Hadi leo najiuliza, ilikuwaje tukajenga SGR kwenda Burundi na kuacha kuboresha TAZARA kuwa SGR ambapo tungefika Congo kirahisi sana

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,221
26,031
Siku Saba zilizopita shirika la habari la Ujerumani DW wametoa makala nzuri sana kuelezea upekee wa Reli ya Tazara inayotoka Tanzania hadi Ndola nchini Zambia.

Wameelezea upekee wa reli hii na namna inavyopita kwenye mbuga maarufu za Selous na Mikumi na inavyopita mwenye milima ya Iringa hadi kuingia Zambia.

Waandaaji wa Makala hii wamehoji sana uchakavu wa reli hii na namna ambavyo serikali za nchi zetu zimeipuuza na kiufanya ichakae sana na kutoleta matunda yaliyokusudiwa!

Baada ya kuiona Makala hii nimegundua kuwa Reli ya Tazara inafika hadi Zambia ambapo Kuna urefu wa kilomita chache sana Kwenda Congo ambazo Pia zimeunganishwa na reli nyingine Kwenda Congo, Mji wa Lubumbashi ambao ni mji Mkuu wa kibiashara.

Kwa ninavyojua reli ya kati kwa Kiwango cha SGR mpaka mwanza na Kigoma itagharimu kiasi cha Trilioni si chini ya 25 kwa ujumla wa vipande vyote.

Jambo lililonishangaza ni kuwa tayari Reli ya Tazara inafika hadi Ndola Zambia na kuna Reli nyingine inafika hadi Lubumbashi , Congo kutoka Zambia.

Je haikuwa sahihi kwetu kuboresha Reli ya Tazara kwa Kiwango cha SGR na kuiwekea umeme na kuongea na Zambia kidiplomasia tukawakopesha hela za kuboresha reli kutoka Zambia hadi Lubumbashi Congo kwa Kiwango cha SGR?

Kwa mtazamo wangu naona gharama za kuboresha Reli ya Tazara kwenda Congo kwa Kiwango cha SGR ingekuwa ndogo sana kuliko kuijenga upya hadi Burundi na kuanza kuongea na Burundi ili waifikishe Congo jambo ambalo sidhani kama litakamilika hivi karibuni kutokana na hali ya kiuchumi ya Burundi! Na uhohehae wao kutokana na vita!

Nauliza swali hili kwenu wadau! Je kulikuwa na haja Kweli ya kujenga Reli ya SGR kwenda Kigoma na Mwanza? Au Tungeboresha tu TAZARA kuwa Kiwango cha SGR ambapo tungetumia gharama ndogo na kufika Congo kirahisi sana?



Hii ndo ramani ya Zambia inavyoonesha ukaribu wa Zambia na Lubumbashi Congo na urahisi wa kufika Congo kupitia reli ya TAZARA

CF09BAF9-37EA-4BC4-8FF2-4A60CC015512.jpeg
 
Reli ya TAZARA alijenga kihistoria, Mkopo wa ujenzi wa Reli hii ulikamilika kulipwa awamu ya 5 ila hatujui mikataba iliyokaingiwa huko nyuma maana mchina nae mjanja lazima alichungulia fursa ya miaka 100 mbele.

Reli ya kati mkakati wake ni mizigo pamoja na abiria, ni Rahisi sana kupata abiri kwa reli ya kati kuliko Tazara japo sisemi kuwa si bora.

Reli ya kati itaenda kutuunganisha na kuboresha biashara kati ya Tanzania na Uganda, Tanzania na Rwanda, Tanzania na Burunduni pamoja na Congo

Kuna inchi kama 4 hapo ambazo zitarahusisha biashara na ndiyo maana awamu iliyopita iliwekeza sana kwenye miundombinu na usafirisha mpaka kwenye maji na ndiyo maana uliona MV Victoria kule Ziwa Victoria inaanza na nyingine inaendelea kuundwa, Ziwa Nyasa pia na Tanganyika.

Issue ni Strategic Plan tu
 
Siku Saba zilizopita shirika la habari la Ujerumani DW wametoa makala nzuri sana kuelezea upekee wa Reli ya Tazara inayotoka Tanzania hadi Ndola nchini Zambia....
Nijuavyo Mimi Reli ya Tazara Ni Standard Gauge Railway (SGR) ndio maana hata Train za South Africa huwa zinakuja kwa kutumia SGR ya Tazara kasoro ya Tazara sio Electrified Railway
 
Siku Saba zilizopita shirika la habari la Ujerumani DW wametoa makala nzuri sana kuelezea upekee wa Reli ya Tazara inayotoka Tanzania hadi Ndola nchini Zambia...
Treni ya kisasa blue train ya South Africa huwa inakuja Tanzania na watalii, kwahiyo tatizo la Tazara siyo reli.

Pia uelewe Tazara ni Tanzania na Zambia kuna protocal lazima mkubaliane na mkurugenzi mkuu ni lazima awe Mzambia.
 
Reli ya TAZARA alijenga kihistoria, Mkopo wa ujenzi wa Reli hii ulikamilika kulipwa awamu ya 5 ila hatujui mikataba iliyokaingiwa huko nyuma maana mchina nae mjanja lazima alichungulia fursa ya miaka 100 mbel...
Reli ya Kati haifiki Kagera inaenda Mwanza ambapo kufika Uganda lazima upande tena meli na kusafiri si chini ya masaa 24!

Reli ya kati SGR imeenda Mwanza na Kigoma na hapo hakuna tena Reli kwenda Burundi!

Kulikuwa na haja gani kujenga Reli ya kati kwa Kiwango cha SGR?
 
Treni ya kisasa blue train ya South Africa huwa inakuja Tanzania na watalii, kwahiyo tatizo la Tazara siyo reli.

Pia uelewe Tazara ni Tanzania na Zambia kuna protocal lazima mkubaliane na mkurugenzi mkuu ni lazima awe Mzambia.
Na makao makuu lazima yawe Tanzania!
 
Treni ya kisasa blue train ya South Africa huwa inakuja Tanzania na watalii, kwahiyo tatizo la Tazara siyo reli.

Pia uelewe Tazara ni Tanzania na Zambia kuna protocal lazima mkubaliane na mkurugenzi mkuu ni lazima awe Mzambia.
Izo Protokali ndo zimezuia kuboresha reli ya Tazara kuwa SGR?

Mbona hoja zako nyepesi sana?
 
bado hata tazara haihitaji kujengwa kuwa sgr. Tazara ni cape gauge ambayo bado ni modest sana. tatizo ni siasa zetu za kiafrica. Siasa ya ccm imeisusa tazara ambayo inafeed nchi kama zambia na southern drc na imeikumbatia rwanda yenye ukubwa wa 26,000kmsq kama mkoa wa Tanga. Ni aibu sana.
Very bold

Siasa inapeleka sgr kwenda Rwanda na burundi nchi ambazo hazina zinacho exoprt
Sgr.

Hata ikifika huko itakuwa inarudi na mabehewa empy kama maroli ya rwanda, burundi ,shinyanga na mwanza yanavyorudi Dar.
 
bado hata tazara haihitaji kujengwa kuwa sgr. Tazara ni cape gauge ambayo bado ni modest sana. tatizo ni siasa zetu za kiafrica. Siasa ya ccm imeisusa tazara ambayo inafeed nchi kama zambia na southern drc na imeikumbatia rwanda yenye ukubwa wa 26,000kmsq kama mkoa wa Tanga. Ni aibu sana.
Hoja yako inafikirisha sana
 
TAZARA - Tanzania to Zambia

Reli mpya ya SGR - Tanzania to Rwanda, Burundi, Uganda na target ni kuwaunganisha DRC na wasudani (kupitia Uganda).

Nadhani tofauti ni kubwa!
SGR haiendi Uganda!
Inaishia Mwanza!

Kama target ni Congo , kulikuwa na haja gani kuipeleka Burundi na Rwanda tena kwa gharama kubwa sana?

Kwa nini tusingeboresha TAZARA na kufika Congo kirahisi sana?
 
Afrika mtu akiwa cheti anafanya kazi na kujituma sana.

Akipata Diploma anaongeza juhudi na ubunifu na kufanya kazi Kwa uaminifu .

Akipata digrii Moja anafanya kazi Kwa majivuno.

Akipata mastars anafanya kazi Kwa majivuno na dharau. Akipata PhD anafanya kazi Kwa mikataba,vikao na kuangalia maslahi tuu.

Bila posho hafanyi kazi. Yaani PhD yake ni ya kupata mshahara mkubwa na marupurupu basi na anafanya kazi Kwa muda kidogo huku akisema kuwa afadhali Sasa napata mshahara mkubwa Kwa kazi kidogo,Tena ya kufanyiwa na walioko chini yake.

Akiwa Professor anaingia Jalalani na kuanza upya kama ombaomba mitaani ,tofauti yake ni kuwa ombaomba Kwa wakuu wenye kuweza kumtoa Jalalani na kumpa neema ya maisha Bora.

Mchezo unaishia hapo anakua ni mtu wa kusifu na kuabudu wanadamu wenzake Tena wenye Elimu ndogo kuliko yeye.

Usitegemee wasomi na watawala wa afrika wafanye jambo lenye maslahi mapana Kwa Taifa zaidi ya kuangalia matumbo yao. Miradi mikubwa Ina pesa nyingi sana za wizi.

Kila mtawala anawaza miradi mipya na kutelekeza miradi iliyoko tayari na inayozalisha. Mfano Mradi wa gesi.

Wapya walikuja wakautelekeza mradi wa gesi na kuturudisha wanakotaka wao kisa walituaminisha kuwa mradi wa gesi una ifisadi lakini hawawachukulii hatua hao waliofanya ifisadi.

Reli ya TAZARA ni standard G Railwas imekosa umeme tu kuendesha train ya umeme.
 
Back
Top Bottom