Growing up African-EA Tv

Donkey

JF-Expert Member
Dec 17, 2010
1,431
1,448
Nimekuwa nikiangalia kipindi cha growing up african kinachorushwa na EA TV, Kuelezea maisha ya watanzania wanaoshi marekani, kwa kweli inasikitisha sana, tunaonyeshwa nini hasa kwa manufaa na maendeleo ya wana africa mashariki ? kujaribu kuongea kingereza kama wamerekani, kuonyeshwa nyumba wanazo ishi na mengineyo, je mbona huwatuambii ukweli wana fanya kazi gani, kwa mimi niliyefika kule najua mengi na watu wanahangaika sana kwa kufanya kazi za hovyo na hata kuuza mwili kupitia web camera.

Kwanini wasingekuwa wanaongea kiswahili ? kweli utumwa bado upo, ndani ya marekani kuna wa spanish,ni watu wanaojali lugha yao sana.

kwa yule ambaye hajafika angalia usije ukapotea ukaona kama ni maisha mazuri sana-ni lazima ufanye kazi ili uishi na wabongo wengi sasa wanarudi nyumbani
 
Back
Top Bottom