Hadithi: Gamboshi

SEHEMU YA TATU

Wakiwa wanaendelea na safari afande baraka alikuwa akiendelea kupitia baadhi ya mafaili huku akiangalia huku na kule ndani ya gari ndipo alipo fungua kwenye dashboard na kitu cha kwanza alichoona kwa haraka kilikuwa ni kiboski kidogo kilicho fungwa na matilio ya kung’aa alitaka kujua ni basi alitoa na kuuliza
“Nini hiki”
“Au ndo ulikuwa unataka kumpa veronica hii” aliongezea kabla hata hajajibiwa
“ Iyo ni zawadi nimepewa na mke wang” alimjibu akiwa anamtazama
“alf kwa nini uwaze na nataka kumpa veronica” akaongezea
“Kwani mimi sina macho, mkubwa anaambiwi tazama”
“We unachofikilia hakipo, me mwaminifu”
“ Sawa lakini, macho nayo yanaongea ”
“Chunga usiruhusu watu wakakusoma kilahisi”
“ unamanisha nini.” Afande mwita aliweka kituo na kuuliza baada ya kupewa fumbo ambalo hakulielewa
“ We angalia mbele bana”
“Usije kuniingiza machakani” akaongezea kisha akarudisha zawadi ile pahari alipo ikuta lakini bado alikuwa haamini kama inatoka kwa mke wake na alikuwa anataka sana kujua ina nini ndani.
Afande mwita baada ya kuachwa kwenye fumbo kubwa alikuwa hana budi ya kuendelea kuendesha gari huku waki wapo robo ya safari yao.
Walitembea kilometa nyingi bila kusimama ikafika pahari Afande mwita alikuwa anahitaji kutulia na kutoa haja ndogo pia mda huo afande baraka alikuwa kapitiwa na usingizi, alishuka kwenye gari na kwenda kichaka kilichokuwa pembene ya barabara. Kipindi anatoka kujisaidia aliona watu wakiwa kwenye msululu wakiwa wanavuka barabara aliwatazama kwa mbali na alielekea kwenye gari, aliingia na kuwasha injini na kuondoa gari lakini baada ya kuendesha akiwa kwenye kasi ghafla watu aliona wanavuka barabara kwa mbali walitokea kwa mbele ndipo alipo minya bleki kwa kasi kubwa nusra awagonge mpka afande baraka shituka usingizi
“Mungu wangu nakufa!” alikuwa ni afande baraka baada ya kushituka kwenye usingizi mzito
Afande mwita alikuwa bado katahamaki haelewi nini kimetokea,mikono ikiwa ipo kwenye ushukani akiwa hata haskii afande baraka akimsemesha
“oya kaka” afande mwita alimshutua afande mwita kwa kupiga makofi kumtoa kwenye kitu kama msongo wa mawazo
“Naam”
“kaka utaniua na presha”
“ unajua kuendesha familia, gari inataka kukushinda” akaongezea
Afande mwita hakujibu chochote alichukua chupa ya maji na kunywa alijisahau na kuiweka pembene huku akiwa ajaifunga na kuwasha injini ndipo kichupa kilidondoka na kumwaga maji
“ Ah kaka nini tena”
“ uko sawa kweli?” afande baraka alipata wasiwasi
“ Ndio kaka” aliwasha injini kwa mara nyingine baada ya gari kuwa limezima na kuendelea na safari.
Baada ya kutembea robo tatu ya safari walipita kibao kimoja kilichopo pembene upande wa kulia wa barabrara ambacho kilikuwa na kutu lakini kinaonekana kinasomeka “Gamboshi Kilometa 12”
Walikipita baada ya kama dakika kumi na tano gari lao lilizima injini ndipo walipaki pembene
“Shida nini tena “ Afande mwita alijiuliza
“ Hii gari imeshachoka” Afande baraka alimjibu akiwa anashuka kwenye mwita nae alifwata na kwenda kufungua boneti ya gari kutazama kuna shida gani
Alitazama kwa sekund lakini sababu yeye hakuwa mtaalamu wa magari alirudishia boneti kwanza na kuchukua simu yake mfukoni alipo washa alikuta mnara wa mtandao umebaki mmoja kwenye ndipo alikumbuka alipewa namba za mwenyeji atakae wapokea, aliwahi na kufungua mlango wa gari lakini mda anaangaza aliona karatasi ndogo imeloana na majI
“Aaaah baraka!”
“Nini hiki” akaongezea huku akiwa kaishika karatasi ndo iliyokuwa na namba za simu za mtu atakae wapokea watakapo fika
“We ndo ulimwaga maji” alijibiwa na afande baraka
“ Sa tunafanyaje” aliuliza tena
“Kwani ulikuwa hujasave kwenye simu” Afande baraka aliuliza
“Hapana” Alijibu huku akipitia phonebook yake
“ Tuko karne ya 20 na unashindwa kusave kitu cha msingi kwenye simu unaacha kwenye karatasi”
“Sasa unanambia au unafoka” Afande mwita aliuliza huku akimtazama
“ Hapa cha kufanya ni kutafuta plan b” akaongezea
“Kuna plan b” Afande baraka akauliza
“Haipo ndo naifikiria”
“ Tupo katikati ya poli wewe upo kufikiria plan b”
“Sasa unataka nifanye nini”
“Wewe unawazo gani” Afande mwita aliuliza
“Sina!” Afande baraka alimjibu huku akiendelea kumtazama
Afande mwita aliangaza huku na kule na kweli walikuwa katikati ya poli na mda unaenda hajui afanye, alichukua maamuzi ya kushuka kwenye kichaka kilicho pembene yao na kumwacha afande akiwa kasimama mbele ya gari
“Plan b yako ni kunitelekeza hapa!?” Afande baraka aliuliza huku akimtazama afande mwita akiishiria kwenye machaka, alibaki peke yake akiangalia huku na kule lakini kulikuwa hakuna dalili ya kupata msadaa.
Afande akiwa kichaka alikuwa akitembea bila kujua anaelekea wapi alitembea kwa mwendo wa dakika kumi ndipo alisikia sauti ikitokea nyuma yake na kumwita “Mwita choma Maige” aligeuka kwa kasi na kutoa buduku yake aina ya pisto iliyokuwa kwenye pembene ya kiuno chake. Aliinyoosha kwa mtu huyo alikuwa ni mzee sio chini ya miaka 40 afande mwita alimtazama na kuuliza
“We nani?”
“Weka bunduki chini” mzee huyo alimwambia bila wasiwasi
“Naongea kwa mara ya mwisho sitarudia”
“We nani?” alimwambia huku akiweka bunduki yake tayari kwa kupiga
Mzee huyo aliuliza swali moja ambalo lilimfanya afande baraka arudishe bunduki yake ilipokuwa
“Yuko wapi Veronica”
“ Nimeamwacha hosipitali” alijikuta hakijibu bila kutaka huku akilegeza mikono yake
“Na wewe ni nani yake”
“Mme wake” akaongezea
“Hapana, Boss wake” alijibu akiwa anamtazama kwa makin sana
“Haya basi twende kijijini” Mzee alimwambia huku akimwosha njia kwa mkono
“Kuna askari mwenzangu nilimwacha kwenye gari “
“Naomba tumwende” akaongezea
“Kuna mtu mwingine tofauti na veronica?” mzee aliuliza kwa mshangao ambayo hata Afande mwita hakuelewa. Afande mwita aliongoza njia kwenda kumrudia alipo mwacha afande baraka lakini wakitembea walikutana nae njia kabla hata hawajafika mbali
“Mkuu”
“Ulikuwa umeenda wapi?”afande baraka aliuliza
“Na huyo ni nani”Akaongezea
“Mwenyeji wetu”
“Umempataje”
“Ilo sio swali” Afande mwita alimjibu na kumgeukia yule mzee na kumwambia tunaweza kwenda
Mzee aligeuka kulia kwake na kuongoza njia huku afande mwita na baraka wakifwata.
Ilikuwa ni majira ya saa kumi na moja jioni walitembea kufikia mpaka afande baraka kuhitaji maji ya kunywa aliona maji yakitililika na kuamua kusogea pale alipotaka kutafuta namna aweze kunywa maji mzee alimkataza na kusogea karibu yake alichukua jani dogo na kuchukua tone ya maji yaliyokuwa yakitililika akamwambia ageuke mkono wake afande baraka alifanya ivo alimwekea yale maji juu ya mkono wake ndipo afande baraka alihisi kama kuna moto umedondoka kwenye mkono wake alishutka na kurusha mkono juu, Yule mzee hakuongea mengi aliendelea kuwa ongoza walitembea kwa mda wa masaa mawili walifika gamboshi mida ya saa moja jion cha kushangaza palikuwa kimya hamna kelele wala mtu hata mmoja afande mwita ndoa alikuwa haelewi
“Ndo hapa?” aliuliza akiwa hana wakika na swali lake
“Ndio” mzee alimjibu bila kumtazama huku akiendelea kutembea
“Wanasema huku usiku huwa ni ulaya mbona buza pazuri sasa” Afande baraka alijuliza mwenyewe bila kupata jibu
Walikuwa kitembea huku kila hatua waliyokuwa wakitembea ilikuwa ikisikika, mpaka walipofika kwenye nyumba ndogo pia napo kulikuwa kimya kabisa mzee aliwafungulia mlango palikuwa giza akawaambia waingie walianaglia na kuingia kishingo upande aliwafungia mlango na kuwasha taa kwa nje akawaogaza kwa kuwaambia pumzikeni afande baraka alipo jaribu komeo palikuwa pamefungwa kwa nje
“Huyu mzee vipi”
“Kafunga kwa njee” alijiuliza mwenye huku akimtazama afande mwita akiwa tayari kashasinzia sababu ya uchovu wa kutembea na kuendesha gari na yeye alibakiwa hana njisi na kujilaza na kupumzika kama walivoambiwa na mzee yule nae alielekea kitandani na kupumzika.
Sehemu ya tatu hii hapo mkimaliza kusoma natamani kuskia maoni yenu mpka hapo
 
UTANGULIZI

Ni hadithi inayohusu kijiji kilichopo mkoa wa simiyu wilaya ya bariad ambacho kiko umbali wa takribani kilometa 12 za mlaba kutoka simiyu mjini, kama hili jina litakuwa geni kwako na hujawahi kuliskia kabisa basi ngoja nikufamishe kidogo.

Gamboshi ni kijiji kinachofahamika kwa uchawi nchi Tanzania kikifahamika ni makao makao makuu ya wachawi ukiachana na mkoa wa sumbawanga basi kwa lugha nyingine unaambiwa ni kitovu cha wachawi yani mizimu yote inapatikana huko, ndo kijiji pekee unaambiwa mchana giza usiku ulaya.

Julai mwaka 1999 serikali ilichukua maamuzi ya kukitenga kijiji hicho baada ya vifo vya zaidi ya watu hamsini [50] vilivoketea ndani ya siku moja ikiaminika ilikuwa na uhusiano na mambo ya kishirikina basi watu waliambiwa kuhamaka makazi na kutafuta sehemu zingine za kuishi.

Kwa muda wa takribani miaka ishirini [20] hamna ambae amekuwa na taarifa zozote kuhusu eneo hilo basi ndo mda serikali kutoka kwenye ofisi ya rais, ilitumwa barua kwa mkuu wa mkoa wa simiyu barau ya agizo la kukifungua kijiji hicho kwa upya ikiwezekana atume maaskari mara moja na kufunguliwe kituo kidogo cha polisi nae mkuu wa mkoa wa simiyu alitii maagizo yaliyo kuwa yametoka kwa rais na kuitisha kikao cha maaskari wa jeshi la polisi, kutoka wilaya zote za simiyu.

Mkuu wa mkoa kwa kutambua kuwa askari wengi wangekuwa na uonga wa kufanya kazi kijiji kule lakini bado ilikuwa inamlazimu kuchagua sababu pia alikuwa na mamlaka ya kufanya hivyo, basi alifanya maamuzi na kumchagua Mwita Choma na Baraka Kulwa kama maaskari teule kwenda kijijini gamboshi.
Lakini bila kufaham wamejiigiza kwenye shida kubwa nao walikuba kazi ile kwa mikono yote.

SEHEMU YA KWANZA

Tarehe 13 mwezi wa sita mwaka 2019 saa kumi na mbili afajiri [06:00am] akiwa amelala kwake kengele ya mezani [ Alarm] ilikuwa ikipiga kelele kumanisha mda wa kuamka umefika nae taratibu akijinyoosha kutoa uchovu wa usiku, akamudu kufungua macho huku akiwa anatazama aliona mtu akija ghafla kurukia kitandani kama kwa kishindo alishutka sana maana alikuwa na wenge la usingizi lakini hakuwa mwingine bali mke wake Mwita choma

“Habari za asubuhi, mme wangu”. alikuwa ni mke wake mwita akitoa salam huku akilukia kwa kitanda alipo mume wake
“ unajua umenishutua” mwita alimuliza mke na kueka kituo bila kujibu salam yake
“ kumbe umeogopa, basi pole mume wangu”anaomba radhi huku sura yake ikiwa inatabasamu kama anataka kucheka .
“ Umeamkaje kipenzi changu” bado aliuzua huku sura yake ikiwa na tabasamu lilelile
“ salama tu mke wangu.” alijibu salam ya mke wake akaambatanisha na swali,
“mbona umeamka mapema sana leo”
“ kuna kitu konki nimekuandalia kabla ya hujaondoka” alimjibu swali la mume akimtazama kwa ukalibu
“Aah konki” mwita alianza kumtenkenya mke wake huku akirudia neno “konki”
Konki! konk, konki! konki! Mwita aliendelea kumtenkenya huku mke wake akicheka na kumwomba aache anahisi atajikojolea!
Mwita aliacha huku mke wake akiwa ameweka sura ya kununua nae alijirudi na kumwambia
“ kumbe umeumia, basi pole mke wangu” huku sura yake ikiwa inatabasamu kama anataka kucheka

Wakiwa bado wapo kitandani mke wake hakujibu chochote bali alisogeza uso wake karibu na kushika kidevu cha mume wake na kumpiga busu la wakika, na kulikatisha haraka huku akishuka kitandani na kumwambia mume wake amfate bafuni. Nae Mwita alishuka kitandani haraka akiwa na boxer tu na kuelekea bafuni, basi huko kilikuwa ni kitendo cha kuendelea kudumisha ndoa yao ambayo imeishi kwa muda wa miaka mitano sasa wakiwa bado hawajafanikiwa kupata mtoto.

Mwita choma ni kijana wa miaka therathini [30] kabila mkulya urefu wake nin wastani, akiwa na miaka 25 alibahatika kupata mke aitwae ni Janeth. akiwa na miaka 27 aliteuliwa kuwa ofisa msimamizi wa kituo kidogo kilichopo wilaya ya bariadi mkoani simiyu alifanya kazi kwa waminifu huku sifa zikimndondokea kama kijana jasiri. Badaa ya kutumikia jeshi la polisi kwa kipindi wa muda mrefu akiwa ofisa msimamizi alipewa kazi ya kwenda kuwa mkuu wa kituo kijijini gamboshi kama ilivotoka kwa ofisi ya raisi kuwa wateuliewe askari wawili waende wakafanye kazi kijijini huko.

Na ndo ilikuwa siku yenyewe akiwa ameamka salama akiwa nyumbani kwake na mke wakiwa bafuni wanamlizia kuoga. Akiwa amejifunga taulo kiunoni alisikia sauti ya simu yake ya mkononi ilikuwa ikiita aliishika na kuangalia jina lilikuwa ni rafiki yake Baraka kulwa alikuwa anapiga alikuwa amemsave [ Partern in crime] alipokea na kuongea nae

“Kaka, habari yako” ndo kitu cha kwanza aliskia alipo pokea simu ilikuwa ni salam kutoka kwa rafiki yake
“ salama kaka, kwema?”
“uko wapi”
alijibu salam huku akikaa kitandani. Akaongezea swali jingine
“Kwema! Niko nyumbani napata breakfast” baada ya kujibu swali mwita alicheka na kuuliza
“Haha haha”
“Hivi mdogo wangu huna mpango wa kuoa kabisa!”
“Maana kila siku ujipikie mwenyewe ufue kwa nini usioe?”
Aliuliza na kubaki kusubiri atasema nini
“Mimi ntaoa tu kaka ata usijali ni mipango tu”
“Sawa, wahi kituo sababu tutakuwa tunaondoka mapema si unalewa sehemu tunayoenda unaambiwa usiku ni ulaya” alikubali kisha kumpa taarifa nyingine
“Haha haha, sawa kaka” alicheka kidogo kwa taarifa mwita aliyompa kisha akakubali na kukata simu maongezi yakawa yameishia hapo
Mwita akaweka simu kitandani iliavae nguo za jeshi la polisi ambazo zilikuwa zinamkaa vizuri sana sababu pia ya mwili wake uliokuwa umekaa kimtindo wenye mpangilio na kwenda kupata chai ambayo mke alikuwa kamwandalia, alikuta janeth akiwa anamsubiri seblen akiwa tayari kashaweka chai mezan alikuwa kavaa kitenge tu.
“Karibu chai mme wangu” alimkaribisha chai mme wake kwa tabasamu nzuri kabisa huku akimtengenezea kiti aweze kuketi
“Ahsante mke wangu” alishukuru na kuketi kwenye kiti huku mke wake akiwa ubavu wake wa kushoto
Hakika kilikuwa chakula kitamu ambacho hata mwita alishambulia kama hana akili timamu
“wewe umeshakula mke wangu” aliuliza huku akiendelea kula
“ hapana babo ntakula baadae kidogo, saivi nataka nikae karibu na wewe” alimjibu mme wake na kuongezea shida yake kwa huo mda
Mwita alitambua kwa nini mke wake alisema maneno yale na alikuwa hana jinsi zaid ya kumfariji
“ usijali mama angu, mimi ni wako siku zote “ alimwambia maneno mazuri akiwa anambembeleza kwa kumshika shavu akitumia mkono wake wa kushoto
Janeth alisimama na kumwambia mme wake asuburi na kuelekea chumbani alipo rudi alikuwa na kiboski kidogo ambacho kilikuwa kimefungwa vizuri
“ Kwa ajili yako mme wangu” alimpatia kwa mikono miwili likiabatinishwa na taabasam kama ilivyo kawaida yake kutabasamu
“Ahsante mke wangu” mwita alifurahi alionesha kabisa kashukuru alisamama na kumpatia busu mke wake, alipo jaribu kufungua mke wake alikataa na kumwambia utaifungua baadae
“kuna nini kwani “ akaongezea na swali
“ utaona tu, lakini usikifungue hapa” alimwambia akiwa anamtazama machoni bila kupepesa
“ sawa” mwita alikubali lakini alibaki na maswali kutakuwa na nini kwenye boski maana kilikuwa kidogo sana chenye urefu wa 5 na upata wa 3
tayari kamaliza kupata chai alichukua begi lake la mgongoni lilokuwa mezani na kuelekea nje akiwa anatoka alimgeukia mke wake na kumwambia
“ usisahau kufunga milango mda wa kulala na ukiwa unatoka”
“ na ukiwa na shida yoyote nipigie mimi kwanza”akaongezea huku akiwa anafungua mlango
“sawa , mme wangu” alikubali huku akimtazama mme wake akielekea kupanda gari la jeshi la polisi aina ya toyota landa cruiser ikiwa inafahamika kama [ Defender ]
Mwita aliwasha injini ya gari na kushusha vioo huku mke wake akiwa bado anasubiri aondeke
“ kwaheri, ubaki salama” alimwaga akiwa anamtazama kwa mbali
“ sawa, safari njema mme wangu” alimjibu na kuingia ndani
Mwita alipandisha vioo na kuondoa gari kuelekea kituoni.
Ni hadithi au ni simulizi ya kweli?
 
SEHEMU YA NNE

Tarehe 19 mwezi wa 3 mwaka 1999 siku iyo kulikuwa na sherehe kubwa ya binti aitwae Anjella kunti alikuwa akitimiza miaka 12 hapo mzee kunti akiwa ni baba yake mzazi, alikuwa mwenye furaha sana huku anjella akiwa ni mtoto wake watu tatu huku wa kwanza akiwa anaitwa john pamoja katerina. Kunti akiwa ni mtu mkubwa sana kijiji hapo basi sherehe ilileta watu tofauti kutoka ndani na nje ya kijiji watu wakubwa viongozi mashuhuri lakini wao walikuwa wamekuja kwa kuzungumza mambo amabayo yalikuwa hayahusiani na sherehe kabisa, hata njisi walivoingia hamna aliyekuwa anajua wapo kwenye sherehe hiyo alikuepo katibu mkuu wa chama tawala mwenyekiti wa chama pamoja na raisi wa jamuhuri ya muugano wa Tanzania ilikuwa ni sehemu ya siri kabisa na maongezi yalipo kuwa yakiendelea mtoto wake na mzee kunti akiwa anazunguka ghafla alisikia watu wakibishana
“Naomba uniambie nini kinahitaji kuipata iyo dawa chochote nitakupatia” Mh rais alikuwa akizungumza na mzee kunti kuhusu dawa anayohitaji, nini kinahitaji mpatie aweze kumsaidia
“Mh Rais naelewa na nakuheshimu sana lakini unachohitaji kiko nje ya uwezo wangu sizani kama naweza kukusaidia”
“Tumekuwa marafiki kwa mda mrefu staki kuona hiki kitu kikifunja urafiki wetu”
“Fanya unavoweza hakikisha unanipa majibu kabla ya wiki mbili hazijaisha” aliongezea kisha akaondoka na akiwa na viongozi wenzake waliokuwa wamemsindikiza
John akiwa kajibanza pembene aliskia mazungumzo hayo na alibaki anajiuliza ni dawa gani baba anaombwa na Mh rais
Siku iyo mzee kunti alikuwa yupo mezani peke akiwa na gazeti mkononi na maji ya kunywa pembene akiendelea kusoma mwanae wa kiume john alikuja na kukaa pembene
“Hali ya hewa leo nzuri sana” john aliuliuza huku akimzatama baba
Mzee kunti alimtzama mtoto wake na hakujibu chochote
“Hivi unazan mtu kama mh rais huwa anashida yoyote” john aliendelea kuongea
“sababu anakila kitu pesa, nguvu lakini baba kuna vitu anahitaji huku akiomba”
Mzee kunti alimtazama mwanae na kumuuliza
“unataka nini”
“nataka nikusaidie”
Mzee kunti alicheka na kuuliza
“wewe unisaidie na nini”
“Mimi ndo mtu pekee nae jua kwamba mh rais alikuepo hapa siku ya sherehe ya anjella na sijamwambia”
“ata mama sijamwambia”Aliongezea
Ghafla sura ya mzee kunti alibadilika na kuongea akiwa anamtazama mtoto wake machoni
“ulichokiona au kuskia kiishie pale nikiskia kwa mama yako ntakufanya vibaya “mzee alimwambia bila kupepesa macho
“siwezi kuongea chochote nataka nikusaidie” ingiwa na vitisho john alimjibu baba yake
“nambie Mh rais anataka dawa gani”
“Hili swala halikuhusu niache mimi na wewe uendelee kufaanga mdomo wako”
Mzee kunti alikataa msaada ambao alikuwa anataka atoe mwanae japo alikuwa hajui anataka kutoa msaada gani alichomtaka ni asije kuskia izo taarifa kwa mama yake kwahiyo alimtaka afunge mdomo
John akiwa ni mtoto wake wa kwanza alikuwa na umri wa miaka 16 kwa mira na desturi za kijijini hapo alikuwa tayari kashatambulishwa kwenye mizimu na alikuwa na uelewa na baadhi ya mambo aliyokuwa akifundishwa na babu yake.Mzee kunti alibaki na mawazo mengi sana akijiuliza vipi mwanae alikuwa anataka kutoa msaada gani. Baadae jioni wakiwa wako wanaendelea kupata chakula cha jioni mzee kunti alikuwa bado hajafika mezani ki mila walikuwa hawatakiwi kuanza kula kama baba wa familia hajakaa mezani kwahiyo mama alimwagiza john aende kumwita baba yake john alinyanyuka na kwenda kumwangalia baba aliingia mpka chumbani wanapo lala wazazi wake huku akiita baba lakini kulikuwa kimya alivoendelea kuangaza aligundua kuna kama mlango mdogo sana upo wazi aliuzatama na kufikiria unaelekea wapi sababu ulikuwa mlango mgeni kwake aliingia na kuwacha wazi kidogo alifika mpka ndani huku kukiwa na mishumaa kusaidia kuona kwa mbali aliona mtu alivojaribu kutazama vizuri alikuwa ni baba yake mzee kunti aliposkia sauti alikuwa na nguvu ya kufunga akili ya mtu basi alifunga akili ya mtu bila kujua ni nani na kutokezea nyuma ya huyo mtu ndipo aligundua mwanae
“Anatafuta nini huku huyu” alijiuliza kwa hasira sana
Kwa uwezo aliokuwa nao alikuwa anaweza kufunga akili na kukufanya usahau vitu vilitokea mda mfuopi aliopita sasa aliwaza sana amfanayaje mwanae kumfungua ni kama kumwonesha iyo sehemu aliwaza kipi kitakuwa sahihi akaona mfungue tu
“Baba” alikuwa ni john baada ya kufungulia akili
“unafanya nini huku” aliongezea
“Mama kaniagiza nije nikuite tukale”
“Njoo nikuoneshe” Mzee kunti baada ya kumtazama alimwita huku akiendelea kutembea
John alimfata taratibu baba yake anapokelea, walifika sehemu kuna sinia likiwa na maji na makabati mengi mzee kunti alielekea kwenye moja ya makabati na kutoa kitabu kidogo na kumpatia john
“Fungua ukarasa wa kumi na moja”alikuwa ni mzee kunti akimweleza mwanae
John alifanya hivyo
“Haya soma inasemaje” aliongezea
“Mimi kama mkuu na mwakilishi wa mizimu naapa kuitumikia mizimu kwa uaminifu bila kufunja sheria wala desturi za kijiji” john alimaliza na kubaki akimwangalia baba yake
“Fungua ukurasa wa sita “ mzee kunti aliendelea kumwambia afungue kurasa mwingine
John alifungua tena kwa mara nyingine
“Soma”
“Zifwatazo ni sheria za mila na desturi za mizimu, moja usidanganye mizimu pili usifanye maamuzi bila kuhusisha mizimu tatu usifanye kafara kumuhudumu shetani”
“Haya maji unayoyaona hapa ni hatari sana usije ukawahi kuyashika wala kugusa ni hatari sana” aliendelea kumkazia kuwa yale maji anayo yaona ni hatari sana
Mzee kunti alimwambia mwanae na kumwelewesha kwamba babu yake alikula kiapo mbele ya mizimu lakini bado alifanya kinyume na kuizunguka mizimu na kupelekea kutokea maafa makubwa sana hayuko tayari kufanya ivo tena . Alichukua kitabu alichokuwa amempatia na kukirudisha alipo kitoa na kumwambia mwanae aongeze njia watoke nje, sehemu hiyo ilikuwa ya siri sana hata kipindi john anaingia aliacha mlango wazi lakini kipindi anarudi alikuta pamejifunga .
Basi mzee kunti alipafungua na kuelekea mpka mezani kupata chakula cha jion , john alibaki na maswali kesho yake asubuhi na mapema alijia ni mtu mmoja pekee ndo anaweza kujibu maswali yake na si mwingine ni babu yake kulikuwa na moja ya jengo kubwa pale kijijini lilikuwa limeandikwa “kwa mkombozi” humo ndani ndo alizikwa “ZAWA KEWA KUNTI” babu yake John.
Yalikuwa ni mazoea yake toka yuko mtoto kuongea na babu kila anapokuwa na shida lakini kwa kipindi hiki alikuwa hajaongea nae kwa kipindi kirefu baada ya kupigwa maarufu na baba baada ya kugundua mwanae anafundiswa uchawi.
Alifika mpka ndani kawaida ilkuwa lazima utoe salama na uchukue kisu kilicho pembene utoe damu kidogo uweke kwenye kikombe kilikuwa mezani kwa mbele kiufupi mazingira ya mule ndani yalikuwa yanafanana na makanisa ya wakatoliki. Baada ya kufata kila kitu alipa goti na kusuburi ghafla aliskia sauti
“Mjukuu wang”
“Naam babu”
“Unaendeleaje”
“Naedelea vizuri”
Yalikuwa ni mazungumzo ya john na babu yake.
Babu yake alitambua mjukuu anashida ikambidi aulize
“Una shida gani mjukuu wangu”
“Ni baba”
“kafanya nini”
“Mara ya mwisho alinikataza kuja kuonana na wewe”
“Pili kuna jambo ananificha hataki kunambia wala hajamwambia mtu yoyote”
“Na…” alisita alichokuwa anataka kuuliza
“Nambie mjukuu wangu wala usiwe na wasi wasi”
“Ni kweli ulisaliti mizimu”
“Hapana mizimu ndo ilitaka kunisaliti mimi baada mimi kutaka kuishi kitakatifu, nilikuwa nataka nibatizwe niwe mkristu mizimu ilikataa na kupanga njama za kuniua ndo mpka leo unaona zimezikwa kwenye kanisa hili la wakatoliki”
“Baba yako hataki kuona huo ukweli mimi ndo nilizungukwa” alishusha pumzi na kuendelea
“Saiv baba yako anapanga kutoa kafara na ni kafara haramu”
“la kumuhudumu shetani” John aliuliza
“Ndio”
“Kwa nini baba anataka kufanya hivo” John aliuliza tena huku taarifa iyo ikiwa imemfunja moyo
“Sijui lakini nataka nikusaidie na wewe umsaidie baba yako”
“Niskilize kwa makini mda mrefu hakujakuwa na sikukuu ya kusafishwa kwahiyo nataka uirudishe tena na unahitaji baadhi ya vitu kufanya hivo”
“Vitu gani”
“Kuna chumba katikati ya chumba ya baba yako na mama yako wanapo lala kile chumba ni dhahabu kuna kila kitu unachohitaji”John hakuelewa akauliza
“Chumba ambacho kuna sinia kubwa linamaji”
“umeshawahi kufika humo ndani” mzee zawa alishangaa sana baada ya kujua kwamba mjukuu wake anakijua hicho chumba na ilikuwa faida kwake alianza kuona kama mpango wake unaanza kwenda anavotaka
“Ndio, ilikuwa ni jana nilimkuta baba akiomba”
“Vizuri yale maji uliona ndo unayohitaji pamoja na kitabu kilicho ukuta wa tatu”
“Usiniulize maswali mengi ukishakamilisha njoo navyo kwangu”
Lakini bila kujua kila kitu alichoambiwa na babu yake kilikuwa ni uongo na baba yake alikuwa na mipango mingine kabisa wala sio kusaidia mtu.
 
Kwenye hii simulizi ndo kama tunaanza kuna uchawi mpka mtashangaa nawa ahid hutajuta kuisoma simulizi hii
 
Na kitu cha tofauti najaribu kufikilia ambacho kitaleta mamillion kuja kusoma kitabu changu nipen muda sehemu ya tano ni alhamisi
 
SEHEMU YA TANO
Ilikuwa jumapili asubuhi alfajiri ya saa kumi na mbili na robo [06:45] afande baraka akiwa anajinyoosha taratibu kitandani baada ya usingizi mzito na uchovu walikuwa na baada ya kutembea umbali mrefu mpka kufika kijijini hapo hatimae aliamka alikuwa ndani ya nguo zake za jeshi la polisi pembene kulikuwa na kitandana kingine ambacho alikuwa amepumzika afande mwita. Afande baraka alitoka kitandani na kuvaa jaketi lake kilikuwa chumba kikubwa sana alikitzama kwa makini kisha kuelekea mlango
“Huyu mzee alitufungia mlango sijui yuko wapi” alikiwa akijiuliza huku akielekea kushika kitasa cha mlango
Lakini alishangaa baada ya mlango kufunguka alitoka njee alichokioona hakuamini macho yake
Kulikuwa na watu wengi sana tofauti na walivo ingia jana yake usiku palikuwa kimya ndege zilikuwa zikilia juu ya miti na watu wakiendelea na shughuli zao kiukweli ile sehemu ilimfutia sana akiwa bado anatahamaki mazingira afande mwita nae alikuwa anaamka kutoka kitandani alifika mpka nje na kubaki ameshangaa
“Kaka tumeamka mkoa gani huu” Afande mwita alimuuliza afande baraka
“Sijui kaka”
“Habarini za Asubuhi”ilikuwa ni sauti ya mzee aliyewaleta jana akiwapa salam
“Salama tu”walimtazama na kuitikia wote kwa pamoja
“Poleni na safari pili msiongeleshe mtu msiemjua”
“Kwani tunamjua nani huku” Aliuliza Afande baraka
“Ndo nacho jaribu kusema hamna mnaemjua na kuongelesha mtu usimjua”
“Kingine jana mliacha gari itabidi mlifate ndo mambo mengine yaendelee”aliongezea
“Sawa.” waliitikia wote kwa pamoja
Basi aliwambia wamfate na waendee kufata gari walipo liacha jana usiku baada ya kuchelewa kufika na kutumia njia ya miguu kufika kijijini, lakini kilicho washangaza ni walitembea umbali mfupi sana
Kama dakika 15 tu kufika ambapo gari waliliacha usiku wa jana
“Kwa nini hatukutumia hii njia jana”Afande baraka aliuliza
“usije kujaribu kupita hiyo njia mida ya usiku” alijibiwa maneno machache sana na kiukweli aliogopa kuskia ivyo
Walikuta gari ikiwa kwenye usalama ulele waliliacha nao afande baraka ndo alikuwa na ufunguo basi ndo alichukua jukumu la kuendesha gari walifungua milango na kila mtu kuingia kwenye gari simu ya afande mwita aliita alitoa jina lilikuwa ni “Veronica” Alitoa tabasamu kigodo n huku afande baraka akichungulia kwa mbali akitamani kujua ni nani kapiga simu, afande mwita alipokea simu
“Habari za asubuhi mtoto mzuri”
“nzuri tu”
“Umeamkaje?”
“Salama vp nyie”
“Salama kabisa”
“Mama anaendeleaje?”
“Anaendelea vizuri nilikuwa nimemaliza kumlisha hapa”
“Basi ni habari njema kuskia ivo”
“Kweli kabisa”
“Nambie” Baada ya kusalimia na kujuliana hali, afande mwita alitaka kujua kwa nini veronica kapiga asubih

“Naomba niongee na mwenyeji wenu” aliomba aongee na mzee aliewapokea na kuwapeleka mpka kwenye makazi walipofikia
“Sawa” afande mwita alikubali na kumpatia simu mzee yule alikuwa kakaa siti ya nyuma kwenye gari
Mpaka sasa walikuwa bado hajui mzee anaitwa nani na kilicho washangaa sana ni baada ya kumpa simu maongezi yaliyoenda walibaki na maswali mengi
“Naam” mzee alishika simu huku akiitika
“Ndio”
“Hapna”
“mh”
“Ndio”
“Ndio”
“Sawa” Alimaliza na kuludisha simu kwa afande baraka
Sababu walikuwa hawawezi kuskia alichokuwa anaongea veronica waliishia kuskia majibu ya mzee tu ambayo walishangaa kwani walikuwa wanazungumza nini
Afande Baraka aliwasha gari na kuondoa kuelekea kijijini
“una mahusiano na veronica” Swali ambalo liliwafanya wote wageuke nyuma na kumwangila mzee
“ Hapana mimi na mke” afande mwita alijuwa swali lilikuwa linamlenga yeye basi alijibu
“unamwonaje kwenye kazi yake anaweza” aliuliza kwa mara nyingine tena
“Ndio anaweza ni mwanamke ambae kiukweli huwa ananishangaza sana an
aujasiri sijui kalisi kwa nani”
“na huwa ni mtu anajari kila mtu”aliongezea
“Sasa kwa nini cheo chake hakipandi siku zote”
Afande mwita alishindwa kujibu ilo swali na kubaki akimwangali mzee kupitia kioo cha mbele ya gari
“Lakini huwa anatabasamu sana akiona simu ya veronica” alikuwa ni afande baraka akiwa anajaribu kupunguza ukimya uliokuwa umetawala
“Embu acha masihara”
“Kwani uongo” Afande baraka aliuliza kwa matani tena lakini afande mwita hakujibu kitu alitabasamu tu.
Safari ikiwa inaendelea waliskia sauti kwa mbali ikipiga kelele afande baraka alifunga breki na kusimamisha gari waliskiliza kwa makini ni kweli kelele hizo zilikuwa zipigwa sio mbali na hapo basi walishuka na kuelekea mpka eneo la tukio walikuta watu wamekusanyika wengi afande mwita kutazama vizuri aliona mtu akiwa amelala kifudifudi kwenye maji kando kando ya dimbwi huku mwita akisogeza watu pembene kidogo afande mwita alipima kama mtu huyu bado yupo hai kwa kuweka vidole shingoni aligundua mtu yule kashafariki mda alisimama na kuendelea kuangalia mazingira yale alioona watu wawili wakiwa kwa mbali sana mmoja akiwa yuko ndani ya nguo aina ya suti alikuwa ni mwanaume mweye urefu inch 7 na akiwa na miwani pia rangi yake ilikuwa maji ya kunde sababu alikuwa basi hakuona sura yake vizuri afande alimtazama sana kisha kumwita afande baraka waje wasaidiane kuubeba mwili ule.
Walipo ugeuza mwili alikuwa ni binti wa umri kama miaka 25 afande baraka alirudi kwenda kusogeza gari iliwaze kuuweka mwili kwenye gari yao inayofamika kama defender alipoweka gari alishuka pamoja na yule mzee alimfuata nyuma kusaidiana kubeba maiti ya yule dada walipo maliza kuweka ilibidi afanye utaratibu watu watawanyike
“Naomba tuskilizane” afande mwita aliongea kwa sauti ya juu
“Kwa usalama wa kila mmoja wetu naomba turudi kwenye majumba yote tukae ndani” Basi alitoa maagizo hayo na watu walitawanyika na wao walipanda gari na kuondoa hata ivyo walikuwa wameshafika kijijini huku afande mwita akiwa na maswali mengi nani atakuwa anahusika na kwa nini wamtupe mtoni alishuka haraka kwenye gari na kuelekea chumbani akiwa anafungua mlango simu yake ya mkononi iliita alitoa mfukoni na kuangalia alikuwa ni imeandikwa “Wife” alipokea
“Jamani we mwanaume unataka kunitoa roho mimi” ilikuwa ni sauti ya mke wake kwenye simu akiuliza
“Hapana”
“Umeamkaje”afande mwita akaongezea baada ya kukataa sio kweli
“Sitaki” mke wake alijibu kwa kinyonge
“Nisamehe mpenzi wangu”
“kweli toka jana usiku hupokei simu”
“nilifika nimechoka alfu nimeamka na kazi kidogo”
“Sawa “
“umesha…” mke wake akiwa anataka kusema kitu ghafla afande baraka alikuja chumban na kumwita
“kaka njoo uone kitu mara moja” afande baraka alihitaji afande mwita aje aone kitu ambacho wenda anaweza toa msaada wowote
“Ntakupigia baada sawa kipenzi changu”
“Nakupenda , bye” alimalizia na kukata simu huku akitoka chumbani kwenda kuangalia nini afande baraka anamwitia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom