NASHUKURU SANA KWA COMENTS ZENU, naomba nifafanue mambo machache
Lakwanza..TUMEKAGUA UJENZI WA BARABARA kwani ni sehemu ya ahadi zilizokwenye Ilani ya CCM ya uchaguzi kwahilo mambo si mabaya pamoja na kwamba tumeitaka serikali kuhakikisha speed inaongezeka na kuhakikisha ubora.
La pili tumezungumzia hali ya maisha.
.. Chama kimeiagiza serikali bajeti ijayo kuhakikisha ina angalia maeneo ambayo yakibadilishwa yatapunguza bei ya vitu nchini hivyo kupunguza ugumu wa maisha.
Tumekagua ufungaji wa majenereta manne yenye uwezo wa kuzalisha 1.25Meg kila moja kwa ajili ya Sumbawanga, Namanyele na viunga vyake.
Tumezungumzia uhusiano uliopo kati ya BAJETI,MIUNDOMBINU kama BARABARA na UPATIKANAJI wa nishati kama UMEME na MAJI na maisha ya watu ya kawaida.
Nape tunakushukuru kwa kufanya kazi kubwa ambayo unaifanya pamoja na kwamba pengine siyo majikumu yako kama kiongozi wa Chama. Swali moja kwako: hawa watoto wazazi wao wako wapi?