Habari Leo - Wasichana vyuo vikuu hufaulishwa kwa kuridhia ngono kwa wahadhiri

Nimeufuatilia huu mjadala unafurahisha sana. Napenda kuchangia nami kidogo. Kwanza siwezi kukataa kuwa walimu wa vyuo wanaweza kuwa na mahusiano na wanafunzi wao. Kwa hali ya kawaida hakuna sheria inayokataza kuwa na mahusiano na mwanafunzi. Wanafunzi wengine ni wake za waalimu wa chuo. Kuwa na mahusiano ambayo yanaenda kinyume na utaribu za kazi kama kupendelea mwanafunzi kwa sababu mnauhusiano naye wa kimapenzi ni 'moral decay' ambayo huwezi kuitumia kuonyesha kuwa walimu wote wa chuo kikuu wameoza. Moral decay kwa sasa ni national crisis, ndiyo maana leo hii unaweza kununua kura! Kila siku tunasikia watu tuliowaamini wanaiba mali ya umma! Kwa hili kama taifa tuna tatizo.
Pili, Mwandishi wa makala hii nafikiri ameandika hisia zake, maana mimi nimekaa 'university' kwa miaka 13 sijaona hiyo hali kama mwandishi alivyowasilisha. Nikiwa kama mwanafunzi wakati nasoma UDSM, hii 'rumours' ilikuwepo kuwa fulani kapewa mtihani! lakini matokeo ya huyo anayesemekana amepewa mtihani unakuta amefaulu kwa margin ya 'D'.
Tatu, Uzoefu wangu unaonyesha kuwa msichana akiwa 'smart' darasani na amekuwa anafulu vizuri kuliko wanaume hisi kuwa anapewa mtihani ndipo inakoanza na kupata kasi! Hili tunahitaji kulifanyia utafiti/nitalifanyia utafiti zaidi. Mimi nina rafiki yangu mwanamke nimesoma naye Chemistry darasa moja UDSM, yule dada alikuwa na uwezo wa hali ya juu sana, mimi binafsi sijawahi kukutana na binadamu mwenye akili kama yeye! Sasa hivi anamalizia PhD yake ya chemistry huko Uholanzi. Wakati tunasoma kulikuwa na hisia kuwa anapewa mtihani. Lakini huyo dada alikuwa anapata 'A' kila somo.
Nne, hawa watu au wanafunzi wanaolalamika kuwa wasichana wanapewa mtihani wamechukua hatu gani kuzuia hilo tatizo?Nauliza hivi kwa sababu chuo kikuu watu wanafundishwa 'critical thinking' and beyond'! Chuo kikuu ni sehemu ya kukuza maarifa na kuleta mabadiliko! ya kifikra na kimatendo!Kama mwanafunzi wa chuo kikuu anaweza kuwa mtumwa kiasi hicho hapaswi kuwa chuo kikuu akatafute mahali pengine pa kusoma maana hatasaidia jamii akimaliza chuo
Tano, Chuo kikuu haiwezekani mwalimu akamfelisha mwanafunzi mtihani ambaye ameandika majibu sahihi. Kuna utaratibu ambao unamlinda mwanafunzi na mwalimu. Mwanafunzi akiona kuwa anaonewa anaweza kukata rufaa. Hili la kuwa professor anaweza kukufelisha kwa sababu umetembea na binti yake au na mpenzi wake sio kweli. Mwandishi nafikiri ameaandika hisia zake kwa sababu hajui mitihani ya chu kikuu inavyoendeshwa.
6. Sasa hivi kuna 'mfumuko' wa vyuo hapa Tanzania, vingine huwezi kuamini kuwa ni vyuo! vinafanana na high schools! labda huko hiyo biashara inakofanyika! ingawa sina uhakika maana sijafanya utafiti.
Kama hayo mambo yapo popote tuchukue hatua sote.
 
Bado naamini kwa asilimia kubwa 80% wahadhiri si chanzo cha matatizo ya ngono vyuoni, nafikiri ni wadada zetu ambao ni weak wanajilengesha zaidi, kama mdada anauwezo wake sidhani kama anaweza kufelishwa na mwalimu lazima huyo mwalimu atakuwa mnyama ajabu na with new technology mbona rahisi tu kuwakamata...

Lakini mimi naamini kuwa wahadhiri wetu pia wana wakati mgumu kwa dada zetu ( I stand to be corrected).

Mtoto wa kike anayeonewa, kufanyia undue force wafanye ngono na mwalimu huyu ana kila sababu ya kusaidiwa tena kwa nguvu zote; maana hiyo ni LAANA aisee...

Wanafunzi ni kama watoto wadogo. Wanaweza fanya cho chote hata kilicho kinyume cha maadili au sheria ili mradi afaulu. Mhadhiri tunamwona anakuwa na upeo mkubwa wa kuelewa mambo mengi, na si kufundisha masomo tu ila kumjenga mwanafunzi kimaadili. Lakini anaporidhia mitego ya wanafunzi tunatafsiri kwamba si mkomavu na hana upeo wa kutosha katika taaluma na majukumu yake katika utumishi wake kwa wanafunzi.

Wanafunzi nao hasa wa kike jambo moja ambalo katika uchunguzi wangu nimeliona na kulalamikiwa na baadhi ya wanafunzi wenzao wa kike wakilalamikia ukosekanaji wa maadili kwa baadhi ya wanafunzi wa kike ni behaviour yao wawapo vyuoni na madarasani. Hii ni pamoja mivao waingiapo madarasani au waendapo kwa wahadhiri wao kuvaa mivao ya wagombea umiss world. Kuonyesha wazi baadhi ya maungo nyeti ya miili yao ambayo huamsha hisia na mvuto wa kumhamasisha mwanaume kufanya ufuska na wanafunzi hao. Wahadhiri wengine bado wako singles sasa kuanikiwa vya bure yanajilia hayo ya kuishia msichana kurithia kuweka rehani mwili wake kwa mhadhiri ili ammegee siri za mitihani ili afaulu.

Rais Kikwete inaelekea anawajua sana tu hawa wanafunzi wa kike wanaojihusisha na ngono pale alipotamka hadharani kwenye mkutano kwamba ni kiherehere chao, sijajua alifahamia wapi kiherehere cha hawa wanafunzi wa kike hadi kusababisha kupata mima wawapo shuleni au vyuoni.
 
Kwa mtu yeyote uliyesoma vyuo vya bongo huna haja hata ya kufanya uchunguzi kuhusu swala hili, unless umesoma nje au hujawahi gusa korido za UD, SUA, MZUMBE nk. Tabia hii ipo karibu vyote , lakini CBE na IFM hali ni mabaya zaidi.

Vilevile kumbuka hii ni rushwa kama rushwa zingine ambazo zimetapakaa kila sehemu katika nchi hii. Watu wamepata kazi, vyeo, ubunge, zabuni, scholarships kwa rushwa ya ngono.

Mkuu umenena! Yaani hapa IFM ni balaa tupu. Kuna mkuu wa idara ya Social Protection anaitwa Magoti, yaani ni anakera sana na hiyo tabia yake chafu ya kuua watoto wa watu maana nasikia tayari anako kale kaugonjwa ketu. Hivi TAKUKURU wenyewe kazi yao ni kupambana na rushwa ya pesa tu?
 
kwa hiyo tusiwaoe kwani top layer imeliwa tiyari au wote tunaowaona kuwa wana shahada tiyari wazee walishapita
 
Mkuu umenena! Yaani hapa IFM ni balaa tupu. Kuna mkuu wa idara ya Social Protection anaitwa Magoti, yaani ni anakera sana na hiyo tabia yake chafu ya kuua watoto wa watu maana nasikia tayari anako kale kaugonjwa ketu. Hivi TAKUKURU wenyewe kazi yao ni kupambana na rushwa ya pesa tu?


:juggle::juggle::juggle::juggle::juggle::juggle::juggle::juggle:
 
Mkuu habari hii ni dhana zaidi kuliko ukweli halisi kwasababu

Nimefanya kazi vyuoni kabla sijaenda kwenye private sector, kupewa marks vyuon na lecturers ni dhana na wanafunzi weak hupenda kuitumia kuonyesha kuwa wameonewa au excuses

a. Utaratibu wa ku-mark mitihani ni wa panel si mwalimu moja hivyo si rahisi kuweka marks kwa ajili ya mwanafunzi fulani

b. Mwalimu anasimimia only 40% ya CW yako, while 60% ni final ambayo mwalimu si lazima asahihishe script yako; wanafunzi wazuri hawana hata sababu ya kuhangaika na mwalimu na wanapasua

c. Kama hiyo haitoshi kuna external examiner anapitia scripts zote na huwa huyu anatoka chuo kingine au kwenye private sector, ana rekebisha marks na marking ya panel; mara nyingi wako in fever of students..

d. Ni bahati mbaya sana wasichana weak hupenda kujipendekeza kwa walimu hasa kwa zile mark 40% za CW lakini hata hivyo mara nyingi hufeli kwasababu kuna another 60% ambazo mwalimu hana control..

Huo ndio uzoefu wangu chuoni lakini kama mambo yamebadilika basi kuna haja ya kufanya utafiti wa kina ili tusiwa onee wahadhiri na wanafunzi pia..

Nakubaliana nawe kuwa ni dhana zaidi kuliko ukweli.
Ni dhana tu kama dhana nyingine potofu kama vile "wachaga ni wezi", "Wapare/wangoni/wahaya ni malaya" "Watu wa dodoma ni ombaomba" Wasichana wakipita JKT wanabakwa". Katika dhana zote hizi utaona kuwa inawezekana kuna some isolated cases mbili au tatu zimetokea, halafu watu wana-conclude kuwa mambo ndio yako hivyo siku zote.

Stori kama hiyo hapo juu, mara nyingi huanzishwa na wanafunzi wa kiume katika mazingira yafuatayo:

1. Mwanafunzi wa kiume mwenye wivu, ambaye hataki kupitwa marks na msichana, siku zote atadai msichana huyo aliyempita marks, amependelewa na Lecturer/ametoa ngono.

2.Mwanafunzi wa kiume aliyefeli mtihani na anatafuta sababu ya kukubalika na jamii; atadai amefelishwa kwa vile kuna mwalimu alikuwa anamtokea demu wake.

3.Mwanafunzi wa kiume ambaye anatamani kuwa na uhusiano na msichana, sasa katolewa nje, halafu yule msichana anatokea kutembea na mhadhiri, hata kama mhadhiri huyo hawafundishi wao, basi, mwanafunzi wa kiume anajaribu kuonesha kuwa amekataliwa kwa vile Lecturer ametumia ubabe wa marks kwa yule msichana. Hii ni sawa na mvulana mtaani ambaye anatolewa nje na mrembo, halafu mrembo anachukuliwa na kigogo au tajiri fulani, mvulana anaweza kudai kuwa pesa au madaraka vimetumika, wakati inawezekana kabisha ni "pure chemistry" between the two.

Mimi naamini kuwa wasichana vyuoni ni watu wazima wenye akili zao, na lecturer anao uhuru wa "kumtokea" kama ambavyo watu wa manzese wanao uhuru wa kumtokea msichana huyo. Suala ni makubaliano. Aina yoyote ya vitisho/blackmail/coercion kwenye mahusiano hayo, ndivyo havikubaliki.

Iliwahi kutokea kwenye chuo fulani kikubwa hapa nchini, miaka ya 2000, ambapo mwanafunzi mmoja wa kike alikuwa anafaulu sana mitihani, akawa anaongoza. Kijana mmoja (mwanaume) ambaye alikuwa mara nyingi ndio anashika nafasi ya pili, akazusha kuwa yule binti anapewa marks za chupi. Alisema hivyo bila kujali kuwa hata mitihani mingine ilikuwa ni ya wahadhiri wa kike.
Bahati nzuri, huyo kijana akaja kuongoza mtihani mwingine ambao ulikuwa ni wa mhadhiri wa kiume. Yule mdada naye akaenda mbele ya darasa na kutangaza kuwa yule mvulana "aliinamishwa" ndio maana aliongoza ule mtihani....

Watu wakumbuke kuwa mwanafunzi ndani ya chuo na hasa inapokuja swala la mtihani, huwa ana haki nyingi sana na analindwa sana. Kuna kukata rufaa, mtihani usaishwe upya, kuna moderation ya mtihani kiasi kuwa maswali ambayo mhadhiri anasubmit idarani, sio lazima ndio yatoke kwenye mtihani, na juu ya hayo yote, mwanafunzi bado analindwa na by-laws pamoja na sheria za nchi. Kuwepo kwa mhadhiri mmoja au wawili ambao wanatembea na wanafunzi, haimaanishi kuwa uhusiano wao ni wa marks-ngono na wala haimaanishi wanafunzi wote na wahadhiri wote wanafanya hivyo.
 
Bado naamini kwa asilimia kubwa 80% wahadhiri si chanzo cha matatizo ya ngono vyuoni, nafikiri ni wadada zetu ambao ni weak wanajilengesha zaidi, kama mdada anauwezo wake sidhani kama anaweza kufelishwa na mwalimu lazima huyo mwalimu atakuwa mnyama ajabu na with new technology mbona rahisi tu kuwakamata...

Lakini mimi naamini kuwa wahadhiri wetu pia wana wakati mgumu kwa dada zetu ( I stand to be corrected).

Mtoto wa kike anayeonewa, kufanyia undue force wafanye ngono na mwalimu huyu ana kila sababu ya kusaidiwa tena kwa nguvu zote; maana hiyo ni LAANA aisee...


Kweli mkuu. Lakini vyuo vyetu siku hizi vimejaa vijana tu...kuanzia UDSM, UDOM, SUA, ARU etc. Sasa hawa vijana wanatekeleza ule usemi kwamba ujana maji ya moto kwa kuwachezea watoto wa watu. Ingawa naweza kukiri kwamba pande zote zinashiriki; nikimaanisha kuna cases ambazo watoto wa kike ndio wanajilengesha kwa wahadhiri na kuna cases ambazo wahadhiri wanawatega kwa makusudi watoto wa kike.

Mfano pale UDSM kuna mhadhiri mmoja ambae alimpenda binti mmoja wa kike wa kiislamu (alikua anavaa hijab), lakini hakujua jina lake; sasa huyu mhadhiri alichofanya ni kuwafelisha (test, part ya 40% CW) wanafunzi wote wa kike wenye majina ya kiislamu na kuwaambia wakamwone ofisini kwake. Mabinti kwenda,jamaa akamwona yule binti aliekua anamtaka, basi wale wengine wakaambiwa warudi kwani alikosea!! Jamaa akamweka binti sawa, mambo yakakamilika. Binti alimaliza shahada ya kwanza, mhadhiri akafanya mpango, binti akaunganisha shahada ya pili kwenye idara ambayo mhadhiri yupo, nako mchezo ukaendelea.......

Mifano ya namna watoto wa kike wanavyoshiriki katika suala hili, rejea post yangu nyuma kidogo katika uzi huu.
 
nanyie sasa mnatisha miaka ya nyuma mtu akifaulu kwao wanawaita wachawi, ukiwa sekondari utaambiwa walipewa mtiani, chuoni eti alitoa ngono. Achana na mwazo mgando, kufaulu mpaka chuo kikuu bila kikwazo ulikuwa unamsomea?
 
Mkuu umenena! Yaani hapa IFM ni balaa tupu. Kuna mkuu wa idara ya Social Protection anaitwa Magoti, yaani ni anakera sana na hiyo tabia yake chafu ya kuua watoto wa watu maana nasikia tayari anako kale kaugonjwa ketu. Hivi TAKUKURU wenyewe kazi yao ni kupambana na rushwa ya pesa tu?

Aisee wasaidie hao wanafunzi mkuu, mpelekeni huyo mkuu wa idara kwa wakubwa zake...

Besides, mkuu wa idara si atakuwa anafundisha somo moja au mbili tu?? bado sijawaelewa nini matatizo yenu..

Ukute hao wadada wa IFM wanajilengesha kwa huyo mkuu...
 
Tafuteni mashairi ya Wimbo unaoitwa Mathematics wa Roma, sehemu ya tungo zake zinasikika hivi '...Wanapata alama za juu kwa kumhonga Penzi Profesa, ...FATAKI anatoa mkopo ndani ya T.I.A kisha mimba hazina uhakika hadi kwa D.N.A...Makahaba wanaongezeka Boom linapokata.....
 
Mademu wengi niliosoma nao chuo walikuwa na kamsemo "I will do anything for A" nawalikuwa wanazipata!
 
01_12_32h45c.jpg


rushwa ya ngono imekithiri vyuo vikuu

leo wazalendo wenzangu nina mada ambayo imejificha kidogo, ambayo imekuwa ikirudisha nyuma maendeleo ya taifa kwa namna moja. Kama macho yako yatakuwa yametazama kichwa cha habari hapo juu, utakuwa pamoja nami na kufahamu nini nataka kuzungumzia.

Jana katika harakati za shughuli zangu za kila siku niliweza kutembelea moja ya chuo cha elimu ya juu hapa nchini. Mandhari ya chuo hicho ni mazuri yanayovutia sana, binafsi nimevutiwa na hali ya usafi wa mazingira ya chuo hicho. Nilikuta wanafunzi wakijisomea makundi kwa makundi, wanawake na wanaume.

Kuna malalamiko kuwa eti baadhi ya wahadhiri wa vyuo vikuu huwa wanataka wapewe rushwa ya ngono ili watoe majibu ya mitihani kwa wanafunzi wanawake! Hili ndilo lililopelekea mimi kufanya uchunguzi ili niweze kugundua ukweli wa mambo. Najua yawezekana kama wewe ni mwanafunzi mwanamke umewahi kukutana na tatizo hili!
Naamini kabisa wapo baadhi ya wanafunzi wanaokubali kutoa rushwa ya ngono ili waweze kufaulu lakini wengi wao hawapendi kitendo hicho cha udhalilishaji.

Nikafika chini ya mti mmoja ambao walikuwa wameketi wanafunzi wanawake na kuwasabahi kabla ya kuanza uchunguzi wangu juu ya jambo hilo. Wakanieleza kuwa tatizo la rushwa ya ngono lipo na wahadhiri wanalitumia kama silaha pekee kufanikisha jambo hilo.

Mmoja wa wale wanafunzi alisema, “yaani hata ukiwa na rafiki yako wa kiume ni tatizo, mnaweza kufelishwa mitihani yenu kwa sababu eti umekataa kutembea na mhadhiri!” tatizo la rushwa ya ngono lipo karibu vyuo vingi vya elimu ya juu hapo nchini, lakini hebu tujiulize ni hatua gani zimechukuliwa mpaka sasa!

Kuna malalamiko mengi katika vyuo kuwa baadhi ya wahadhiri wana tabia ya kuwataka kimapenzi wanafunzi wa kike ili waweze kuwapa majibu ya mtihani. Malalamiko ya wanachuo ambao wanatakiwa kutoa rushwa ya ngono yanapopelekwa hakuna hatua zozote zinazochukuliwa dhidi ya hao, hilo ni tatizo ambalo linapaswa kutafutiwa dawa. .....

habari leo


huko ni kuwadhalilisha dada zetu na mama zetu kwamba wao hawajiwezi mpaka watoe rushwa ya ngono? Acheni hizo. Mbona wengi tu tumesoma nao na walikuwa na uwezo mkubwa sana hata kuwazidi wanaume.
 
huko ni kuwadhalilisha dada zetu na mama zetu kwamba wao hawajiwezi mpaka watoe rushwa ya ngono? Acheni hizo. Mbona wengi tu tumesoma nao na walikuwa na uwezo mkubwa sana hata kuwazidi wanaume.


Wanafunzi ni kama watoto wadogo. Wanaweza fanya cho chote hata kilicho kinyume cha maadili au sheria ili mradi afaulu. Mhadhiri tunamwona anakuwa na upeo mkubwa wa kuelewa mambo mengi, na si kufundisha masomo tu ila kumjenga mwanafunzi kimaadili. Lakini anaporidhia mitego ya wanafunzi tunatafsiri kwamba si mkomavu na hana upeo wa kutosha katika taaluma na majukumu yake katika utumishi wake kwa wanafunzi.

Wanafunzi nao hasa wa kike jambo moja ambalo katika uchunguzi wangu nimeliona na kulalamikiwa na baadhi ya wanafunzi wenzao wa kike wakilalamikia ukosekanaji wa maadili kwa baadhi ya wanafunzi wa kike ni behaviour yao wawapo vyuoni na madarasani. Hii ni pamoja mivao waingiapo madarasani au waendapo kwa wahadhiri wao kuvaa mivao ya wagombea umiss world. Kuonyesha wazi baadhi ya maungo nyeti ya miili yao ambayo huamsha hisia na mvuto wa kumhamasisha mwanaume kufanya ufuska na wanafunzi hao. Wahadhiri wengine bado wako singles sasa kuanikiwa vya bure yanajilia hayo ya kuishia msichana kurithia kuweka rehani mwili wake kwa mhadhiri ili ammegee siri za mitihani ili afaulu.

Rais Kikwete inaelekea anawajua sana tu hawa wanafunzi wa kike wanaojihusisha na ngono pale alipotamka hadharani kwenye mkutano kwamba ni kiherehere chao, sijajua alifahamia wapi kiherehere cha hawa wanafunzi wa kike hadi kusababisha kupata mima wawapo shuleni au vyuoni.
 
Jamani katika mada hii kuna ukweli ndani yake. Mimi nimeyaona haya hapa chuoni kwetu Tumaini Iringa. Ila nilichogundua mimi, asilimia kubwa chanzo ni madada zetu wenyewe kutaka favour, na imefikia hatua hata wengine kuajiriwa hapahapa pindi wamalizapo ilimradi wanamahusiano na wakubwa. Kumbuka hii ni private institution, nadhani utakuwa umepata picha jinsi mambo yanavyokwenda.
 
Tatizo la mwandishi ameongea na wanafunzi meza au kibwete kimoja na kutoa hukumu kuna rushwa ya ngono. Huwezi kuja na hukumu ya aina hiyo mpaka ufanye utafiti mpana
 
Rushwa katika nchi yetu imekomaa kwa kiwango kikubwa. Kwa upana wake si rahisi kutoa jibu la mkato kuwa lililosemwa si kweli kisa halikukidhi vigezo vya utafiti. Hali halisi tunaijua, msichana mwanafunzi asiye na pesa anahonga nini ili apate akitakacho? Tukubali tatizo na sie ambao hatujaridhika na hoja ya mwenzetu tuchukue hatua moja mbele tujue ukweli na tutoe maoni ya hatua muafaka za kuchukua.
 
Tatizo kubwa ni maisha katika nchi yetu, hali ya uchumi ni ngumu sana kwa mtu wa kawaida hivyo ni vigumu sana kuyadhibiti haya. Mfano unafamilia ya watu wengi tuseme kama hamsini hivi lakini unawapa chakula cha kutosha watu ishirini lazima kutakuwa na kugombania. Hali hiyo ndiyo inayosababisha mambo yote haya. Inamaana kila kitu kinapatikana kwa mabavu au rushwa kama rushwa za ngono. kwahiyo kusipokuwa na ustahimilifu wa tamaa katika jamii lazima yatokee mambo ya namna hiyo. Jibu la haya ni viongozi kubuni njia za kuongeza uzalishaji ili kuwe na nafasi za kutosha kila sekta.
 
Ndo maana kuna polisi, mahakama, sheria, usalama wa taifa, n.k. Kama vyombo hivi havifanyi kazi zake vizuri uhalifu kama huo utaendelea tu kea sababu ni uhalifu kama mwingine tu.

Kwa lugha nyingine hii ni rushwa ni sawa na Ngeleja alivyopewa zile mil. 4 ktk kuhakikisha bajeti inakwenda mswano.
 
Hili jambo ni gumu,
kuna baadhi ya maeneo limekuwa jambo la kawaida mtu akiferi anaringa 'nitazipata tu' wapi? haya yote ni matatizo ya wakati ambao tupo. thamani ya viungo vya mwanadamu vimeshuka bei, na ndo maana hata walafanya mapenzi na wanyama. kuhusu hili ni moja wapo ya mambo yanayotokea na tayari wengi wa wanaofanya hivyo si rahisi kuacha watafanya hivyo hata kabda na baada ya ajira. kitu cha kufanya ni kwa wale ambao hawajafanya hivyo wasikubari kuiga; nasema kuiga kwa maana si ndo wanavyoamini ukitaka maksi baada ya kuferi hulala na walimu wao. vile vile unaweza kujumulisha kuwa wote ni wanachuo basi wana tabia nzuri! chuo kama sehemu nyingine kuna wazuri na wabaya. hapa unaweza kukuta kuna machangudoa walipata zali la mentali wakawa chuo sasa huyu kazi yake si hiyo na wengine wanamwiga huyu kwa kutoa rushwa ya ngono. kama kuna walimu wanaofanya hivyo nao wanamatatizo, hawajashtuka wanafanya mapenzi na watu ambao si mara yao ya kwanza, wanafikiri wameanza wapi na nani? kweli tuwe na msimamo na maisha yetu.
 
Back
Top Bottom