Habinder Sethi aomba msamaha na kukiri makosa yanayomkabiri ya Uhujumu Uchumi

Habinder Seth, anayekabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi amemuandikia barua mkurugenzi wa mashtaka (DPP) kukiri makosa na kuomba msamaha, wakili wake Michael Ngalo ameieleza Mahakama ya Kisutu leo.

---
Harbinder Sethi anayekabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi ameandikia barua kwenda kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kukiri makosa yake na kuomba msamaha

Wakili wake, Michael Ngalo amesema hayo leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Huruma Shaidi wakati kesi hiyo ilipotajwa

Sethi, Mwenyekiti Mtendaji wa PAP pamoja na James Rugemalira ambaye ni Mkurugenzi wa VIP wanakabiliwa na mashtaka 12 wanayodaiwa kuyatenda jijini Dar, Afrika Kusini, Kenya na India

Wakili wa Jamhuri, Wankyo Simon ameeleza kuwa wamepokea barua ya Seth wanaifanyia kazi na majibu yatatolewa ila kuhusu upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika

Miongoni mwa mashtaka yao ni kujihusisha na mtandao wa uhalifu, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu, kutakatisha fedha na kusababisha hasara ya Dola za Marekani 22,198,544.60 na Tsh. Bilioni 309.

Puto halijafanyiwa usafi mda mrefu sana itakuwa limechafuka sana. Shikamoo JPM. Hao ilikuwa hawaguswi na mtumishi wa serikali ukiwagusa unaharibikiwa.
 
Kumshinikiza mtu akiri kosa ni failure kubwa sana kwamba wameshindwa kuja na fact za kumshtaki, sema ni kwa vile upande unao shinikiza una nguvu so no way out mtu anakaa ndani miaka na miaka upelelezi hauishi kwani kuna nn? kwaio wameshindwa kuja na hoja wana bana ukubali what if umeonewa? anywai acha akiri tu atoke maana uko aliko sio kuzuri
Hawajashinikizwa, unaomba mwenyewe msamaha na kukiri alafu unarudisha pesa! Kama huwezi kukiri na kurudisha pesa, basi kesi inaendelea na wapo ambao hawajakiri makosa na wanaendelea na kesi kama kawaida!
 
Hivi hizo hela huwa zinarudi kweli au maneno tuu kuonyesha ushujaa wa kushinda kila kitu
 
Mbona lile tumbo la puto halipo tena? Au ndio mazoezi hayo? Mzee atakuwa amefaidika sana kutoa hilo tumbo bila upasuaji, pamoja na hasara ya pesa atakzorudisha ila atakuwa na faida ya kiafya.
Dah kweli aiseh! Aliingia na shepu ya pipa anatoka amenyooka kama muwa!
 
Mwenye akili timamu lazima akubali hata kama hakufanya kosa. Hakuna namana mahakamani hakuna haki ukikataa ndo kwanza unaongeza hasira kwa Mtukufu utafia jela!
Nasubiri kusikia wote 2 wamerudisha zile bil 309!!
 
Mwenye akili timamu lazima akubali hata kama hakufanya kosa. Hakuna namana mahakamani hakuna haki ukikataa ndo kwanza unaongeza hasira kwa Mtukufu utafia jela!
Nasubiri kusikia wote 2 wamerudisha zile bil 309!!
Rugemalila yeye bado amekomaa
 
Kafanya la maana Sana akitutajia aliowagawia rushwa na kutupatia vielelezo wamwachie maramoja, tkkr mtumieni huyu Kama shahidi namba moja.
Pesa irudi. Isijekuwa kuna mchezo umebuniwa na wakubwa kupiga pesa.
 
Ingelikuwa ni vyema hao waliotuhumiwa, masharti ya kukiri iwe ni pamoja na kuchoma ramani nzima ya vita...

Waeleze ni namna gani walikuwa wakihujumu uchumi, na wamekuwa wakishirikiana na kina nani...
Wakiweka masharti hayo yataumbua wengi sana waliopo sarikalini hivi sasa.

Yaani itakuwa ni aibu.

Viongozi wengi wamepatikana kifisadi, kwa hiyo wengi wataumbuka.

Lakini kama tumeamua kujenga Tz mpya, tungefanya kama walivyofanya S.Africa ya Mandela baada ya utawala wa ubaguzi wa rangi, iliundwa kamati ya maridhiano.

Waliotubu bila kujali walifanya kosa gani la kibaguzi, walisamehewa, na waliodinda wakaadhibiwa.

Kwa hiyo na sisi kama unavyoshauri mkuu, wangetajana angalau raia tukaambulia kuwatambua ikatosha.
 
Seth na Rugemalira ndio walikuwa walengwa wakubwa wa msamaha huu.
"wengine wamekonda kweli"
Alisikika akijisemea Rais mmoja huko Afrika mashariki.
Na siyo utani, kwa picha hiyo Seth na huyo mwenzake Ruge wamekonda na kuzeeka sana, tofauti na picha walivyoingia!
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom