Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 7,049
- 12,417
Hadithi hizi zinapatikana katika kitabu Someni kwa furaha kitabu cha kwanza. Unaweza kuzisoma na nyingine nyingi bure ndani ya Maktaba app(by pictus), Icheki playstore.
Kalume-Kenge
Kalume-Kenge alikataa kwenda shule, baba yake akamwambia mbwa: je, mbwa, wataka kumwuma Kalume-Kenge? Hataki kwenda shule.
Mbwa akakataa.
Baba yake akasema kwa fimbo: je, fimbo, hutaki kumpiga mbwa? Yeye hataki kwenda shule.
Fimbo ikakataa.
Baba kaukamata moto, akasema: je, moto, wataka kuichoma fimbo? Kwa maana haitaki kumpiga mbwa, naye hataki kumwuma Kalume-Kenge, naye hataki kwenda shule.
Moto ulikataa.
Baba akasema kwa maji: je, maji, wataka kuzima moto?
Moto hautaki kuchoma fimbo,
Nayo haitaki kumpiga mbwa,
Naye hataki kumwuma Kalume-kenge.
Naye hataki kwenda shule.
Maji yalikataa
Baba kamwendea mbuzi: je, mbuzi, hutaki kunywa maji?
Kwa sababu hayataki kuzima moto.
Nao hautaki kuichoma fimbo,
Nayo haitaki kumpiga mbwa,
Naye hataki kumwuma Kalume-Kenge.
Naye hataki kwenda shule.
Hata mbuzi alikataa.
Baba akamwendea sultani.
Je, sultani. Hutaki kumchinja mbuzi?
Amekataa kunywa maji,
Nayo hayataki kuzima moto,
Nao hautaki kuichoma fimbo,
Nayo haitaki kumpiga mbwa,
Naye hataki kumwuma Kalume-Kenge,
Naye hataki kwenda shule.
Sultani akakubali.
Akamchinja mbuzi
Naye akanywa maji,
Nayo yakazima moto,
Nao ukaichoma fimbo
Nayo ikampiga mbwa,
Naye akamwuma Kalume-Kenge,
Naye Kalume-Kenge akaenda shule.
Kalume-Kenge
Kalume-Kenge alikataa kwenda shule, baba yake akamwambia mbwa: je, mbwa, wataka kumwuma Kalume-Kenge? Hataki kwenda shule.
Mbwa akakataa.
Baba yake akasema kwa fimbo: je, fimbo, hutaki kumpiga mbwa? Yeye hataki kwenda shule.
Fimbo ikakataa.
Baba kaukamata moto, akasema: je, moto, wataka kuichoma fimbo? Kwa maana haitaki kumpiga mbwa, naye hataki kumwuma Kalume-Kenge, naye hataki kwenda shule.
Moto ulikataa.
Baba akasema kwa maji: je, maji, wataka kuzima moto?
Moto hautaki kuchoma fimbo,
Nayo haitaki kumpiga mbwa,
Naye hataki kumwuma Kalume-kenge.
Naye hataki kwenda shule.
Maji yalikataa
Baba kamwendea mbuzi: je, mbuzi, hutaki kunywa maji?
Kwa sababu hayataki kuzima moto.
Nao hautaki kuichoma fimbo,
Nayo haitaki kumpiga mbwa,
Naye hataki kumwuma Kalume-Kenge.
Naye hataki kwenda shule.
Hata mbuzi alikataa.
Baba akamwendea sultani.
Je, sultani. Hutaki kumchinja mbuzi?
Amekataa kunywa maji,
Nayo hayataki kuzima moto,
Nao hautaki kuichoma fimbo,
Nayo haitaki kumpiga mbwa,
Naye hataki kumwuma Kalume-Kenge,
Naye hataki kwenda shule.
Sultani akakubali.
Akamchinja mbuzi
Naye akanywa maji,
Nayo yakazima moto,
Nao ukaichoma fimbo
Nayo ikampiga mbwa,
Naye akamwuma Kalume-Kenge,
Naye Kalume-Kenge akaenda shule.