Hadithi: Kifo Mikononi Mwangu

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Apr 29, 2016
20,744
25,439
MSICHANA mwenyewe nilikuwa simfahamu. Tulikutana tu kwenye harusi ya rafiki yangu, akaniambia ananifahamu.


Msichana alikwenda mbali zaidi, akaniambia niliwahi kuwa mpenzi wake kisha nikamtoroka na siku ile ndiyo alikuwa ananiona.






Kila nilivyomkatalia kwamba sikuwa nikimfahamu na kwamba mimi siye niliyekuwa mpenzi wake, msichana hakuniamini kabisa. Ilibidi baada ya tafrija kumalizika tuondoke pamoja. Alinipeleka nyumbani kwake na kunipa kinywaji. Sikufahamu kinywaji hicho alikitia nini na kwa madhumuni gani kwani baada ya kunywa tu kinywaji hicho, usingizi mzito ulinipitia.





Niliamka saa kumi na moja alfajiri na kumkuta mwenyeji wangu huyo ameuawa kando ya mlango kwa kupigwa na kitu kizito kichwani. Balaa likaniangukia mimi. Je, msichana huyo alikuwa nani, kwa nini alisema nilikuwa mpenzi wake na ni nani aliyemuua na kwa sababu gani?





SASA ENDELEA…


K
AMA wasemavyo wahenga maisha ni safari ndefu. Safari yenyewe si tambarare moja kwa moja. Ni safari yenye mabonde na milima. Naitwa Denis Wiliam Makita. Nilizaliwa miaka thelathini na nane iliyopita.





Kwa rehema ya Mungu nilizaliwa na mwenzangu wa kiume tukiwa pacha. Mwenzangu alikuwa akiitwa Charles Wiliam Makita.


Baada ya kumaliza masomo yetu ya kidato cha sita, mimi nilijiunga na Jeshi la Polisi. Niliomba kazi ya upolisi nikiwa Dar, lakini baada ya mafunzo ya upolisi nilikwenda kuanza kazi Wilaya ya Lushoto.





Mwenzangu hakutaka kufanya kazi ya kuajiriwa. Alijiingiza kwenye biashara na misukumo ya maisha ikatukutanisha tena huko Tanga. Wakati mimi nikiwa Lushoto, yeye alikuwa Tanga mjini.


Hapo Lushoto nilifanya kazi kwa mwaka mmoja, nikahamishiwa Tanga mjini. Baada ya kufanya kazi kwenye kituo cha Tanga kwa miaka saba ndipo nilipopendana na polisi mwenzangu aliyehamishwa kutoka Moshi na kuletwa Tanga. Alikuwa anaitwa Miriam.





Baada ya kuridhika na tabia zake na urembo wake, nilimchumbia Miriam na kuoana naye huko kwao Moshi.


Baada ya kuishi na Miriam kwa miaka miwili ndipo siku moja mke wangu huyo aliponipa habari nilizozifanyia kazi.





Aliniambia kwamba huko alikokwenda kusukwa alipata taarifa kwamba kulikuwa na watu ambao walikuwa wakifanya biashara ya meno ya tembo. Na walikuwa wakiyatoa meno hayo katika Msitu wa Handeni.


Akanieleza kwamba meno hayo husafirishwa hadi Kitongoji cha Mwambani kilichoko kilometa kadhaa nje ya Jiji la Tanga, pembezoni mwa Bahari ya Hindi.





Allinieleza kwamba meno hayo huhifadhiwa chini ya ardhi kwenye ufukwe wa bahari katika eneo hilo. Aliendelea kunieleza kwamba watu hao huchimba shimo usiku na kuyafukia meno hayo.


Baada ya hapo kuna usiku mwingine meno hayo hufukuliwa na kupakiwa kwenye majahazi kisha kusafirishwa kwenda kuuzwa nchi za nje.


Wakati huo mke wangu alikuwa na cheo cha ukoplo, mimi nilikuwa na cheo cha Sajin Meja. Kicheo mimi nilikuwa nimemzidi na tulikuwa tunafanya kazi katika kituo kimoja.





Mke wangu aliniambia habari ile badala ya kuiripoti kituo cha polisi kwa sababu nilikuwa mkuu wake. Aliona akinipa mimi taarifa hiyo ndiyo itakuwa imefika kituo cha polisi. Inawezekana pia aliniambia mimi ili tufanye uchunguzi kabla ya kuiripoti kituoni.


Na mimi nikafanya uchunguzi wangu. Baada ya uchunguzi wa siku tatu, nikagundua kuwa habari ile ilikuwa ni ya kweli na nilimgundua aliyekuwa akihusika na meno hayo.





Alikuwa ni mtu mmoja mwenye asili ya Mombasa nchini Kenya, lakini raia wa Tanzania aliyekuwa akiitwa Azzal Mubarak.


Baada ya kupata data zote nikaripoti kwa wakuu wangu. Siku hiyo tuliondoka usiku polisi kumi tukaenda katika eneo hilo kwa kutumia boti tatu za polisi.


Tulipofika mahali hapo tulikuta watu wakichimba. Walipotuona walitupa machepe na kukimbia. Baada ya kufukuzana nao tulikamata mtu mmoja.





Baada ya kumkamata mtu huyo tukaendelea kupafukua pale mahali. Tulikuta karibu vipande themanini vya meno ya tembo.


Vipande hivyo vilipakiwa kwenye boti zote tatu na kusafirishwa hadi jijini.


Baada ya kumhoji yule mtu tuliyemkamata alituambia yeye alikuwa anachukuliwa kama kibarua tu wa kufukua yale mashimo na kutoa meno yaliyozikwa ili jahazi likija yapakiwe.





Alipotakiwa kuwataja wahusika wenyewe alisema alikuwa hawafahamu ila anawafahamu watu watatu wa kati waliokuwa wakiishi Mwambani.


Alipotajiwa jina la Azzal Mubarak, mtu aliyekuwa akishukiwa kumiliki meno hayo alituambia alikuwa akimfahamu Azzal kwa jina tu, lakini hakuwahi kukutana naye.





Msako ukaanza usiku uleule. Baadhi ya polisi walikwenda Mwambani kwa gari wakiwa na yule mtu ambaye aliwapeleka polisi hao katika nyumba walizokuwa wakiishi watu hao aliowataja, lakini hakukuwa na mtu yeyote miongoni mwao aliyepatikana. Wote walishakimbia.


Polisi wengine nikiwemo mimi tulikwenda kumkamata Azzal Mubarak aliyekuwa akiishi katika eneo la Raskazoni.





Yeye na yule mtu aliyekamatwa kwanza walifunguliwa mashitaka. Polisi tulifuatilia kesi ile kwa miezi nane. Azzal Mubarak alikuwa ameweka wakili wa kumtetea.


Wakati kesi yake ikiendelea nilipata pigo. Ndugu yangu, Charles alifariki dunia. Alifariki dunia kwenye ajali ya basi. Basi alilokuwa akisafiria kutoka Dar kuja Tanga liligongana uso kwa uso na basi lingine lililokuwa likitoka Tanga kwenda Dar. Abiria watatu akiwemo ndugu yangu walifariki dunia hapohapo.





Kifo cha Charles kilinifanya nigundue kuwa ndugu yangu huyo pamoja na kujiingiza katika biashara zisizoeleweka alikuwa jambazi. Chumbani kwake nilikuta bastola na risasi kumi. Pia nilikuta vielelezo vilivyobainishia kuwa kazi yake halisi ilikuwa ujambazi na alihusika katika matukio mengi ya ujambazi na mauaji.





Nilishukuru kwamba sikumgundua mapema kwani angeniharibia kazi.


Kule kugundua kwangu kwamba Charles hakuwa mtu muaminifu, nilimsahau mara moja. Mtu wa namna ile akifa unashukuru Mungu hata kama ni ndugu yako.


Kwenye ile kesi ya Azzal Mubarak, mwisho wa siku mahakama ilimuachia huru kwa kukosekana ushahidi thabiti wa kumtia hatiani. Yule mshitakiwa wa pili alihukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela.





Akiwa nje ya mahakama, Azzal aliniambia;


“Ulinikamata kwa kunionea tu.”


Aliniambia mimi hivyo kwa sababu nilikuwa mpelelezi wa kesi yake. Pia katika wale polisi waliokwenda kumkamata siku ile, mimi ndiye niliyekuwa mkubwa niliyetoa amri akamatwe.


“Unasemaje?” Nikamuuliza nikiwa nimemkunjia uso.





“Nimekwambia ulinikamata kwa kunionea tu.”


“Kumbe ulitaka tukuachie hata kama unashukiwa?”


“Kuwa na roho mbaya haitakusaidia.”


“Kama mahakama imekuachia, shukuru Mungu. Usinilaumu mimi. Mimi niko kazini.”


“Sawa. Tutaonana.”


Nikashtuka. “Tutaonana kwa heri au kwa shari?” Nikamuuliza.





Azzal hakujibu, akaelekea kwenye gari lake la kifahari lililokuwa likimsubiri hapo mahakamani. Akajipakia na kuondoka. Wakati gari linaondoka alinipungia mkono wa kuniaga. Nikampuuza.


Hata hivyo, kwa vile alikuwa mtu tajiri na katili kwa mujibu wa sifa zake tulizozisikia, maneno yake yalinitia wasiwasi sana.





Polisi wengi hatukuwa tumeridhika na ile hukumu kwa sababu tulikuwa na uhakika kwamba Azzal ndiye aliyehusika na yale meno ya tembo. Lakini tulitambua tatizo letu ni kukosekana kwa ushahidi wa kutosha wa kumuhusisha na meno hayo ambayo aliyakana.


Mimi na mke wangu siku nyingine tulikuwa tunatofautiana kuingia kazini. Mimi nikiingia mchana, yeye anaweza kuingia usiku. Au mimi nikiingia usiku, yeye anaweza kuingia mchana.





Baada ya wiki moja hivi tangu kumalizika kwa kesi ya Azzal, nilialikwa kwenye harusi ya rafiki yangu mmoja ambaye zamani alikuwa polisi na nilikuwa naye Lushoto, lakini baadaye alifukuzwa kazi kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa.


Mtu huyo baada ya kufukuzwa kazi alikuja Tanga na kujiingiza kwenye biashara ziliompa mafanikio.


Katika kadi yake ya mwaliko aliyonipa ilionesha kuwa tafrija ilikuwa ikifanyika katika Hoteli ya Mkonge usiku. Hoteli ya Mkonge ilikuwa katika eneo la Raskazoni, pembezoni mwa Bahari ya Hindi.





Mwaliko ulikuwa ni wa mimi na mke wangu, lakini siku ile mke wangu alikuwa na zamu ya kuingia kazini usiku. Kabla ya kwenda kazini aliniambia kwa vile yeye alikuwa anakwenda kazini, nisiende huko kwenye tafrija.


“Kama unaenda kazini si ninaweza kwenda peke yangu?” Nikamwambia.





“Kwa nini uende peke yako wakati kadi yako imeandikwa bwana na bibi? Nakushauri ulale.”


“Si vizuri. Huyu mtu ni rafiki yangu na nimemthibitishia kuwa nitahudhuria.”


“Sawa. Tutaonana hapo asubuhi nikitoka kazini.”


Mke wangu alipotoka kwenda kazini kwake, nikaanza kujiandaa. Nilivaa ile suti yangu niliyokwenda


Je, nini kiliendelea? Usikose Ijumaa kwenye Gazeti la Ijumaa.


FAKI A. FAKI


SIMU: 0655 340572
 
SEHEMU YA 02


ILIPOISHIA WIKIENDA…


“Kama unakwenda kazini si ninaweza kwenda peke yangu?” Nikamwambia.


“Kwa nini uende peke yako wakati kadi yako imeandikwa bwana na bibi? Nakushauri ulale.”


“Si vizuri. Huyu mtu ni rafiki yangu na nimemthibitishia kuwa nitahudhuria.”


“Sawa. Tutaonana hapo asubuhi nikitoka kazini.”


Mke wangu alipotoka kwenda kazini kwake, nikaanza kujiandaa. Nilivaa ile suti yangu niliyokwenda kuolea, nikafunga kikuba cha rangi nyekundu na kutoka.






SASA ENDELEA…


NILIKODI teksi ya kunipeleka kwenye Hoteli ya Mkonge ilikokuwa inafanyika tafrija.



Teksi ilisimama mbele ya mlango wa hoteli. Wakati nashuka kwenye teksi nikakumbuka kwamba nilisahau kuchukua ile kadi ya mwaliko.


Ilinichukua kama sekunde thelathini kujipekua kwenye mifuko yangu yote nikiwa mbele ya mlango wa teksi. Nikaamini kwamba kadi yangu niliiacha nyumbani.


Kadi hiyo ilikuwa kama tiketi yangu ya kuingilia kwenye ukumbi huo. Bila kadi hiyo nisingeweza kuingia.





Nilifikiria kurudi nyumbani kuchukua kadi hiyo na kuja tena hoteli hapo. Niliona utakuwa ni mzunguko usio na maana. Kulikuwa na teksi nyingine iliyokuwa ikisimama nyuma ya teksi iliyonileta..


Nilitoa pesa, nikamlipa dereva wa teksi. Teksi iliondoka. Mimi nikabaki nimesimama nikiwaza. Ndani ya teksi iliyosimama, alishuka msichana mmoja, akanitazama kama mtu aliyekuwa akinifahamu, lakini mimi sikumpatiliza kwa sababu nilikuwa simjui.





Alinitolea tabasamu kabla kunisalimia.


“Habari ya siku?”


“Nzuri,” nilimjibu kwa mkato kwa sababu nilikuwa nimefadhaika baada ya kugundua nilikuwa nimesahau kadi yangu.


“Mbona umesimama kama uliyefadhaishwa na kitu?” Akaniuliza.


“Ni kweli,” nilimwambia na kuongeza;





“Nimesahau nyumbani kadi yangu ya kuingilia.”


“Oh si tatizo. Unaweza kuingia kwa kadi yangu. Kadi yangu imeandikwa bwana na bibi, lakini niko peke yangu. Tunaweza kuingia pamoja,” akaniambia.


“Nashukuru sana kwa sababu nilikuwa nimeshachanganyikiwa.”


Msichana huyo aliitoa kadi yake kwenye pochi akawa anatabasamu.


“Unasahauje kadi nyumbani. Una mawazo gani?” Akaniuliza.


“Kusahau ni kitu cha kawaida kwa binadamu, nilisahau tu,” nikamwambia.


“Twen’zetu.”





Nikaingia ndani ya hoteli hiyo na msichana huyo niliyekuwa simfahamu, lakini wakati wote alikuwa akinitolea tabasamu. Tulikwenda katika eneo la ukumbi ambako tafrija hiyo ilikuwa inafanyika, tukaingia ndani ya ukumbi huo kwa kutumia kadi ya msichana huyo.


Mara tu baada ya kukaa kwenye viti, msichana huyo aliniuliza.


“Msami umekuwa wapi siku nyingi?”


Nikashtuka kidogo kisha nikamuuliza.





“Nani…mimi…?”


“Ndiyo, nakuuliza wewe.”


“Mimi nipo hapahapa Tanga, lakini isije ikawa umenifananisha. Mimi siitwi Msami.”


“Una maana umenisahau mimi niliyekuwa mpenzi wako halafu ukanitoroka bila kosa?”


“Hapana. Siye mimi. Labda umenifananisha tu.”


“Sijakufananisha. Ninakufahamu wewe ni Msami. Sijui nilikukosea nini. Unakumbuka kwamba dada yangu alifariki dunia?”


“Simfahamu.”





“Msami mbona uko hivyo! Una maana hata shemeji yako, Ester humfahamu?”


Nikahisi huenda msichana huyo alikuwa amenifananisha na mtu aliyekuwa mpenzi wake.


Mimi nilikuwa nimefanana sana na ndugu yangu Charles aliyekuwa amefariki dunia. Angeniita kwa jina la Charles ningejua amenifananisha naye, lakini jina alilotumia lilikuwa geni kwangu.


Msichana alipoona ninakana kufahamiana naye akanyamaza kimya na kubaki kunitazama.





Nilibadilisha mazungumzo, tukawa tunazungumza mazungumzo mengine huku tukinywa vinywaji. Muziki ulipomkolea msichana huyo aliniomba twende tukacheze, nikaenda kucheza naye. Alikuwa hodari sana wa kucheza na kwa kweli alinifurahisha.


Nilikwenda kucheza naye karibu mara nne. Mtu aliyekuwa akishughulika kupiga video alikuwa akimrikodi sana msichana huyo kwa jinsi alivyoonesha umahiri wa kucheza.


Sherehe ilimalizika saa nane usiku. Tukatoka. Tulipanda teksi moja na yule msichana.





“Unaishi wapi?” Nikamuuliza.


“Kwa sasa ninaishi Kwaminchi. Nilihama kule Sahare.”


“Basi acha teksi ikupeleke wewe kwanza.”


“Ni vizuri ili upajue nyumbani kwangu.”


Teksi ikatupeleka Kwaminchi. Msichana huyo ambaye sikutaka kumuuliza jina lake wala kumtambulisha jina langu alimuelekeza dereva wa teksi nyumba aliyokuwa anaishi.


Teksi iliposimama mbele ya nyumba hiyo msichana aliniambia.





“Karibu ndani.”


“Kwa vile nimeshaijua nyumba tunaweza kutembeleana siku nyingine.” Nikamwambia.


“Lakini kwa leo si umeshafika? Kwa nini uishie nje? Ingia ndani upumzike kidogo tu halafu utarudi kwako. Teksi ziko nyingi hapa.”


Msichana alinishawishi mpaka tukashuka pamoja kwenye teksi.


Nilitaka kumlipa dereva, lakini yeye ndiye aliyewahi kutoa pesa. Alimlipa mwenye teksi. Teksi ikaondoka.


“Karibu.”





Tukaelekea kwenye mlango wa nyumba wa upande wa kushoto. Nyumba yenyewe ilikuwa na milango miwili. Mlango wa upande wa kulia na mlango wa upande wa kushoto.


“Tuko wakazi wawili, lakini kila mtu ana upande wake,” msichana huyo aliniambia.


Kitu ambacho kilionesha kuwa alikuwa akiishi peke yake alitoa ufunguo kutoka kwenye pochi yake akafungua mlango huo na kunikaribisha ndani.


Tulipoingia ndani tulitokea kwenye sebule pana na nadhifu.





“Karibu ukae.” Akaniambia.


Nikakaa kwenye kochi. Msichana aliingia ndani zaidi. Baada ya muda kidogo alirudi tena akiwa amevua zile nguo zake na kujifunga khanga kifuani akiwa ameshika chupa mbili za bia na bilauri mbili. Aliziweka kwenye kochi, akavuta meza ya kioo karibu na kochi kisha akaweka zile chupa pamoja na bilauri.


Alikaa karibu yangu, akazibua chupa zote mbili na kumimina kilevi kwenye bilauri zote mbili.





“Karibu ujichangamshe kidogo.” Akaniambia huku akinisogezea bilauri moja. Sikuhitaji kuendelea kunywa muda ule, lakini nilishindwa kumkatalia. Nikaipokea ile bilauri na kupiga funda kilevi hicho kisha nikairudisha bilauri juu ya meza.


Niseme ukweli kwamba katika kuingia kwenye nyumba ya msichana huyo ambaye nilikuwa simfahamu na kukubali kunywa naye kilevi humo ndani sikutumia kabisa taaluma yangu ya ukachero.


Kweli wanawake ni watu wepesi sana kumzuga mtu, pengine ni kutokana na maumbile yao na mvuto wao kwa wanaume.





Nakumbuka nilipiga mafunda matatu tu ya bia halafu sikuweza kufahamu tena kilichoendelea. Nilipitiwa na usingizi mzito, nikalala palepale. Sikujua aliniwekea kitu gani kwenye pombe.


Nilipokuja kuzinduka, nilijiona nilikuwa nimelala kitandani chumbani kwa msichana huyo, lakini mwenyeji wangu hakuwepo kitandani. Nilikuwa peke yangu na taa ilikuwa inawaka.





Nikainuka na kukaa. Kichwa changu kilikuwa kina mawengemawenge kama mtu niliyekuwa nimelewa sana. Suti yangu bado nilikuwa nayo mwilini. Sikuwa nimeivua. Miguu ilibaki na soksi. Viatu vyangu vilivuliwa na kuwekwa kando ya kitanda.


Kumbukumbu zangu ziliniambia kwamba nilikuwa nimekaa sebuleni na msichana aliyenikaribisha mle ndani, tukinywa bia, lakini sikuweza kufahamu niliendelea kunywa hadi muda gani na nini kingine kilitokea. Fahamu zilinipotea.





Nikajiuliza iwapo fahamu zilinipotea baada ya kulewa sana. Lakini mimi mwenyewe sikukumbuka kama niliendelea kunywa sana. Nikajiuliza tena kama fahamu zilinipotea nikiwa nimekaa sebuleni, ni nani aliyeniingiza chumbani na kunilaza kitandani au niliingia na kulala mwenyewe nikiwa sijifahamu?





Maswali yote niliyojiuliza yalikosa majibu. Ilikuwa vigumu kupata majibu kwa sababu mambo yote hayo yalipokuwa yakitokea nilikuwa sijielewi. Kama kulikuwa na majibu yalikuwa ya kukisia tu yasiyo na usahihi. Inawezekana nilikunywa sana. Yule msichana alipoona nimelala alinishika na kuniburuza chumbani mwake na kunilaza kitandani.





Nikaitazama saa yangu iliyokuwa mkononi. Ilikuwa saa kumi na dakika kumi alfajiri. Nikashuka kitandani na kuvaa viatu vyangu. Baada ya kuvaa viatu nikaenda kwenye mlango. Nilijaribu kuufungua nikaona unafunguka. Nikatoka. Nilitokea kwenye sebule mahali ambapo nilikuwa nimekaa awali na yule msichana.


Juu ya ile meza kulikuwa na chupa moja tu ya bia iliyokuwa upande niliokuwa nimekaa mimi. Chupa hiyo ilikuwa imebaki na pombe. Kiasi kilichonywewa kilikuwa kidogo, hali iliyoonesha kuwa sikuwa nimekunywa sana.





Nikayazungusha macho yangu huku na huku. Macho yalipokwenda kwenye mlango wa nje nilishtuka. Mlango ulikuwa wazi uliofunguka kidogo. Kando ya mlango kwa ndani msichana aliyenikaribisha ndani alikuwa amelala chini kichalichali, mwili wake ukiwa na khanga aliyokuwa amevaa.


Upande wa kichwani kwake alikuwa amelalia dimbwi la damu nyeusi iliyoganda!


Macho yake yalikuwa wazi, lakini yasiyoona chochote.


“Nini tena?” Nikajiuliza.





Nilisogea karibu na mlango huo, nikainama na kumtazama msichana huyo vizuri.


Kutokana na uzoevu wangu wa kutazama nyuso za maiti, niligundua mara moja kuwa msichana huyo hakuwa hai. Alikuwa ameuawa.


Pembeni mwa kichwa chake kulikuwa na vipande vya chupa ya bia iliyovunjika ambavyo navyo vilikuwa na damu. Nilishuku kwamba chupa hiyo ndiyo iliyokuwa na bia aliyokunywa msichana huyo.


“Sasa hili ni balaa!” Nikawaza.





Kutokana na mbinu zetu za kazi ya upolisi, mimi niliyekuwa na msichana huyu ndiyo ninakuwa mtuhumiwa namba moja. Lazima nikamatwe na kuwekwa ndani kwa tuhuma za mauaji. Balaa limeshaniangukia mimi wakati msichana mwenyewe hata simjui ni nani!


Je, nini kiliendelea?
 
SEHEMU YA 03


ILIPOISHIA IJUMAA…


Pembeni mwa kichwa chake kulikuwa na vipande vya chupa ya bia iliyovunjika ambavyo navyo vilikuwa na damu. Nilishuku kwamba chupa hiyo ndiyo iliyokuwa na bia aliyokuwa akiinywa msichana huyo.


“Sasa hili ni balaa!” Nikawaza.


Kutokana na mbinu zetu za kazi ya upolisi, mimi niliyekuwa na msichana huyu ndiye ninakuwa mtuhumiwa namba moja. Lazima nikamatwe na kuwekwa ndani kwa tuhuma za mauaji. Balaa limeshaniangukia mimi wakati msichana mwenyewe hata simjui ni nani!


SASA ENDELEA…


KUSEMA
kweli nilijuta kukutana na msichana huyo na kukubali kuingia nyumbani kwake wakati nikiwa simfahamu. Kumbe janga lilikuwa linanisubiri.


Nikajiuliza huyu msichana ameuawa na nani na kwa sababu gani? Nikajiuliza tena polisi wakifika hapa watamkamata nani?


Kama watanikamata mimi na ni lazima wanikamate mimi niliyekutwa kwenye tukio, nitafikiriwa nini? Si nitafikiriwa kwamba mimi ni polisi mlevi na malaya na kwamba nilifika nyumbani kwa msichana huyo kuendeleza umalaya wangu kukatokea kutokuelewana, nikachukua maamuzi ya kumuua!


Dhana hii ya kuwa mimi ni polisi mlevi na malaya haikunipendeza hata kidogo. Ilikuwa dhana iliyokuwa kinyume na ukweli na ingenidhalilisha na kufanya nionekane kuwa nilikuwa kijana nisiye na maana si tu katika jeshi la polisi bali kwa jamii nzima.


Kibaya zaidi ni kuwa upo uwezekano mkubwa wa kukamatwa na kufikishwa mahakamani kwa sababu mimi ndiye niliyekutwa na marehemu. Hivyo basi ili kuepukana na balaa kubwa zaidi, niliona niondoke haraka mahali hapo kabla hakujakucha na kabla ya kufahamika kwamba msichana huyo ameuawa.


Nilirudi tena mle chumbani nilimokuwa. Unaweza kunicheka nikikwambia kwamba nilirudi humo chumbani kwa kunyata kama vile nilitaka hatua zangu zisisikike. Kitasa cha mlango wa chumba hicho nilikifutafuta kwa kitambaa na safari hii nilikishika kwa kitambaa na kufungua mlango. Hakukuwa na kitu chochote cha maana kilichofanya nirudi humo chumbani zaidi ya kukitupia macho hicho chumba.


Niliporidhika kwamba hakukuwa na kitu changu chochote nilichokiacha, nilitoka, nikafunga mlango kwa kutumia kitambaa. Sikukishika kitasa hicho kwa mikono mitupu. Niliogopa alama zangu za vidole zisije zikabaki hapo. Kama zitabaki, hata kama ningeondoka humo ndani, alama hizo zingeweza kuja kunikamatisha.


Nilipofika sebuleni napo niliangaza macho kabla ya kuuruka mwili wa msichana huyo uliokuwa chini usawa wa mlango wa kutokea nje. Nilipotoka nje, bado niliona chembechembe za damu mbele ya mlango.


Nilipotoka nje, nilifunga mlango kisha nikakipangusa kitasa cha mlango kwa kutumia kitambaa. Sikupenda nifute alama zilizokuwa kwenye kitasa hicho kwa sababu alama za muuaji zingeweza kupatikana hapo, lakini niliona kwa vile nilikuwa nimeingia ndani kwa kutumia mlango huo kulikuwa na uwezekano wa kuwepo alama zangu. Ndipo nikaona nikifute hicho kitasa ili nijiondoe kwenye matatizo.


Baada ya hapo, nikasepa. Nilitembea kwa miguu harakaharaka kuelekea mtaa wa pili ambako kulikuwa na kituo cha teksi. Nikakodi teksi iliyonipeleka nyumbani kwangu. Wakati ninafika nyumbani ilikuwa saa kumi na moja na nusu. Ilibaki nusu saa tu kuwa saa kumi na mbili kamili asubuhi ambapo mke wangu angerudi kutoka kazini.


Nyumba yangu ilikuwa katika kambi ya makazi ya polisi iliyokuwa karibu na kituo chetu cha polisi.


Teksi iliponishusha niligundua kuwa sikuwa na pochi ya pesa mfukoni. Iliwezekana pochi niliiangusha nyumbani kwa yule msichana au msichana huyo alinichomolea pochi yangu alipoona nimelala.


Nikafikiria, kurudi tena Kwaminchi kuitafuta pochi yangu, lilikuwa jambo la hatari sana. Ilikuwa ni sawa na kujipeleka mwenyewe kwenye tatizo nililokwisha kulikimbia. Muda ule kulikuwa kumeanza kupambazuka, ningeweza kuonekana na watu nikiingia au nikitoka humo ndani au ninaweza kuja kufumwa na mtu yeyote atakayefika nyumbani kwa msichana yule kwa dharura yoyote ile.


Nikajiuliza nilikuwa nimeweka vitu gani ndani ya pochi ile? Wakati nikijiuliza hivyo nilikuwa nikijipekua kwenye mifuko yangu mingine kutafuta kitambulisho changu ambacho ndicho kilichonitia shaka.


Kitambulisho changu nilikuwa nacho kwenye mfuko wa ndani wa koti langu. Ndani ya pochi yangu mlikuwa na pesa tu ambazo hazikuzidi shilingi laki moja. Kupoteza pesa hizo kwa ajili ya kuokoa maisha yangu sikuona tatizo.


Kwa vile pochi iliyokuwa na pesa zangu sikuwa nayo, nilikosa pesa ya kumlipa dereva teksi.


“Subiri nikuchukulie pesa,” nikamwambia dereva wa teksi huku nikielekea kwenye mlango wa nyumba yangu.


Nilitoa funguo nikafungua mlango na kuingia ndani. Niliingia chumbani nikafungua kabati na kuchukua shilingi elfu hamsini na kuzitia mfukoni mwangu.


Nilitoka tena nikamlipa dereva teksi pesa aliyoitaka kisha nikarudi ndani. Kitu cha kwanza nilikwenda kupiga mswaki kuondoa harufu ya kilevi kinywani mwangu kisha nikaoga maji baridi.


Baada ya kuoga nikaingia chumbani kwangu na kujitupa kitandani. Lengo langu halikuwa kulala, lilikuwa ni kujituliza na kuwaza kuhusu lile tukio lililotokea.


Nikajiuliza ni nani aliyemuua yule msichana na alitokea wakati gani? Wazo la kwanza kunijia ni la wezi. Nilishuku kwamba wakati nikiwa nimelala kuna wezi walivunja mlango na kuingia ndani ambapo walimuua yule msichana ili waibe.


Wazo hilo la wezi lilikataliwa akilini mwangu. Nilijiambia kama ni wezi mbona hakukuwa na kitu chochote kilichoibwa na wala mlango haukuwa umevunjwa? Nikaona hawakuwa wezi.


Nikawaza tena huenda aliyemuua msichana yule ni mwanaume wake aliyemfungulia mlango na kugombana naye kutokana na kuingiza mwanaume mwingine mle ndani. Wazo hilo ndilo nililoliona lilikuwa sahihi.


Nikafahamu kuwa kama ni kuripotiwa, tukio hilo lingeripotiwa katika kituo chetu na iliwezekana kwamba hata mimi ningehusika katika uchunguzi huo.


Ingawa usingizi ulikuwa umeniruka, sikutaka nilale kwa sababu saa moja asubuhi nilitakiwa niwe kituoni.


Saa kumi na mbili na robo mke wangu akawasili nyumbani. Sare yake ilikuwa imechafuka.


“Habari ya asubuhi?” Nikamsalimia.


“Nzuri. Umeamkaje?”


“Nimeamka salama.”


“Ulikwenda kwenye part?”


“Nilikwenda, lakini sikukaa sana nikarudi nyumbani.” Nikamdanganya.


“Part yenyewe ilikuwaje?”


“Ilikuwa nzuri ila niliona niondoke mapema niweze kulala kidogo kwa sababu asubuhi ninatakiwa kazini.”


“Bia zilikuwepo za kutosha?”


“Zilikuwa za kumwaga.”


“Mmh…ulikunywa mpaka..!”


“Sikunywa sana. Nilikunywa chupa mbili tu.”


“Mmh…usinidanganye…”


“Nakwambia ukweli, nilikunywa chupa mbili tu nikaondoka…”


Ili kubadili yale mazungumzo nikamuuliza.


“Mbona umechafuka?”


“Nilipangwa kwenye doria ya usiku. Si unajua kufukuzana na wezi na wavuta bangi, sehemu nyingine ni za mashimo. Inabidi uchafuke.”


“Kumbe ulipangwa kwenye doria?”


“Tumezunguka na gari usiku kucha. Saa kumi na mbili ndiyo tumerudi kituoni. Nimechoka. Hapa nataka kulala tu.”


“Njoo ulale. Mimi natoka, nakwenda kazini.”


“Mpaka nioge kwanza. Si umeona nilivyochafuka. Kuna vibaka tuliwafufukuza usiku nikamshika mmoja. Sasa akawa ananiminya ili nimuachie akaniangusha chini na yeye akaanguka kwa sababu nilikuwa nimemshika…”


“Hao vibaka walikuwa wanafanya nini?”


“Tuliwakuta wamekaa kikundi tukahisi walikuwa wanavuta bangi au wanapanga njama za kwenda kuvunja nyumba za watu. Wale walikuwa wezi. Mahali walipokuwa tulikuta bisibisi mbili na koleo.”


“Hizo bisibisi na koleo zilikuwa za kuvunja kufuli.”


“Tumewakamata watatu, wengine waliingia kwenye vichochoro na kutupotea.”


Wakati tunazungumza tulikuwa chumbani. Nilikuwa nimekaa kitandani, nikainuka.


“Saa ngapi?” Nikamuuliza.


Mke wangu akaitazama saa yake mkononi.


“Saa moja kasoro robo,” akaniambia.


“Ngoja nivae nitoke.”


Nikavaa sare zangu za polisi nikimuacha Miriam akivua sare zake na kuvaa khanga. Alichukua sare hizo na kutoka nazo chumbani.


Baada ya kuvaa sare zangu, nilivaa kofia, nikachukua kifimbo changu cha umeja na kukishika mkononi kisha nikatoka chumbani. Nilikwenda uani mwa nyumba yetu nikamuaga mke wangu na kuondoka.


Mahali ilipokuwa kambi yetu na kilipokuwa kituo cha polisi, ulikuwa ni mwendo mfupi sana. Dakika chache tu baadaye nikawa kituoni hapo. Filimbi ya paredi ilipopigwa polisi wote tulijipanga msitari na kufanya paredi kabla ya kufanyika ukaguzi wa usafi na ndevu. Ndevu katika jeshi la polisi haziruhusiwi. Kinachoruhusiwa ni sharubu.


Je, nini kiliendelea? Usikose Ijumaa kwenye Gazeti la Ijumaa.


FAKI A. FAKI


SIMU: 0655 340572
 
SEHEMU YA 04


ILIPOISHIA WIKIENDA…


Nikashtuka na kutambua kuwa huyo ndiye yule msichana aliyeuawa mikononi mwangu.


Mimi na polisi wenzangu tukatazamana kwa mshangao.


“Mauaji yameanza tena kwenye jiji letu!” Nikajidai kuwaambia wenzangu.


“Mauaji yalikuwa yamekoma kwa muda mrefu kutokana na kuimarisha doria zetu za usiku,” polisi mmoja akasema.


“Lakini huyu aliyearifiwa ameuawa nyumbani,” polisi mwingine akasema kisha akamtazama yule aliyetupa taarifa.


“Huyu si ameuawa nyumbani kwake?” Akamuuliza.


SASA ENDELEA…


TAARIFA imesema ameuawa nyumbani kwake. Nafikiri anaishi pake yake.”


Kwa bahati njema nikawa kiongozi wa msafara uliopangwa kwenda huko Kwaminchi nyumbani kwa msichana huyo aliyeuawa.


Tulipofika katika mtaa huo tulikwenda nyumbani kwa mwenyekiti wa mtaa huo, akatufahamisha nyumba iliyotokea tukio hilo ingawa mimi nilikuwa ninaifahamu.


Tulipofika tulimkuta yule mjumbe aliyetupigia simu. Mjumbe mwenyewe alikuwa mwanamke. Mbali ya yeye, tulikuta watu kadhaa wakiwa wameizunguka nyumba hiyo. Si unajua panapotokea tatizo watu hujazana kutaka kujua kumetokea nini?


Tuliingia ndani ya nyumba hiyo na kuikuta ile maiti mahali palepale nilipoiacha.


“Kumetokea nini?” Nikajidai kumuuliza yule mjumbe.


“Kilichotokea hatukifahamu. Huyu msichana ambaye ni jirani yetu na ni mwenzetu amekutwa ameuawa hii asubuhi.”


“Mtu wa kwanza kugundua kuwa kuna maiti humu ndani ni nani?”


Mwanamke huyo alinywea kabla ya kujibu.


“Ni mimi.”


“Mbona umenywea?”


“Hapana, sijanywea. Tunazungumza.”


“Uliigunduaje hii maiti?”


“Nilikuwa nimekuja kufuata mchango wa maziko. Katika mtaa wetu tuna chama chetu cha kuzikana. Mtu anapokufa watu wengine wanatoa mchango wa gharama ya maziko au kusafirisha maiti kama inapelekwa mji mwingine. Sasa nilikuja kufuata mchango wake. Kuna mtu alifariki dunia jana katika mtaa wetu na maiti yake bado iko Hospitali ya Bombo.”


Mwanamke huyo akaendelea kutueleza.


“Sasa nilipofika nikakuta mlango umesindikwa, nikabisha hodi kwa muda mrefu, lakini sikupata jibu. Nilipousukuma mlango ndiyo nikaiona hiyo maiti.”


“Baada ya kuiona ulichukua hatua gani?”


“Nilkwenda kumuarifu mwenyekiti wangu kisha nikapiga simu polisi.”


Uchunguzi wa kwanza tuliofanya mimi na polisi mwenzangu ni kuchunguza mlango wa mbele ili kujua kama ulikuwa umevunjwa au ulifunguliwa kabla ya msichana huyo kuuawa. Tuligundua kuwa mlango haukuvunjwa bali msichana mwenyewe ndiye aliyeufungua.


Tukachunguza pia kama kulikuwa na kitu kilichoibwa. Pia tuligundua kuwa hakukuwa na kitu kilichoibwa. Kulikuwa na vitu vingi vya thamani vinavyobebeka kirahisi ambavyo vilikuwepo. Kama kungefanyika wizi wowote, vitu hivyo pia visingekuwepo.


Kwa kule kuviona vitu hivyo sebuleni na chumbani kwa msichana huyo tuligundua hakukuwa na kitu kilichoibwa.


Hapo tuligundua kuwa mtu aliyemuua aliingia humo ndani kwa ajili ya kufanya mauaji hayo kisha akaondoka.


Kwa kawaida polisi tunajaribu kukisia kila kitu tunapokuwa katika uchunguzi wetu. Tulihisi kwamba mtu huyo alifika usiku na kubisha mlango. Msichana alipomfungulia ndipo alimpiga na kitu kizito, akamuua na kuondoka.


“Lakini mimi naona si rahisi kwa mwanamke kumfungulia mlango mtu asiyemjua wakati wa usiku.” Polisi mmoja akatoa hoja yake.


“Wewe ndiye unasema kwamba mtu asiyemfahamu na mimi nakubaliana na hoja yako. Kwa vile tumeridhika kwamba ni msichana mwenyewe aliyemfungulia mlango, basi tuchukulie kwamba alikuwa mtu anayemfahamu. Pengine alimuuliza nani wewe, akajitambulisha ni nani.” Nikamwambia polisi huyo.


“Okey, inawezekana ni mtu anayemfamu.”


“Kama ni hivyo tutafute alimuua kwa kitu gani kisha tutafute mtu huyo anaweza kuwa ni nani.” Nikaendelea kutoa muongozo.


“Sawa afande,” polisi mmoja akanikubalia.


“Hapa kuna vipande vya chupa ya bia vyenye damu. Inaonesha kwamba msichana huyu aliuawa kwa kupigwa chupa hii,” nikasema.


Polisi wenzangu wote walikubaliana na hilo kwa vile kwenye utosi wa msichana huyo palikuwa na jeraha lililoonesha kupigwa na kitu kizito.


Nikaendelea kuwaeleza polisi wenzangu.


“Kuna chupa nyingine ya bia iko kwenye meza. Inaonesha kuwa huyu msichana alikuwa anakunywa bia na mwenzake.”


“Afande nimefikiria vingine,” polisi mmoja ambaye ananifuatia kwa cheo aliniambia.


“Umefikiria nini?” Nikamuuliza.


“Nimefikiria kwamba mtu aliyemuua huyu msichana anaweza kuwa ni mpenzi wake. Walikuwa wanakunywa halafu ukatokea ugomvi kati yao. Katika ugomvi huo, mtu huyo akampiga chupa msichana huyu kisha akafungua mlango na kukimbia.”


“Fikra yako pia tutaifanyia kazi. Ya kwanza ni ile ya mtu aliyekuwa anamfahamu aliyembishia mlango usiku na alipomfungulia mlango akampiga chupa na kumuua na fikra ya pili ni ya mtu aliyempiga chupa na kumuua alikuwa akinywa naye. Kwa vile tumegundua kuwa mlango umefunguliwa kwa ndani fikira hii ina mashiko.” Nikasema na kuongeza;


“Sasa kitu kingine cha kuchunguza katika tukio hili, ni kutaka kujua aliyemuua huyu msichana ni nani. Kutokana na uchunguzi wetu wa mwanzo tumeshagundua kuwa aliyemuua atakuwa ni mpenzi wake au mtu anayemfahamu au mtu aliyekuwa akinywa naye. Sawa au si sawa?”


“Ni sawa.”


Nikamtazama yule mjumbe ambaye alikuwa amesimama palepale akitusikiliza.


“Tusaidie kitu kimoja. Wewe unafahamu huyu msichana alikuwa akiishi na nani?”


“Alikuwa na mwanaume wake, lakini huyo mtu sijamuona kwa karibu wiki tatu. Inawezekana amesafiri au wameachana,” mjumbe akatueleza.


“Baada ya kutomuona huyo mtu kwa wiki tatu hukuwahi kumuona huyu msichana na mtu mwingine?”


“Siko karibu naye sana kiasi cha kujua maisha yake. Huyo mwanaume wa kwanza nilimgundua kwa sababu alikuwa akiishi naye humu ndani. Ninapofika kwa dharura yoyote ile ninamuona.”


“Wewe kama mjumbe utatusaidiaje. Una hisia juu ya mtu unayemfahamu anayehusika na tukio hili?”


Mjumbe huyo akatikisa kichwa.


“Kwa kweli sina hisia na mtu yeyote.”


Baada ya kujadiliana na polisi wenzangu, polsi mmoja alitoa hoja ambayo haikunipendeza. Alitaka tuwasiliane na kitengo cha polisi cha uchukuaji wa alama za vidole ili kutafuta alama za vidole za mhusika kwenye mlango.


Kitasa nilishakifuta usiku. Kwa hiyo kusingekuwa na alama zozote za vidole labda za mjumbe aliyeingia mle ndani wakati wa asubuhi na kuikuta maiti ile.


