Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,339
- 51,883
GWAJIMA UNAIKUMBUKA HII? NGOJA NAWE UKERWE
Na, Robert Heriel
Wewe uliwakera wenzako, uliwanyima mate kooni. Uliwachachafya mimbarini mbele ya waumini wako. Ulijisikia raha bila karaha. Tena kwa mdomo mpana hukuwa na simile wala machale ya kuwa nawe siku moja utaingia kwenye kumi na nane za unaowakera.
Ati ulisema ukweli, Ukweli?
Gwajima nitakukumbusha kidogo kidogo kero ulizowafanyia watu. Hii ni kero ya tatu.
Naomba ninukuu kukukumbusha;
"Dini ya kiislamu ni ya majini na niya mpinga Mkristo; Dini ya Kikatoliki niya kwenye nchi na niya nabii wa uongo. Shauri yako kama utakerwa, ila natakiwa nikusaidie"
Hata kama dini yetu iwe ya mashetani wewe inakuhusu nini?
Hata tuabudu majini na mizimu, wewe unapungua wapi?
Hata kama tuabudu mpinga Kristo inakukera nini?
Tukiabudu dini ya Nabii wa uongo inakuwasha washa nini?
Nani alihitaji msaada wako?
Unaita dini za wenzako ni za majini kwani walikuja kusalia kanisani kwako? Au walikuja nyumbani kwako kufanya ibada zao? Nini kinakukera?
Tunakubali sisi dini zetu ni za majini na mpinga Kristo, ya kwako ndio ya malaika na Yesu Kristo.
Tunakubali dini zetu niza nabii wa uongo ila ya kwako ndio ya nabii wa kweli.
Sasa kama ulitaka kutukera utasubiri sana.
Muda wa Kukerana umefika, wewe si ulijisikia raha kuongea na kupata sifa. Sawa. Subiri nasi tutajibu mapigo october.
Jambo moja nikupongeze, hongera Sana nilikuona na Mzee Pengo juzi juzi, Bila shaka ulimuomba msamaha.
Sasa unakazi ya kuomba msamaha wenye dini za majini na mpinga Kristo, wenye dini za Nabii ya uongo ambao umewataja wewe mwenyewe kwa jina kabisa.
Hivi huko Kawe hakuna wenye hizo dini ulizozitaja hapo juu? Kama wapo basi subiri Kukerwa.
Tumekubali sisi tunaabudu majini
Tumekubali dini yetu niya nabii wa uongo
Tukikuchagua ujue tumekubali kuwa dini zetu ndivyo ulivyozitaja
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Dar es salaam
Na, Robert Heriel
Wewe uliwakera wenzako, uliwanyima mate kooni. Uliwachachafya mimbarini mbele ya waumini wako. Ulijisikia raha bila karaha. Tena kwa mdomo mpana hukuwa na simile wala machale ya kuwa nawe siku moja utaingia kwenye kumi na nane za unaowakera.
Ati ulisema ukweli, Ukweli?
Gwajima nitakukumbusha kidogo kidogo kero ulizowafanyia watu. Hii ni kero ya tatu.
Naomba ninukuu kukukumbusha;
"Dini ya kiislamu ni ya majini na niya mpinga Mkristo; Dini ya Kikatoliki niya kwenye nchi na niya nabii wa uongo. Shauri yako kama utakerwa, ila natakiwa nikusaidie"
Hata kama dini yetu iwe ya mashetani wewe inakuhusu nini?
Hata tuabudu majini na mizimu, wewe unapungua wapi?
Hata kama tuabudu mpinga Kristo inakukera nini?
Tukiabudu dini ya Nabii wa uongo inakuwasha washa nini?
Nani alihitaji msaada wako?
Unaita dini za wenzako ni za majini kwani walikuja kusalia kanisani kwako? Au walikuja nyumbani kwako kufanya ibada zao? Nini kinakukera?
Tunakubali sisi dini zetu ni za majini na mpinga Kristo, ya kwako ndio ya malaika na Yesu Kristo.
Tunakubali dini zetu niza nabii wa uongo ila ya kwako ndio ya nabii wa kweli.
Sasa kama ulitaka kutukera utasubiri sana.
Muda wa Kukerana umefika, wewe si ulijisikia raha kuongea na kupata sifa. Sawa. Subiri nasi tutajibu mapigo october.
Jambo moja nikupongeze, hongera Sana nilikuona na Mzee Pengo juzi juzi, Bila shaka ulimuomba msamaha.
Sasa unakazi ya kuomba msamaha wenye dini za majini na mpinga Kristo, wenye dini za Nabii ya uongo ambao umewataja wewe mwenyewe kwa jina kabisa.
Hivi huko Kawe hakuna wenye hizo dini ulizozitaja hapo juu? Kama wapo basi subiri Kukerwa.
Tumekubali sisi tunaabudu majini
Tumekubali dini yetu niya nabii wa uongo
Tukikuchagua ujue tumekubali kuwa dini zetu ndivyo ulivyozitaja
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Dar es salaam