Habari njema kwa wapenda ngono !!!!

KadaMpinzani

JF-Expert Member
Jan 31, 2007
3,715
86
‘Chanjo ya ukimwi yaonyesha mafanikio'


na Lucy Ngowi

MRADI wa utafiti wa chanjo ya ukimwi unaosimamiwa na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kwa ushirikiano na Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba Muhimbili (MUCHS), unaendelea vizuri, kwa kuwa haujaleta madhara yoyote kwa wote waliofanyiwa chanjo hiyo.

Mtafiti Mkuu wa majaribio ya kuchunguza usalama kwa binadamu na uwezo wa chanjo hiyo kujenga kinga mwilini, Profesa Freddy Mhalu, alieleza hayo jana alipozungumza na Tanzania Daima.

Profesa Mhalu, alisema mradi huo unaendelea vizuri kwa kuwa nusu ya watu waliotegemewa kufanyiwa majaribio wamepatikana na hakujatokea madhara ya aina yoyote.

"Dalili nzuri ya uwezo wa hiyo chanjo kuweza kujenga kinga mwilini zimeanza kuonekana," alisema Profesa Mhalu.

Kwa mujibu wa Profesa Mhalu, utafiti huo utaendelea mpaka mwaka 2009. "Kupata chanjo itachukua muda mrefu na majaribio mengi kabla haujapatikana ufumbuzi, hivyo itahitaji uvumilivu," alisema.

Alisema tatizo wanalokabiliana nalo katika kipindi hiki cha utafiti, ni kutokana na kusambaa kwa fununu zisizo za kweli kwamba wanapofanya majaribio hayo, wanawaachia virusi vya ukimwi watu waliokubali kuchanjwa, jambo ambalo amesema halina ukweli wowote.
 
It is too early to celebrate. I know so many drug companies in developed countries have tried to come up with the same solution but without any success....JUST WRAP IT UP!
 
hii kitu itatoka tanzania, na ikitokea tanzania yaani bab kubwaaaaaaa !
usije ukashangaa nchi zote zilizojaribu zimeshindwa, ikaja tanzania ikawin !
 
hii kitu itatoka tanzania, na ikitokea tanzania yaani bab kubwaaaaaaa !
usije ukashangaa nchi zote zilizojaribu zimeshindwa, ikaja tanzania ikawin !

It is too early to celebrate, JUST WRAP IT UP. There is no love without protection.
 
KadaMpinzani;87044“Dalili nzuri ya uwezo wa hiyo chanjo kuweza kujenga kinga mwilini zimeanza kuonekana said:
Mind you.. Prof Mhalu hajasema kwamba dalili hizo nzuri "zimethibitishwa"... Kasema kwamba "zimeanza kuonekana".
 
Mwanakijiji upo wapiiiiiiiiiiiiiiiii ?????????? Umejichimbia wapi tena ??
 
huyu kada anatumiwa na mafisadi kututoa kwenye issue jamani mpuuzieni ni ukoma huyu
 
huyu kada anatumiwa na mafisadi kututoa kwenye issue jamani mpuuzieni ni ukoma huyu

how about you proove what you just said ? nani kwani yupo kwenye hiyo list ya mafisadi. cuz it was made by opposition party member , right that means i can create one too for the opposition party members! labda slaa ananitumia since he has nothing to do !

Nitakuja na list ya mafisadi yangu wa JF, na ya wanasiasa tanzania !! so stay tuned.

halafu wewe Shalow....you've been craving for Kada for a long time, i'll give you what you've been waiting for.
 
Hiyo dawa kutopatikana Bongo labda kwa muujiza!

Hayo majibu ya kwamba kuna dalili njema ni ya mashaka! Nahisi ni ya kushawishi zaidi watu wajitokeze kwa ajili ya chanjo ili utafiti uendelee kwani kama alivonukuliwa watu wameanza kuikimbia hiyo chanjo kwa uvumi kwamba wanawekea virusi!
 
oohh, kama mambo ya kuwawekea virusi tena basi taifa zima litaangamia within 50 yrs ! hizo chanjo si wakafanyie huko yurop basi !
 
Hizi chanjo si wametoa hivi karibuni tu? Na ninakumbuka mmoja wa waliopewa chanjo hiyo ni afande. Mi nadhani wangesubiri angalau miaka miwili ndipo watoe tathmini. Waende pole pole.
 
Kama kutakuwa na mafanikio yoyote katika kukabiliana na UKIMWI basi wanaotakiwa kufurahi zaidi si wapenda ngono bali ni watu wote wanaopenda usalama na maendeleo. kwa mtu yeyote anayependa ngono UKIMWI si tatizo kubwa sana!!

UKIMWI ni tatizo kwa taifa linalopoteza wataalamu wengi wanaokufa kwa hili janga. Ni tatizo kwa watoto wasio na hatia wanaopoteza wazazi na kuanza kuishi maisha ya uyatima na mashaka. UKIMWI ni tatito kwa wenye ndoa waaminifu ambao wake/waume zao wamegeuka dungadunga/dungwadungwa!!

Mungu isaiidie Tanzania, Isaidie na Africa
 
hii kitu itatoka tanzania, na ikitokea tanzania yaani bab kubwaaaaaaa !
usije ukashangaa nchi zote zilizojaribu zimeshindwa, ikaja tanzania ikawin !

..kada taratibu mkuu!

..hii chanjo chanzo chake ni nchi moja ya nordic!na ndo inayofadhili mradi!

..huko kwao tayari walishafanya majaribio yakawa ni mazuri na sasa wanaendeleza huku!

..but it's too early kuanza kushangilia!
 
..kama hujaupata,dawa yake ni kwenda ishi iceland tuu!

..usije huku hata kidogo!maana ukija ukaumwa ukiwekewa damu,upo hatarini!ukitolea macho vyakula vya huku ukavila[kuku wa kienyeji],uko hatarini!

..yaani,ubaki huko huko!

nb;dawa nyingine wala si dawa!
 
..eeh!kumbe hata humu wamo sio!ndo maana huwa mijadala inapoteza mwelekeo now and then!



..mupe!mupe!.muzee!, mupe ile kitu rokho yake inapenda!

Babu hata humu mafisadi wamo ! na nitawataja siku za karibuni.

huyu shalow nadhani nimuache tu maana nitakuwa namtengeneza baada ya kumdestroy !
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom