Shukurani
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 253
- 11
Akataa kuteta na wabunge
*Ni mpaka atangaze Baraza la Mawaziri
* Walikwenda kumwona warudi patupu
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
RAIS Jakaya Kikwete jana amekataa kukutana na wabunge na baadhi ya waliokuwa mawaziri hadi hapo atakapotangaza Baraza jipya leo.
Habari za kuaminika kutoka Ikulu ya Chamwino mjini Dodoma, zinasema kwamba Rais Kikwete jana aliwaambia wasaidizi wake kuwa hataki kukutana na wabunge wala mawaziri waliopita hadi leo baada ya kutangaza kwa Baraza jipya.
"Rais amekataa miadi ya aina yoyote na wabunge na waliokuwa mawaziri mpaka Jumatatu baada ya kutangazwa kwa Baraza la Mawaziri," kilisema chanzo cha habari kutoka Ikulu ya Chamwino.
Habari zaidi zinasema kwamba jana kuna mbunge ambaye alikuwa waziri kamili alikwenda kwa lengo la kuonana na Rais, lakini alikataliwa kwa maelezo kuwa kiongozi huyo wa nchi ametoa maagizo kwamba ataonana na watu baada ya kutangazwa kwa mawaziri wapya.
"Huyu alikuwa waziri kamili, ni rafiki yake Rais, lakini amekataliwa kumuona na hii ni ishara kwamba hataki kuteua watu ambao ni rafiki zake," alisema.
Jana mchana Rais, Makamu wa Rais Dk Mohammed Shein walikuwa na kikao kwa ajili ya kuchambua majina ya watakaokuwa mawaziri.
Rais Kikwete alivunja Baraza la Mawaziri juzi baada ya kuridhia kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na anatarajiwa kutangaza jingine leo na kuwaapisha Jumatano.
Katika maeneo mengi ya mji wa Dodoma, wabunge wamekuwa wakiuliza kuhusiana na majina yatakayokuwako katika baraza hilo.
*Ni mpaka atangaze Baraza la Mawaziri
* Walikwenda kumwona warudi patupu
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
RAIS Jakaya Kikwete jana amekataa kukutana na wabunge na baadhi ya waliokuwa mawaziri hadi hapo atakapotangaza Baraza jipya leo.
Habari za kuaminika kutoka Ikulu ya Chamwino mjini Dodoma, zinasema kwamba Rais Kikwete jana aliwaambia wasaidizi wake kuwa hataki kukutana na wabunge wala mawaziri waliopita hadi leo baada ya kutangaza kwa Baraza jipya.
"Rais amekataa miadi ya aina yoyote na wabunge na waliokuwa mawaziri mpaka Jumatatu baada ya kutangazwa kwa Baraza la Mawaziri," kilisema chanzo cha habari kutoka Ikulu ya Chamwino.
Habari zaidi zinasema kwamba jana kuna mbunge ambaye alikuwa waziri kamili alikwenda kwa lengo la kuonana na Rais, lakini alikataliwa kwa maelezo kuwa kiongozi huyo wa nchi ametoa maagizo kwamba ataonana na watu baada ya kutangazwa kwa mawaziri wapya.
"Huyu alikuwa waziri kamili, ni rafiki yake Rais, lakini amekataliwa kumuona na hii ni ishara kwamba hataki kuteua watu ambao ni rafiki zake," alisema.
Jana mchana Rais, Makamu wa Rais Dk Mohammed Shein walikuwa na kikao kwa ajili ya kuchambua majina ya watakaokuwa mawaziri.
Rais Kikwete alivunja Baraza la Mawaziri juzi baada ya kuridhia kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na anatarajiwa kutangaza jingine leo na kuwaapisha Jumatano.
Katika maeneo mengi ya mji wa Dodoma, wabunge wamekuwa wakiuliza kuhusiana na majina yatakayokuwako katika baraza hilo.