiyo” nilijibu

“sawa namfahamu, ni ndugu yako?”

“hamna ni rafiki yangu tu, tumesoma wote shule ya msingi”

“aaaaah! Yupo bwana anakaa bweni hilihili chumba namba 1 huku kwa nyuma”

“anhaa…ngoja basi midamida tutaenda kumcheki”

“poa” alijibu mwanafunzi huyo.

baada ya hapo nikawa kimya. Mimi na wenyeji wangu ambapo kwa muda huo tulikuwa tunasubiri chakula cha mchana tuliendelea kutulia bwenini huku mimi nikitumia muda wangu kuzungusha macho nje kuangalia mazingira. Wenyeji wangu wao walikuwa wanapiga story za hapa na pale ili kusogeza muda. Story zao zilinivuta kiasi name nikavutika kusikiliza.

“oyaa mwanangu leo nilipata zari la mentali, yaani…haaaa” alisema mmoja

“lipi hilo dogo?” mwingine aliuliza

“bwana leo nilikuwa nimetoka canteen, si nikakutana na Aisha pamoja na Jennifer…..” kabla hajaendelea kuna mwingine akadakia

“yaani hadi hapo hii story ni ya uongo…ngoja nilale”

“aaaah acha mambo ya ajabu, we lala tu acha tupewe story bhana. Mbuzi jike wewe” alidakia mwingine.

“jamaa ni wivu unamsumbua tu. Yaani kutaja tu majina ya hao mademu karoho kamemuuuma kinoma..unaona bhana, nikampa hi Aisha pale kisha nikamalizia kwa kifaa chenyewe pale kwa Jennifer paa..walikuwa wanaelekea class nikawa nawasindikiza huku nikimpigisha story jennifer, mtoto ni anacheka tu yaani. Hadi Aisha akawa anajisikia vibaya” alisema msimuliaji huku akipigapiga mbao za kitanda kwa kujigamba kisha akaanza kukitikisa kitanda kwa nguvu.

“kudadeki we mbwa huko juu tulia bwana, utavunja kitanda” alisema mwingine aliyekuwa amekaa deka ya chini ya Yule jamaa msimuliaji.

“hahahaha we jamaa ni muongo, peleka maujinga yako bafuni huko” Yule aliyesema hadithi ni ya uongo ni bora alale alimbeza mleta story.

“we mjinga si ulisema unalala?” alihoji msimuliaji.

“hahaha….jamaa unamuumiza mshkaji, anammaindigi sana Jennifer ila udomo zege ndo unamponza, domo lake limejaa uji hawezi kuongea kabisa” mwingine naye alisema kumuunga mkono msimuliaji.

“mi mbona najua… na ngoja, kesho naanza kutema sumu kwa mtoto” alisema msimuliaji kwa sauti ya majigambo.

“hivi unadhani kuna mtu atakuwa anabeba sahani lako kwenda kukuchukulia chakula ukishapigwa kibuti….kamuulize mgeta kilichompata, siku nne hatoki bwenini alikuwa anashinda amelala kama anaumwa vile” alisema Yule aliyesema tangu mwanzo kuwa story ile ilikuwa ni ya uwongo, jamaa alionekana kuwa mpinzani mkuu wa msimuliaji.

“we fala nini unanilinganisha mimi na lile lisukuma lishamba lishamba halijui hata kutongoza, sasa jitu linasema ‘kamoyo kangu kamekudhondokea’ unategemea lijibiwe nini?” msimuliaji alihoji.

“sawa wewe ni mjanja….ila si kwa Jennifer mzee, ngoja tu mi nitangulize salamu zangu za rambirambi maana kibuti utakachopewa kitakuwa kibuti kitakatifu. Lazima tutakuzika mbwa wewe” alisema mpinzani mkuu.

“fala wewe, we endelea kupiga magoli yako ya mkono huko bafuni, hizi mambo tuachie sisi.” akisema msimuliaji.

“sawa sawa bwana, tutaona” alisema mwingine ambaye alikuwa kimya tangu story ile ilipoanza.

“usimpe moyo… kwanza jenifer ni mtoto mkali, tena ni mboga saba, hawezi kukubali kuwa na boya ka yeye, Mbona utahama shule dogo, shauri yako” alisema Yule mpinzani mkuu huku akiwa anatoka nje.

“aaaah kwenda zako na wewe…domo zege mkubwa” msimuliaji alimsema mkosoaji wake aliyekuwa amefika nje.

Mabishano na maongezi yaliendelea. Kulingana na jinsi mabishano yalivyokuwa nilijikuta navutiwa kumjua Jennifer. Nilitaka kufahamu Jennifer alikuwa anafananaje, kwa nini azungumziwe sana, kwa nini watu wapigizane makelele bwenini kwa ajili yake, alikuwa na nini hasa.?

Jioni ilifika, tukaenda kumtafuta Denis. Tukampata, tuliongea mengi kuhusu nyumbani na matukio mengine yaliyokuwa yamepita. Alinitembeza sehemu tofauti katika shule hiyo na kunielekeza kila sehemu tuliyokuwa tunapita. Nilijihisi kuondokewa na ugeni niliokuwa nao.