Tulikubaliana mtaalam wa kuchukua alama za vidole afike. Baada ya kumpigia simu haikupita hata nusu saa, akawasili kwa gari.


Alipata alama za vidole kwenye mlango upande wa nje na wa ndani wa mlango wa mbele. Alama hizo zinapochukuliwa huwezi kutambua ni za nani mpaka zikafanyiwe uchunguzi. Baada ya alama hizo kufahamika mtu atakayeshukiwa kuhusika na mauaji hayo naye anachukuliwa alama zake za vidole na kulinganisha na zile zilizochukuliwa kwenye kitasa. Kama zitakwenda sawa, muuaji atakuwa ni yeye. Lakini nilishafahamu kuwa katika kitasa hicho cha mlango hapakuwa na alama za muuaji.


Mtaalam wetu wa kuchukua alama za vidole hakutosheka na alama alizoipata kwenye mlango ambazo nilihisi zilikuwa za mjumbe au mtu mwingine aliyeingia humo ndani asubuhi, alichukua pia alama kwenye ile chupa iliyokuwa juu ya meza na kwenye vipande vya ile chupa iliyovunjika. Alituambia kuwa alama zitakazopatikana katika chupa hizo zitakuwa muhimu zaidi.


Ikumbukwe kwamba ile chupa iliyokuwa kwenye meza niliishika mimi wakati ule wa usiku wakati ninakunywa bia. Sasa nikaona balaa linaweza kuniangukia mimi itakapobainika kwamba alama zilizoko katika moja ya chupa hizo ni za kwangu.


Moyo wangu ukaanza kufadhaika hapohapo.



Itaendelea…
 
SEHEMU YA 05


ILIPOISHIA IJUMAA…


KUNA mtu mwingine aliyekuwa amepiga picha akiwa na msichana huyo katika pozi lililoonesha kuwa alikuwa mpenzi wake. Tukashuku kuwa huyo aliweza kuwa mpenzi wake aliyetueleza yule mjumbe ambaye alituambia kuwa alikuwa hamuoni kwa wiki tatu hivi. Tukahisi kwamba atakuwa amesafiri au wameachana.


Kwa vile polisi wenzangu walikuwa hawatambui kwamba Charles alikuwa ndugu yangu, waliamini kuwa muuaji anaweza kuwa mmoja wa watu hao. Picha zile mbili zilitolewa na kuchapwa kwenye karatasi kisha kupachikwa kwenye ubao wetu ambao hukaa kwenye matangazo yetu.


Picha hizo zilipachikwa zikiwa na maelezo kwamba watu hao wanatafutwa na polisi.


Inspekta Mwakuchasa ambaye alikuwa msaidizi wa mkuu wa kituo chetu ndiye aliyekabidhiwa faili la uchunguzi huo, mimi nikiwa mmoja wa wasaidizi wake.


SASA ENDELEA…


INSPEKTA Mwakuchasa aliniita ofisini kwake, akaniambia kwamba vile vipande vya chupa vyenye damu pamoja na ile michirizi ya damu iliyopatikana mbele ya mlango, vitapelekwa kwa mkemia mkuu ili kutambua ile damu ilikuwa ni ya nani.


Maneno yake yakanishtua kidogo.


“Afande unasema vile vipande vya chupa vitapelekwa kwa mkemia mkuu wa Serikali ili kutambua ile damu ni ya nani wakati tunajua ile damu ni ya marehemu!” Nikamwambia.


“Katika uchunguzi kila kielelezo kinatakiwa kuthibitishwa. Tusichukulie tu ni damu ya marehemu kwa sababu ipo kwenye vipande vya chupa tunavyodhani kuwa ndiyo alipigiwa marehemu.”


“Unahisi kwamba ile damu inaweza kuwa ya mtu mwingine?”


“Ninachotaka mimi ni kuwa na uthibitisho kwamba ni damu ya marehemu na uthibitisho unaotakiwa ni wa kitaalam si wa kukisia au maneno matupu.”


“Nimekuelewa afande. Kwa hiyo vitapelekwa lini kwa mkemia mkuu?”


“Nafikiri vitasafirishwa kesho kwenda Dar.”


“Kwa upande wa muuaji nina wasiwasi sana na wale watu wawili ambao picha zao tumezipachika kwenye ubao wa tangazo. Mmojawao anaweza kuwa muuaji. Kwa vile picha yake tunayo itakuwa rahisi kumkamata.”


“Usiseme kuwa itakuwa rahisi kumkamata kwa sababu picha yake tunayo. Inawezekana ameshakimbilia mji mwingine baada ya kuona ameua.”


“Afande umesahau kwamba tuna mtandao wetu wa kipolisi ambao uko nchi nzima. Picha za wahalifu zinaweza kuonekana katika vituo vyote vya polisi. Atakimbilia mji gani ambako hakuna kituo cha polisi? Labda akimbie nchi na si rahisi kufanya hivyo.”


“Mimi imani yangu ni kuwa yupo hapahapa jijini. Kwa vile alipoua hakuonekana, imani yake ni kuwa hatafahamika. Mtu anayekimbia ni yule anayehisi anatafutwa.”


“Ni kweli afande, anaweza akawa hapahapa jijini.”


“Kama ni kukamatwa, atakamatwa hapahapa.”


Pakapita kimya kifupi kabla ya inspekta huyo kuendelea kuniambia.


“Halafu kuna kitu kimoja muhimu ambacho ni lazima tukifanyie utafiti. Ilipaswa tufahamu huyu msichana anaitwa nani, anafanya kazi gani na kama alikuwa na ndugu zake wanaofahamika. Kingine ni kuchukua alama zake za vidole ili tuwe nazo.”


“Ni kweli afande. Kujua jina la marehemu na kujua alikuwa anafanya kazi gani ni muhimu.”


“Sasa chukua gari nenda Kwaminchi muone yule mjumbe akupe jina lake na akufamishe marehemu alikuwa anafanya kazi gani ili tuweke kwenye kumbukumbu zetu. Sawa?”


“Sawa afande, acha niende mara moja.”


Nikainuka na kutoka mle ofisini. Dakika chache baadaye nikawa barabarani nikiwa kwenye gari la polisi nikielekea Kwaminchi. Nilipofika katika ule mtaa, nilikwenda kwenye nyumba ya mwenyekiti wa mtaa huo.


Baada ya kufanikiwa kumuona, nilimueleza tatizo lililonipeleka kwake.


“Mimi sifahamu yule msichana anaitwa nani wala sifahamu alikuwa anafanya kazi wapi. Subiri nimpigie mjumbe wangu,” mwenyekiti akaniambia.


“Sawa, mpigie.”


Mwenyekiti huyo alimpigia simu mjumbe wake. Nikamsikia akimuuliza.


“Eti yule msichana aliyeuawa anaitwa nani?”


Mwenyekiti alisikiliza kisha akaniambia.


“Anaitwa Matilida, kabila lake ni Mmakonde.”


“Anaitwa Matilida nani?” Nikamuuliza.


Mwenyekiti akauliza tena kwenye simu.


“Anaitwa Matilida nani?”


Mwenyekiti baada ya kuambiwa aliniambia.


“Anasema hafahamu jina la baba yake.”


“Muulize alikuwa anafanya kazi wapi?”


Mwenyekiti akauliza kisha akanijibu.


“Alikuwa akifanya kazi baa.”


“Una maana alikuwa baamedi?”


“Ndivyo alivyoniambia mjumbe wangu.”


“Sasa atufahamishe ni baa gani alikokuwa akifanya kazi?”


Mwenyekiti akamuuliza mjumbe huyo kisha akanijibu.


“Baa ya Nane-Nane iliyopo Gofu.”


Ilikuwa baa maarufu. Alipoitaja tu nikaifahamu.


“Hebu muulize anawafahamu ndugu zake?”


“Eti unawafahamu ndugu zake?” Mwenyekiti akauliza kwenye simu. Akasikiliza kidogo kabla ya kunitazama.


“Anasema hawafahamu ndugu zake,” aliniambia.


“Basi inatosha. Nitakwenda kazini kwake. Ninaweza kupata mengi zaidi.”


Nikamshukuru mwenyekiti huyo na kurudi kwenye gari. Nilipoliwasha nililiendesha hadi eneo la Gofu. Dakika chache baadaye nikawa ndani ya Baa ya Nane-Nane. Kwa vile nilikuwa nimevaa sare za polisi niliwashtua wengi nilipoingia humo. Nilikwenda kaunta nikamsalimia msichana aliyekuwa akihudumia.


Msichana alipokea salamu yangu kwa wasiwasi.


“Nataka nikuulize kidogo.”


“Uliza,” akaniambia.


“Unamfahamu Matilida?”


“Matilida hajafika kazini tangu jana.”


“Yuko wapi?”


“Alituambia alikuwa hajisikii vizuri.”


Nikanyamaza kidogo na kuyapeleka macho yangu upande mwingine.


“Amefanya nini?” Msichana akaniuliza.


“Labda hamna taarifa. Huyu msichana ameuawa jana usiku.”


Nilipomwambia hivyo msichana alishtuka na kunikazia macho.


“Matilida ameuawa?”


“Ameuawa jana usiku nyumbani kwake. Maiti yake ilikutwa na majirani zake leo asubuhi na kuiarifu polisi.”


Msichana akatikisa kichwa kusikitika.


“Ameuawa na nani?”


“Haijafahamika, ndiyo tuko kwenye uchunguzi. Tulikuwa tunawatafuta ndugu zake.”


“Ndugu zake wako Dar, wengine wako Mtwara.”


“Ni nani anayewafahamu?”


“Hapa hakuna yeyote anayewafahamu ndugu zake. Alikuwa akituambia tu kwamba ndugu zake wako Dar na wengine wako kwao Mtwara.”


“Yeye ni mtu wa Kusini, siyo?”


“Ndiyo, ni mtu wa Kusini.”


“Alikuwa na bwana?”


“Alikuwa naye, lakini waliachana muda mrefu.”


“Anaitwa nani?”


“Bwana’ke anaitwa Msami halafu umefanana naye sana. Ulipotokea nilidhani ni yeye.”


“Binadamu wanaweza kufanana. Baada ya kuachana na mwanaume huyo hakuwa na mwanaume mwingine aliyewahi kuwa naye?”


“Labda wapitanjia tu.”


“Kuna mmojawapo unayemfahamu?”


Msichana alinyamaza kimya. Nikamuuliza tena.


“Kuna yeyote unayemfahamu?”


“Kuna kijana mmoja anaitwa Mdachi, ndiye aliyekuwa akionekana naye mara kwa mara.”


“Jana au juzi alionekana naye?”


“Anakuja kunywa hapa kila siku.”


“Jana alikuja?”


“Alikuja, lakini Matilida hakuwepo. Akatuuliza, sisi tukamwambia Matilida anaumwa. Sasa hatujui kama alimfuata nyumbani kwake.”


Kwa vile picha ya mtu tuliyekuwa tunamtuhumu ukiacha ile ya Charles niliingiza kwenye simu yangu, nilifungua simu na kumuonesha ile picha.


“Ni huyu hapa?” Nikamuuliza.


“Ndiye yeye Mdachi!”


Nikaona sasa kazi imekuwa nyepesi.


“Tuseme alipoondoka hapa alikwenda nyumbani kwake akagombana naye na kumuua?”


Je, nini kiliendelea? Usikose Ijumaa kwenye Gazeti la Ijumaa.
 
SEHEMU TYA 06


“Alikuja, lakini Matilida hakuwepo. Akatuuliza sisi tukamwambia Matilida anaumwa. Sasa hatuji kama alimfuata nyumbani kwake.”


Kwa vile picha ya mtu tuliyekuwa tunamtuhumu ukiacha ile ya Charles niliingiza kwenye simu yangu, nilifungua simu na kumuonesha ile picha.


“Ni huyu hapa?” Nikamuuliza.


“Ndiye yeye Mdachi!”


Nikaona sasa kazi imekuwa nyepesi.


“Tuseme alipoondoka hapa alikwenda nyumbani kwake akagombana naye na kumuua?”


SASA ENDELEA…


NILIKUWA nikisema peke yangu, lakini yule mhudumu alinisikia. Akabetua mabega na kunijibu.


“Hatujui, hatukuwepo.”


“Inawezekana kuwa ni hivyo. Uchunguzi wetu umeonesha mauaji yake yametokana na wivu wa kimapenzi. Sasa kama alimfuma na mwanaume mwingine, tutajua hapo baadaye, lakini muhimu kwa sasa ni kumtafuta huyo Mdachi, atakuwa mtuhumiwa wetu namba moja. Wewe ndiye utakayetusaidia kumpata.”


“Mimi sifahamu anapoishi.”


“Tafadhali jaribu kutupa ushirikiano. Itakuwaje usifahamu anaishi wapi wakati ni mwanaume wa rafiki yako?”


“Mimi nimemfahamu kwa kumuona hapahapa baa, hata Matilida alijuana naye hapahapa baa.”


“Hebu nieleze tabia yake ikoje?”


“Ni mtu mwenye wivu mwingi na pia ana hasira za harakaharaka.”


“Unaamini kwamba anaweza kuwa muuaji?”


“Hapo ndiyo sina uhakika napo.”


“Lakini ulishawahi kuwaona wakigombana?”


“Walishawahi kugombana.”


“Hapahapa baa?”


“Ndiyo, hapahapa baa.”


“Sasa unadhani tutampata wapi huyu Mdachi?”


“Anakuja kunywa hapa kila siku. Muda wake ni saa mbili au tatu usiku. Anakaa hapa hadi saa sita tunapofunga baa anaondoka na Matilida.”


“Sasa sikiliza, nitakupa namba yangu. Ukimuona tu amefika hapa nipigie simu unifahamishe, lakini usimueleze chochote. Jifanye kama hujui kama Matilida ameuawa.”


“Sawa.”


Nikampa msichana huyo namba yangu ya simu, akaiandika kwenye simu yake.


“Sasa ufanye hivyo. Ukimuona tu nipigie bila kumshtua. Tutafika mara moja kumkamata. Sawa?”


“Sawa.”


Nikamuaga msichana huyo na kuondoka. Maelezo ya msichana huyo yalinipa matumaini makubwa. Niliendesha gari nikiwa nimejaa faraja ya kufanikiwa kwa uchunguzi wangu katika dakika za mapema.


Uwezekano wa Mdachi kumuua yule msichana ndiyo uliokuwa katika akili yangu.


