Gray Mgonja, mwenye kuonja vinavyoonjwa!

Ben Saanane

JF-Expert Member
Jan 18, 2007
14,581
18,123
Heshima yenu wakuu,

Kila nikisikia na kusoma sakata zima la BOT na jinamizi zima la ufisadi jinsi linavyotishia uhai wa Taifa letu Tukufu Tanzania na wananchi wake,huwa ninapata uchungu mkali kwani kwa dhamana na Ridhaa ya watanzania waliokua wanahimizwa kwa kampeni chungu nzima za kuhamasisha uandikishaji na upigaji kura na hatimaye kuwapa baadhi dhamana halali za kuongoza achilia mbali wale wliotumia njia haramu kuhalalisha ridhaa bado kwa miaka mingi sasa tumejitahidi kuvumilia aidha kutokana na asili za malezi yetu au kwa kuzidiwa na vitisho,dharau , kejeli na matusi yaliyopindukia kutoka kwa viongozi walewale waliotokana na Dhamana yetu huku wakimis-use the term "Gorvernment servant".Eti wao ni watumishi wa serikali .

Pia,naona itakua ni jambo la busara na la ujasiri na la kuonyesha mfano wa kukataa na kupambana na mfumo au kasumba ya kutoreact dhidi ya mawaziri wanaotusababishia umaskini.Leo hii ukiangalia Japan serikali yao ina nidhamu kwani kuna kasumba ya kuwajibisha au ya mhusika kuwajibika mwenyewe pale linapotokea suala linalomuhusu mtumishi wa serikali ktk kuhusika na ubadhirifu.Ukiangalia nchi zilizopiga hatua Afrika hgakuna utovu mkubwa wa nidhamu kama uliopo hapa Tanzania.

Hivyo basi kama tunayo nia ya kujenga taifa lenye uchumi mkubwa linaloheshimika duniani na linalojitahidi kuinua hali ya maisha ya wananchi wake basi sisi kama kikundi flani chenye maslahi tunaweza kuanzia hatu hiyo huku tukimulika wale ambao wanabomoa huku tulikoanza kujenga,basi kwenye hili sakata la BOT kama tunataka kumkaripa na kumwajibisha Bi.Zakia Meghji,basi hatuna Budi kumuwajibisha Basil Pesambili Mramba na Katibu wa wizara Mhe.Mgonja kwani hawa kwa nafasi zao wangeweza kuwa kiini cha kuokoa maisha ya Watanzania kadhaa waliofarikia au kuwa maskini ambao walisababishwa na upotevu wa fedha hizo.

Kwa mfano huyu mhe.Mramba amekua mtu wa matusi na ambaye ameliingizia taifa hasara kubwa huku akitoa majibu ya kejeli na Matusi kwa watanzania waliompa dhamana ya kuwa hapo alipo

Rejea kauli zake za kutetea Ununuzi wa ndege ya Rais,Rada nk
Rejea utetezi wake wa safari za Rais
Rejea hotuba za mkutano wake wa kisiasa huko Jimboni kwake Rombo baada ya Bunge kupitisha bajeti tata na iliyokua na udhaifu mkubwa akiwa waziri wa Miundombinu hapo mwaka juzi.

Kwa jamii iliyostaarabika na yenye kuangalia huko mbele tuendako na kujal hali ya vizazi vyetu vya baadae na KUFUTA KABISA huu utovu wa nidhamu wa viongozi wetu basi baada ya huyu mheshimiwa kuruka vizingiti vyote basi ni muda muafaka kwetu kuanzisha kampeni au mchango wowote wa kumwajibisha waziri huyu.

Mtanzania yoyote mwenye uchungu na nchi yako jitolee kwa jasho na Damu kuliokoa Taifa letu.Kumbuka Amerika ilijengwa kwa Moyo wa wananchi na viongozi wenye uchungu na nchi yao na wenye uzalendo wa kweli.Sasa tuanzie hapa tulipo kwa Tanzania inawezekana tu.

Mungu ibariki Tanzania

Naomba kutoa hoja
 
Mkuu,
Utamaduni wa kujiuzu has gone with the wind. Tukianza kutoa list ya wanatakiwa kujiuzulu nchi si ni wengi tu Msolla(Sakata la Ukraine, Karamagi(Buzwagi),Sitta(Hoja ya BOT),Ballali(Ye si ndo alitoa mpaka press conference).

Mimi nathani kurisign is a big honor for mafisadi. They should be fired and sent pale Segerea. Lakini nani wa kumfunga paka kengele?

"THERE IS HONOR AMONG THIEVES"-Geofrey Archer.
 
Mkuu nadhani tukianza na pressure kama aliyofanyiwa Ballali hata mkuu wa kaya ataogopa na atamfukuza kazi.

Pia si unakumbuka ya Omari Mahita? Ilibidi mkuu aepuke lawama na kumtolea nje

Sasa na hawa inabidi siafu tuandamane
 
Kama kuna jina la Mtanzania??? ambaye jina lake linatajwa katika madili machafu ya nchi hii na ambaye hadi hivi sasa hakuna mwenye kuthubutu kumwajibisha ni huyu Bwana.
Tpic1.jpg
Jina lake linatokea sehemu nyingi katika mazingira ya kifisadi hadi inawezekana neno ufisadi linapotajwa basi jina lake haliko mbali. Hata hivyo licha ya kutajwa kuanzia kwenye:

IPTL
Richmond
Tangold
Mwananchi
n.k

Huyu bwana hagusiki; anaendelea kutia sahihi mikataba mibovu kama alivyofanya hivi karibuni alipoidhisha udhamini wa serikali kwenye dege la Airbus baada ya kuchelewesha udhamini huo kwa miezi karibu sita bila maelezo ya kueleweka na kusababisha ATC ilipe faini ya mamilioni ya shilingi.

Nashindwa kuelewa huyu ndugu ana ubia gani na serikali? Je ni kitu gani kitatokea nchini endapo atatimuliwa kazi au kupangiwa shughuli nyingine isiyohusiana na fedha?

It boggles my mind!! Kwa sababu kama ningekuwa fisadi, ningependa kuwa Gray Mgonja.

On the other hand though... kuanguka kwake kuko karibu sana na ningekuwa yeye ningeomba nipumzike na kujiondoa taratibu kwani vya jikoni vinasema vimeiva..
 
Huyu jamaa ni fisadi mkubwa kama Dalali oops I meant Balali. JK anajua kabisa kuwa akimtimua jamaa anaweza kunyea kambi. Unaweza kusikia kateuliwa kuwa balozi somewhere ili mradi tu afiche kile anachokijua.
Labda tutumie njia ile kama tuliyoitumia kwa Chenge kumpa vidonge JK ili aone juwa wananchi are very serious about UFISADISM. Huyu jamaa sioni tofauti yake na Balali au Chenge. Tofauti kubwa inaweza kuwa ni ya KIJIOGRAFIA lakini mambo mengine wanafanana.
 
27.09.2007 0910 EAT
Mgonja kama Karamagi

*Naye kuwashitaki Slaa, Mwanahalisi, Printech

Na Reuben Kagaruki

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Fedha, Bw. Gray Mgonja, ametangaza rasmi kumburuta mahakamani Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Willbrod Slaa, kwa alichodai ni kuchafuliwa jina kwa tuhuma za ufisadi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam jana, Bw. Mgonja, alisema amefikia uamuzi huo kwa sababu tuhuma zilizotolewa dhidi yake katika mkutano wa hadhara uliofanyika Mwembeyanga hivi karibuni, si za kweli.

"Nitafungua kesi mapema iwezekanavyo, kwa sababu nimechafuliwa jina na tuhuma zimetolewa kwa nia mbaya ya kunipaka matope, hasa nikizingatia uadilifu wangu katika utumishi wa umma kwa miaka 33," alisema Bw. Mgonja.

Mbali ya Dkt. Slaa, alisema ataliburuza mahakamani gazeti la Mwanahalisi na kiwanda cha Printech kwa kusambaza taarifa alizodai kuwa za uongo.

Alisema tuhuma hizo haziwezi kumfanya ajiuzulu wadhifa wake kwa sababu si za kweli. Alisema kazi ya kumfikisha Dkt. Slaa mahakamani inafanywa na mawakili wake. Hata hivyo alikataa kutaja majina yao.

Alipoulizwa anatarajia kudai fidia kiasi gani, alisema suala hilo pia linashughulikiwa na mawakili wake. Alipotakiwa na waandishi wa habari aeleze ukweli kuhusiana na tuhuma zilizotolewa dhidi yake, Bw. Mgonja, alisema kwa sasa hawezi kuziongelea, kwa sababu huo ndio utakuwa utetezi wake mahakamani.

Alisema tuhuma alizotupiwa ni pigo kubwa kwake, hivyo hana njia nyingine ya kujitetea zaidi ya kumfikisha Dkt. Slaa mahakamani.

Bw. Mgonja alisema anamburuta mahakamani Dkt. Slaa yeye binafsi na si kwa kutumia wadhifa wake wa ukatibu Mkuu wa Hazina.

Alisema majibu ya tuhuma dhidi yake akiwa Katibu Mkuu Hazina, zitatolewa na Serikali. Alipoulizwa iweje atumie raslimali za Serikali kukanusha tuhuma zinazomkabili yeye binafsi, Bw. Mgonja alisema aliomba kutumia ukumbi wa mikutano wa ofisi yake ili kuzungumza na waandishi wa habari.

Ingawa Bw. Mgonja alisema anakanusha tuhuma dhidi yake binafsi, taarifa aliyoitoa kwa vyombo vya habari kuhusiana na nia yake ya kumfikisha Dkt. Slaa mahakamani ilikuwa imechapishwa kwenye karatasi zenye nembo ya Serikali.

Bw. Mgonja alipoulizwa kama tuhuma dhidi yake na viongozi wa Serikali zimeanza kuiathiri nchi kwa kunyimwa misaada, alisema hakuna kitu kama hicho.

"Kama tuhuma zingekuwa za kweli nchi ingeathirika, lakini kwa sasa hakuna kitu kama hicho."

Kuhusu kauli ambazo zimekuwa zikitolewa na mabalozi wakiitaka Serikali kuzitolea ufafanuzi, Bw. Mgonja alisema: "Hatufuati maneno ya mabalozi, wao wana vikomo vyao, sisi ni nchi."

Alipoulizwa ni kwa nini tuhuma hizo zitolewe dhidi yake na si kwa makatibu wakuu waliomtangulia, Bw. Mgonja alisema hali hiyo inaweza kuwa imechangiwa na upana wa demokrasia. Alisema tuhuma dhidi yake zina viashiria vya kisiasa.

Bw. Mgonja alipoulizwa anamiliki mali kiasi gani alizochuma katika kipindi chake cha utumishi wa Serikali, alijibu kuwa ni ndogo sana.

"Nina mali kidogo sana na mara kwa mara nimekuwa nikijaza fomu (za kuanisha mali ) na kuzipeleka Utumishi wa Umma, kuna taratibu zake, mnaweza mkaenda mkaomba mkapewa ili muone," alisema Bw. Mgonja.

Kuhusu tuhuma zilizotolewa dhidi ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Mgonja hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo akisisitiza kuwa ni chombo kinachojitegemea. Hata hivyo alisema tuhuma hizo nazo zina majibu yake.

Bw. Mgonja anakuwa kiongozi wa pili kutangaza kufungua kesi mahakamani dhidi ya tuhuma hizo.

Juzi Waziri wa Nishati na Madini, Bw. Nazir Karamagi, alitangaza kumpeleka mahakamani, Dkt. Slaa na wenzake, kwa kile alichosema ni kumchafulia jina na kuonekana kuwa mtu asiyefaa mbele ya jamii.
 
hahahhah inatia sisimua sana wajuaa tulijua its matter of 3 days ngoma ingekuwa inaunguruma mahakamani duuu amekimbiaa kivuli chake?mbona hatujamsikia tenaa??au alikuwa anamtutishia nyau?jamaa ni kweli hagusiki..ila nilishasema huko nyuma kuwa ndani ya sirikali.........wote wanaogopanaaaaaaaa.......hakuna anaeweza kumgusaaaa mwenzake maana wote wanalindanaa na wanajuanaa maovu yaoo
 
Kituumacho wengi, ni kwa nini TAKUKURU, MKUU WA POLISI, WASIMDHIBITI HUYU BWANA, au wanamgawo wanagawiwa?
 
.....huyu jamaa hana uchungu ..mkewe na watoto wanatesa hapo VEGAS ..usa,ambako wanamiliki nyumba ..so hapa yupo peke yake tu,

huku wife akitesa na dogodogoz wa kikenya , Ghana, na Nigerians... kwenye jiji la mastaa... ambako tayari ni RESIDENT..ITS matter of time kabla na yeye haja wajoin huko...

lakini another side of the coin jamaa wanamsifia kuwa ana akili nyingi ...ndio maana hadi leo anadunda!!
 
Nasikia huyu jamaa nooma sana viongozi wote hapo serikalini akina Luhanjo wanamgwaya sana amejizindika balaa kamekula mizizi balaa hakuna anaye mgusa huyu atakuwepo na ataendelea kuwepo.
Jk mwenyewe kasalimu amri richa ya kelele zote tunazopiga lakini kenyewe rahaaaaa mstarehe....Haka ndo kabingwa ka kusuka dili chafu serikalini JK mwenyewe akamemsukia dili lileeee la uchaguzi kamechota mihela jamaa huyoo kashindwa kwa tsuname sasa nani atakaye mtoa wakati yeye ana ubia na uraisi wa JK kwa 50% katadumu tu panga pangua.MM naona haka kajamaa dawa ni kukapiga mawe au tukaaue tu kwa styre ileile wanayo ulia viongozi kwani iwa hata maji iwa hawaombi mtu anachomoka huku akitembea kesho majibu ya madakitari mtasikia shinikizo la damu hii ndo dawa.
 
lakini another side of the coin jamaa wanamsifia kuwa ana akili nyingi ...ndio maana hadi leo anadunda!![/B]

Hii mimi sina uhakika nalo. Inawezekana kwa wale ambao tayari ameishakuwa nao ndio anawazidi.

Ukiwa FISADI hata kama una akiri kiasi gani sidhani kama hiyo inatakiwa iwe hoja.

Akili ni pale ambapo inatumika katika kuleta maendeleo, lakini ikitumika ktk upande wa pili hiyo siyo akili tena.
 
Kama kuna jina la Mtanzania??? ambaye jina lake linatajwa katika madili machafu ya nchi hii na ambaye hadi hivi sasa hakuna mwenye kuthubutu kumwajibisha ni huyu Bwana.
Tpic1.jpg
Jina lake linatokea sehemu nyingi katika mazingira ya kifisadi hadi inawezekana neno ufisadi linapotajwa basi jina lake haliko mbali. Hata hivyo licha ya kutajwa kuanzia kwenye:

IPTL
Richmond
Tangold
Mwananchi
n.k


Huyu bwana hagusiki; anaendelea kutia sahihi mikataba mibovu kama alivyofanya hivi karibuni alipoidhisha udhamini wa serikali kwenye dege la Airbus baada ya kuchelewesha udhamini huo kwa miezi karibu sita bila maelezo ya kueleweka na kusababisha ATC ilipe faini ya mamilioni ya shilingi.

Nashindwa kuelewa huyu ndugu ana ubia gani na serikali? Je ni kitu gani kitatokea nchini endapo atatimuliwa kazi au kupangiwa shughuli nyingine isiyohusiana na fedha?

It boggles my mind!! Kwa sababu kama ningekuwa fisadi, ningependa kuwa Gray Mgonja.

On the other hand though... kuanguka kwake kuko karibu sana na ningekuwa yeye ningeomba nipumzike na kujiondoa taratibu kwani vya jikoni vinasema vimeiva..

Mzee Mwanakijiji,
Najua utakasirika kama ambavyo ulifanya katika thread nyingine zinazohusu ATCL ambapo nilionyesha wasiwasi wangu wa kuhujumu maoni ya wachangiaji kutokana na uswahiba au undugu ulionao na David Mattaka.

Sihitaji PhD au microscope kujua kuwa lengo lako ni kufikisha ujumbe wa Mattaka kwa Mgonja. Si nia yangu kutetea mabaya ya Mgonja (kama yapo) lakini ipo haja ya kupiga vita ufisadi kama huu wako.
 
Mzee Mwanakijiji,
Najua utakasirika kama ambavyo ulifanya katika thread nyingine zinazohusu ATCL ambapo nilionyesha wasiwasi wangu wa kuhujumu maoni ya wachangiaji kutokana na uswahiba au undugu ulionao na David Mattaka.

Sihitaji PhD au microscope kujua kuwa lengo lako ni kufikisha ujumbe wa Mattaka kwa Mgonja. Si nia yangu kutetea mabaya ya Mgonja (kama yapo) lakini ipo haja ya kupiga vita ufisadi kama huu wako.

Pundamilia,

na wewe umeanza kuwa "Chinga", naomba tafadhali onesha ushahidi ulio nao wa undugu wangu na Matakka maana hii ni mara nyingine umerudia jambo hili. Matakka ni fisadi kama mafisadi wengine tu.
 
Mwanakijiji,

Chapa mzigo. Hizo hoja achana nazo kabisa.

Ukiona mtu kama huyu anakuletea naomba nitupia mie mpira nianze kumla chenga!
 
This may not have a bearing on this issue of longevity of Mr. Mgonja in the system but in this case of ATC it may well be the fact that Mgonja and Mataka [ATC CEO] were classmates in Kibaha from Form I to IV in 1965 to 68 may have catalyzed the process of signing for the Airbus plane after the departure of Chenge. Ironically another student in the same school was J Jakaya Mrisho Kikwete who was in Form I to IV during 1965 to 69.
 
mamaaaa hizi ndizo zinaitwa data...

hivyo matakka, mgonja, na kikwete ni Schoolmates eh..?
Mzee Mwanakijiji,

Connecting to the dot.. Mwanyika alimaliza Mlimani mwaka 1973 huku chenge alimaliza pale pale Faculty of Law 1975..unadhani kwanini wanapata wapi viburi hivi??na kipindi hiki ndicho Jk naye alikuwapo pale Mlimani.They know each other since then.
 
duh.. yaani kuna kacircle fulani ka ushirika... kwa hiyo yawezekana tunachovuna sasa kilipandwa zamani sana...
 
duh.. yaani kuna kacircle fulani ka ushirika... kwa hiyo yawezekana tunachovuna sasa kilipandwa zamani sana...
Hili suala mie nilishawahi kulitilia mashaka sana,mpakwa mwaka juzi baada ya Jk kumaliza kuhutubia bunge kwa mara ya kwanza pale dodoma,Katika Hafla ya usiku ule nikaja kugundua hawa waheshimiwa ni marafiki wa muda mrefu pamoja na Mkuu wetu wa majeshi wa sasa...

ukichimba zaidi utajua urafiki wa Lowassa na Rostam ulianzia wapi,na utajua ni kwanini Rostam wakati Mwalimu alipokuwapo alikuwa hana sauti katika Chama.utamfahamu na aliyemharibu Mkapa.

Ngoja nikwambie kwanini mwalimu alimwamini sana Mkapa,wakati mkapa yuko pale foreign aliweza kudhibiti ubadhirifu uliokuwa unatokea pale na pia alikuwa akirudisha pesa hazina kama zikibadi tufauti na mawaziri wengine ambao walikuwa wansema Ruksa kutumia pesa iliyobaki,hapa akiwamo na yule ambaye kura zake hazikutosha 1995,yule rrafiki yake na mkurugenzi wa Tanzania Explorerers,nmazungumzia msanii na Muungwana ambaye ni rafiki yake na Lowassa.Mwanakijiji unamfahamu??
 
wenyewe wanajiita vichwa vya mlimani.
vichwa kweli kweli, maana wanahujumu kwenda mbele. wanafanya nchi kama chakula cha mchana kwenye canteen ya hcuo, wanagaiana vitoweo na chachandu, huku wanapiga soga kwa staarehe.
ama kweli, wajinga ndo waliwao
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom