Utotole
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 6,604
- 4,259
Mimi bado haijaniingia akilini kwa nini [kama ni kweli] hao wahusika waliongea na kituo cha redio.
Walifanya hivyo kwa minajili gani?
Nani mwenye akili timamu anaweza kuongelea suala la fedheha namna hiyo kwenye chombo cha habari?
Akili yangu imegoma kabisa hapo.
Halafu sasa...hizo picha mbona kama zipo mtandaoni tokea zamani.
Nakumbuka kama nilishawahi kuziona pahala [Kanusho: mimi siyo kwamba ni mdau wa hayo mapicha na masinema ya ngono. Kwenye hizi zama za utandawazi kukutana na hayo makitu ni jambo la kawaida].
...halafu picha zenyewe haziendani na zama ambazo zinatajwa kwenye audio clip, yaani miaka saba tokea sasa kurudi nyuma yaani 2009.
Mwanadada mwenyewe anaonekana akichezea smartphone ya halotel, mtandao uliongia nchini mwaka jana tu. Kifupi yale mapicha hayahusiani na story ya redioni.
Na sasa, kama story zenyewe za redioni ni za kutunga au za kweli it's a different matter
Kifupi naona kuna michezo isiyoeleweka mitandaoni.