Wakati nipo kwenye Barabara ya Chumbageni huku mawazo yangu yakiwa kwa Mdachi, niliipita pikipiki moja. Aliyepanda pikipiki hiyo alikuwa mtu aliyefanana sana na huyo mtu niliyeambiwa anaitwa Mdachi. Niligundua hivyo kutokana na kuitazama mara kwa mara picha yake iliyokuwa kwenye simu yangu.


Ilibidi nisimamishe gari pembeni mwa barabara ili niweze kumuona vizuri. Pikipiki ikanipita tena, lakini sura ya mtu huyo aliyekuwa akiiendsha ilikuwa ni ileile ya Mdachi. Mawazo yangu yakaona yule alikuwa Mdachi. Nikimuacha huenda hatutampata tena na nitajuta kwa nini nilipomuona sikumkamata.


Nikaanza kumfukuza. Sikuweza kufahamu ni kitu gani kilichomshtua, mtu huyo, naye akaongeza mwendo kama aliyekuwa akinikimbia mimi.


Tukaanza kufukuzana kwenye Barabara ya Chumbageni, tukaingia Barabara ya Kisosora. Pikipiki mbele, gari la polisi nyuma.


Tulivuka daraja la Mtofu, sasa tukawa tunaelekea eneo la Amboni. Nikaona mtu huyo atanifikisha mbali, nikambana njia huku nikimuonesha ishara ya kumsimamisha. Kwa vile ilikuwa pikipiki iliweza kuchomoka kwa pembeni mwa barabara ikaendelea na safari. Kama ningembana zaidi, kutokana na kasi yake kingekuwa ni kifo.


Huko mbele kulikuwa na gari linakuja na ndilo lililomchanganya. Alikwenda kujiingiza mwenyewe mbele ya gari hilo, akarushwa juu kisha akatua kwenye boneti ya gari hilo.


Nusura ilikuja kwa sababu gari hilo lilikuwa tayari limesimama. Mtu huyo akasalimika.


Nilisimamisha gari pembeni mwa barabara kisha nikashuka haraka kwenye gari. Nilimfuata mtu huyo na kumuuliza.


“Ulikuwa unakimbia nini?”


Mtu huyo alikuwa akihema tu, hakunijibu chochote.


“Shuka kwenye boneti ya gari,” nikamwambia.


Alishuka kutoka kwenye boneti, akasimama mbele yangu. Nilimtazama vizuri.


Kusema kweli sasa niligundua tofauti kati ya Mdachi niliyemuona kwenye picha na huyu.


Nikataka kumuuliza jina lake, lakini niliona angeweza kunidanganya. Nikamwambia.


“Nipe leseni yako.”


Akatia mkono kwenye mfuko wa suruali yake akatoa pochi yake ambayo aliifungua na kunitolea leseni yake.


Nilisoma jina lake kwenye leseni. Leseni iliandikwa jina la Ibrahim Shukuru.


“Wewe unaitwa Ibrahim Shukuru?” Nikamuuliza.


“Ndiyo.”


“Unamfahamu mtu anayeitwa Mdachi?” Nikamuuliza.


Akatikisa kichwa.


“Simfahamu.”


“Huna undugu naye?”


“Sina undugu naye,” akanijibu.


“Sasa niambie ulikuwa unakimbia nini hadi ukasababisha ajali?”


“Sikuwa nikikukimbia wewe. Nilikuwa na haraka zangu mwenyewe.”


“Haiwezekani. Nilihisi wazi kuwa ulikuwa unanikimbia mimi. Umebeba nini kwenye pikipiki yako?”


“Ni mbogamboga tu.”


Pikipiki ilikuwa imelala miguuni kwangu. Nikainama na kukifungua kifurushi kilichofungwa nyuma ya siti.


Baada ya kikufungua nikakuta mirungi iliyokuwa imefungwa kwenye majani ya mgomba.


Kwa vile niligundua hakuwa Mdachi nikaona kilichomkimbiza baada ya kuona gari la polisi, ilikuwa ni ile mirungi aliyokuwa amebeba.


Niliinusa kisha nikamuuliza.


“Nini hii?”


“Mirungi,” akaniambia.


“Ndiyo iliyokufanya unikimbie?”


Akanyamaza kimya.


Nikaona gari la polisi lililokuwa likitokea upande wa Amboni likisimama hapohapo.


Sajenti mmoja alishuka na kuniuliza.


“Vipi afande?”


“Huyu jamaa alikuwa ananikimbia akaja kugongana na gari. Kumbe alikuwa ananikimbia kwa sababu ya hii mirungi.”


“Alikuwa na hii pikipiki?”


“Ndiyo alikuwa akikimbia kwa kutumia pikipiki hii.”


“Hao ndiyo zao. Tunaweka doria, lakini siku hizi wanatumia pikipiki ili waweze kupita njia za panya kutukwepa.”


“Sasa mtashughulika naye. Mirungi yake hii hapa.”


Nilimpa ile mirungi nikarudi kwenye gari na kuondoka. Wakati mwingine matukio ya aina hii hutokea katika kazi zetu. Kumkamata mtu au kumfukuza mtu na hatimaye kugundua siye aliyekuwa anatafutwa.


Watu wengine huwakimbia polisi wakiwa na sababu nyingine na wengine wakiwa hawana sababu yeyote. Wanakuwa na uoga tu wa kipumbavu.


Nikarudi kituoni kwangu.


Niliingia ofisini kwa bosi wangu Inspekta Mwakuchasa na kumuelea kuhusu upelelezi nilioufanya ulioniwezesha kugundua kuwa yule mtu tunayemtafuta anaitwa Mdachi.


Mbali na kumueleza kuhusu mtu yule niliyemfukuza na kugundua kuwa hakuwa Mdachi, nilimueleza maelezo niliyoyapata ambayo yalionesha kuwa Mdachi ndiye aliyemuua Matilida.


“Umefanya kazi nzuri sana. Hata kama huyo mtu hatujampata, lakini ile kugundua kuwa anafahamika na watu, ni matokeo mazuri. Ninaamini kuwa tutamkamata,” Mwakuchasa akaniambia na kuongeza;


“Unajua nini kimetokea. Mimi nahisi kwamba huyo Mdachi alipokwenda hapo baa jana usiku na kumkosa mpenzi wake huyo alimfuata nyumbani kwake na akamkuta anakunywa pombe na mtu mwingine. Kwa kuwa ni mtu mwenye hasira za harakaharaka kama ulivyosema waligombana na matokeo yake aliamua kumpiga chupa ya kichwa na kumuua kisha akakimbia.”


“Hivyo ndivyo ninavyofikiri mimi, lakini yule msichana nimemuachia namba yangu ya simu, akitokea tu pale baa atanipigia na kunifahamisha.”


“Umefanya kitu kizuri kumpa namba yako.”


Wakati ninazungumza na Inspekta Mwakuchasa, akaingia Sajin Meja mwenzangu, Sajin Meja Mwinchumu ambaye alikuwa mtaalam wa alama za vidole.



Itaendelea…
 
SEHEMU YA 07



“Umefanya kazi nzuri sana. Hata kama huyo mtu hatujampata, lakini ile kugundua kuwa anafahamika na watu, ni matokeo mazuri. Ninaamini kuwa tutamkamata,” Mwakuchasa akaniambia na kuongeza;


“Unajua nini kimetokea? Mimi nahisi huyo Mdachi alipokwenda hapo baa jana usiku na kumkosa mpenzi wake huyo alimfuata nyumbani kwake na akamkuta anakunywa pombe na mtu mwingine. Kwa kuwa ni mtu mwenye hasira za harakaharaka kama ulivyosema waligombana na matokeo yake aliamua kumpiga chupa ya kichwa na kumuua kisha akakimbia.”


“Hivyo ndivyo ninavyofikiri mimi, lakini yule msichana nimemuachia namba yangu ya simu, akitokea tu pale baa atanipigia na kunifahamisha.”


“Umefanya kitu kizuri kumpa namba yako.”


Wakati nazungumza na Inspekta Mwakuchasa akaingia Sajin Meja mwenzangu, Sajin Meja Mwinchumu ambaye alikuwa mtaalam wa alama za vidole.


SASA ENDELEA…


AFANDE kuna jambo limetushtua na kutushangaza,” akamwambia Inspekta Mwakuchasa.


“Jambo gani?”


“Katika chupa ya bia ambayo haikuvunjwa tulikuta alama za vidole vya Afande Denis Wiliam Makita!”


Kama unalikumbuka jina langu, Denis Wiliam Makita nilikuwa ni mimi. Chupa ile niliishika usiku halafu nikasahau kufuta alama zangu za vidole.


Nikajiambia mbio za sakafuni huishia ukingoni. Na ukingoni kwangu ndiyo hapa!


Pengine utashangaa na kujiuliza jinsi mtaalam huyo wa alama za vidole alivyozijua alama zangu wakati hakuniita kuchukua alama zangu na kuzilinganisha na hizo aliozikuta kwenye chupa.


Unapoajiriwa katika jeshi la polisi alama zako za vidole zinachukuliwa na kuwekwa katika maktaba yetu ya alama za vidole. Siku hizi kuna mitandao ya komputa ambapo alama zote huwekwa humo kuanzia alama za wahalifu wanaokamatwa, watumishi muhimu katika Serikali na wengineo. Ukiweka tu alama za vidole, jibu linakuja ni alama ya nani.


Hivyo ndivyo alama zangu zilivyotambulika. Kama alama zangu za vidole zisingekuwepo katika maktaba yetu, pengine ingemuia vigumu mtaalam huyo kujua kuwa alama hizo zilikuwa ni zangu.


Sasa nikajiuliza nitatumia uongo gani nijiokoe. Kama unavyojua binadamu hakubali kufa kirahisi. Lakini kabla sijawaza chochote nilimuona Inspekta Mwakuchasa akinitazama kwa taharuki.


“Imekuwaje? Mbona ni alama zako wewe zilizokutwa kwenye ile chupa?” Akaniuliza akiwa amenikazia macho.


“Wakati ule wa uchunguzi nafikiri niliishika ile chupa,” nikamjibu ingawa nilitambua jibu hilo lisingetosheleza.


Mwakuchasa akatikisa kichwa kusikitika.


“Unasemaje? Uliishika ile chupa kabla ya kupigwa picha?”


“Wakati ule hata hayo mawazo ya kuchukua alama za vidole hatukuwa nayo.”


Mwakuchasa aliendelea kutikisa kichwa.


“Lakini si unatambua kanuni zetu kwamba vielelezo kama vile ni lazima vipigwe picha za kutambua alama za vidole?”


“Unajua afande ile chupa ilikuwa mbali na mahali alipouawa marehemu. Sikufikiria kama ingehusika.”


“Sasa unatuchanganya. Maelezo yako hayaridhishi. Ni lazima ujieleze kwa maandishi ni kwa nini alama zako za vidole zimekutwa katika chupa ile. Vinginevyo unaweza kuwa mtuhumiwa namba moja.”


“Nitajieleza kwa maandishi afande. Ilikuwa kama bahati mbaya tu.”


“Bahati mbaya si sababu ya kueleza. Tueleze kitu cha msingi kitakachotufanya tusikutuhumu wewe.”


“Sawa. Nitaandika maelezo yangu.”


“Sawa. Sasa uwende hospitalini Sajin Meja mwenzako mkachukue alama za vidole za marehemu.”


“Sawa afande.”


Nikainuka kwenye kiti na kumpigia saluti mkuu wangu. Sajin Meja Mwinchumu naye akapiga saluti yake kisha tukatoka.


Wakati tuko kwenye gari tukielekea Hospitali ya Bombo nilijikuta nikimwambia Mwinchumu.


“Unajua nilifanya kitendo cha kizembe sana kuishika ile chupa kabla ya kupigwa picha.”


“Ni kweli, unajua tulishangaa sana tulipogundua ilikuwa na alama zako. Sikufikiria kabisa kwamba uliishika kwa uzembe wala kwa bahati mbaya.”


“Kwanza mimi sikuona kama chupa ile ilikuwa na umuhimu wa kupigwa picha. Umuhimu ulikuja baadaye tulipogundua kuwa marehemu alikuwa anakunywa bia na mpenzi wake.”


“Sasa ajabu ni kwamba tulikuta alama zako peke yake. Hakukuwa na alama zingine. Kama ingeshikwa na watu wawili alama zenu nyote zingeonekana.”


“Labda wakati wa kuishika nilizifuta.”


“Labda, lakini si kawaida.”


Nikanyamaza kimya na kuhisi kuwa mawazo ya wenzangu yalikuwa yameshaanza kubadilika.


Tulipofika hospitalini tuliingia mochwari ulikowekwa mwili wa yule msichana. Sajin Meja Mwinchumu akachukua alama zake za vidole kisha tukaondoka.


“Unajua Denis kutokana na kukua kwa teknolojia, unatakiwa uwe mwangalifu sana. Mara moja unaweza kujisababishia matatizo usiyoyatarajia.”


“Ni kweli,” nikamwambia.


“Mimi bado niko kwenye tukio la alama zako za vidole kukutwa kwenye ile chupa.”


“Nilishakuelewa. Ninajua nilifanya kosa.”


“Unaona afande hakuelewi. Anakwambia lazima uandike maelezo kwa nini alama zako za vidole zikutwe kwenye ile chupa.”


“Anajaribu tu kunifanyia nongwa, lakini bahati mbaya pia ipo ingawa yeye anaikataa.”


“Unajua ni kwa nini anakataa? Ni kwa sababu ya cheo chako. Kufanya kitu halafu unasema umekifanya kwa bahati mbaya, hawezi kukuelewa. Angalau angekuwa polisi mdogo asiye na uzoevu….”


“Kwa vyovyote vile ninafahamu kuwa nitashutumiwa. Na mimi kwa vile nimefanya kosa lazima nikubali shutuma.”


“Si kwangu mimi. Mimi sina tatizo.”


Mwinchumu aliponiambia hivyo tukanyamaza kimya, lakini nilifahamu kitendo changu hakikuwafurahisha wenzangu.


Jioni nilipotoka kazini nilimueleza mke wangu mkasa uliotokea na jinsi alama zangu zilivyokutwa kwenye chupa ambayo tuliichukua katika tukio kwa ajili ya uchunguzi.


“Kwani wewe ulikuwa hujui kwamba huruhusiwi kugusa kitu ambacho kinatakiwa kuchukuliwa alama za vidole?” Mke wangu akaniuliza.


“Ilitokea kama bahati mbaya tu.”


“Ukisema bahati mbaya wenzako watakufikiria vingine.”


“Vingine vipi?”


“Hicho ni kitendo cha kizembe.”


“Mama yangu! Mke wangu pia unaniambia hivyo?”


“Usinielewe vibaya, lakini hivyo ndivyo walivyochukulia ingawa hawakukwambia wazi, lakini mimi ninakuambia.”


Nikanyamaza kimya. Na mke wangu naye akanyamaza. Pengine alikuwa anajiuliza kama alikuwa sahihi kuniita mzembe.


Kwa vile marehemu nilikuwa naye mimi sikuona sababu ya kukasirika. Nikatuliza moyo wangu.


“Hivi sasa tunamtafuta huyo Mdachi. Tukimpata tutakuwa tumefanikiwa kumpata muuaji.”


“Mpaka iwe ni yeye kweli. Alama za vidole ziwe za mtu mwingine halafu muuaji awe mtu mwingine?”


Swali la mke wangu lilikuwa la msingi sana.


“Mazingira yanaonesha ni yeye.”


“Kwa ushahidi gani mlioupata?”


“Yule mhudumu wa baa anakofanya kazi marehemu aliniambia marehemu hakufika kazini usiku wa jana. Huyo Mdachi alipofika alimuulizia, akaambiwa Matilida hakufika kazini. Alipomalia kunywa alimfuata nyumbani. Iliwezekana alimkuta na mwanaume ndipo alipompiga chupa na kumuua.”


“Hayo sasa unayapanga wewe. Nani alikwambia huyo Mdachi alimfuata huyo msichana nyumbani kwake? Nani alikwambia kama alimkuta na mwanaume? Na nani kakwambia kwamba yeye ndiye aliyempiga chupa na kumuua?”


Mke wangu alizidi kunikoroga.


“Uchunguzi wetu ndiyo umeonesha hivyo,” nikamwambia.


“Una maana kwamba unahusisha mambo yasiyo na ushahidi.”


“Ushahidi utapatikana. Tunamtafuta muuaji huku tukiwa kwenye uchunguzi.”


“Sasa kwa nini afande Mwakuchasa anataka ujieleze kwa maandishi? Ina maana hakuamini au….?”


“Yeye ni mkubwa. Kwa hiyo anataka kuonesha ukubwa wake. Kama hili suala angeliacha isingekuwa chochote.”


“Kwani kuna tatizo gani. Si unaandika tu maelezo yawekwe kwenye faili basi.”


“Nitaandika maelezo. Hilo halina tatizo.”


Ilipofika saa tatu usiku msichana mhudumu wa Baa ya Nane Nane alinipigia simu. Nilikuwa nimekaa sebuleni na mke wangu tukinywa bia mojamoja. Nikapokea simu yake.


“Hello, naongea na Afande Denis?”


“Ndiyo. Bila shaka wewe ni mhudumu wa Baa ya Nane Nane?”


“Ndiyo. Yule mtu wako ameshafika.”


Nikagutuka.


“Amefika, yuko hapo?”


“Amefika na ameagiza bia.”


“Hajakuuliza wala kukwambia chochote?”


“Amefikia kwenye meza, hajafika hapa kaunta.”


“Sawa. Usimwambie chochote. Sisi tunakuja.”


Nikakata simu na kusimama.


“Yule mtu tunayemtafuta ameshafika pale baa. Acha twende tukamkamate.” Nikamwambia mke wangu.



Je, nini kiliendelea? Usikose Ijumaa kwenye Gazeti la Ijumaa.





FAKI A. FAKI


SIMU: 0655340 572
 
SEHEMU YA 08


NIKAKATA simu na kusimama.


“Yule mtu tunayemtafuta ameshafika pale baa. Acha twende tukamkamate,” nikamwambia mke wangu.


SASA ENDELEA…


MKE wangu hakushangaa. Alikuwa akizijua kazi zetu za kijeshi kwa vile yeye mwenyewe alikuwa polisi. Polisi unaweza kuamshwa saa nane usiku, ukaambiwa unatakiwa kituoni. Hapo unamuacha mkeo au mumeo bila kujali mlikuwa mnafanya nini na kuitikia wito.


Kwa vile sikuwa katika zamu ya kazi, nilikwenda vilevile na nguo zangu za kiraia. Koti jeusi la mtumba, shati jekundu na suruali ya kijivu.


Nilipofika kituoni nilimfahamisha aliyekuwa akisimamia kituo usiku ule kwamba nimepigiwa simu na msichana mhudumu wa Baa ya Nane Nane kwamba Mdachi ambaye alikuwa mtuhumiwa tunayemtafuta, ameshafika hapo baa. Nilipewa gari na polisi wanne nifuatane nao wakiwa na bunduki mikononi.


Tulipofika nilishuka peke yangu nikaingia baa. Nilikwenda moja kwa moja kaunta ambapo nilimkuta yule msichana aliyenipigia simu.


“Yuko wapi?” Nikamuuliza kwa pupa.


“Mmechelewa, ameshaondoka.”


Nikamkunjia uso na kumuuliza.


“Unasemaje?”


“Ameondoka sasa hivi hata bia yake hakuimaliza.”


“Mmemshtua?”


“Kuna msichana alimwambia kuwa Matilida ameuawa jana usiku akataharuki.”


“Nilisema msimueleze kitu.”


“Ulinieleza mimi, lakini hapa tuko wengi. Kuna msichana alimwambia. Nafikiri alikuwa hajui kama Matilida amekufa, asingetaharuki vile.”


“Sasa amekwenda wapi?”


“Inaelekea hakuamini kama Matilida amekufa, ameondoka kwenda nyumbani kwake kuhakikisha kama amekufa kweli!”


“Naona kama alikuwa anazuga tu, yeye ndiye tunayemtuhumu halafu anajifanya kuwa hajui, hajui nini?”


Msichana huyo alinyamaza kimya.


“Aliondoka sasa hivi?” Nikamuuliza.


“Ni sasa hivi tu. Huko nyumbani kwa marehemu pia atakuwa hajafika.”


“Ana usafiri gani?”


“Wakati mwingine anakuja kwa pikipiki, wakati mwingine anatumia miguu, sijui leo alikuja kwa usafiri gani.”


Nikatoka bila kumuaga msichana huyo. Nilipotoka nje niliwaambia wenzangu.


“Huyu jamaa ameshaondoka, nimeambiwa amekwenda nyumbani kwa marehemu, tumfuate hukohuko.”


Nilifungua mlango wa gari nikajipakia. Gari la polisi likaondoka.


“Ni wapi?” Polisi aliyekuwa akiendesha gari hilo akaniuliza.


“Twende Kwaminchi.”


Hapo Gofu na Kwaminchi ni kama pua na mdomo. Palikuwa karibu sana. Dereva alikata kushoto. Baada ya mwendo mfupi tu tuliingia eneo la Kwaminchi. Nilimuelekeza mtaa aliokuwa akiishi marehemu. Tulipofika katika nyumba ya marehemu tuliona msichana aliyekuwa amesimama barazani.


Tulisimamisha gari nikashuka na kumsalimia msichana huyo.


“Hujambo?”


“Sijambo. Shikamoo.”


Katika mazingira ya kawaida hakupaswa kuniamkia kwa vile kama tulipishana ilikuwa ni kidogo tu. Lakini nilifahamu aliniamkia kutokana na uoga wa kuona polisi.


“Marahaba. Wewe nani, mbona uko hapa?” Nikamuuliza.


“Mimi ni rafiki yake Matilida. Nilikuja kumsalimia, lakini naona nyumba imefungwa.”


“Unaishi wapi?”


“Naishi Chumbageni.”


“Hujakutana na Matilida tangu lini?”


“Tangu juzi.”


Nilinyamaza kimya nikawaza kidogo kisha nikamwambia.


“Matilida ameuawa usiku wa jana. Kwa hiyo hutaweza kuonana naye tena.”


“Kuna mtu alikuja hapa nyumbani sasa hivi, akaniambia amekwenda kazini kwake Matilida na kuambiwa Matilida ameuawa, lakini hakuamini, akaja hapa nyumbani kwake kuthibitisha. Mimi nikamwambia sijui.”


“Huyo mtu yuko wapi?”


“Baada ya kuona nyumba imefungwa ameondoka.”


“Ni muda gani aliokuja?”


“Ni sasa hivi tu. Hata mimi nilikuwa naondoka.”


Nikahisi huyo mtu alikuwa ni Mdachi.


“Alikuwa na usafiri gani?”


“Alikuwa akiendesha pikipiki.”


“Alipoondoka alielekea wapi?”


“Alielekea huo upande mliotokea ninyi.”


Nikamuacha yule msichana na kurudi kwenye gari.


“Huyu jamaa amefika hapa na ameshaondoka. Huenda amerudi tena kule kule baa. Turudi tena,” nikawaambia polisi wenzangu.


Tukageuza gari na kurudi tena kwenye ile baa. Kama kawaida nilishuka peke yangu. Nikaingia ndani. Nilimfuata yule mhudumu wa kaunta nikamuuliza.


“Yule mtu alirudi tena hapa baa?”


Msichana akatikisa kichwa.


“Hajarudi tena. Kwani hamkukutana naye?”


“Hatukukutana naye. Tuliambiwa alifika na kuondoka, tukadhani amerudi huku.”


“Huku hajafika bado.”


Baada ya kuzugazuga hapo baa, nikatoka na kujipakia kwenye gari.


“Naona bora turudi, safari yetu haikuwa na mafanikio.”


Tulipofika kituoni nilimfahamisha msimamizi wa kituo kwamba hatukufanikiwa kumpata Mdachi. Polisi wenzangu waliendelea na kazi, mimi nikarudi nyumbani kwangu.


Mke wangu alikuwa ameshalala. Nilibisha mlango, akaja kunifungulia. Niliingia ndani tukasimama sebuleni kidogo.


“Vipi mmemkamata?” Akaniuliza.


“Hatukumpata.”


“Kwa nini?”


“Kuna mtu alimwambia kuwa Matilida ameuawa, akaondoka pale baa na kwenda nyumbani kwake. Sisi tulipofika tukaambiwa ameondoka. Tulipofika nyumbani kwa marehemu tukaambiwa alifika na kuondoka.”


“Inaonesha wazi huyo jamaa siye aliyeua.”


“Kwa nini?”


“Kama ni yeye kwa nini alipoambiwa Matilida ameuawa aliondoka na kumfuata nyumbani kwake!”


“Binadamu wajanja. Inawezekana alikuwa anawazuga wale wasichana ili asifahamike kuwa amemuua yeye.”


“Haya, mbivu na mbichi zitafahamika mtakapompata.”


Mke wangu akaingia chumbani.


Kusema kweli usiku huo sikupata usingizi kwa mawazo. Wakati mwingine mtu anakupa ushauri unaukataa halafu baadaye unagundua alikupa ushauri wa maana.


Mke wangu aliniambia nisiende katika ile sherehe ya harusi kule Mkonge Hoteli, nikakataa. Baada ya kwenda nilichokutana nacho kinanifanya nijute kutosikiliza ushauri wake.


Kama ningemtii na kutokwenda, nisingekutana na mkasa ule. Na moyo wangu ungekuwa umetulia. Sasa nimefikwa na kizungumkuti kiasi kwamba sielewi muuaji halisi alikuwa nani. Mwanzo niliamni asilimia kwa mia kwamba muuaji alikuwa Mdachi kutokana na vigezo mbalimbali.


Lakini sasa zile asilimia za kumtuhumu Mdachi kuwa muuaji zimekuwa zikipungua kidogodogo. Kile kitendo cha Mdachi kuambiwa kuwa Matilida ameuawa na yeye akataharuki na kuamua kumfuata nyumbani kwake, kinaonesha alikuwa hajui kuwa Matilida ameuawa. Na kama alikuwa hajui kama Matilida ameuawa, maana yake ni kwamba si yeye aliyemuua.


Katika kuwazawaza kwangu, nikamkumbuka mtu mmoja muhimu sana.


Unajua nilimkumbuka nani?


Nilimkumbuka Azzali Mubarak, mfanyabiashara ya magendo ya meno ya tembo ambaye aliwahi kushitakiwa na kuachiwa na mahakama kwa kukosekana kwa ushahidi wa kutosha.


Nilimkumbuka kutokana na maneno aliyoniambia alipoachiwa na mahakama.


Alinikuta nimesimama nje ya mahakama, akaniambia.


“Ulinikamata kwa kunionea tu.”


“Unasemaje?” Nikamuuliza nikiwa nimemkunjia uso.


“Nimekwambia ulinikamata kwa kunionea tu.”


“Kumbe ulitaka tukuachie hata kama unashukiwa?”


“Kuwa na roho mbaya haitakusaidia.”


“Kama mahakama imekuachia, shukuru Mungu. Usinilaumu mimi. Mimi niko kazini.”


“Sawa. Tutaonana.”


Nikashtuka. “Tutaonana kwa heri au kwa shari?” Nikamuuliza.


Azzal Mabruki hakujibu kitu, akaelekea kwenye gari lake la kifahari lililokuwa likimsubiri hapo mahakamani. Akajipakia na kuondoka. Wakati gari linaondoka alinipungia mkono wa kuniaga. Nikampuuza.


Sasa nilianza kupata wasiwasi kutokana na yale maneno aliyoniambia. Nikajiambia isije kuwa ni yeye aliyesuka mpango huu wa kuuawa kwa Matilida ili anitie mimi katika balaa!


Je, nini kiliendelea?
 
SEHEMU YA 09


“NIMEKUWA na shaka naye sana. Katika pitapita zangu nilipata habari kwamba huyu Mabruki alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Matilida. Nilisikia siku aliyouawa Matilida, Mabruki alikuwa ameegesha gari lake nyumbani kwa akina Salma, huyu msichana niliyekuja kumuonesha picha.”


Nikaendelea kumwambia.


“Sasa wasiwasi wangu isijekuwa kulikuwa na mambo ya kufumaniana kati ya Mdachi na Mabruki na kusababisha Mabruki amuue yule msichana….”


ILIPOISHIA IJUMAA…


Sikukumbuka kwamba usiku ule niliporudi na Matilida niliona gari hilo kwenye ile nyumba.


Lakini kama lilikuwepo, basi ni Azzali Mabruki aliyemuua Matilida. Alituona wakati tunashuka kwenye teksi na akatambua kuwa nilikuwa ni mimi. Baadaye akaja kubisha mlango. Matilida alipomfungulia, akampiga chupa ya kichwa na kuondoka.


Hili suala nisingeweza kulichunguza peke yangu. Ilinipasa nitengeze hoja ya kulifikisha kituoni ili Mabruki akamatwe.


SASA ENDELEA…


BADALA ya kurudi kituoni nilikwenda Gofu kwenye Baa ya Nane Nane, nikamuona yule msichana ninayemkuta kaunta.


Alikuwa kwenye sehemu yake ya kazi akihudumia wateja. Nikamsubiri pembeni mwa kaunta.


Alipomaliza kuhudumia aliokuwa akiwahudumia alinifuata.


“Shikamoo.” Akaniamkia.


“Marahaba. Hujambo?”


“Sijambo. Mambo vipi?”


“Mambo ni poa tu.”


“Umetutembelea leo?”


“Nimekuja kukuuliza, vipi yule mtu hajafika tena hapa?”


“Hajafika. Angefika ningekupigia.”


Nilinyamaza kidogo kwa fadhaa kabla ya kumuuliza;


“Unahisi ni kwa nini ameacha kawaida yake ya kuja hapa?”


“Sijui mwenyewe.”


“Siyo kwa sababu ameona ameua?”


“Sijui.”


“Sisi tunadhani ni kwa sababu ameona ameua na anatafutwa na polisi.”


“Labda.”


“Mtu anayekimbia polisi aghalabu anahisi ana hatia.”


Msichana alinyamaza kimya.


“Sijui huyu mtu tutampata wapi?”


“Tatizo ni kwamba sisi sote hapa hatufahamu anakoishi.”


“Mlishaulizana?”


“Tuliulizana, lakini hakuna aliyefahamu anaishi wapi.”


“Mimi naamini iko siku atafika. Hawezi kupotea moja kwa moja. Atakapoona watu wamesahau atafika tu. Sisi tutaendelea kumtafuta hata kwa mwaka mzima.”


“Nitakapomuona siku yeyote nitakupigia.”


“Ole wake nitakapomtia mikononi kwa maana amenisumbua sana.”


Nilitamani ninywe bia moja, lakini nikakumbuka nilikuwa kazini. Inspekta Mwakuchasa akinisikia ninanuka pombe nitakuwa nimejipalia makaa ya moto.


Nikamuaga yule msichana na kurudi kwenye gari, nikaondoka.


Nilirudi kituoni nikamfahamisha Mwakuchasa kuwa nimesharudi kisha nikaenda ofisini kwangu. Wakati nimekaa nikitafakari, nikawaza kwamba muuaji lazima awe ni mtu mmoja. Na kama ni watu wawili, mmoja atakuwa ametumiwa. Lakini kwenye meza yangu kulikuwa na watuhumiwa zaidi ya mmoja. Kulikuwa na Mdachi na mwenzake na sasa nimemtumbukiza Azzal Mabruki.


Unaweza kuhisi ni suala la kujichanganya, lakini siyo hivyo. Siku zote polisi hukamata watuhumiwa wengi ingawa anayetakiwa ni mmoja tu.


Watuhumiwa hao wakishakamatwa inakuwa ni rahisi kuwachuja na kujua ni yupi mhusika halisi. Hata hivyo, katika suala la kuuawa Matilida, nilikuwa ninamtuhumu Azzal Mabruki kwa asilimia nyingi kuliko nilivyomtuhumu Mdachi.


Kwa upande wa Mdachi nilimtuhumu kumuua Matilida kutokana na wivu wa mapenzi. Imani yetu ni kwamba Mdachi alipoingia nyumbani kwa Matilida na kumkuta akinywa pombe na mtu mwingine au alipokuta mtu amelala chumbani kwake, alikasirika na kuamua kumpiga chupa Matilida na kukimbia.


Tuhuma hizi zina ushahidi wa kukisia kuliko uhalisia. Lakini Azzal Mabruki huenda alikuwepo wakati ninawasili na Matilida nyumbani kwake. Kwa vile alikuwa na kisasi na mimi, akaona atumie nafasi hiyo kumuua Matilida ili kunikomoa mimi. Hapa utaona tuhuma dhidi ya Azzal Mabruki zina mashiko zaidi ya Mdachi.


Baada ya saa moja hivi alikuja polisi akaniambia ninaitwa na Inspekta Mwakuchasa. Nilipofika ofisini kwake aliniambia.


“Kaa kitini.”


Nikakaa kwenye kiti. Mezani kwake kulikuwa na bahasha ya kaki na karatasi nyeupe yenye maandishi ya yaliyopigwa chapa.


“Matokeo ya sampuli ya damu iliyokuwa kwenye vipande vya chupa na ile michirizi iliyopatikana barazani nyumbani kwa Matilida imewasilishwa sasa hivi kutoka kwa mkemia mkuu,” Mwakuchasa aliniambia huku akiishika ile karatasi iliyokuwa juu ya meza.


Akaendelea kuniambia.


“Damu iliyokutwa katika vipande vya chupa ni tofauti na damu iliyokutwa kwenye ile michirizi iliyokutwa barazani upande wa nje.”


Mwakuchasa alisita akanitazama kuonesha mshangao.


“Sisi tulihisi hii damu yote ni ya marehemu,” akasema.


“Kwani ni damu ya nani?”


“Damu iliyokutwa kwenye vipande vya chupa ilikuwa ya marehemu, lakini ile iliyokuwa kwenye michirizi ni damu ya mtu asiyejulikana!”


“Ni aina ya damu tofauti au ni ya watu wawili tofauti?”


“Makundi ya damu yenyewe ni tafauti. Damu ya marehemu ni kundi A na damu iliyokuwa kwenye michirizi ni kundi O.”


“Unadhani ilikuwaje?”


“Hapa tayari umeshaingia utata…”


Nikawaza kidogo kisha nikamwambia.


“Unaweza usiwe utata afande. Hii damu iliyokutwa nje itakuwa ni ya yule mtu aliyempiga chupa marehemu. Huenda alikatwa kiganjani na vipande vya chupa baada ya kumpiga Matilida. Sasa wakati ule anakimbia damu ikawa inamtiririka.”


“Ni pointi nzuri uliyotoa. Inawezekana ilikuwa hivyo. Kwa hiyo mtuhumiwa ni lazima awe na mambo mawili. Kwanza damu yake iwe kundi O kama hili na pili awe na jeraha la kukatwa na chupa kwenye moja ya viganja vyake.”


“Sawasawa.”


“Hawa watu tunaowatafuta ni lazima tupime damu zao, tukague na viganja vyao. Tukimuona mtu na jeraha hata kama ni dogo tunamchuguza damu yake, ikionekana kundi lake ni kama hili tutakuwa tumeshampata muuaji.”


“Sawasawa.”


Matokeo hayo kidogo yalinipa ahueni. Kama tuna ushahidi wa sampuli ya damu ya muuaji isingekuwa rahisi kutuhumiwa mimi hata kama ndiye niliyekuwa na Matilida.


Pia mimi sikuwa na jeraha mkononi mwangu. Hivyo hata kama utapatikana ushahidi kuwa aliyeshuka na msichana huyo kwenye teksi nilikuwa mimi, lakini itaonekana siye niliyemuua.


Wazo hilo lilinipa amani kidogo moyoni mwangu.


Kingine kilichonifurahisha ni kwamba hatutakuwa na sababu ya kuwalazimisha watuhumiwa wakiri kosa. Kazi yetu itakuwa ni kutazama jeraha kwenye viganja pamoja na kuwapima damu. Tukimpata Mdachi tunampima damu na tukimkamata Mabruki pia tunampima damu.


Nikawaza kimoyomoyo, sasa kazi ni kumkamata Mabruki. Ilikuwa ni lazima niandae hoja ya kumkamatisha hata kama ni za uongo.


“Sasa naona tumepiga hatua nyingine nzuri zaidi katika uchunguzi wetu.” Inspekta Mwakuchasa aliniambia.


Hapohapo nikaoana nimueleze inspekta huyo kuhusu Azzal Mabruki.


“Afande kuna kitu nataka pia tukiingize katika uchunguzi huu.”


“Kitu gani?”


“Unamkumbuka Azzal Mabruki, yule mshitakiwa wa meno ya tembo aliyeachiwa na mahakama.”


“Namkumbuka, ana nini?”


“Nimekuwa na shaka naye sana. Katika pitapita zangu nilipata habari kwamba huyu Mabruki alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Matilida. Nilisikia siku aliyouawa Matilida, Mabruki alikuwa ameegesha gari lake nyumbani kwa akina Salma, huyu msichana niliyekuja kumuonesha picha.”


Nikaendelea kumwambia.


“Sasa wasiwasi wangu isijekuwa kulikuwa na mambo ya kufumaniana kati ya Mdachi na Mabruki na kusababisha Mabruki amuue yule msichana.”


“Huyo Salma ndiye aliyekuambia hivyo?”


“Hizo habari nilizipata mitaani tu, lakini Salma aliniambia Mabruki ana mpenzi wake nyumba anapoishi yeye. Inawezekana amenificha. Habari za kuaminika ni kuwa Matilida ndiye aliyekuwa mpenzi wake.”


“Wewe ulikuwa unashauri nini?”


“Nashauri kwamba na yeye tumuingize katika orodha yetu ya watuhumiwa ili aweze kukamatwa.”


Mwakuchasa aliwaza kidogo kisha akaniambia.


“Kuna watu ambao kidogo ni wazito, wana wanasheria wao. Unapompa mtu wa aina hiyo tuhuma kama hiyo ni lazima uwe na ushahidi wa kutosha.”


“Afande umesahau, tuna sampuli ya damu yake na tuna alama ya jeraha kwenye kiganja. Huo ni ushahidi wa kutosha.”


“Wanasheria wake wanaweza kupinga asitolewe damu.”


“Tunaweza kutumia nguvu ya mahakama kumlazimisha atolewe damu kwa ajili ya uchunguzi wetu.”


“Sawa. Unadhani itakuwa vyema akamatwe leo?”


“Kesho asubuhi.”


“Anaweza kupatikana wapi?”


“Nyumbani kwake.”


“Sawa. Asubuhi tunaweza kwenda kumkamata kumhoji na kuangalia uwezekano wa kupima damu yake.”


Je, nini kiliendelea? Usikose Ijumaa kwenye Gazeti la Ijumaa.





FAKI A. FAKI | SIMU: 0655-340 572
 
SEHEMU YA 10


NILIPOSHUKA tu nikamuona mwenyekiti akichungulia mlangoni. Aliposikia gari linasimama nyumbani kwake akachungulia.


“Vipi afande?” Akaniuliza.


“Mlipoondoka nikakumbuka kwamba nilisahau kitu.”


“Kitu gani?”


“Nilisahau kumuonesha picha za watu wawili ambao tunawashuku. Huenda huyo aliyemuona akawa mmojawapo.”


“Sasa ameshakwenda nyumbani kwake.”


“Tafadhali nipeleke anakoishi.”


Ingawa hapakuwa mbali na nyumbani kwake, mwenyekiti huyo alinipeleka nyumbani kwa msichana huyo. Nyumba aliyokuwa anaishi ilikuwa ikitazamana na nyumba aliyokuwa akiishi Matilida.


SASA ENDELEA…


NILIVYOPIMA zile nyumba zilivyo, niligundua ni kweli ulikuwepo uwezekano wa Salma kumuona Matilida akishuka kutoka kwenye teksi. Hata hivyo, kwa vile ilikuwa usiku inakuwa ni vigumu kuigundua sura ya mtu. Pengine ndiyo sababu alishindwa kunitambua.


Mwenyekiti aliposhuka kwenye gari na mimi nikashuka. Mwenzangu alitangulia kufika mlangoni, akamuita Salma.


Mpaka mimi nafika kando ya mlango huo, Salma alikuwa ameshatoka nje.


“Salma nimekufuata tena. Nilikuwa na tatizo dogo,” nikamwambia Salma kabla hajauliza kulikoni.


“Tatizo gani afande?” Salma akauliza kwa sauti ya wasiwasi.


“Kuna picha mbili za watu ambao tunawatuhumu kuhusika na mauaji ya Matilida. Nilisahau kukuonesha picha hizo. Angalau ungeziona ungeweza kutueleza kama huyo mtu uliyemuona akishuka kwenye teksi na Matilida ni mmojawapo.”


Salma akanyamaza na kunitazama. Nikahisi kama vile aliona ingemuia vigumu kumtambua mtu huyo kwenye picha.


“Si ulisema ukimuona unaweza kumtambua?” Nikamuuliza.


“Ndiyo nikimuona nitamjua kwa sababu sura yake si ngeni kwangu.”


Aliporudia kusema hivyo niliuelekeza uso wangu upande mwingine ili asiuone vizuri.


“Sasa ukiziona picha hizo kama huyo uliyemuona ni mmojawapo utatuambia.”


“Sawa.”


“Sasa turudi kituoni mara moja utusaidie katika zoezi hili.”


“Sawa. Tunaweza kurudi.”


Iliwezekana kumuonesha picha hizo hapohapo kupitia kwenye simu yangu, lakini sikutaka kufanya hivyo. Kitendo hicho kilikuwa sawa na kujidanganya mwenyewe kwa sababu nilikuwa nikifahamu kwamba walioko katika picha hizo siyo walioshuka na Matilida kutoka kwenye teksi. Aliyeshuka na Matilida nilikuwa mimi.


Hivyo niliona kumuonesha picha hizo hapohapo huku nikijua kwamba hakukuwa na yeyote ambaye angemtambua, niliona ilikuwa sawa na kujidanganya mwenyewe.


Lengo langu lilikuwa kumdanganya Inspekta Mwakuchasa. Kwa hivyo niliona niende naye kituo cha polisi ili Mwakuchasa aone kuwa zoezi hilo limefanyika japokuwa nilijua msichana huyo asingemtambua yeyote kati ya watuhumiwa hao.


Nilipokubaliana na msichana huyo kwamba nirudi naye kituoni, nilimpakia kwenye gari na kwenda naye kituoni.


Tulipofika nilimwambia Inspekta Mwakuchasa.


“Nimekuja naye, ninakwenda kumuonesha zile picha.”


Mwakuchasa akatufuata. Tulikwenda kwenye ubao uliokuwa umepachikwa matangazo na picha mbalimbli za watuhumiwa.


Nilimuona mke wangu akipita nyuma yetu na kututazama. Laiti asingekuwepo Inspekta Mwakuchasa hapo, msichana huyo kutokana na wivu wake angekuja kusimama hapohapo akajifanya anatazama zile picha.


Lakini alipita na kwenda kaunta.


Nilimuonesha Salma picha hizo mbili za watuhumiwa hao ikiwemo picha ya Mdachi.


Salama alizitazama picha hizo kisha akatikisa kichwa.


“Hizi sura sizo kabisa,” alisema.


“Umeziangalia vizuri?” Mwakuchasa akamuuliza.


“Ndiyo. Nimezingalia viuri. Hapa hayupo.”


Mwakuchasa akanitazama.


“Huyo sasa atakuwa mtuhumiwa wetu wa tatu?” Akaniambia.


“Ndiyo afande.”


Mwakuchasa akamtazama Salma.


“Wewe humfahamu?”


“Mimi simfahamu, lakini sura yake si ngeni kwangu.”


“Huwa unamuona wapi?” Mwakuchasa aliendela kumuuliza.


“Namuona humuhumu mjini, sura yake si ngeni kwangu kabisa,” msichana alisema kisha akanitazama mimi mara moja kabla ya kuyarudisha macho yake kwenye zile picha.


Jinsi alivyonitazama na jinsi alivyopenda kuyarudia yale maneno yake kwamba sura yake si ngeni na anamuonaona humu mjini, vilifanya nijishuku kwamba huenda ananisema mimi. Huenda alishagundua kuwa aliyeniona ni mimi, lakini aliogopa kutamka hivyo.


“Sasa sikiliza. Ushirikiano wako ni muhimu kwetu. Wakati wowote utakapomuona mahali popote, tupigie simu haraka utuarifu,” Mwakuchanasa alimwambia msichana huyo kisha akanitazama mimi.


“Utampa namba yako ya simu.”


“Sawa afande.”


“Mrudishe.”


Mwakuchasa aliondoka na kurudi ofisini kwake na mimi nikaondoka na Salma. Nilipotoka tu nje ya kituo, mke wangu akanifuata.


“Unakwenda wapi?” Akaniuliza huku akimtazama yule msichana.


“Namrudisha huyu msichana nyumbani kwake.”


“Kwani alikuwa na tatizo gani?”


“Yule msichana aliyeuawa juzi, huyu anaishi jirani yake na pia ni rafiki yake. Amekuja kutupa maelezo.”


“Sasa pale mlikuwa mnatazama nini?”


“Anatazama zile picha za watuhumiwa tulizoziweka. Tulitaka atambue kama kuna mmojawapo anayemfahamu.”


“Sasa ndiyo unamrudisha nyumbani kwake?”


“Acha nimfikishe mara moja.”


Nilimtazama Salma, nikamwambia.


“Salma twende.”


Tukaenda kujipakia kwenye gari. Nilihisi kama mke wangu aliona uchungu sana, lakini ni mambo ya kikazi. Hata yeye akihudumia wanaume, mimi siwezi kuchukia.





Nikaliwasha gari na kuondoka.


Wivu mwingine hauna maana kabisa. Yule msichana sikuwa nikimtamani na wala sikuwa na nia ya kumtongoza. Adabu niliyoipata kwa Matilida imetosha.


Nilipomfikisha Salma nyumbani kwake, nikashtuka, nilipoliona gari la kifahari ambalo niliamini lilikuwa gari la Azzal Mabruki. Lilikuwa limeegeshwa nje ya nyumba ileile. Ndani halikuwa na mtu.


Wakati nimesimamisha gari mbele ya gari hilo, nilimuuliza Salma;





“Hili ni gari la nani?”


”Ni la jamaa mmoja…” Salama alinijibu, lakini nilihisi alikuwa amebakisha maneno.


Nilipomuona amefungua mlango ili ashuke nikahisi kwamba hakutaka tuendelee kuzungumza kuhusu mtu huyo.


“Hebu subiri,” nikamwambia.


Msichana akarudi kwenye siti.


“Huyu jamaa amemfuata nani hapa?”


“Kuna msichana wake humu ndani.”


“Anaitwa nani?”


“Anaitwa Uaridi.”


“Anaitwa Uaridi?”


“Ndiyo.”


“Yuko naye muda mrefu?”


“Ndiyo yuko naye muda mrefu.”


“Baadaye nitakuwa na mazungumzo na wewe.”


“Saa ngapi?”


“Nipe namba yako nitakupigia usiku.”


Msichana alinipa namba yake.


“Yangu nilishakupa.”


“Ndiyo yako ninayo.”


“Basi wewe nenda, ni hapo nitakapokupigia.”





Msichana alifungua mlango na kushuka. Na mimi nikaliondoa gari. Kwa mbali nilihisi mwili wangu ukitetemeka. Kitendo cha kukuta gari la mtu niliyekuwa nikimshuku kuhusika na mauaji ya Matilda, mbele ya nyumba ya msichana aliyedai kwamba alimuona Matilida usiku akishuka na mwanaume kutoka kwenye teksi, kwa kweli kilinishtua sana.





Nilihisi mambo mengi. Nilihisi kwamba huyu msichana huenda anajua siri ya kuuawa kwa Matilida, lakini anaficha. Sikukumbuka kwamba usiku ule niliporudi na Matilida niliona gari hilo kwenye ile nyumba.





Lakini kama lilikuwepo basi ni Azzali Mabruki aliyemuua Matilida. Alituona wakati tunashuka kwenye teksi na akatambua kuwa nilikuwa ni mimi. Baadaye akaja kubisha mlango. Matilida alipomfungulia akampiga chupa ya kichwa na kuondoka.


Hili suala nisingeweza kulichunguza peke yangu. Ilinipasa nitengeze hoja ya kulifikisha kituoni ili Mabruki akamatwe.


Je, nini kiliendelea?
 
SEHEMU YA 11



“Wanasheria wake wanaweza kupinga asitolewe damu.”


“Tunawweza kutumia nguvu ya mahakama kumlazimisha atolewe damu kwa ajili ya uchunguzi wetu.”


“Sawa. Unadhani itakuwa vyema akamatwe leo?”


“Kesho asubuhi.”


“Anaweza kupatikana wapi?”


“Nyumbani kwake.”


“Sawa. Asubuhi tunaweza kwenda kumkamata kumhoji na kuangalia uwezekano wa kupima damu yake.”


SASA ENDELEA…


INSPEKTA Mwakuchasa alipokubali kwamba Azzal Mabruki akakamatwe asubuhi nilifurahi. Tulipomaliza mazungumzo yetu nilimuaga na kuondoka.


Mimi na mke wangu tuliondoka kazini muda mmoja. Tuliporudi nyumbani aliniuliza tumefikia wapi katika upelelezi wetu.


“Mpaka sasa tuna watuhumiwa watatu.”


“Si uliniambia mnawashuku watu wawili?”


“Ameongezeka mtu mwingine wa tatu.”


“Ni nani?”


“Azzal Mabruki, si unamkumbuka?”


“Yule aliyewahi kushitakiwa kwa kujihusisha na biashara ya meno ya tembo?”


“Ndiye huyohuyo.”


Mke wangu akacheka mpaka nikachukia.


“Sasa unacheka nini?” Nikamuuliza.


“Nimefurahi tu uliponitajia huyo mtu.”


“Ana nini?”


“Sasa Azzal Mabruki anahusikaje jamani?”


“Wewe huwezi kujua, lakini anaweza kuhusika. Unajua siku ile alipoachiwa na mahakama aliniambia maneno ya kutisha.”


“Alikwambia nini?”


“Aliniambia tutaonana. Maana yake nini?”


“Si alikwambia wewe. Ilimuhusu nini huyo msichana aliyeuawa?”


Hapo nikakumbuka sikupaswa kumueleza mke wangu habari ile. Nilitaka nimueleze kwamba Azzal Mabruki aliniona wakati ninashuka na Matilida kwenye teksi nyumbani kwake. Tulipoingia ndani alikuja kubisha mlango. Matilida akamfungulia wakati mimi nikiwa niko chumbani nimelala. Mabruki akachukua chupa na kumpiga nayo kichwani na kumuua ili nionekane nimemuua mimi.


Nilikuwa nimejisahau kidogo. Kama nisingeshtuka na kumueleza mke wangu maneno hayo, ningekiona cha moto. Ningekuwa nimemdhihirishia kuwa mimi ni malaya na ndiye niliyemuua Matilida. Kusingehitajika tena uchunguzi wa kumtafuta muuaji. Mke wangu angekwenda kuniripoti kuwa mimi ndiye muuaji wa Matilida.


Hapohapo nikageuza maneno.


“Nilisikia Mabruki alikuwa na uhusiano na Matilida na siku alipouawa gari lake lilionekana jirani na pale. Tuna wasiwasi kwamba yeye ndiye aliyemuua.”


“Sasa nani atakuwa muuaji wa kweli. Naona kila siku watuhumiwa wanaongezeka!”


“Si unajua taratibu za kipolisi. Tunakamata watu halafu tunawachuja. Katika hao watu watatu mmojawapo atakuwa muuaji.”


“Na hakuna hata mmoja aliyepatikana hadi sasa!”


“Mabruki tutakwenda kumkamata kesho asubuhi nyumbani kwake.”


“Mimi kwa mawazo yangu sidhani kama mtu kama yule anaweza kujihusisha na jambo la kipuuzi kama lile.”


“Watu kama wale ndiyo wanaofanya mambo ya kipuuzi zaidi.”


“Lakini si kama kumuua msichana bila sababu.”


“Wewe huwezi kujua, uchunguzi ndiyo utabaini kila kitu.”


Wakati ule tunazungumza, simu yangu ikaita. Nilipotazama skrini ya simu nikaona namba ya yule mhudumu wa Baa ya Nane Nane ninayewasiliana naye. Nikaipokea.


“Hujambo?” Nikamsalimia mara tu nilipopokea simu yake.


“Sijambo. Shikamoo.”


“Marahaba. Habari ya kazi?”


“Nzuri. Nilitaka kukufahamisha Mdachi amefika. Sasa ukichelewa ataondoka.”


“Yuko hapo anakunywa?”


“Ndiyo anakunywa!”


“Tunakuja sasa hivi.”


Sikuwahi hata kubadili zile sare zangu za kipolisi. Nikamwambia mke wangu.


“Nimearifiwa yule mtuhumiwa mmoja yuko Baa ya Nane Nane anakunywa pombe, acha twende tukamkamate.”


“Una maana kwamba unatoka tena?”


“Ndiyo ninakwenda hivi.”


Nilikuwa nimeshafika kwenye mlango. Nilisita kidogo nikamtazama mke wangu. Nilidhani angeniambia kitu, lakini alikuwa amenyamaza akinitazama. Nikafungua mlango na kutoka.


Nilirudi kituoni. Inspekta Mwakuchasa alikuwa ameshaondoka. Nikatoa taarifa kwa ofisa aliyekuwa akisimamia kituo, akanipa polisi watatu na gari.


Tukaondoka. Tulipofika tuliegesha gari mbele ya Baa tukashuka. Polisi wawili tuliingia baa, polisi wawili walibaki nje ya baa.


Nilizungusha macho kwenye viti. Kulikuwa na watu kadhaa wakinywa pombe. Macho yangu hayakuweza kumtambua yeyote. Kaunta palikuwa na mhudumu peke yake. Wenzangu wawili walibaki kwenye mlango, mimi nikaenda kaunta.


“Yupo?” Nikamuuliza mhudumu wa kaunta.


“Amekwenda kujisaidia, atatoka sasa hivi. Alikuwa amekaa meza ile pale.”


Alinionesha meza aliyokuwa amekaa Mdachi ambayo haikuwa mbali sana na kaunta. Kulikuwa na chupa mbili za bia zikiwa tupu na bilauri.


“Amevaa shati la rangi gani?”


“Amevaa tisheti ya bluu.”


“Sawa.”


Nilikwenda kukaa kwenye meza ileile.


Wateja walikuwa wametaharuki walipotuona. Pengine kutokana na hofu isiyo na sababu, wateja wawili waliacha kunywa, wakatoka. Wengine waliobaki walikuwa matumatu. Hawakujua kilichokuwa kikiendelea.


Ghafla nikamuona mtu aliyekuwa amevaa tisheti ya bluu akitokea uani. Nilipomtazama tu nikamtambua. Alikuwa Mdachi. Alipoona polisi wawili wamesimama kwenye mlango na mimi nimekaa kwenye meza aliyokuwa amekaa yeye, hakurudi tena kukaa. Akaelekea kwenye mlango wa kutokea. Nikainuka na kumshika bega.


“Uko chini ya ulinzi!” Nikamwambia.


Mdachi alishtuka, akanikazia macho.


“Nimefanya nini?” Akaniuliza.


“Nimekukamata kwa tuhuma za mauaji ya Matilida,” nilimwambia wazi.


Mdachi akashtuka tena na kuanza kupayuka.


“Kwani Matilida nimemuua mimi? Nani amesema kama nimemuua mimi? Sijamuua Matilida!”


Polisi waliokuwa wamesimama kwenye mlango walipoona Mdachi anapayuka, walisogea karibu wakamdhibiti.


“Twende. Wewe umeshaambiwa uko chini ya ulinzi unatakiwa kutii amri ya polisi!” Polisi mmoja alimwambia akiwa amemshika kwenye kiuno.


“Sasa nisiulize ninakamatwa kwa kosa gani?” Mdachi akauliza kwa taharuki.


“Unauliza nini? Kwani mnapofanya uhalifu mnafikiri nini?”


“Uhalifu gani nimefanya?”


“Usitujibishie. Twende!”


Tulimkokota hadi nje ya baa, tukampakia kwenye gari. Tulisahau kuchukua pingu. Tungekuwa nazo tungemtia nazo mikononi. Mtuhumiwa wa mauaji ni mtu hatari.


Tulikwenda naye kituo cha polisi. Tukamuingiza kwenye chumba cha mahojiano.


Kwa vile mimi nilikuwa mmoja wa wapelelezi wa kesi ile ndiye niliyemhoji.


“Unaitwa nani?”


“Naitwa Mdachi Mwinyihatibu.”


“Inaelekea baba yako ni mwinyi na alwatani wa hapa Tanga. Hili Mdachi ni jina lako halisi?”


“Hili nilipewa tu tangu nikiwa mtoto. Jina langu halisi ni Zuberi Mwinyihatibu.”


“Kwenu ni wapi?”


“Kijiji cha Mwarongo.”


“Una umri gani?”


“Miaka arobaini na mitano.”


“Mkazi wa wapi?”


“Chumbageni.”


“Unafanya kazi gani?”


“Biashara.”


“Biashara gani?”


“Ya kununua na kuuza vitu vilivyotumika.”


“Biashara yako unaifanyia wapi?”


“Hapohapo Chumbageni.”


“Hebu kunjua viganja vyako, nataka kuviona.”


Mdachi akakunjua viganja vyake.


Je, nini kiliendelea?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom