Wadau nimekufa ganzi asubuhi hii baada ya kuona gazeti la mtanzania la leo,limeandika habari za matusi makubwa dhidi ya Chadema.Limeandika kwamba Chadema wamevurugana kwa sababu ya udini waliouanzisha,pili wamesema vurugu za Arusha wamewahadaa wananchi kwa sababu ya udini wao na tatu wanasema mauaji ya Arusha yamesababishwa na Chadema.Ni habari mbaya kwa mtu yeyote akisoma.Habari hii kwa jinsi ilivyoandikwa nikihusisha na kipindi maalum kilichorushwa na ITV juzi inaonekana kuna mkakati maalum umesukwa wa kuichafua na kuiangamiza Chadema.Yeyote anayeweza kulipata hilo gazeti alisome aone hayo matusi.....kwa uandishi huu sijui kama tutafika.