Habari Leo - Wasichana vyuo vikuu hufaulishwa kwa kuridhia ngono kwa wahadhiri

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,885
6,885
01_12_32h45c.jpg


Rushwa ya ngono imekithiri vyuo vikuu

LEO wazalendo wenzangu nina mada ambayo imejificha kidogo, ambayo imekuwa ikirudisha nyuma maendeleo ya taifa kwa namna moja. Kama macho yako yatakuwa yametazama kichwa cha habari hapo juu, utakuwa pamoja nami na kufahamu nini nataka kuzungumzia.

Jana katika harakati za shughuli zangu za kila siku niliweza kutembelea moja ya chuo cha elimu ya juu hapa nchini. Mandhari ya chuo hicho ni mazuri yanayovutia sana, binafsi nimevutiwa na hali ya usafi wa mazingira ya chuo hicho. Nilikuta wanafunzi wakijisomea makundi kwa makundi, wanawake na wanaume.

Kuna malalamiko kuwa eti baadhi ya wahadhiri wa vyuo vikuu huwa wanataka wapewe rushwa ya ngono ili watoe majibu ya mitihani kwa wanafunzi wanawake! Hili ndilo lililopelekea mimi kufanya uchunguzi ili niweze kugundua ukweli wa mambo. Najua yawezekana kama wewe ni mwanafunzi mwanamke umewahi kukutana na tatizo hili!
Naamini kabisa wapo baadhi ya wanafunzi wanaokubali kutoa rushwa ya ngono ili waweze kufaulu lakini wengi wao hawapendi kitendo hicho cha udhalilishaji.

Nikafika chini ya mti mmoja ambao walikuwa wameketi wanafunzi wanawake na kuwasabahi kabla ya kuanza uchunguzi wangu juu ya jambo hilo. Wakanieleza kuwa tatizo la rushwa ya ngono lipo na wahadhiri wanalitumia kama silaha pekee kufanikisha jambo hilo.

Mmoja wa wale wanafunzi alisema, "yaani hata ukiwa na rafiki yako wa kiume ni tatizo, mnaweza kufelishwa mitihani yenu kwa sababu eti umekataa kutembea na mhadhiri!" Tatizo la rushwa ya ngono lipo karibu vyuo vingi vya elimu ya juu hapo nchini, lakini hebu tujiulize ni hatua gani zimechukuliwa mpaka sasa!

Kuna malalamiko mengi katika vyuo kuwa baadhi ya wahadhiri wana tabia ya kuwataka kimapenzi wanafunzi wa kike ili waweze kuwapa majibu ya mtihani. Malalamiko ya wanachuo ambao wanatakiwa kutoa rushwa ya ngono yanapopelekwa hakuna hatua zozote zinazochukuliwa dhidi ya hao, hilo ni tatizo ambalo linapaswa kutafutiwa dawa. .....

Habari Leo
 
pia kwa chuo kama st joseph na sua wasichana hufaulishwa kwa sababu ya jinsia yao. Hata akiandika madudu ktk mtihani maksi anazo
 
​leo gazeti la CCM limeamua kutukana dada zetu na kuwadhalilisha badala ya kuandika mambo ya msingi
 
Tatizo hatujajikita kwenye MANUFACTURING OF LECTURERS.....


Hatuna vipaumbele, kila sehemu ni ubabaishaji. Watu wenye uwezo wanaachiwa kwenda kufanya kazi kwenye makampuni binafsi, unatagemea nini mkuu? Nchi zingine, vijana wenye uwezo mkubwa wa kuchambua mambo, kufanya mambo, kufikiria huwa ni lulu kwa taifa. Vijana hawa ndiyo hupewa sehemu/nafasi kwenye secta nyeti za nchi kama Elimu, Afya, Usalama wa Taifa, Jeshi, wahandisi wa sehemu husika. Lakini nchi yetu kipaumbele ni siasa, ufisadi na kutajiirika haraka haraka.
 
Tatizo la rushwa ya ngono lipo sehemu nyingi sana. kupata maksi, ajira, cheo nk. Hili ni kosa na udhalilishaji kama wadau wengine walivosema. Japo wengi wanaridhia. Kwamba hatua zinachukuliwa au la inategemea kama wanaodhalilishwa wanashitaki. Masuala ya ngono mara nyingine yanakuwa ya usiri. Umefika wakati yeyote anaedhalilshwa achukue hatua dhidi ya hawa wakware. chukua hatua acha kulalama tu. Poleni mliodhalilishwa/mliojidhalilisha
 
Tatizo kama hili linahtaji mwandishi wa kike mdogomdogo ajiunge na chuo kikuu flani halafu afanye uchunguzi na inabidi afanye kwa muda kidogo ndiyo majibu yaje' siyo mtu anakwenda kuongea na wanafunzi ndani ya nusu saa anaibuka na majibu.Hii ni habari ya kichunguzi tena unachunguza tabia za watu inabidi ichukue muda kidogo ili zisitoke habari za uongo!
 
Ni hatari sana kujenga taswira ya namna hiyo dhidi ya dada zetu. Isolated case kama hizo zipo, lakini si kwa kiwango kikubwa kiasi cha kutufanya tuamini kuwa kila msichana anayemaliza chuo kikuu alipendelewa. Binafsi nakumbuka wasichana walivyokuwa wanatupa wakati mgumu tukiwa A-level (PCM) na hata Engineering pale UDSM. Hadi leo huko waliko kwenye ajira zao wanafanya mambo makubwa.

Ni vyema kabla ya kuandika tuhuma kama hizo magazetini, waandishi husika wakafanya utafiti wa kina. Naamini wakifanya uchunguzi watakuwa na takwimu sahihi juu ya tatizo husika badala ya kufanya 'fallacy of generalization'.
 
Tatizo la rushwa ya ngono lipo sehemu nyingi sana. kupata maksi, ajira, cheo nk. Hili ni kosa na udhalilishaji kama wadau wengine walivosema. Japo wengi wanaridhia. Kwamba hatua zinachukuliwa au la inategemea kama wanaodhalilishwa wanashitaki. Masuala ya ngono mara nyingine yanakuwa ya usiri. Umefika wakati yeyote anaedhalilshwa achukue hatua dhidi ya hawa wakware. chukua hatua acha kulalama tu. Poleni mliodhalilishwa/mliojidhalilisha

Huo ndiyo ukweli kabisa,mimi naamini kuwa akina dada nao wana matatizo!kwanini wanashindwa kuchukua hatua!!?kama madai yake ni sahihi akitoa taarifa kwa uongozi hatua stahiki zitachukuliwa,mara nyingi wakuu wa chuo uwa ni watu wanaojiheshimu hivyo akitoa taarifa kwake au kwa wasaidizi wake watachukua hatua,na hii ilishawai kufanywa na baadhi ya wanafunzi na malecture wakabaki kupiga magoti ili wasamehewe,la msingi binti awe na akili za darasani.

Kinachofanyika taarifa inapotolewa uwa mwalimu husika awamwambii then ukifanyika mtihani na huyo binti akafeli uambiwa akate rufaa ambapo uongozi usimamia hilo zoezi kwa ukaribu na ikibainika kuwa alifelishwa lecture uitwa na kusomewa tuhuma zake huku ushahidi wakiwa nao mkononi hapo ndipo uwa kizaazaa,na huyo binti kamwe hataburuzwa.
 
Nashukuru wadau wengi mmeona uzushi wa habari hii. Nakukosoa mwandishi mchunguzi kama ifuatavyo;
1. wasichana uliowahoji ulijuaje kama hawa hakika ni wanachuo tena elimu ya juu? Justification of respondents
2. Ulipoambiwa na dada mmoja tu ukathibitsha uvumi badala ya kufanya extensive and intensive study (longitudinal) badala ya hiyo unjustifiable case study
3. hivyo vyuo vina wahadhiri wa kike, nao uliwaweka wapi kwenye study hii? Nao wangeshuhudia uwepo wa hili au unatka kutuaminisha kuwa wanashadadia (kukumbatia tabia ya wahadhiri wenzao)?
4. Ungekuwa mwanafunzi wa elimu ya juu ungekuwa unapata karibu na zero vinginevyo ungeanzisha kundi lakutafta kufaulu kwa migongo isiyoeleweka ambayo nayo ingefanyiwa uchunguzi na wengine.

Nakushauri kuwa yanayokutuma ubongoni mwako yasiwe sehemu ya jamii
 
Tatizo kama hili linahtaji mwandishi wa kike mdogomdogo ajiunge na chuo kikuu flani halafu afanye uchunguzi na inabidi afanye kwa muda kidogo ndiyo majibu yaje' siyo mtu anakwenda kuongea na wanafunzi ndani ya nusu saa anaibuka na majibu.Hii ni habari ya kichunguzi tena unachunguza tabia za watu inabidi ichukue muda kidogo ili zisitoke habari za uongo!

Wewe unaonekana ni mmoja wapo wa waadhiri wa vyuo vikuu unajenga utetezi wa kuficha maovu yanayofanywa vyuo vikuu. Wasichana wenye uwezo mzuri kimasomo mnawaangusha na kuwafaulisha vibonde wanaojiruhusu kujirusha na waadhiri, ni aibu ilioje? Sote tunajua yanayojilia vyuo vikuu halafu unakuja na utetezi unaopingana na uchunguzi uliofanywa.
 
Hili llinataka umakini katika kulifuatilia na kupata ukweli wake...kuna wahadhiri wanaotaka rushwa ya ngono na hawaoni haya kumfelisha mtu...ila kuna kina dada pia ambao wako tayari kufanya lolote ili wapate maksi na kufaulu tena kwa alama za juu kwenye masomo yao. Hayo yapo na si kila unaloambiwa linakuwa limebeba ukweli wote.
 
Kwa mtu yeyote uliyesoma vyuo vya bongo huna haja hata ya kufanya uchunguzi kuhusu swala hili, unless umesoma nje au hujawahi gusa korido za UD, SUA, MZUMBE nk. Tabia hii ipo karibu vyote , lakini CBE na IFM hali ni mabaya zaidi.

Vilevile kumbuka hii ni rushwa kama rushwa zingine ambazo zimetapakaa kila sehemu katika nchi hii. Watu wamepata kazi, vyeo, ubunge, zabuni, scholarships kwa rushwa ya ngono.
 
Nashukuru wadau wengi mmeona uzushi wa habari hii. Nakukosoa mwandishi mchunguzi kama ifuatavyo;
1. wasichana uliowahoji ulijuaje kama hawa hakika ni wanachuo tena elimu ya juu? Justification of respondents
2. Ulipoambiwa na dada mmoja tu ukathibitsha uvumi badala ya kufanya extensive and intensive study (longitudinal) badala ya hiyo unjustifiable case study
3. hivyo vyuo vina wahadhiri wa kike, nao uliwaweka wapi kwenye study hii? Nao wangeshuhudia uwepo wa hili au unatka kutuaminisha kuwa wanashadadia (kukumbatia tabia ya wahadhiri wenzao)?
4. Ungekuwa mwanafunzi wa elimu ya juu ungekuwa unapata karibu na zero vinginevyo ungeanzisha kundi lakutafta kufaulu kwa migongo isiyoeleweka ambayo nayo ingefanyiwa uchunguzi na wengine.

Nakushauri kuwa yanayokutuma ubongoni mwako yasiwe sehemu ya jamii

Sote ni watanzania tumepitia shule na vyuo mbalimbali na tumeshuhudia mambo haya, hawa dada ni victims na wengi kwa hulka yao hawana nafasi au uwezo wa kujenga hoja za utetezi. Wachangiaji wengi hapa ni wale wenye nafasi ya kucheza na key board ambao wengi wao ni waadhiri vyuo vikuu, waandishi wa habari na maofisa, kashfa hii kwa vyovyote inawahusu baadhi ingawa si wote. Makazini nako jambo hili lipo ngono zimekuwa ni siri ya kuajiriwa baadhi ya wanawake. Hapa Tanzania tuko nyuma sana katika mambo mengi ya haki za msingi kibinadamu, na hata mataifa mengi ya Kiafrika.

Vema tungekuwa tunajadili namna ya kuondoa kero hizi badala ya kukazana kujengo hoja ya utetezi wakati tatizo linazidi kuota mizizi.

Imeshalalamikiwa mara kadhaa hapa JF kwamba mfano vyuo vikuu vya Dodoma vimekuwa bustani ya waheshimiwa, ingawa jambo hili linawavunjia heshimwa jumuiya ya waheshimiwa, lakini 2-5% yao wakifanya hivyo tenga la samaki lililosheheni samaki wote wataonekana wananuka kumbe ni wawili tu waliochanganywa ndio wenye kutoa harufu hiyo.
 
nitamshangaa mtu atakayeinuka na kusema kuwa aliyeandika mada kuwa hajafanya uchunguzi wa kutosha,,, hili jambo ni kweli kabisa na inawezekana na wewe ni mmoja wa hao mnaofanya hivi..... wakati ninasoma nilikuwa na mwalimu mmoja rafiki yangu lecture ameoa lakini alikuwa anotoka na fafiki yangu wa kike,,, sasa wakati tunasoma kuna coz moja kwa kweli ilikuwa ngumu ( international Finance) huyo dada alipewa mtihani wote pamoja na marking scheme ili asome na afaulu sasa huu si ushaidi wa kuprove hilo......
 
nitamshangaa mtu atakayeinuka na kusema kuwa aliyeandika mada kuwa hajafanya uchunguzi wa kutosha,,, hili jambo ni kweli kabisa na inawezekana na wewe ni mmoja wa hao mnaofanya hivi..... wakati ninasoma nilikuwa na mwalimu mmoja rafiki yangu lecture ameoa lakini alikuwa anotoka na fafiki yangu wa kike,,, sasa wakati tunasoma kuna coz moja kwa kweli ilikuwa ngumu ( international Finance) huyo dada alipewa mtihani wote pamoja na marking scheme ili asome na afaulu sasa huu si ushaidi wa kuprove hilo......

Umenena iliyo kweli kabisa maana sote ni watanzania tuliopitia shule na vyuo tukishuhudia madudu hayo, halafu uchunguzi gani zaidi wanaotetea? Huyo mwandishi kwa kipindi kifupi alichofika pale chuoni kufanya uchunguzi ilikuwa ni kwa ajili ya kujiridhisha kujenga hoja ya makala yake ingawa anajua vika yanayojilia na pengine alishayahuhudia hayo alipokuwa chuoni au mmoja na pengine kadhaa waathirika wamemlalamikia hadi kujituma kufanya utafiki.
 
nitamshangaa mtu atakayeinuka na kusema kuwa aliyeandika mada kuwa hajafanya uchunguzi wa kutosha,,, hili jambo ni kweli kabisa na inawezekana na wewe ni mmoja wa hao mnaofanya hivi..... wakati ninasoma nilikuwa na mwalimu mmoja rafiki yangu lecture ameoa lakini alikuwa anotoka na fafiki yangu wa kike,,, sasa wakati tunasoma kuna coz moja kwa kweli ilikuwa ngumu ( international Finance) huyo dada alipewa mtihani wote pamoja na marking scheme ili asome na afaulu sasa huu si ushaidi wa kuprove hilo......

Kuna mwingine anafundisha international relationship chuo fulani kikongwe....akimtaka mdada halafu akamkataa, lazima amfelishe au kumrudisha mwaka. Na yule anayempenda atampambania mpaka kwenye kazi zile nzuri nzuri...of course siku moja moja haoni shida kubeba boksi la pizza kama lunch box kwa kazi nzuri dada aliyomfanyia hata akiwa kazini.
All in all, kuna wachache pia ambao kina dada wanatumia mbinu mbali mbali kuona wanawakamata ili mambo yao yanyooke. That is why naamini inataka umakini sana kuliangalia swala kama hili ili tuweze kupata balance.
 
Hayo ndo marupurupu ya ma Lecturers!, St Augustine wale madem vicheche wanawafaidi sana. Kuna lecturer mmoja nilimchukua dem wake alikuja juu, hadi sasa hatusalimiani. Kuna sheria zinazowafunga kutokuwa na uhusiano na wanachuo. Kwenye mikataba yao wanawazuia.
 
Kuna mwingine anafundisha international relationship chuo fulani kikongwe....akimtaka mdada halafu akamkataa, lazima amfelishe au kumrudisha mwaka. Na yule anayempenda atampambania mpaka kwenye kazi zile nzuri nzuri...of course siku moja moja haoni shida kubeba boksi la pizza kama lunch box kwa kazi nzuri dada aliyomfanyia hata akiwa kazini.
All in all, kuna wachache pia ambao kina dada wanatumia mbinu mbali mbali kuona wanawakamata ili mambo yao yanyooke. That is why naamini inataka umakini sana kuliangalia swala kama hili ili tuweze kupata balance.

Vyuo vyetu vinakosa ile nafasi nyeti ya idara ya ushauri. Vyuo vya majuu lazima idara hiyo iwepo ambayo imesheheni wataalamu wa kike na kiume ambao wanapigania haki za wanafunzi dhidi ya wahadhiri. Wahadhiri vyuo vya majuu wanaogopa wanafunzi wa vyuo kujihusisha kimapenzi kama ukoma, maana ikitokea ni kashfa nzito ya kupelekwa mahakamani na kuanikwa kwenye luninga na kuaibishwa hata mijusi wajue kilichojilia.

Hatuna ofisi za makada washauri katika vyuo,na wachache waliopo hawafanyi kazi kwa uzito stahiki, kwani wataalamu hao wangekuwa na nafasi ya kuwaelimisha wanafunzi na kutetea haki zao, na pale linapotokea jambo kama hilo wangetetewa, lakini mambo yanavyokwenda ni kama mwanafunzi akithubutu kufanya hivyo utaona wahadhiri wanalindana na kumsikisha adabu mwanafunzi kwa utetezi kwamba hakuna ushahidi kwa kuwa mambo hayo hufanyika kwa siri.

Kungekuwa na idara hiyo ya ushauri, litokeapo jambo kama hilo mwanafunzi anaweza kushirikiana na washauri kwa kuweka mtego wa picha na kinasa sauti mbinu ambayo majuu imewaangamiza wahadhiri wengi na kuishia kwenda kufanya kazi za construction au warehouse kuendesha folk lift kwa hisani tu.
 
Back
Top Bottom