Hadharani: Shigongo Alivyomsema Rais Magufuli Kijasiri Marekani

Sir Lindege

Member
Sep 10, 2013
34
180


MKURUGENZI Mtendaji wa Makampuni ya Global Group, Eric Shigongo amempongeza Rais Dk John Pombe Magufuli kwa uamuzi wake wa kipekee wa kutoifunga Tanzania (lockdown) katika kipindi hiki cha Ugonjwa wa COVID-19 na kuwataka wananchi wake kuendelea kuchapa kazi huku wakichukua tahadhari za kujikinga na janga hilo kama mamlaka za afya zinavyoelekeza ili kunusuru uchumi wa Taifa letu.

Akizungumza na Shirika la Habari la Sauti ya Amerika (Voice of America- VoA), Shigongo amesema uamuzi wa Rais Magufuli ni wa kijasiri kwa kiongozi yeyote shupavu na kwamba hali hiyo imesaidia kwa kiasi kikubwa kutokushusha uchumi wa Taifa licha ya janga hilo kutikisa dunia nzima.

“Kwa kweli ninaweza kusema Rais Magufuli ana maono makubwa, amesema siwezi kukopi na kupesti njia wanazotumia wengine, badala yake ni kuwaruhusu wananchi waendelee kuchapa kazi huku wakichukua tahadhari. Jifikirie Tanzania ifungwe hata kwa miezi mitatu au sita, hali ya uchumi wake itakuwaje? Sisi tutaendelea kumuunga mkono kwa kila jema anachokifanya kwa manufaa ya Tanzania yetu," alisema Shigongo.

Akizungumzia hali ya biashara katika janga hili la Corona, Shigongo amesema Global Publishers imeanzisha mifumo mbalimbali ya biashara zake mitandaoni kwa njia za kidijitali ambapo wasomaji wa magazeti yote yanayochapishwa na kampuni hiyo; Uwazi, Amani, Risasi, Ijumaa, Ijumaa Wikienda, Championi na Spoti Xtra sasa wanaweza kuyapata kupitia Application ya Global App wakanunua na kusoma kirahisi kabisa kwa njia ya simu au kompyuta zao hata kama wakiwa nyumbani.

Licha ya hivyo, Shigongo amebainisha pia kuwa, Global Group ina Televisheni ya Mtandaoni ya Global TV Online na Radio ya Mtandaoni ya +255 Global Radio, kurasa za mitandao ya kijamii ya Facebook, Twitter na Instagram ambazo zote kwa pamoja zimekuwa zikiwapasha habari wananchi kwa njia ya mtandao.

Akijibu swali la Mtangazaji wa VoA, Paul Ndiho kuhusu iwapo ataingia kwenye siasa mwaka huu, Shigongo amesema ikimpendeza Mungu atagombea Ubunge katika Jimbo la Buchosa, Sengerema mkoani Mwanza kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu (2020).

“Ikimpendeza Mungu nitawawakilisha Bungeni wananchi wenzangu wa Jimbo la Buchosa kupitia chama changu cha Mapinduzi (CCM), ninaaamini ninao uwezo mkubwa wa kuongoza, wananchi wa Buchosa wananihitaji niwatumikie, kupitia Ubunge nitaweza kupaza sauti zao na kuwasemea Bungeni..... na kwa kuishirikiana na Serikali yetu pendwa kupeleka maendeleo makubwa Buchosa na Tanzania kwa ujumla,” alisema Shigongo.

 
2397479_2396248_20200511_084948.jpg
 
Angeendelea kutaja na takwimu ili na hao waliojifungia pengine kwa woga tu waone ufanisi wa hii "CHAPENI KAZI KWA TAHADHARI"

Na pengine hata wenyewe ingetusaidia kujua muenendo wa ugonjwa ili shule na vyuo viendelee kuchapa masomo kwa tahadhari.
 
Unategemea aseme nini? Tofauti ha hilo wakati anafukuzia kuteuliwa! Jitu zima hovyo kabisa!
Ana bahati mbaya,huwa anapigwa chini kwenye kura za maoni jimbo la busanda Geita,safali hii aneanza kulamba miguu mapema ili aonekane.
 
Unategemea aseme nini? Tofauti ha hilo wakati anafukuzia kuteuliwa! Jitu zima hovyo kabisa!
Wewe ndio hovyo!! Kwani hujasikia mataifa kibao yameamua kuachana na lockdown japo maambukizi mapya yaki juu? Trump mwenyewe ameruhusu majimbo kuachana na lockdown wakati Jana tu maambukizi mapya kwa siku yalikuwa 27,000 na vifo vipya takriban 1,700!!,
Hata WHO wamesema tujiandae kuishi na corona cha maana kuzingatia taratibu za kujikinga wakati maisha yanaendelea!! Wanafuata kwa kuchelewa kitu ambacho Magufuli alikiamua tangu mwanzo!! Wasipomtambua na kumpongeza leo historia itamtambua!!
 



MKURUGENZI Mtendaji wa Makampuni ya Global Group, Eric Shigongo amempongeza Rais Dk John Pombe Magufuli kwa uamuzi wake wa kipekee wa kutoifunga Tanzania (lockdown) katika kipindi hiki cha Ugonjwa wa COVID-19 na kuwataka wananchi wake kuendelea kuchapa kazi huku wakichukua tahadhari za kujikinga na janga hilo kama mamlaka za afya zinavyoelekeza ili kunusuru uchumi wa Taifa letu.

Akizungumza na Shirika la Habari la Sauti ya Amerika (Voice of America- VoA), Shigongo amesema uamuzi wa Rais Magufuli ni wa kijasiri kwa kiongozi yeyote shupavu na kwamba hali hiyo imesaidia kwa kiasi kikubwa kutokushusha uchumi wa Taifa licha ya janga hilo kutikisa dunia nzima.

“Kwa kweli ninaweza kusema Rais Magufuli ana maono makubwa, amesema siwezi kukopi na kupesti njia wanazotumia wengine, badala yake ni kuwaruhusu wananchi waendelee kuchapa kazi huku wakichukua tahadhari. Jifikirie Tanzania ifungwe hata kwa miezi mitatu au sita, hali ya uchumi wake itakuwaje? Sisi tutaendelea kumuunga mkono kwa kila jema anachokifanya kwa manufaa ya Tanzania yetu," alisema Shigongo.

Akizungumzia hali ya biashara katika janga hili la Corona, Shigongo amesema Global Publishers imeanzisha mifumo mbalimbali ya biashara zake mitandaoni kwa njia za kidijitali ambapo wasomaji wa magazeti yote yanayochapishwa na kampuni hiyo; Uwazi, Amani, Risasi, Ijumaa, Ijumaa Wikienda, Championi na Spoti Xtra sasa wanaweza kuyapata kupitia Application ya Global App wakanunua na kusoma kirahisi kabisa kwa njia ya simu au kompyuta zao hata kama wakiwa nyumbani.

Licha ya hivyo, Shigongo amebainisha pia kuwa, Global Group ina Televisheni ya Mtandaoni ya Global TV Online na Radio ya Mtandaoni ya +255 Global Radio, kurasa za mitandao ya kijamii ya Facebook, Twitter na Instagram ambazo zote kwa pamoja zimekuwa zikiwapasha habari wananchi kwa njia ya mtandao.

Akijibu swali la Mtangazaji wa VoA, Paul Ndiho kuhusu iwapo ataingia kwenye siasa mwaka huu, Shigongo amesema ikimpendeza Mungu atagombea Ubunge katika Jimbo la Buchosa, Sengerema mkoani Mwanza kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu (2020).

“Ikimpendeza Mungu nitawawakilisha Bungeni wananchi wenzangu wa Jimbo la Buchosa kupitia chama changu cha Mapinduzi (CCM), ninaaamini ninao uwezo mkubwa wa kuongoza, wananchi wa Buchosa wananihitaji niwatumikie, kupitia Ubunge nitaweza kupaza sauti zao na kuwasemea Bungeni..... na kwa kuishirikiana na Serikali yetu pendwa kupeleka maendeleo makubwa Buchosa na Tanzania kwa ujumla,” alisema Shigongo.


Kumbe Shigongo ni Musukuma wa hukohuko haishangazi kutoa sifa namna hiyo kwa mtu wa hukohuko aliyejificha hukohuko akijifukiza kujikinga na Covid-19. Mkorogo wa Madagascar bado haujasaidia tu atoke mafichoni?
 
Who is Trump? Trump hana tofauti na Jiwe kwa taarifa yako. Kama unasikliza CNN obsevers views hatapata tena kuchaguliwa kwa jinsi alivyo handle hii pandemic in USA!
Hata 2016 walisema hatachaguliwa lakini akachaguliwa!! Vyombo vya habari ndivyo vinampiga vita lakini wananchi wanamkubali!! Huyo CNN si mpiga kura!!
 
Unasikiliza TBC1 ndilo tatizo lako!
Ingia Worldometer uthibitishe hizo takwimu nilizokuwekea!! Hata TBC1 iko vizuri!! Mwana hujisifia vitu vilivyopo nyumbani, lakini mtumwa hana furaha na kitu chochote cha nyumbani. Watumwa wa mabeberu utawatambua tu!!
 
Lazima kuanza kujikomba komba mapemaa tenda la kofia na Tshirts za CCM uchaguzi ushakaribia huu
 
Back
Top Bottom