KakaJambazi
JF-Expert Member
- Jun 5, 2009
- 18,711
- 12,067
MWANAFUNZI mmoja wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Ualimu Dar es Salaam (Duce), ameuawa kwa kuchomwa kisu mara nne na mwanafunzi mwenzake kwa madai ya wivu wa mapenzi.
Inadaiwa mwanafunzi huyo, Bertha Mwarabu, 23, wa mwaka wa pili, alitofautiana na mpenzi wake, Masamba Musiba, 27, katika masuala ya mapenzi wakiwa katika hosteli ya wanafunzi wa Chuo Kikuu iliyopo Mabibo.
Tukio hilo limetokea juzi majira ya saa 2:30 usiku kwenye varanda ya Jengo 'C' la hosteli hiyo linalotumiwa na wanafunzi wa kike na kiume, lakini mauaji yalifanyika katika upande wa wanawake.
Kamanda wa Mkoa wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema Bertha alifariki njiani wakati akipelekwa Hospitali ya Wilaya ya Mwananyamala.
Kalunguyeye alisema baada ya tukio hilo, Musiba alijeruhiwa vibaya baada ya kushambuliwa na wanafunzi wengine na hivyo kukimbizwa katika hospitali hiyo hiyo kwa matibabu.
"Musiba anashikiliwa na polisi katika kituo kidogo cha polisi, Mbezi jijini hapa," alisema Kalunguyeye.
Inadaiwa Musiba alifanya tukio hilo baada ya marehemu Bertha kuvunja uhusiano wao wa kimapenzi.
Kwa mujibu wa habari kutoka kwa mashuhuda wa tukio hilo, Musiba alichukua uamuzi huo baada ya kubaini kuwa Bertha ameanzisha uhusiano mpya wa kimapenzi na mwanamume mwingine.
"Baada ya Musiba kubaini hilo, aliamua kumwadhibu. Alimchoma kisu mara nne, kimoja katika ziwa la upande wa kushoto, mara mbili tumboni na kusababisha utumbo kutokeza nje na kingine alimchoma kifuani. Kisu hicho kilipinda na mpini wake ukaanguka chini," alisema shuhuda huyo ambaye alikataa jina lake kuandikwa gazetini.
Habari zaidi zinasema wakati tukio linatokea, wanafunzi wengi walikuwa nje ya hosteli na hasa kwenye kiwanja cha mpira kilichopo eneo hilo wakiangalia tamasha la muziki.
Habari zinasema kabla ya kumshambulia kwa kisu msichana huyo, Musiba alimwita Bertha kwa ajili ya maongezi ambayo alitaka yafanyike ndani ya chumba ambacho msichana huyo alikuwa akiishi na wenzake watatu. Ilikuwa majira ya saa 2:00 usiku.
Wakati huo, Bertha alikuwa ametoka kujiandaa kwenda kuimba kwaya kwa ajili ya mazoezi ya Jumapili. Alikuwa ni mwanakwaya ya kanisa moja la Roma lililopo Bunju wilayani Kinondoni.
"Ndipo akaitikia wito na wakakutana chumbani humo. Waliyoyazungumza hatukuweza kuyajua, lakini ghafla tulisikia kelele za mwanamke na tulipofika tulimkuta Bertha akiwa amejiegemeza kwenye ukuta na damu nyingi zikiwa zimetapakaa koridoni huku akiwa ameshikilia sehemu ya utumbo ambao ulikuwa umejitokeza nje," alisema.
Mpashaji habari huyo alisema, Bertha alifanikiwa kuchoropoka chumbani mara baada ya kuonyeshwa kisu na alidondoka kwenye korido hiyo na ndipo zahama yote ikamkuta.
"Kuna dada mmoja alikuwa chumba kingine ambaye alisikia purukushani na alipochungulia akamwona Bertha anagaragara chini, ndipo alipoanza kupiga kelele za kuomba msaada," alisema.
Baada ya kufanya tukio hilo, Musiba alitokea kwenye moja ya dirisha na kuanza kukimbia, lakini baadhi ya wanafunzi waliokuwa chini ya ghorofa hilo walidhani kuwa ni mwizi na wakamkamata na kumpa kipigo.
Inaelezwa kuwa matatizo ya kutoelewana kati ya wawili hao yalianza baada ya Bertha kubaini Musiba anatumia vilevi vya pombe, bangi na sigara.
Inadaiwa kuwa Bertha alimkataza kuendelea kutumia vilevi hiyo kama alikuwa na nia ya kuendelea kuwa mpenzi wake, lakini hakujirekebisha.
"Bertha alimpa miezi mitatu ili jamaa aache kuvuta sigara, bangi na kunywa pombe, lakini jamaa alishindwa masharti hayo na ndipo uhusiano wao ukavunjika," alidai mpashaji huyo.
Taarifa tulizozipata kutoka kwa mtu wa karibu na Musiba zilidai kuwa, kabla ya kufanya tukio hilo, alinunua kisu kipya na alikusanya vitu vyake ikiwemo nguo.
"Juzi alinunua kisu kipya na alipakia vitu vyake kwenye mfuko aina ya 'Volcano'. Wakati huo mimi nilikuwa sijui ana lengo gani" alisema mtu huyo bila kutaja jina lake.
Uchunguzi unaonyesha kuwa, Musiba ni mwenyeji wa wilaya ya Musoma mkoani Mara, wakati Bertha ni mwenyeji wa Mkoa wa Morogoro.
Source: Mwananchi Read News
MUNGU AMLAZE MAHALI PEMA,AMEN
Inadaiwa mwanafunzi huyo, Bertha Mwarabu, 23, wa mwaka wa pili, alitofautiana na mpenzi wake, Masamba Musiba, 27, katika masuala ya mapenzi wakiwa katika hosteli ya wanafunzi wa Chuo Kikuu iliyopo Mabibo.
Tukio hilo limetokea juzi majira ya saa 2:30 usiku kwenye varanda ya Jengo 'C' la hosteli hiyo linalotumiwa na wanafunzi wa kike na kiume, lakini mauaji yalifanyika katika upande wa wanawake.
Kamanda wa Mkoa wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema Bertha alifariki njiani wakati akipelekwa Hospitali ya Wilaya ya Mwananyamala.
Kalunguyeye alisema baada ya tukio hilo, Musiba alijeruhiwa vibaya baada ya kushambuliwa na wanafunzi wengine na hivyo kukimbizwa katika hospitali hiyo hiyo kwa matibabu.
"Musiba anashikiliwa na polisi katika kituo kidogo cha polisi, Mbezi jijini hapa," alisema Kalunguyeye.
Inadaiwa Musiba alifanya tukio hilo baada ya marehemu Bertha kuvunja uhusiano wao wa kimapenzi.
Kwa mujibu wa habari kutoka kwa mashuhuda wa tukio hilo, Musiba alichukua uamuzi huo baada ya kubaini kuwa Bertha ameanzisha uhusiano mpya wa kimapenzi na mwanamume mwingine.
"Baada ya Musiba kubaini hilo, aliamua kumwadhibu. Alimchoma kisu mara nne, kimoja katika ziwa la upande wa kushoto, mara mbili tumboni na kusababisha utumbo kutokeza nje na kingine alimchoma kifuani. Kisu hicho kilipinda na mpini wake ukaanguka chini," alisema shuhuda huyo ambaye alikataa jina lake kuandikwa gazetini.
Habari zaidi zinasema wakati tukio linatokea, wanafunzi wengi walikuwa nje ya hosteli na hasa kwenye kiwanja cha mpira kilichopo eneo hilo wakiangalia tamasha la muziki.
Habari zinasema kabla ya kumshambulia kwa kisu msichana huyo, Musiba alimwita Bertha kwa ajili ya maongezi ambayo alitaka yafanyike ndani ya chumba ambacho msichana huyo alikuwa akiishi na wenzake watatu. Ilikuwa majira ya saa 2:00 usiku.
Wakati huo, Bertha alikuwa ametoka kujiandaa kwenda kuimba kwaya kwa ajili ya mazoezi ya Jumapili. Alikuwa ni mwanakwaya ya kanisa moja la Roma lililopo Bunju wilayani Kinondoni.
"Ndipo akaitikia wito na wakakutana chumbani humo. Waliyoyazungumza hatukuweza kuyajua, lakini ghafla tulisikia kelele za mwanamke na tulipofika tulimkuta Bertha akiwa amejiegemeza kwenye ukuta na damu nyingi zikiwa zimetapakaa koridoni huku akiwa ameshikilia sehemu ya utumbo ambao ulikuwa umejitokeza nje," alisema.
Mpashaji habari huyo alisema, Bertha alifanikiwa kuchoropoka chumbani mara baada ya kuonyeshwa kisu na alidondoka kwenye korido hiyo na ndipo zahama yote ikamkuta.
"Kuna dada mmoja alikuwa chumba kingine ambaye alisikia purukushani na alipochungulia akamwona Bertha anagaragara chini, ndipo alipoanza kupiga kelele za kuomba msaada," alisema.
Baada ya kufanya tukio hilo, Musiba alitokea kwenye moja ya dirisha na kuanza kukimbia, lakini baadhi ya wanafunzi waliokuwa chini ya ghorofa hilo walidhani kuwa ni mwizi na wakamkamata na kumpa kipigo.
Inaelezwa kuwa matatizo ya kutoelewana kati ya wawili hao yalianza baada ya Bertha kubaini Musiba anatumia vilevi vya pombe, bangi na sigara.
Inadaiwa kuwa Bertha alimkataza kuendelea kutumia vilevi hiyo kama alikuwa na nia ya kuendelea kuwa mpenzi wake, lakini hakujirekebisha.
"Bertha alimpa miezi mitatu ili jamaa aache kuvuta sigara, bangi na kunywa pombe, lakini jamaa alishindwa masharti hayo na ndipo uhusiano wao ukavunjika," alidai mpashaji huyo.
Taarifa tulizozipata kutoka kwa mtu wa karibu na Musiba zilidai kuwa, kabla ya kufanya tukio hilo, alinunua kisu kipya na alikusanya vitu vyake ikiwemo nguo.
"Juzi alinunua kisu kipya na alipakia vitu vyake kwenye mfuko aina ya 'Volcano'. Wakati huo mimi nilikuwa sijui ana lengo gani" alisema mtu huyo bila kutaja jina lake.
Uchunguzi unaonyesha kuwa, Musiba ni mwenyeji wa wilaya ya Musoma mkoani Mara, wakati Bertha ni mwenyeji wa Mkoa wa Morogoro.
Source: Mwananchi Read News
MUNGU AMLAZE MAHALI PEMA,AMEN