Waliopania kumshitaki Dk. Slaa waendelea kujiandaa?
na Happiness Katabazi
HADI jana hakuna hata mmoja miongoni mwa watu waliotajwa wakituhumiwa kuwa ni mafisadi, aliyekuwa ametekeleza azima ya kumfungulia mashitaka Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa.
Watu hao, akiwamo Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, Katibu Mkuu katika Wizara ya Fedha, Gray Mgonja, na Patrick Rutabanzibwa, walishatangaza azima yao ya kumfungulia Dk. Slaa mashitaka kwa madai kuwa alikuwa amewakashifu kwa kuwatuhumu kuwa ni mafisadi.
Akihutubia umati uliofurika katika mkutano wa hadhara katika viwanja vya Mwembeyanga, Dk. Slaa alitoa orodha ya watu 11 aliowatuhumu kuwa ni mafisadi na wabadhirifu wa mali ya umma.
Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima kuanzia Septemba 18 hadi jana katika Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na mahakama za wilaya jijini hapa, umegundua kwamba hakuna hata mmoja aliyekwishatekeleza azma hiyo.
Siku chache baada ya Dk. Slaa kutaja majina hayo, baadhi ya watuhumiwa hao walikana tuhuma hizo na kusema ni za uongo na kuahidi kumfungulia kiongozi huyo kesi ya kashfa kwani amewachafulia majina.
Kwa upande wake, Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono (CCM), alishasema wazi kuwa hatomshitaki Dk Slaa, wakati Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge, alisema kwamba tuhuma hizo ni utumbo mtupu na hakusema atamfikisha mahamakani.
Wakati akizungumza na waandishi wa habari, Karamagi alisema kuwa atafungua kesi hiyo katika kipindi kisichozidi saa 48, lakini ni zaidi ya wiki sasa na bado hajatekeleza azma yake.
Alipoulizwa na gazeti hili wiki iliyopita, alisema bado dhamira yake ipo pale pale na alikuwa anajiandaa kufungua kesi hiyo.
Hata hivyo, baadhi ya watu waliliambia gazeti hili kuwa suala hilo ni gumu kutokana na mtego uliowekwa na Dk Slaa, ambaye hajaweka bayana aina ya ushahidi alionao dhidi ya watu anaowatuhumu.
Hata wao waliotuhumiwa wana hofu kuwa iwapo suala hili litafikishwa mahakamani, kuna uwezekano wa mambo mengine mengi kufichuka na kuzidi kuwagandamiza, alisema mwanasheria mmoja ambaye hakupanda jina lake litajwe gazetini.
Hata hivyo, wakili mwingine, Robert Rugemalila, alisema kitendo cha watuhumiwa hao kushindwa kwenda mahakamani hadi sasa kinaleta hisia kwa wananchi kuwa huenda tuhuma zilizotolewa na Dk. Slaa zina ukweli ndani yake.
Hawa wana uwezo wa kifedha wa kuweka wanasheria wazuri wa kuendesha kesi zao sasa ni kitu gani kinachowakwamisha hadi kumfikisha mahakamani Dk.Slaa wanayesema amewachafulia majina yao?
Haiingii akili kabisa mtu akuvunjie heshima na kukuchafulia jina mbele ya jamii halafu ukae kimya na ushindwe kumpeleka mahakamani, kwa hili serikali na watuhumiwa hao wanawahaada wananchi, alisema Rugemalila.
Source:Tanzania Daima.
Dr. Slaa alitega bomu,je ni nani wa kulilipua au walikua wanamsubiria Kikwete?
na Happiness Katabazi
HADI jana hakuna hata mmoja miongoni mwa watu waliotajwa wakituhumiwa kuwa ni mafisadi, aliyekuwa ametekeleza azima ya kumfungulia mashitaka Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa.
Watu hao, akiwamo Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, Katibu Mkuu katika Wizara ya Fedha, Gray Mgonja, na Patrick Rutabanzibwa, walishatangaza azima yao ya kumfungulia Dk. Slaa mashitaka kwa madai kuwa alikuwa amewakashifu kwa kuwatuhumu kuwa ni mafisadi.
Akihutubia umati uliofurika katika mkutano wa hadhara katika viwanja vya Mwembeyanga, Dk. Slaa alitoa orodha ya watu 11 aliowatuhumu kuwa ni mafisadi na wabadhirifu wa mali ya umma.
Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima kuanzia Septemba 18 hadi jana katika Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na mahakama za wilaya jijini hapa, umegundua kwamba hakuna hata mmoja aliyekwishatekeleza azma hiyo.
Siku chache baada ya Dk. Slaa kutaja majina hayo, baadhi ya watuhumiwa hao walikana tuhuma hizo na kusema ni za uongo na kuahidi kumfungulia kiongozi huyo kesi ya kashfa kwani amewachafulia majina.
Kwa upande wake, Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono (CCM), alishasema wazi kuwa hatomshitaki Dk Slaa, wakati Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge, alisema kwamba tuhuma hizo ni utumbo mtupu na hakusema atamfikisha mahamakani.
Wakati akizungumza na waandishi wa habari, Karamagi alisema kuwa atafungua kesi hiyo katika kipindi kisichozidi saa 48, lakini ni zaidi ya wiki sasa na bado hajatekeleza azma yake.
Alipoulizwa na gazeti hili wiki iliyopita, alisema bado dhamira yake ipo pale pale na alikuwa anajiandaa kufungua kesi hiyo.
Hata hivyo, baadhi ya watu waliliambia gazeti hili kuwa suala hilo ni gumu kutokana na mtego uliowekwa na Dk Slaa, ambaye hajaweka bayana aina ya ushahidi alionao dhidi ya watu anaowatuhumu.
Hata wao waliotuhumiwa wana hofu kuwa iwapo suala hili litafikishwa mahakamani, kuna uwezekano wa mambo mengine mengi kufichuka na kuzidi kuwagandamiza, alisema mwanasheria mmoja ambaye hakupanda jina lake litajwe gazetini.
Hata hivyo, wakili mwingine, Robert Rugemalila, alisema kitendo cha watuhumiwa hao kushindwa kwenda mahakamani hadi sasa kinaleta hisia kwa wananchi kuwa huenda tuhuma zilizotolewa na Dk. Slaa zina ukweli ndani yake.
Hawa wana uwezo wa kifedha wa kuweka wanasheria wazuri wa kuendesha kesi zao sasa ni kitu gani kinachowakwamisha hadi kumfikisha mahakamani Dk.Slaa wanayesema amewachafulia majina yao?
Haiingii akili kabisa mtu akuvunjie heshima na kukuchafulia jina mbele ya jamii halafu ukae kimya na ushindwe kumpeleka mahakamani, kwa hili serikali na watuhumiwa hao wanawahaada wananchi, alisema Rugemalila.
Source:Tanzania Daima.
Dr. Slaa alitega bomu,je ni nani wa kulilipua au walikua wanamsubiria Kikwete?