Siku ya jumatatu ilifika, tukafanya shughuli za usafi, tukaenda kusikiliza matangazo paredi kisha tukaenda madarasani. lakini kabla sijaenda darasani nilimchukua Denis kwenda kuchukua kiti na meza ambavyo nilikuwa nimepewa na kiranja wa vifaa. Kwa kuwa nafasi zilikuwa zimejaa sikuweza kupata nafasi nyuma au katikati, ilinibidi kukaa mbele, kitu ambacho nilikuwa sijazoea. Maisha yangu ya shule mara nyingi nilikuwa nakaa nyuma au katikati. Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kukaa mbele kabisa. Lakini nilikuwa najua kuwa sitokaa kwa muda mrefu sana, ni lazima ningehama tu.

Baada ya kufika darasani kitu cha kwanza ilikuwa ni kutaka kumfahamu Jennifer. Niliamini kuwa ningemfahamu mapema maana darasa lilikuwa na wanafunzi wachache, tulikuwa kama sitini hivi kwa mahesabu ya haraka haraka. Na sikutaka kumuuliza mtu yoyota, hata Denis sikutaka kumuuliza maana angeanza kunihoji ni kwa nini. “nitamjua tu” nilijisemea.

Baada ya kukaa kidogo mwalimu aliingia. Tukasimama tukamsalimia. Alikuwa ni mwalimu wa kike, mweusi kidogo hivi ambapo kwa siku za baadae nilikuja kufahamu kuwa aliitwa Madam Tabu. Alienda ubaoni akaandika jina la somo “Biology” kisha akipiga mstari akaandika kwa chini “classification of kingdom fungi” kasha akaligeukia darasa.

Kabla hajaanza kufundisha, macho yake yakatua kwangu. Akawa ananiangalia. “Wewe ni mgeni eti, maana sijawahi kukuona”

“ndiyo” nilimjibu

“karibu sana, umetokea shule gani”

“chikola” nilimjibu.

“karibu sana bwana, sasa inabidi utufungulie kipindi, utaratibu wangu ni kuwa ukishindwa kujibu swali unasmama hadi kipindi kiishe, ndiyo utaratibu wangu ulivyo. Sawa mgeni? Kwanza unaitwa nani?” aliuliza

“barry” nikamjibu huku nikiwa nimeanza kutetemeka maana sikuwa nimejiandaa kabisa kwa kilichokuwa kinafuata.

“aaah barry, leo tutaendelea kujifunza classification of kingdom fungi” alisema mwalimu akiwa hana sura ya utani hata kidogo huku akiwa ananingalia mimi. Ni kama vile darasa zima lilikuwa na mwanafunzi mmoja ambaye ni mimi tu. “sasa barry hebu nitajie phylum zinazopatikana katika kingdom fungi” kama unajua kuchanganyikiwa, basi ni siku ile. Ugeni na uoga vilichanganyika na kunifanya niwe nimesimama tu kama sanamu nikiwa sijui hata niseme nini. Nilisimama huku nikiwa sina cha kujibu. Mwalimu aliniangalia kwa macho makali hali ambayo ilinifanya niogope zaidi.

“mgeni…unatoa toa macho tu, shule hiyo ulikotoka walimu walikuwa hawafundishi?” aliuliza huku akinisogrlea. Mimi nilibaki namtizama tu. “nakuuliza wewe, mlikuwa hamsomi?” aliniuliza tena, mara hii akiwa amesimama mbele kabisa ya meza yangu.

“walikuwa wanafundisha” nilimjibu kwa sauti ya chini ambayo sidhani kama wanafunzi wengine walisikia..

“sasa…” alihoji mwalimu huyo. Sikuwa na cha kujibu.

“ukiwa tayari kujibu niambie nikupe swali jingine ama sivyo utasimama hadi mwisho wa kipindi kama ulivyo utaratibu wangu. Jennifer hebu tukumbushe hapo.” Mwalimu alipotaja jina la Jennifer akili yangu ilizinduka ghafla. Nikaanza kuzungusha macho ili nimuone maana nilikuwa na shauku hiyo tangu nilipofika shuleni hapo siku ya kwanza. Mara akasimama. Alikuwa ni msichana wa umbo la wastani, maji ya kunde, sura yake ilikuwa na mwoekano wa kuvutia. Mimi sio mtaalamu sana wa kuwaelezea watu ila itoshe kusema kuwa alikuwa ni msichana aliyevutia kumtazama. Mara baada ya kusimama akaanza kujibu swali.

“Kingdom fungi includes five phyla that are; Chytridiomycota or chytrids, Zygomycota Glomeromycota, Ascomycota and Basidiomycota” alijibu Jennifer bila kukwamakwama kisha alipomaliza akakaa.

“vizuri sana Jennifer, haya darasa mpigieni makofi jennifer” alisema mwalimu.

“pwaaa! Pwaa! Pwa! Pwa! Pwa! Pwaaa!” zilisikika sauti za makofi.

Nilishangaa, nilishangaa sana. Sikutegemea kama mwanafunzi wa form one katika shule zetu za kata angeweza kujibu swali kwa kujiamini vile. Tena cha zaidi alikuwa na mtoto wa kike. Mimi ilikuwa ni vigumu hata kuongea sentensi moja tu ya kiingereza japokuwa uwezo wangu darasani ulikuwa ni mkubwa. Niliona aibu sana.

“unaona wenzako waliokuja shule kusoma” mwalimu alisema, kisha akaendelea “vipi unataka nikupe swali lingine ujibu ili ukae?” ningejibu swali gani, nilibaki kimya. Nilisimama hadi mwalimu alipomaliza kufundisha. Baada ya hapo wanafunzi wenzangu walianza kunitania kwa kuniita mgeni msimamizi, Sikujali.

