GSM yatangaza kujiondoa kwenye udhamini mwenza wa Ligi Kuu Tanzania Bara

ESPRESSO COFFEE

JF-Expert Member
Sep 6, 2014
6,170
7,661
1644311230822.png


Kampuni Ya GSM, Leo Tarehe 07/02/2022 imetangaza kujiondoa Kwenye Udhamini Mwenza Wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Ikimbukwe kuwa Kampuni Ya GSM iliingia Makubaliano Ya Kuidhamini Ligi Kuu Tanzania Bara Na Kuweka Dau la Bilioni 2.5.

Lakini Udhamini Huo Ulipingwa Vikali na Simba Sc huku Vilabu vingine 16 vyote vya Ligii kuu Tanzania Bara Vikiridhia Udhamini Huo, Lakini Kwa Sasa GSM wamejiondoa Na Si wadhamini Tena.

Leo Kampuni Ya GSM imeeleza Ya Sababu Ya Kujitoa kuwa ni Kwasababu, TFF na Bodi La Ligi Kushindwa Kutimiza Matwaka ya Kimkataba.

Bado Haijaelezwa Wazi Matakwa Hayo ya Kimkataba ni Yapi Ambayo TFF na Bodi Ya Ligi Hawajatimiza hadi kupelekea Mkataba kuvunjwa. Lakini moja Ya Matakwa ya Kimkataba ilikuwa ni Vilabu Vyote kuvaa Nembo ya Mdhamini Upande Mmoja Wa Bega katika Jezi na Simba Sc Ndio Club Pekee iliyokuwa haijafanya Hayo.

Takwa jingine ilikuwa ni Mabango ya Mdhamini mwenza kuwepo Uwanjani lakini Simba Sc Ilipinga vikali na kutokuweka mabango hayo katika Mechi Zake.

gsm.jpg

Kwenu Studio
 
Hahaha angalau timu ziliweza toa ushindani kwa timu kubwa, yanaenda kujirudia ya timu A kukodiwa fuso na timu B alafu wanaipiga 8 bongo ngumu mno
 
Kampuni ya GSM imetangaza kujiondoa udhamini wa Ligi Kuu ya Tanzania NBC Premier League ikielezwa sababu ni TFF na Bodi ya Ligi Kuu kutotimiza makubaliano ya kimkataba.

NB: Isiishie kujiondoa udhamini tu.. Nadhani mamlaka husika ianze mara moja kuchunguza kuhusu huu mkataba kati ya GSM na TFF na Bodi ya Ligi Kuu

Lazima kuna jambo lisilo la kawaida ambalo huenda ingeathiri afya ya michezo kwa ujumla.

Asante TFF pamoja na Bodi ya Ligi kuitema Ndoano..!
 
SABABU ZA JIESIEM KUONDOLEWA KWENYE UDHAMINI WA LIGI KUU TANZANIA.
1. CAF.
Shirikisho la soka Afrika limeiandikia barua TFF kuwaonya kwa kushiriki uhuni kwenye mpira wa miguu. Hii inatokana na namna mwenendo wenyewe wa ligi unavyoenda, yaani timu yenye ushindani na Yanga inafanyiwa figisu nyingi sana nje ya uwanja.

Na baada ya JIESIEM hawa kujitoa tayari Yanga imeanza kusuasua kwani jiesiem anakosa nguvu ya moja kwa moja kwa timu ndogo. Ama niweke wazi ni kuwa katika 2.5B,JIESIEM walibakia na 500M ili kuzipa ruzuku timu ndogo pale zinapokutana na Simba.

2. 500M zinaelekea kuisha na ndio kwanza round ya 2 bado
Hapa nampa kongole sana jiesiem kwani ameng'amua mapema kuwa akiendelea kutoa zile 10M ili simba ifungwe au Yanga ishinde basi atafilisika, hivyo amebaki ma change ya 17.8M
 
Afisa Biashara Mkuu wa GSM, Alan Chonjo amezungumza kwa niaba ya uongozi wa GSM na kusema kuwa wamejiondoa katika nafasi ya udhamini mwenza wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Ameeleza kuwa sababu kubwa ya kujiondoa ni kutokana na yaliyotokea baina ya TFF na Bodi ya Ligi, ikumbukwe kuwa lengo lilikuwa ni kukuza tasnia ya michezo, na GSM ilifanya hivyo kama mdau kukuza tasnia ya mpira wa miguu.

“Maamuzi ya kujitoa hayakuwa maamuzi mepesi kwetu, lakini tumeamua kuchukua maamuzi magumu. Tunawatakia kila la kheri na tutaendelea kuacha milango wazi kwa ajili ya kukuza mchezo wa soka Tanzania,” amesema na kuongeza:

“Vipengele vipo na tumeshawaandikia barua TFF kuwajulisha juu ya hilo.

“Kuhusu suala la Serikali kwenda FCC sitaweza kulizungumzia, kuhusu udhamini wa klabu (Yanga) lipo palepale.”

Kumekuwa na mawasiliano kati yetu na TFF, kuna baadhi ya mambo ya kimkataba tumeona hayajaenda kama tulivyopanga.
 
Back
Top Bottom