Mpauko
R.I.P
- Jan 19, 2019
- 2,323
- 3,353
Mwandishi: RM the brave
faili namba 25
01
Hisia za kukumbatiwa na mtu pale kitandani zilinigutusha toka kwenye usingizi mzito,nilijigeuza kivivu na kukutana uso kwa uso na mpenzi wangu wa siku nyingi, Bibiana Mgaya.
Alikuwa ni binti mrefu kiasi, maji ya kunde, hakuwa mnene wala mwembamba huku akijaaliwa wowowo la wastani lililotosha kumpagawisha mwanaume yeyote rijali, akiwa na sura ya duara ambayo daima ilipambwa na tabasamu maridadi kabisa.
"mmmh umeshaamka"niliuliza swali la kipumbavu maana ni wazi kabisa kuwa Bibiana alikuwa macho.
"ndio mpenzi wangu saa moja hii jiandae uwahi kazini" aliongea kwa upole huku akiwa kajawa na tabasamu.
"eeeh saa moja hivi" niliulza kivivu huku nikijinyoosha.
"amka bwana"
"sawa mama naamka, hivi maji ya kuoga tayari? "
"ndio amka sasa" Bibiana aliongea huku akivuta shuka na kuliondoa mwilini mwangu.
"aaagh kwani saa moja tayari? " nililalama kizembe.
Safari hii sikupata majibu, Bibiana alishayoyoma zake kwenda sebuleni, niliamka na kuingia bafuni maana nyumba hii ya vyumba viwili pamoja na jiko, ilikuwa ni self container.
Ilinichukua dakika takribani 10 hivi kumaliza shida zangu, nilitoka bafuni na kuanza kuyatupia mangwanda yangu ya kazi, mangwanda ya rangi ya khaki!, kifuani ikipambwa na namba E. 1289 nilikuwa ni polisi, konstebo Jackson Makusu au afande Makusu kama wengi walivyozoea kuniita.
Baada ya kuhakikisha nipo sawa nilijongea sebuleni ambapo nilimkuta Bibiana akiwa anapakaa blueband katika silesi za mkate, aliinua uso wake na kuachia tabasamu pana kabla ya kuniambia "karibu chai mume wangu"
Nilimtazama kwa mahaba huku nikijipweteka pembeni yake katika sofa ile ya watu wawili, nikanawa mikono na kuanza kuifakamia chai ile ya maziwa pamoja na silesi za mkate hadi nilipohakikisha ya kuwa nimeshiba hasa.
"Bibiana"
"abee konstebo Makusu" aliitikia na kuingiza mzaha
"umeanza Bibiana nilishakuambia sitaki uniite hilo jina" nililalama
"jamani sasa nikuiteje"
"niite mume wangu Makusu"
"akaaaah mara ngapi nakuambia uje utoe posa kwetu unaishia kunipiga kalenda halafu mara hi unataka uitwe mume? " aliongea huku akirekebisha kofia yangu kichwani.
"sasa si ungenisikiliza kwanza na wewe, ni hivi nataka nichuhue likizo mwezi ujao ili nilete posa" nilisema.
"waooooo unasema kweli mpenzi wangu?" aliruka kwa furaha na kunikumbatia.
"ndio mpenzi wangu acha mimi niwahi kazini tutaongea zaidi baadae" nilisimama na kumbusu kwenye paji la uso, nikatoka nje na kuitia moto gari yangu ndogo aina ya Toyota Swift, safari ya kutoka Mtaa wa Magomeni kwenda kituo kikuu cha polisi Mtwara ilianza.
Ilinichukua dakika kumi na tatu kuwasili kituoni, moja kwa moja nilielekea katika lango la kuingilia na kumkuta konstebo Amina akiandika maelezo ya mze wa makamo niliyemkuta pale, "Makusu mkuu amesema ukifika umuone ofisini haraka" alizungumza Amina huku akiendelea kuandkaandika pasi na hata kunitazama.
Sikutaka kumuuliza chochote nilinyoosha korido moja kwa moja hadi nlipoufikia mlango ulioandikwa RPC niliyatazama maandishi yale kisha nikashusha pumzi kwa nguvu kuusaka ujasiri kisha nikagonga mlango taratibu, "pita" sauti nzito na kali ilisikika, nikasukuma mlango na moja kwa moja nilipiga hatua tatu kwa ukakamavu na kupiga saluti.
"afande" nilizungumza kwa ukakaavu.
"kaa kititi, kaa tafadhali" alizungumza huku akinionyesha moja ya viti kadhaa vilivyokuwa mbele ya meza, nilijongea taratibu na kukaa kitini
"hujamho bwana Makusu"
"sijambo shikamoo mzee"
"marahaba habari za kazi? "
"salama tu mzee"
"vizuri sana,kwanza napenda nikupongeze kwa mafanikio uliyoyapara hivi sasa wewe sio konstebo Makusu bali ni Sajini Jackson Makusu"alinitazama kwa chati huku akifungua mtoto wa meza na kutoa bahasha Akaiweka juu ya meza.
"Jeshi la polisi linajivunia kuwa na vijana wachapakazi na wazalendo kama wewe" mara hii alisimama na kujongea dirishani alitupa macho huku na huko kisha akanigeukia na kunikazia macho kwa sekunde kadhaa.
"ni takribani miaka mitano sasa umekuwa moja ya askari waadilifu na wachapakazi, sote tunafahamu dhima nzito ambayo jeshi letu la polisi limekabidhiwa, kuhakikisha ulinzi na usalama wa raia pamoja na mali zao na mara kadhaa umeweza kuhatarisha maisha yako kutetea haki na usalama wa raia" alisita na kuanza kupiga hatua kunifuata alinishika begani na kunyofoa beji yenye cheo changu cha konstebo.
Akaichukua bahasha aliyoiweka juu ya meza na kutoa beji,kuona vile nilisimama kwa ukakamavu, akaitazama beji ile kwa chati kisha akapachika begani mwangu, nilitoa saluti ya heshima nisiamini kama kweli leo hii nilikuwa ni sajini Jackson Makusu.
"kaa tafadhali sajini mpya bwana jackson Makusu" akafungua mtoto wa meza na kutoa bastola ndogo aina ya Barreta mm9 akaiweka mezani kisha akatoa box tatu ndogo za risasi nazo akaziweka mezani mwisho akatoa bahasha ndogo nayo akaweka mezani
"lakini sasa haya mambo hayatokei kwa bahati mbaya kijana bali yanatokea kwa sababu maalum, mara baada ya kukukabidhi siraha hii tambua wazi kwamba umepewa jukumu kubwa, na natumaini utalitekeleza kwa weledi wa hali ya juu, chukua siraha yako, bahasha hii ina vitambulisho vyako haya inuka kijana inuka mimi nimekwisha kumalizana na wewe" aliongea kwa msisitizo.
"lakini mkuu na...... "
"sajini Makusu nimekwambia mimi nimekwisha kumalizana na wewe toka nje"
"eeeh ntoke nje hivi"niliuliza kizembe maana ikishakuwa tabia yangu kuuliza maswali yasiyo na mantiki na tabia hii ilikwishaota mizizi.
nilimtupia macho RPC Lazaro Ahmad na kumuona wazi akiwa amekereka, nilipiga saluti na kuondoka huku nikikionea fahari cheo changu kipya, Sajini Makusu yaani nilikuwa naelekea kuanza kupigiwa saluti na mimi nilitabasamu.
Baada ya hatua mbili tu simu ilitoa mtetemo niliitoa mfukoni na kutupia macho kwenye kioo, ilikuwa ni namba mpya.
"haloo"
"haloo, sajini Jackson Makusu namba E.1289 kituo kikuu cha polisi Mtwara"
"ndio nani mwenzangu"
"Awadh Mpekula, meja Awadh mpekula toka makao makuu ya polisi dar es salaam kiongozi wa operesheni Faili namba 25 tafadhali fuata maelekezo" akavuta pumzi kama kwamba alitaka maneno yale yaniingie vilivyo.
"una masaa machache ya kujiandaa, tazama katika bahasha uliyopewa kuna tiketi ya ndege ya Air Tanzania ya saa kumi na moja jioni kuelekea mwanza" mlio hafifu wa kukatwa simu ulisikika.
Nikaitupia macho simu ile kwa sekunde kadhaa nisielewe maana ya matukio yale,"eti nimepandishwa cheo halafu tena niende mwanza kwenye operesheni Faili namba 25!" nilizungumza kwa sauti ya chini nikaifungua bahasha na kukutana na kitmbulisho changu kipya pamoja na tiketi ya ndege.
Nikapiga hatua moj kwa moja hadi katika gari yangu na safari ya kurudi nyumbani ikaanza njia nzima nilibaki nikiwaza naanzia wapi kumweleza Bibiana juu ya safari ile ya ghafla.
Niliwasili nyumbani na kumkuta Bibiana akiwa anafua, aliacha kufua na kunikazia macho ya mshangao.
"wewe mwanaume vipi unaumwa au"
"hivi unaniona kama mgonjwa sio" nilimuuliza huku nikiingia ndani.
Bibiana aliacha kufua na kunifuata nyuma, moja kwa moja nilipitiliza chumbani na kukaa kitandani, "hivi una nini wewe? " Bibiana aliniuliza huku nae akikaa pembeni yangu.
"kazi hazifanyiki mpenzi wangu muda wote nakufikiria wewe" nilizungumza huku nikitabasamu
"yani mwanaume wewe huishiwi vituko" alisema huku akiangua kicheko hafifu "hebu niambie bwana una nini mwenzetu maana naona kabisa haupo sawa"
"Bibiana"
"abee"
"nimepata safari jioni hii kwenda Mwanza" na taratibu niliona tabasamu likimyeyuka usoni, akanitazama kwa chati kisha akashusha pumzi.
"Bihiana" niliita bila majibu.
tayari macho ya Bibiana yalikwishazingirwa na machozi, hapo nikaanza kazi nyingine ya kumbembeleza na hatimaye aliridhia suala lile maana ni wazi hata asingelikubali ilikwa ni lazima niende.
Niliutumia mchana ule kujipumzisha ndani na hatimaye saa kumi na nusu ilinikuta Mtwara airport nikiagana na mpenzi wangu niliyempenda sana, Bibiana.
Nilikamilisha taratibu za pale uwanjani na moja kwa moja nikaingia ndani ya ndege ya shirika la ndege la Tanzania aina ya Bombadier Q400.
Hatimaye muda wa ndege kuondoka uliwadia, rubani alitutaka tuzime simu zetu na kufunga mikanda tayari kwa kuanza safari.
Nilifunga mikanda kisha nikaitwaa simu yangu na kuweka airplane mode, kisha moja kwa moja nikaingi katika ujumbe wa maneno, nilianza kusoma sms za mpenzi wangu Bibiana na zote alinitakia safari njema.
Nikaachana nazo kwa lego la kumpigia mara nifikapo Mwanza, macho yaangu yakatua kwenye ujumbe usiokuwa na namba zidi ya neno private nkafungua ujumbe ule na kukutana na maneno matatu tu HOTEL TILAPIA 17A.
****************************
MASAA MAWILI NYUMA
Bibiana baada ya kutoka airport alinyoosha barabara ya airport moja kwa moja hadi alipoifikia stendi ya daladala Mangamba kisha akapinda kulia kuifuata barabara ya Sabasaba.
Alinyoosha hadi alipofikia barabara ya bandari akakunja kushoto kuifuata baraara ya Mnarani mwendo wa dakika tatu akakunja kulia kuelekea soko kuu Mtwara.
Baada ya kufika sokoni akaangaza huku na huko kutafuta parking hadi alipobahatisha nafasi ndogo iliyolitosha vilivyo gari hii ndogo aina ya toyota Swift, akaegesha gari kabla ya kushuka na kuingia sokoni tayari kwa manunuzi ya mahitaji ya nyumbani.
Kitu pekee ambacho hakukijua wala kuwaza kichwani mwake ni kwamba alikuwa anafuatiliwa!
Gari nyeupe aina ya Toyota Prado old model ilikuwa imesimama upande wa pili mkabala na gari ya Bibiana, mwanaume mmoja pande la mtu, mrefu kiasi, mweupe,ndevu zake aliziweka kwa mtindo wa O huku akivalia tisheti nyeupe, jeans ya blue huku chini akiwa kavalia buti ngumu za rangi ya khaki "timbarland".
Akaitoa simu yake na kubofya mara kadhaa kabla hajaiweka sikioni na kusikilizia.
"Fred mko tayari?" aliuliza huku macho yake kayakaza kwenye gari ile ndogo.
"ndio kilia kitu kipo tayari, gari ya wagonjwa imepatikana pamoja na nyaraka zote zenye taarifa za mgonjwa" sauti ya Fred ilisikika.
"Good saa 11 na nusu muwe mmeshafika, kwa sasa yupo sokoni nitaondoka naye hadi kwake natumaini kila kitu kitakwenda kama tulivyopanga" aliongea na kukata simu.
Baada ya dakika takribani 10 Bibiana alionekana akitoka na moja kwa moja akaingia garini na safari ya kuelekea Magomeni ikaanza.
Ile Prado old model nayo ikaunga tela, safari ilichukua nusu saa hivi kufika nyumbani kwa sajini Makusu.
Bibiana akapaki gari na moja kwa moja akajitoma ndani, ile prado nayo ikapitiliza na kwenda kusimama katika duka lililokuwa umbali wa hatua mia moja hivi toka ilipokuwa nyumba ya sajini Jackson Makusu.
Ngo! Ngo! Ngo! Bibiana alishtushwa na hodi ile kwani hakuwa na mazoea yakupokea ugeni wowote hususani muda kama ule takribani saa moja kasoro.
Moja kwa moja akaachana na kutazama taarifa ya habari na kwenda kufungua mlango, hata hivyo alilakiwa na sura ngeni kabisa.
"karibu" aliitikia kwa mashaka kidogo
"asante naitwa Cliford Sanga, konstebo Cliford Sanga" alijitambulisha na kuendelea "nina maagizo yako kutoka kwa shemeji Makusu"
"karibu pita ndani" Bibiana alimkaribisha huku akifungua zaidi mlango na kumpisha Cliford.
Cliford alipiga hatua tatu na kusimama baada ya kusikia mlango ukifungwa, akageuka kumtazama Bibiana safari hii tabasamu likiwa limeyeyuka, hali hii ilimshtua Bibiana na kengele ya hatari ikalia kichwani mwake.
Hata hivyo bahati haikuwa yake kwani kabla hajachukua maamuzi yoyote tayari Cliford kwa kasi alimuwahi kwa kabali ya mkono wa kushoto kabla hajachomoa kitambaa cheupe na kumziba pua na mdomo, taratibu Bibina akalegea na kujilaza pale sakafuni.
Cliford akaitupia macho sebule ile nadhifu akalisogelea jokofu dogo, akafungua na kutoa juisi ya matunda iliyokuwa kwenye chupa ya maji Ndanda, hakuwa na haja na grasi akainua chupa ile na kupiga mafunda kadhaa.
Akajipwetea kwenye kochi na kuanza kutazama taarifa ya habari, muungurumo wa gari inayopaki nje ulimgutusha, akazima televisheni pamoja na taa pekee ya sebuleni iliyokuwa inawaka kwa wakati huo, akafungua mlango na kukutana na wanaume wawili huku mmoja akiwa kavalia koti la daktari.
Cliford aliwapa ishara ya kuingia ndani, wote wakashirikiana kumbeba Bibiana na kumpakiza kwenye gari ile yenye nembo ya Hospitali kuu ya Ligula, land cruiser mkonga.
"Nisubirini nikachukue juisi" Cliford alibwata baada ya kuona dereva akiondoa gari, akachumpa na kuingia ndani, akachukua juisi aliyoibakiza na kutoka mbio akajipakia garini.
Mwendo wa dakika tatu uliwafikisha barabara kuu inayoelekea Dar es salaam, dereva akaegesha gari pembeni kisha akamtazama Cliford.
"Clif nadhani mimi kazi yangu imeishia hapa" aliongea.
"Good job Eddie, sasa kaifate gari ya mzee pale dukani kwa mangi ukampelekee, sisi kama unavyoona moja kwa moja tunakwenda Dar" aliongea Ciford huku akishuka garini na kuzunguka upande wa dereva, Eddie akashuka na kuanza kuondoka kwa mwendo wa haraka.
"dokta hebu njoo ukae huku mbele" aliita huku akicheka
"ha ha ha Clif mara hii nishakuwa dokta" aliongea Fred huku akiingia garini.
"cheki koti lilivyokutoa mzee"
"endesha gari bwana wee" alilalama Fred maana aliona wazi Cliford alikuwa anamkebehi kwani hakubahatika hata kumaliza darasa la saba.
Cliford huku akiwa bado anacheka aliingiza gia na safari kuelekea Dar ikaanza, yapata saa mbili na nusu usiku.
******************
TUKUTANE SEHEMU YA 2
faili namba 25
01
Hisia za kukumbatiwa na mtu pale kitandani zilinigutusha toka kwenye usingizi mzito,nilijigeuza kivivu na kukutana uso kwa uso na mpenzi wangu wa siku nyingi, Bibiana Mgaya.
Alikuwa ni binti mrefu kiasi, maji ya kunde, hakuwa mnene wala mwembamba huku akijaaliwa wowowo la wastani lililotosha kumpagawisha mwanaume yeyote rijali, akiwa na sura ya duara ambayo daima ilipambwa na tabasamu maridadi kabisa.
"mmmh umeshaamka"niliuliza swali la kipumbavu maana ni wazi kabisa kuwa Bibiana alikuwa macho.
"ndio mpenzi wangu saa moja hii jiandae uwahi kazini" aliongea kwa upole huku akiwa kajawa na tabasamu.
"eeeh saa moja hivi" niliulza kivivu huku nikijinyoosha.
"amka bwana"
"sawa mama naamka, hivi maji ya kuoga tayari? "
"ndio amka sasa" Bibiana aliongea huku akivuta shuka na kuliondoa mwilini mwangu.
"aaagh kwani saa moja tayari? " nililalama kizembe.
Safari hii sikupata majibu, Bibiana alishayoyoma zake kwenda sebuleni, niliamka na kuingia bafuni maana nyumba hii ya vyumba viwili pamoja na jiko, ilikuwa ni self container.
Ilinichukua dakika takribani 10 hivi kumaliza shida zangu, nilitoka bafuni na kuanza kuyatupia mangwanda yangu ya kazi, mangwanda ya rangi ya khaki!, kifuani ikipambwa na namba E. 1289 nilikuwa ni polisi, konstebo Jackson Makusu au afande Makusu kama wengi walivyozoea kuniita.
Baada ya kuhakikisha nipo sawa nilijongea sebuleni ambapo nilimkuta Bibiana akiwa anapakaa blueband katika silesi za mkate, aliinua uso wake na kuachia tabasamu pana kabla ya kuniambia "karibu chai mume wangu"
Nilimtazama kwa mahaba huku nikijipweteka pembeni yake katika sofa ile ya watu wawili, nikanawa mikono na kuanza kuifakamia chai ile ya maziwa pamoja na silesi za mkate hadi nilipohakikisha ya kuwa nimeshiba hasa.
"Bibiana"
"abee konstebo Makusu" aliitikia na kuingiza mzaha
"umeanza Bibiana nilishakuambia sitaki uniite hilo jina" nililalama
"jamani sasa nikuiteje"
"niite mume wangu Makusu"
"akaaaah mara ngapi nakuambia uje utoe posa kwetu unaishia kunipiga kalenda halafu mara hi unataka uitwe mume? " aliongea huku akirekebisha kofia yangu kichwani.
"sasa si ungenisikiliza kwanza na wewe, ni hivi nataka nichuhue likizo mwezi ujao ili nilete posa" nilisema.
"waooooo unasema kweli mpenzi wangu?" aliruka kwa furaha na kunikumbatia.
"ndio mpenzi wangu acha mimi niwahi kazini tutaongea zaidi baadae" nilisimama na kumbusu kwenye paji la uso, nikatoka nje na kuitia moto gari yangu ndogo aina ya Toyota Swift, safari ya kutoka Mtaa wa Magomeni kwenda kituo kikuu cha polisi Mtwara ilianza.
Ilinichukua dakika kumi na tatu kuwasili kituoni, moja kwa moja nilielekea katika lango la kuingilia na kumkuta konstebo Amina akiandika maelezo ya mze wa makamo niliyemkuta pale, "Makusu mkuu amesema ukifika umuone ofisini haraka" alizungumza Amina huku akiendelea kuandkaandika pasi na hata kunitazama.
Sikutaka kumuuliza chochote nilinyoosha korido moja kwa moja hadi nlipoufikia mlango ulioandikwa RPC niliyatazama maandishi yale kisha nikashusha pumzi kwa nguvu kuusaka ujasiri kisha nikagonga mlango taratibu, "pita" sauti nzito na kali ilisikika, nikasukuma mlango na moja kwa moja nilipiga hatua tatu kwa ukakamavu na kupiga saluti.
"afande" nilizungumza kwa ukakaavu.
"kaa kititi, kaa tafadhali" alizungumza huku akinionyesha moja ya viti kadhaa vilivyokuwa mbele ya meza, nilijongea taratibu na kukaa kitini
"hujamho bwana Makusu"
"sijambo shikamoo mzee"
"marahaba habari za kazi? "
"salama tu mzee"
"vizuri sana,kwanza napenda nikupongeze kwa mafanikio uliyoyapara hivi sasa wewe sio konstebo Makusu bali ni Sajini Jackson Makusu"alinitazama kwa chati huku akifungua mtoto wa meza na kutoa bahasha Akaiweka juu ya meza.
"Jeshi la polisi linajivunia kuwa na vijana wachapakazi na wazalendo kama wewe" mara hii alisimama na kujongea dirishani alitupa macho huku na huko kisha akanigeukia na kunikazia macho kwa sekunde kadhaa.
"ni takribani miaka mitano sasa umekuwa moja ya askari waadilifu na wachapakazi, sote tunafahamu dhima nzito ambayo jeshi letu la polisi limekabidhiwa, kuhakikisha ulinzi na usalama wa raia pamoja na mali zao na mara kadhaa umeweza kuhatarisha maisha yako kutetea haki na usalama wa raia" alisita na kuanza kupiga hatua kunifuata alinishika begani na kunyofoa beji yenye cheo changu cha konstebo.
Akaichukua bahasha aliyoiweka juu ya meza na kutoa beji,kuona vile nilisimama kwa ukakamavu, akaitazama beji ile kwa chati kisha akapachika begani mwangu, nilitoa saluti ya heshima nisiamini kama kweli leo hii nilikuwa ni sajini Jackson Makusu.
"kaa tafadhali sajini mpya bwana jackson Makusu" akafungua mtoto wa meza na kutoa bastola ndogo aina ya Barreta mm9 akaiweka mezani kisha akatoa box tatu ndogo za risasi nazo akaziweka mezani mwisho akatoa bahasha ndogo nayo akaweka mezani
"lakini sasa haya mambo hayatokei kwa bahati mbaya kijana bali yanatokea kwa sababu maalum, mara baada ya kukukabidhi siraha hii tambua wazi kwamba umepewa jukumu kubwa, na natumaini utalitekeleza kwa weledi wa hali ya juu, chukua siraha yako, bahasha hii ina vitambulisho vyako haya inuka kijana inuka mimi nimekwisha kumalizana na wewe" aliongea kwa msisitizo.
"lakini mkuu na...... "
"sajini Makusu nimekwambia mimi nimekwisha kumalizana na wewe toka nje"
"eeeh ntoke nje hivi"niliuliza kizembe maana ikishakuwa tabia yangu kuuliza maswali yasiyo na mantiki na tabia hii ilikwishaota mizizi.
nilimtupia macho RPC Lazaro Ahmad na kumuona wazi akiwa amekereka, nilipiga saluti na kuondoka huku nikikionea fahari cheo changu kipya, Sajini Makusu yaani nilikuwa naelekea kuanza kupigiwa saluti na mimi nilitabasamu.
Baada ya hatua mbili tu simu ilitoa mtetemo niliitoa mfukoni na kutupia macho kwenye kioo, ilikuwa ni namba mpya.
"haloo"
"haloo, sajini Jackson Makusu namba E.1289 kituo kikuu cha polisi Mtwara"
"ndio nani mwenzangu"
"Awadh Mpekula, meja Awadh mpekula toka makao makuu ya polisi dar es salaam kiongozi wa operesheni Faili namba 25 tafadhali fuata maelekezo" akavuta pumzi kama kwamba alitaka maneno yale yaniingie vilivyo.
"una masaa machache ya kujiandaa, tazama katika bahasha uliyopewa kuna tiketi ya ndege ya Air Tanzania ya saa kumi na moja jioni kuelekea mwanza" mlio hafifu wa kukatwa simu ulisikika.
Nikaitupia macho simu ile kwa sekunde kadhaa nisielewe maana ya matukio yale,"eti nimepandishwa cheo halafu tena niende mwanza kwenye operesheni Faili namba 25!" nilizungumza kwa sauti ya chini nikaifungua bahasha na kukutana na kitmbulisho changu kipya pamoja na tiketi ya ndege.
Nikapiga hatua moj kwa moja hadi katika gari yangu na safari ya kurudi nyumbani ikaanza njia nzima nilibaki nikiwaza naanzia wapi kumweleza Bibiana juu ya safari ile ya ghafla.
Niliwasili nyumbani na kumkuta Bibiana akiwa anafua, aliacha kufua na kunikazia macho ya mshangao.
"wewe mwanaume vipi unaumwa au"
"hivi unaniona kama mgonjwa sio" nilimuuliza huku nikiingia ndani.
Bibiana aliacha kufua na kunifuata nyuma, moja kwa moja nilipitiliza chumbani na kukaa kitandani, "hivi una nini wewe? " Bibiana aliniuliza huku nae akikaa pembeni yangu.
"kazi hazifanyiki mpenzi wangu muda wote nakufikiria wewe" nilizungumza huku nikitabasamu
"yani mwanaume wewe huishiwi vituko" alisema huku akiangua kicheko hafifu "hebu niambie bwana una nini mwenzetu maana naona kabisa haupo sawa"
"Bibiana"
"abee"
"nimepata safari jioni hii kwenda Mwanza" na taratibu niliona tabasamu likimyeyuka usoni, akanitazama kwa chati kisha akashusha pumzi.
"Bihiana" niliita bila majibu.
tayari macho ya Bibiana yalikwishazingirwa na machozi, hapo nikaanza kazi nyingine ya kumbembeleza na hatimaye aliridhia suala lile maana ni wazi hata asingelikubali ilikwa ni lazima niende.
Niliutumia mchana ule kujipumzisha ndani na hatimaye saa kumi na nusu ilinikuta Mtwara airport nikiagana na mpenzi wangu niliyempenda sana, Bibiana.
Nilikamilisha taratibu za pale uwanjani na moja kwa moja nikaingia ndani ya ndege ya shirika la ndege la Tanzania aina ya Bombadier Q400.
Hatimaye muda wa ndege kuondoka uliwadia, rubani alitutaka tuzime simu zetu na kufunga mikanda tayari kwa kuanza safari.
Nilifunga mikanda kisha nikaitwaa simu yangu na kuweka airplane mode, kisha moja kwa moja nikaingi katika ujumbe wa maneno, nilianza kusoma sms za mpenzi wangu Bibiana na zote alinitakia safari njema.
Nikaachana nazo kwa lego la kumpigia mara nifikapo Mwanza, macho yaangu yakatua kwenye ujumbe usiokuwa na namba zidi ya neno private nkafungua ujumbe ule na kukutana na maneno matatu tu HOTEL TILAPIA 17A.
****************************
MASAA MAWILI NYUMA
Bibiana baada ya kutoka airport alinyoosha barabara ya airport moja kwa moja hadi alipoifikia stendi ya daladala Mangamba kisha akapinda kulia kuifuata barabara ya Sabasaba.
Alinyoosha hadi alipofikia barabara ya bandari akakunja kushoto kuifuata baraara ya Mnarani mwendo wa dakika tatu akakunja kulia kuelekea soko kuu Mtwara.
Baada ya kufika sokoni akaangaza huku na huko kutafuta parking hadi alipobahatisha nafasi ndogo iliyolitosha vilivyo gari hii ndogo aina ya toyota Swift, akaegesha gari kabla ya kushuka na kuingia sokoni tayari kwa manunuzi ya mahitaji ya nyumbani.
Kitu pekee ambacho hakukijua wala kuwaza kichwani mwake ni kwamba alikuwa anafuatiliwa!
Gari nyeupe aina ya Toyota Prado old model ilikuwa imesimama upande wa pili mkabala na gari ya Bibiana, mwanaume mmoja pande la mtu, mrefu kiasi, mweupe,ndevu zake aliziweka kwa mtindo wa O huku akivalia tisheti nyeupe, jeans ya blue huku chini akiwa kavalia buti ngumu za rangi ya khaki "timbarland".
Akaitoa simu yake na kubofya mara kadhaa kabla hajaiweka sikioni na kusikilizia.
"Fred mko tayari?" aliuliza huku macho yake kayakaza kwenye gari ile ndogo.
"ndio kilia kitu kipo tayari, gari ya wagonjwa imepatikana pamoja na nyaraka zote zenye taarifa za mgonjwa" sauti ya Fred ilisikika.
"Good saa 11 na nusu muwe mmeshafika, kwa sasa yupo sokoni nitaondoka naye hadi kwake natumaini kila kitu kitakwenda kama tulivyopanga" aliongea na kukata simu.
Baada ya dakika takribani 10 Bibiana alionekana akitoka na moja kwa moja akaingia garini na safari ya kuelekea Magomeni ikaanza.
Ile Prado old model nayo ikaunga tela, safari ilichukua nusu saa hivi kufika nyumbani kwa sajini Makusu.
Bibiana akapaki gari na moja kwa moja akajitoma ndani, ile prado nayo ikapitiliza na kwenda kusimama katika duka lililokuwa umbali wa hatua mia moja hivi toka ilipokuwa nyumba ya sajini Jackson Makusu.
Ngo! Ngo! Ngo! Bibiana alishtushwa na hodi ile kwani hakuwa na mazoea yakupokea ugeni wowote hususani muda kama ule takribani saa moja kasoro.
Moja kwa moja akaachana na kutazama taarifa ya habari na kwenda kufungua mlango, hata hivyo alilakiwa na sura ngeni kabisa.
"karibu" aliitikia kwa mashaka kidogo
"asante naitwa Cliford Sanga, konstebo Cliford Sanga" alijitambulisha na kuendelea "nina maagizo yako kutoka kwa shemeji Makusu"
"karibu pita ndani" Bibiana alimkaribisha huku akifungua zaidi mlango na kumpisha Cliford.
Cliford alipiga hatua tatu na kusimama baada ya kusikia mlango ukifungwa, akageuka kumtazama Bibiana safari hii tabasamu likiwa limeyeyuka, hali hii ilimshtua Bibiana na kengele ya hatari ikalia kichwani mwake.
Hata hivyo bahati haikuwa yake kwani kabla hajachukua maamuzi yoyote tayari Cliford kwa kasi alimuwahi kwa kabali ya mkono wa kushoto kabla hajachomoa kitambaa cheupe na kumziba pua na mdomo, taratibu Bibina akalegea na kujilaza pale sakafuni.
Cliford akaitupia macho sebule ile nadhifu akalisogelea jokofu dogo, akafungua na kutoa juisi ya matunda iliyokuwa kwenye chupa ya maji Ndanda, hakuwa na haja na grasi akainua chupa ile na kupiga mafunda kadhaa.
Akajipwetea kwenye kochi na kuanza kutazama taarifa ya habari, muungurumo wa gari inayopaki nje ulimgutusha, akazima televisheni pamoja na taa pekee ya sebuleni iliyokuwa inawaka kwa wakati huo, akafungua mlango na kukutana na wanaume wawili huku mmoja akiwa kavalia koti la daktari.
Cliford aliwapa ishara ya kuingia ndani, wote wakashirikiana kumbeba Bibiana na kumpakiza kwenye gari ile yenye nembo ya Hospitali kuu ya Ligula, land cruiser mkonga.
"Nisubirini nikachukue juisi" Cliford alibwata baada ya kuona dereva akiondoa gari, akachumpa na kuingia ndani, akachukua juisi aliyoibakiza na kutoka mbio akajipakia garini.
Mwendo wa dakika tatu uliwafikisha barabara kuu inayoelekea Dar es salaam, dereva akaegesha gari pembeni kisha akamtazama Cliford.
"Clif nadhani mimi kazi yangu imeishia hapa" aliongea.
"Good job Eddie, sasa kaifate gari ya mzee pale dukani kwa mangi ukampelekee, sisi kama unavyoona moja kwa moja tunakwenda Dar" aliongea Ciford huku akishuka garini na kuzunguka upande wa dereva, Eddie akashuka na kuanza kuondoka kwa mwendo wa haraka.
"dokta hebu njoo ukae huku mbele" aliita huku akicheka
"ha ha ha Clif mara hii nishakuwa dokta" aliongea Fred huku akiingia garini.
"cheki koti lilivyokutoa mzee"
"endesha gari bwana wee" alilalama Fred maana aliona wazi Cliford alikuwa anamkebehi kwani hakubahatika hata kumaliza darasa la saba.
Cliford huku akiwa bado anacheka aliingiza gia na safari kuelekea Dar ikaanza, yapata saa mbili na nusu usiku.
******************
TUKUTANE SEHEMU YA 2