Siku zilipita, nikayazoea mazingira na watu pia. Kitu nilichojifunza kuhusu Jennifer ni kuwa alikuwa na uwezo mkubwa sana darasani. Niliambiwa kuwa tangu afike shuleni hapo yeye tu ndiye aliyekuwa akishika nafasi ya kwanza tena kwa kuwaacha kwa alama nyingi wale ambao walikuwa wakifuata baada yake. Lakini pia alikuwa akipendwa zaidi na walimu. Ilikuwa kama unataka kugombana na mwalimu, gombana na Jennifer. Jennifer alikuwa ni malkia wa darasa letu. Malkia pasipo mfalme.

Ulifika wakati wa kufanya mid-term test, matokeo yalipotoka nikawa wa pili. Nyuma ya Jennifer kwa wastani wa Alama tisa. Hali hii ilifanya na mimi kuanza kuzungumziwa na kufuatiliwa kwa karibu na walimu. Masomo yaliendelea ikafika wakati wa kufanya mtihani wa mwisho wa mhula wa pili. Nilipopewa ripoti yangu ya matokeo ilionyesha kuwa nilikuwa wa nne. Niliumia kidogo lakini niliona sikuwa na haja ya kujipa msongo wa mawazo.

Shule ikafunguliwa tena. Tukawa kidato cha pili. Baada ya kufika shuleni katika lile wiki la kwanza ulifanyika uchaguzi wa viongozi madarasa. Lakini sidhani kama ulifaa kuitwa uchaguzi maana walimu ndio waliopendekeza majina ya viongozi. Monitor alichaguliwa mwanafunzi aliyeitwa James ambaye alikuwa na umbo kubwa kuliko sisi wengine. Na monitress akachaguliwa Jennifer.

Kwa kipindi chote ambacho tayari nilikuwa nimekiishi sikuwahi kuwa na mawasiliano ya karibu na Jennifer. Japokuwa nilikuwa namchukia yeye na rafiki yake Adela. Niliwachukia kwa sababu walikuwa na tabia ya kujisikia sana. Sikuwa na haja hata ya kushirikiana na nao kwa lolote lile. Huwa sipendi kuwa karibu na watu wa aina kama waliyokuwa wao. Lakini ilikuja siku ambayo mimi na Jennifer tulipambana uso kwa uso. Siku ambayo ilichochea moto wa kumchukia Jennifer. Ilikuwa hivi:

Siku hiyo nilikuwa zamu kufagia darasa pamoja na wenzangu watatu. Lakini kwa bahati mbaya sana wale wenzangu wote niliokuwa nimepangwa nao hawakufika kabisa. Sijui walikwenda wapi maana nakumbuka niliwaona asubuhi mabwenini. Lakini kwa kuwa mimi sipendi matatizo na mtu, nikaamua kwenda kufagia darasa lote mimi pekeyangu. Nilifagia na kumaliza japo nilifanya harakaharaka kwa kuwa muda wa kwenda paredi ulikuwa umekaribia. Kengele ya paredi ikagongwa tukaenda na baadaye tukarudi darasani. Baada ya kuingia darasani na kukaa, Jennifer akasimama na kuomba tumskilize. Kweli tukatii

“ni nani na nani walikuwa wanafagia darasa leo?” nilishangaa kuona linanaulizwa swali kama lile kwa sababu ratiba ya usafi ilikuwa imebandikwa darasani.. Lakini sikuona shida nikanyoosha mkono. Kwa muda huo nilikuwa peke yangu maana wale wenzangu walikuwa hawajaingia darasani bado.

“we barry, hili darasa limefagiliwa kweli?” niliendelea kushangaa, ila kwa kuwa nilikuwa namjua ni mtu mwenye jeuri na mimi niliamua kumjibu jeuri.

“kwani wewe unaonaje?” nilimuuliza.

“halijafagiliwa” alisema jenifer kwa sauti ya mamlaka.

“hili darasa halijafagiliwa, kwa hiyo mimi nilifanyaje?”

“mi sitaki kujua ulifanyaje, ila naomba tu watu watoke nje uwatafute wenzako mje mfagie, sawa” alisema Jennifer. Ukweli ni kuwa darasa halikuwa safi sana kwa kuwa nilifagia nikiwa na haraka. Lakini haikuwa imefika kiasi cha kuambiwa tufagie tena. Hivyo nikaona kulikuwa hakuna haja ya kufagia tena.

“labda kama unawambia watoke nje ili kupunga upepo, mimi sitofagia tena kwa sababu nimeshafagia. Labda mwingine aamue kufanya hivyo lakini si mimi. Utanisamehe tu madam Jennifer.” Nilimjibu, hali iliyosababisha wanafunzi wengine wacheke.

“afagie huyo aacha ujinga, hatuwezi kukaa darasa limejaa vumbi kama hivi” ilikuwa ni sauti ya adela, kiumbe mwingine iliyekuwa namchukia kweli kweli. Sikutaka kuendelea kuongea tena maana nilijua kuwa ujumbe wangu ulisikika na kueleweka vizuri.

Jennifer aliendelea kuniambia kuwa nifagie likini mimi sikumjibu. Hatimaya akasema kuwa ataenda kuripoti kwa mwalimu wa zamu, sikumjibu. Akatoka nje. Alirudi baada ya dakika kama tatu hivi akiwa ameambatana na mwalimu Kachaka ambaye ndiye aliyekuwa mwalimu wa zamu kwa wiki hilo. Nikajua tayari kinaenda kunuka.

“barry ndo nani” mwalimu aliuliza. Nami bila kusita nikanyoosha mkono.

“hili darasa limefagiliwa?” aliuliza mwalimu.

“ndiyo”

“pumbavu mkubwa wewe, unajibu ndiyo. Kwa hiyo unamaanisha kuwa kiongozi wako wa darasa kanidanganya siyo?” aliongea kwa hasira

“hayo mimi siwezi kuyajua, mimi ninachojua kuwa nimefagia” nilijibu kwa kujiamini

“hili darasa limefaguliwa hili?” aliuliza huku akitumia fimbo kuonyesha vipande vichache vya karatasi kilivyokuwa vimezagaa pale mbele. Niliamua kukaa kimya. “hao wenzako wengine wako wapI?” mwalimu aliuliza

“hawajafika bado” alijibu Jennifer

“sasa huyu atabeba msalaba wa wenzake, barry nyanyuka ukatafute fagio ufagie darasa sasa hivi.” Aliamrisha mwalimu. Mimi huwa si mtu wa kuongea sana ila huwa nina kibUri na jaeuri endapo mtu atanikwaza. Nikaamua kukaa kimya maana kama kujibu nilikuwa nimejibu vya kutosha. Niliendelea kukaa. “barry nasema nyanyuka ukatafute ufagio”. Mwalimu alisema kwa ukali zaidi lakii ni kama nilikuwa simsikii. Niliendelea kukaa.

Mwalimu alipandwa na hasira akaja kunishika mkono, alianza kunivuta kunipeleka mbele ya darasa. Aliniamrisha nishike chini anichape nikagona. Akatumia nguvu nikazidiwa, akanichapa fimbo idadi ambayo hadi sasa huwa sikumbuki. Baada ya hapo aliwaambia wanafunzi watoke nje ili nifagie darasa na pia akanipa adhabu ya kuchimbua visiki vinne.

Wakati wanafunzi wanatoka nje mimi nikawa nawaza nifanyaje. Nilikuwa nimepandwa na hasira sana. Nikaamua kuwapa ushindi Jennifer pamoja ma mwalimu, nilikubali kufagia darasa. Wakati naanza kufagia walikuja wanafunzi wengine wachache kunisaidia. Baada ya hapo nilikwenda kuchukua vifaa kwa ajili ya kuchimba visiki. Nilifanya haya yote nikiwa na hasira kali juu ya Jennifer.

Itaendelea…
 
MAISHA YANGU NYUMA YA PAZIA JEUSI

SEHEMU YA 08

Ilipoishia....

“barry, nipo hapa kukusikiliza. Lakini nadhani wajua ni jinsi gani ninavyokupenda” aliongea huku akiupapasa mikono yangu.

“najua, najua Ingrid. Ndiyo maana nimekuita hapa ili nikushirikishe jambo hili kubwa sana katika maisha yagu” niliongea huku macho yangu yakiwa yanaangalia mawimbi ya bahari. Niliendelea kuangalia upande wa bahari, nikazidi kuangalia mawimbi yalivyokuwa yakitembea kwa kasi kuja na kurudi. Nilifanya yote haya ili kuvuta kumbukumbu zote za tukio zima ili nisisahau hata tukio moja. Nilipanga kumwambia kila kitu.

Baada ya kuwa na hakika kuwa nilikuwa nakumbuka kila kitu nikaanza kusimulia.

Miaka sita iliyopita..

Endelea....

Baada ya kufaulu elimu yangu ya msingi nilipangiwa kusoma shule moja ya upili ambayo ilikuwa jirani na kijiji tulichokuwa tunaishi. Nilienda kuanza masomo yangu hapo lakini ilipofika mwezi wa saba kwa sababu ambazo baba yangu aliziona, aliamua kunihamisha shule na kunipeleka shule nyingine iliyokuwa mbali kidogo na eneo lile. Sababu zilizomfanya baba anihamishe ni kwamba alipenda nichanganyike na watu wapya kwa sababu watu wanafunzi wengi niliokuwa nasoma nao kwenye shule ile wengi wao walikuwa ni wale tuliosoma wote shule ya msingi. Kwa hiyo alitaka nipanue wigo ili kufahamiana na watu wengi zaidi kwa kupata changamoto kwa watu tofauti, kitu ambacho hata mimi nilikubaliana nacho. Lakini kitu kingine kizuri zaidi ilikuwa ni kwamba ningweza kuonana na Denis, rafiki yangu ambaye yeye alihamia shule hiyo katika miezi ya mwanzoni kabisa.

Taratibu za kuhamia shule hiyo mpya zilianza. Nilishona sare na kununuliwa mahitaji mengine ambayo yalikuwa yanahitajika. Shule huyo ilikuwa ni ya bweni kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita. Kwa kidato cha kwanza hadi cha nne ilikuwa ni ya mchanganyiko; wavulana na wasichana. Kwa kidato cha tano na cha sita walikuwa ni wavulana pekee.

Ilikuwa ni siku ya jumamosi nilipokafika shuleni hapo kuripoti. Taratibu za malipo zilifanyika kila kitu kikawa kimekamilika. Baada ya hapo nilichukuliwa na wanafunzi wenzangu walioagizwa na mwalimu kunipeleka katika bweni nililokuwa nimepangiwa. Walinisaidia kubeba begi langu na sanduku langu la chuma kama ilivyo jadi ya watu wa nchi hii, ukarimu kwa wageni. Wakati tukiwa tunaenda na wanafunzi hao ambao nao walionekana walikuwa ni kidato cha kwanza kwa kuwa walikuwa ni wadogo wadogo kuliko hata mimi, walikuwa wakinipa maneno ya ukaribisho huku wakiniuliza baadhi ya vitu kama jina langu na sehemu niliyokuwa natoka. Na mimi niliwajibu kadri walivyokuwa wanauliza pia nao walijitambulisha majina yao, mmoja aliitwa Ibrahim na mwingine Jackson. Tulifika katika bweni nililokuwa nimepangiwa, lilikuwa ni bweni la mkwawa chumba nanba 6. Baada ya kufika katika mlango wa chumba namba 6 Jackson alipiga hodi na akaruhusiwa. Tukaingia, tulikuta wanafunzi wakiwa ndani huku wakiendelea na shughuli zao kulikoambatana na stori za hapa na pale lakini walitulia kidogo baada ya sisi kuingia.

“oooi, inakuwaje” Jackson alisalimia

“poa poa” baadhi waliitikia kwa kupishana kidogo.

“mambo vipi?” nami pia nilisalimia

“poa poa” baadhi waliitikia huku wakigeuza shingo zao kuniangalia.

“mbona mabegi, matranka vipi ni mgeni?” mmoja aliuliza.

“ndiyo bwana, room leader yupo wapi?” Jackson aliuliza.

“halafu we Jackson acha dharau, ina maana hadi leo hujajuaga kuwa mimi ndo room leader humu ndani?” alidakia mmoja iliyekuwa kwenye deka ya juu katika moja ya vitanda vilivyokuwemo ndani ya kile chumba. Kauli iliyosababisha kuzuka kwa vicheko na maneno mengi ya utani.

Licha ya yote hayo walinikaribisha vizuri na nikaonyeshwa kitanda ambacho ningekuwa nakitumia. Niliwashukuru sana. Wanachumba wenzangu wapya nao walianza kuniuliza maswali kama waliyokuwa wakiniuliza Ibrahim na mwenzake Jackson nami nikawajibu. Baada ya hapo Ibrahim na Jackson waliondoka.

Nikaonyeshewa mahali pakuweka vitu vyangu kama sanduku na begi. Nilishauriwa kuwa begi la madaftari ni vizuri kama nitakuwa naweka kitandani kwangu. Kiukweli nilikuwa mgeni wa maisha ya shule za bweni. Lakini nilijipa moyo kuwa nitazoea tu, tena ndani ya muda mfupi. Pia nilihitaji kuonana na Denis, maana alikiwa ndiye rafiki yangu pekee niliyekuwa naye shuleni hapo kwa wakati ule. Niliamua kumuuliza mmoja ya wanachumba wenzangu.

“Denis….Denis” alisema huku akifinya jicho moja huku akiwa ameamgalia juu ili kuvuta kumbukumbu vizuri. “aaaaah nimeshampata. Si ni mweusi mnene mnene kidogo?” aliniuliza

“ndiyo” nilijibu

“sawa namfahamu, ni ndugu yako?”

“hamna ni rafiki yangu tu, tumesoma wote shule ya msingi”

“aaaaah! Yupo bwana anakaa bweni hilihili chumba namba 1 huku kwa nyuma”

“anhaa…ngoja basi midamida tutaenda kumcheki”

“poa” alijibu mwanafunzi huyo.

baada ya hapo nikawa kimya. Mimi na wenyeji wangu ambapo kwa muda huo tulikuwa tunasubiri chakula cha mchana tuliendelea kutulia bwenini huku mimi nikitumia muda wangu kuzungusha macho nje kuangalia mazingira. Wenyeji wangu wao walikuwa wanapiga story za hapa na pale ili kusogeza muda. Story zao zilinivuta kiasi name nikavutika kusikiliza.

“oyaa mwanangu leo nilipata zari la mentali, yaani…haaaa” alisema mmoja

“lipi hilo dogo?” mwingine aliuliza

“bwana leo nilikuwa nimetoka canteen, si nikakutana na Aisha pamoja na Jennifer…..” kabla hajaendelea kuna mwingine akadakia

“yaani hadi hapo hii story ni ya uongo…ngoja nilale”

“aaaah acha mambo ya ajabu, we lala tu acha tupewe story bhana. Mbuzi jike wewe” alidakia mwingine.

“jamaa ni wivu unamsumbua tu. Yaani kutaja tu majina ya hao mademu karoho kamemuuuma kinoma..unaona bhana, nikampa hi Aisha pale kisha nikamalizia kwa kifaa chenyewe pale kwa Jennifer paa..walikuwa wanaelekea class nikawa nawasindikiza huku nikimpigisha story jennifer, mtoto ni anacheka tu yaani. Hadi Aisha akawa anajisikia vibaya” alisema msimuliaji huku akipigapiga mbao za kitanda kwa kujigamba kisha akaanza kukitikisa kitanda kwa nguvu.

“kudadeki we mbwa huko juu tulia bwana, utavunja kitanda” alisema mwingine aliyekuwa amekaa deka ya chini ya Yule jamaa msimuliaji.

“hahahaha we jamaa ni muongo, peleka maujinga yako bafuni huko” Yule aliyesema hadithi ni ya uongo ni bora alale alimbeza mleta story.

“we mjinga si ulisema unalala?” alihoji msimuliaji.

“hahaha….jamaa unamuumiza mshkaji, anammaindigi sana Jennifer ila udomo zege ndo unamponza, domo lake limejaa uji hawezi kuongea kabisa” mwingine naye alisema kumuunga mkono msimuliaji.

“mi mbona najua… na ngoja, kesho naanza kutema sumu kwa mtoto” alisema msimuliaji kwa sauti ya majigambo.

“hivi unadhani kuna mtu atakuwa anabeba sahani lako kwenda kukuchukulia chakula ukishapigwa kibuti….kamuulize mgeta kilichompata, siku nne hatoki bwenini alikuwa anashinda amelala kama anaumwa vile” alisema Yule aliyesema tangu mwanzo kuwa story ile ilikuwa ni ya uwongo, jamaa alionekana kuwa mpinzani mkuu wa msimuliaji.

“we fala nini unanilinganisha mimi na lile lisukuma lishamba lishamba halijui hata kutongoza, sasa jitu linasema ‘kamoyo kangu kamekudhondokea’ unategemea lijibiwe nini?” msimuliaji alihoji.

“sawa wewe ni mjanja….ila si kwa Jennifer mzee, ngoja tu mi nitangulize salamu zangu za rambirambi maana kibuti utakachopewa kitakuwa kibuti kitakatifu. Lazima tutakuzika mbwa wewe” alisema mpinzani mkuu.

“fala wewe, we endelea kupiga magoli yako ya mkono huko bafuni, hizi mambo tuachie sisi.” akisema msimuliaji.

“sawa sawa bwana, tutaona” alisema mwingine ambaye alikuwa kimya tangu story ile ilipoanza.

“usimpe moyo… kwanza jenifer ni mtoto mkali, tena ni mboga saba, hawezi kukubali kuwa na boya ka yeye, Mbona utahama shule dogo, shauri yako” alisema Yule mpinzani mkuu huku akiwa anatoka nje.

“aaaah kwenda zako na wewe…domo zege mkubwa” msimuliaji alimsema mkosoaji wake aliyekuwa amefika nje.

Mabishano na maongezi yaliendelea. Kulingana na jinsi mabishano yalivyokuwa nilijikuta navutiwa kumjua Jennifer. Nilitaka kufahamu Jennifer alikuwa anafananaje, kwa nini azungumziwe sana, kwa nini watu wapigizane makelele bwenini kwa ajili yake, alikuwa na nini hasa.?

Jioni ilifika, tukaenda kumtafuta Denis. Tukampata, tuliongea mengi kuhusu nyumbani na matukio mengine yaliyokuwa yamepita. Alinitembeza sehemu tofauti katika shule hiyo na kunielekeza kila sehemu tuliyokuwa tunapita. Nilijihisi kuondokewa na ugeni niliokuwa nao.

Siku ya jumatatu ilifika, tukafanya shughuli za usafi, tukaenda kusikiliza matangazo paredi kisha tukaenda madarasani. lakini kabla sijaenda darasani nilimchukua Denis kwenda kuchukua kiti na meza ambavyo nilikuwa nimepewa na kiranja wa vifaa. Kwa kuwa nafasi zilikuwa zimejaa sikuweza kupata nafasi nyuma au katikati, ilinibidi kukaa mbele, kitu ambacho nilikuwa sijazoea. Maisha yangu ya shule mara nyingi nilikuwa nakaa nyuma au katikati. Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kukaa mbele kabisa. Lakini nilikuwa najua kuwa sitokaa kwa muda mrefu sana, ni lazima ningehama tu.

Baada ya kufika darasani kitu cha kwanza ilikuwa ni kutaka kumfahamu Jennifer. Niliamini kuwa ningemfahamu mapema maana darasa lilikuwa na wanafunzi wachache, tulikuwa kama sitini hivi kwa mahesabu ya haraka haraka. Na sikutaka kumuuliza mtu yoyota, hata Denis sikutaka kumuuliza maana angeanza kunihoji ni kwa nini. “nitamjua tu” nilijisemea.

Baada ya kukaa kidogo mwalimu aliingia. Tukasimama tukamsalimia. Alikuwa ni mwalimu wa kike, mweusi kidogo hivi ambapo kwa siku za baadae nilikuja kufahamu kuwa aliitwa Madam Tabu. Alienda ubaoni akaandika jina la somo “Biology” kisha akipiga mstari akaandika kwa chini “classification of kingdom fungi” kasha akaligeukia darasa.

Kabla hajaanza kufundisha, macho yake yakatua kwangu. Akawa ananiangalia. “Wewe ni mgeni eti, maana sijawahi kukuona”

“ndiyo” nilimjibu

“karibu sana, umetokea shule gani”

“chikola” nilimjibu.

“karibu sana bwana, sasa inabidi utufungulie kipindi, utaratibu wangu ni kuwa ukishindwa kujibu swali unasmama hadi kipindi kiishe, ndiyo utaratibu wangu ulivyo. Sawa mgeni? Kwanza unaitwa nani?” aliuliza

“barry” nikamjibu huku nikiwa nimeanza kutetemeka maana sikuwa nimejiandaa kabisa kwa kilichokuwa kinafuata.

“aaah barry, leo tutaendelea kujifunza classification of kingdom fungi” alisema mwalimu akiwa hana sura ya utani hata kidogo huku akiwa ananingalia mimi. Ni kama vile darasa zima lilikuwa na mwanafunzi mmoja ambaye ni mimi tu. “sasa barry hebu nitajie phylum zinazopatikana katika kingdom fungi” kama unajua kuchanganyikiwa, basi ni siku ile. Ugeni na uoga vilichanganyika na kunifanya niwe nimesimama tu kama sanamu nikiwa sijui hata niseme nini. Nilisimama huku nikiwa sina cha kujibu. Mwalimu aliniangalia kwa macho makali hali ambayo ilinifanya niogope zaidi.

“mgeni…unatoa toa macho tu, shule hiyo ulikotoka walimu walikuwa hawafundishi?” aliuliza huku akinisogrlea. Mimi nilibaki namtizama tu. “nakuuliza wewe, mlikuwa hamsomi?” aliniuliza tena, mara hii akiwa amesimama mbele kabisa ya meza yangu.

“walikuwa wanafundisha” nilimjibu kwa sauti ya chini ambayo sidhani kama wanafunzi wengine walisikia..

“sasa…” alihoji mwalimu huyo. Sikuwa na cha kujibu.

“ukiwa tayari kujibu niambie nikupe swali jingine ama sivyo utasimama hadi mwisho wa kipindi kama ulivyo utaratibu wangu. Jennifer hebu tukumbushe hapo.” Mwalimu alipotaja jina la Jennifer akili yangu ilizinduka ghafla. Nikaanza kuzungusha macho ili nimuone maana nilikuwa na shauku hiyo tangu nilipofika shuleni hapo siku ya kwanza. Mara akasimama. Alikuwa ni msichana wa umbo la wastani, maji ya kunde, sura yake ilikuwa na mwoekano wa kuvutia. Mimi sio mtaalamu sana wa kuwaelezea watu ila itoshe kusema kuwa alikuwa ni msichana aliyevutia kumtazama. Mara baada ya kusimama akaanza kujibu swali.

“Kingdom fungi includes five phyla that are; Chytridiomycota or chytrids, Zygomycota Glomeromycota, Ascomycota and Basidiomycota” alijibu Jennifer bila kukwamakwama kisha alipomaliza akakaa.

“vizuri sana Jennifer, haya darasa mpigieni makofi jennifer” alisema mwalimu.

“pwaaa! Pwaa! Pwa! Pwa! Pwa! Pwaaa!” zilisikika sauti za makofi.

Nilishangaa, nilishangaa sana. Sikutegemea kama mwanafunzi wa form one katika shule zetu za kata angeweza kujibu swali kwa kujiamini vile. Tena cha zaidi alikuwa na mtoto wa kike. Mimi ilikuwa ni vigumu hata kuongea sentensi moja tu ya kiingereza japokuwa uwezo wangu darasani ulikuwa ni mkubwa. Niliona aibu sana.

“unaona wenzako waliokuja shule kusoma” mwalimu alisema, kisha akaendelea “vipi unataka nikupe swali lingine ujibu ili ukae?” ningejibu swali gani, nilibaki kimya. Nilisimama hadi mwalimu alipomaliza kufundisha. Baada ya hapo wanafunzi wenzangu walianza kunitania kwa kuniita mgeni msimamizi, Sikujali.

Siku zilipita, nikayazoea mazingira na watu pia. Kitu nilichojifunza kuhusu Jennifer ni kuwa alikuwa na uwezo mkubwa sana darasani. Niliambiwa kuwa tangu afike shuleni hapo yeye tu ndiye aliyekuwa akishika nafasi ya kwanza tena kwa kuwaacha kwa alama nyingi wale ambao walikuwa wakifuata baada yake. Lakini pia alikuwa akipendwa zaidi na walimu. Ilikuwa kama unataka kugombana na mwalimu, gombana na Jennifer. Jennifer alikuwa ni malkia wa darasa letu. Malkia pasipo mfalme.

Ulifika wakati wa kufanya mid-term test, matokeo yalipotoka nikawa wa pili. Nyuma ya Jennifer kwa wastani wa Alama tisa. Hali hii ilifanya na mimi kuanza kuzungumziwa na kufuatiliwa kwa karibu na walimu. Masomo yaliendelea ikafika wakati wa kufanya mtihani wa mwisho wa mhula wa pili. Nilipopewa ripoti yangu ya matokeo ilionyesha kuwa nilikuwa wa nne. Niliumia kidogo lakini niliona sikuwa na haja ya kujipa msongo wa mawazo.

Shule ikafunguliwa tena. Tukawa kidato cha pili. Baada ya kufika shuleni katika lile wiki la kwanza ulifanyika uchaguzi wa viongozi madarasa. Lakini sidhani kama ulifaa kuitwa uchaguzi maana walimu ndio waliopendekeza majina ya viongozi. Monitor alichaguliwa mwanafunzi aliyeitwa James ambaye alikuwa na umbo kubwa kuliko sisi wengine. Na monitress akachaguliwa Jennifer.

Kwa kipindi chote ambacho tayari nilikuwa nimekiishi sikuwahi kuwa na mawasiliano ya karibu na Jennifer. Japokuwa nilikuwa namchukia yeye na rafiki yake Adela. Niliwachukia kwa sababu walikuwa na tabia ya kujisikia sana. Sikuwa na haja hata ya kushirikiana na nao kwa lolote lile. Huwa sipendi kuwa karibu na watu wa aina kama waliyokuwa wao. Lakini ilikuja siku ambayo mimi na Jennifer tulipambana uso kwa uso. Siku ambayo ilichochea moto wa kumchukia Jennifer. Ilikuwa hivi:

Siku hiyo nilikuwa zamu kufagia darasa pamoja na wenzangu watatu. Lakini kwa bahati mbaya sana wale wenzangu wote niliokuwa nimepangwa nao hawakufika kabisa. Sijui walikwenda wapi maana nakumbuka niliwaona asubuhi mabwenini. Lakini kwa kuwa mimi sipendi matatizo na mtu, nikaamua kwenda kufagia darasa lote mimi pekeyangu. Nilifagia na kumaliza japo nilifanya harakaharaka kwa kuwa muda wa kwenda paredi ulikuwa umekaribia. Kengele ya paredi ikagongwa tukaenda na baadaye tukarudi darasani. Baada ya kuingia darasani na kukaa, Jennifer akasimama na kuomba tumskilize. Kweli tukatii

“ni nani na nani walikuwa wanafagia darasa leo?” nilishangaa kuona linanaulizwa swali kama lile kwa sababu ratiba ya usafi ilikuwa imebandikwa darasani.. Lakini sikuona shida nikanyoosha mkono. Kwa muda huo nilikuwa peke yangu maana wale wenzangu walikuwa hawajaingia darasani bado.

“we barry, hili darasa limefagiliwa kweli?” niliendelea kushangaa, ila kwa kuwa nilikuwa namjua ni mtu mwenye jeuri na mimi niliamua kumjibu jeuri.

“kwani wewe unaonaje?” nilimuuliza.

“halijafagiliwa” alisema jenifer kwa sauti ya mamlaka.

“hili darasa halijafagiliwa, kwa hiyo mimi nilifanyaje?”

“mi sitaki kujua ulifanyaje, ila naomba tu watu watoke nje uwatafute wenzako mje mfagie, sawa” alisema Jennifer. Ukweli ni kuwa darasa halikuwa safi sana kwa kuwa nilifagia nikiwa na haraka. Lakini haikuwa imefika kiasi cha kuambiwa tufagie tena. Hivyo nikaona kulikuwa hakuna haja ya kufagia tena.

“labda kama unawambia watoke nje ili kupunga upepo, mimi sitofagia tena kwa sababu nimeshafagia. Labda mwingine aamue kufanya hivyo lakini si mimi. Utanisamehe tu madam Jennifer.” Nilimjibu, hali iliyosababisha wanafunzi wengine wacheke.

“afagie huyo aacha ujinga, hatuwezi kukaa darasa limejaa vumbi kama hivi” ilikuwa ni sauti ya adela, kiumbe mwingine iliyekuwa namchukia kweli kweli. Sikutaka kuendelea kuongea tena maana nilijua kuwa ujumbe wangu ulisikika na kueleweka vizuri.

Jennifer aliendelea kuniambia kuwa nifagie likini mimi sikumjibu. Hatimaya akasema kuwa ataenda kuripoti kwa mwalimu wa zamu, sikumjibu. Akatoka nje. Alirudi baada ya dakika kama tatu hivi akiwa ameambatana na mwalimu Kachaka ambaye ndiye aliyekuwa mwalimu wa zamu kwa wiki hilo. Nikajua tayari kinaenda kunuka.

“barry ndo nani” mwalimu aliuliza. Nami bila kusita nikanyoosha mkono.

“hili darasa limefagiliwa?” aliuliza mwalimu.

“ndiyo”

“pumbavu mkubwa wewe, unajibu ndiyo. Kwa hiyo unamaanisha kuwa kiongozi wako wa darasa kanidanganya siyo?” aliongea kwa hasira

“hayo mimi siwezi kuyajua, mimi ninachojua kuwa nimefagia” nilijibu kwa kujiamini

“hili darasa limefaguliwa hili?” aliuliza huku akitumia fimbo kuonyesha vipande vichache vya karatasi kilivyokuwa vimezagaa pale mbele. Niliamua kukaa kimya. “hao wenzako wengine wako wapI?” mwalimu aliuliza

“hawajafika bado” alijibu Jennifer

“sasa huyu atabeba msalaba wa wenzake, barry nyanyuka ukatafute fagio ufagie darasa sasa hivi.” Aliamrisha mwalimu. Mimi huwa si mtu wa kuongea sana ila huwa nina kibUri na jaeuri endapo mtu atanikwaza. Nikaamua kukaa kimya maana kama kujibu nilikuwa nimejibu vya kutosha. Niliendelea kukaa. “barry nasema nyanyuka ukatafute ufagio”. Mwalimu alisema kwa ukali zaidi lakii ni kama nilikuwa simsikii. Niliendelea kukaa.

Mwalimu alipandwa na hasira akaja kunishika mkono, alianza kunivuta kunipeleka mbele ya darasa. Aliniamrisha nishike chini anichape nikagona. Akatumia nguvu nikazidiwa, akanichapa fimbo idadi ambayo hadi sasa huwa sikumbuki. Baada ya hapo aliwaambia wanafunzi watoke nje ili nifagie darasa na pia akanipa adhabu ya kuchimbua visiki vinne.

Wakati wanafunzi wanatoka nje mimi nikawa nawaza nifanyaje. Nilikuwa nimepandwa na hasira sana. Nikaamua kuwapa ushindi Jennifer pamoja ma mwalimu, nilikubali kufagia darasa. Wakati naanza kufagia walikuja wanafunzi wengine wachache kunisaidia. Baada ya hapo nilikwenda kuchukua vifaa kwa ajili ya kuchimba visiki. Nilifanya haya yote nikiwa na hasira kali juu ya Jennifer.

Itaendelea…
Shukrani sana mkuu, naendelea kukuzingatia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom