Elections 2010 Graduate, Mtoto wa Fukara, Shabiki wa CCM

Ng'wanangwa

JF-Expert Member
Aug 28, 2010
10,827
4,172
Ninawasikitikia sana vijana wa Tanzania. Vijana wanaotokea familia masikini, mafukara ambao wazazi wao wanaishi kwenye nyumba za tembe na kulala kwenye vitanda vya ngozi za ng'ombe.

Vijana wamejaaliwa vipaji vya elimu. Wazazi wao (wanaoshabikia CCM kwa sababu wanafikiri Nyerere bado yupo hai) wamejikamua kuuza mifugo na mazao wapate elimu. Baadhi ya vijana hawa wamepata bahati ya kufika vyuo vikuu na kupata shahada na stashahada. Wapo mijini. Hawataki kurudi vijijini kwa sababu vijijini hakuna umeme. Vijijini hakuna zahanati na hospitali. Vijijini hakuna lami. Vijijini hakuna daladala wala taxi. Wala vijijini hakuna warembo kama huku mjini. Vijini kupata ‘netweki’ ya simu ni ishu. Vijijini kuchaji simu mpaka ulipie sh. 500 kwa mtu mwenye jenereta.

Mmmh! Vijana. Wasomi. Wanafanya mambo ya aibu. Wanakula takrima za CCM na kufanywa makamanda wa Green Guard. Wanafanya kazi ya kuratibu ugawaji wa fulana na kofia za CCM. Wanasafirishwa kwa malori na wengine kupoteza maisha kwenye ajali kwa ajili ya kuwatumikia mafisadi, wakati watoto wa mafisadi wako Upanga wanagombania rimoti za TV na kupunguza/kuongeza ubaridi wa viyoyozi.

Vijana masikini wa Tanzania wamesahau shida walizonazo wazazi wao. Wamesahau kuwa CCM na watawala wake wanaokula rushwa ndiyo chanzo cha matatizo yote ya nchi hii.

Tanzania inawalilia enyi vijana kutoka familia masikini za Tanzania. Jitengeni na CCM. Waacheni watoto na ndugu zao ndiyo wawe wapambe wao kwenye mikutano yao. Jiungeni na kundi la ukombozi.

Wakati ni huu. 2015 ni kesho tu.
 
Naunga mkono hoja.ni aibu sana! Huwa tunajifikiria *2,w need a change,to change for gud
 
Hoja ni nzito na ya kina naunga mkono kwa nguvu zote na kama tuna nia nzuri naTaifa hili tujipange zaidi kuanzia shule za sekondari Mpaka vyuoni na kuondoa hili tope la vichwani mwa vijana wetu wanaotumia vibaya kwa kuitwa chipkizi kwa manufaa ya chama tawala.
 
Me nshasema kuendelea tz hadi ccm watoke madarakani vinginevyo akili za wanaodhaniwa kuwa ni wasomi zitaendelea kudumaa tu!
 
I real Like This Article. Ngwanangwa Umetouch Issues Nyingi Sana Ambazo Kama Vijana na Wananchi Wengine Wangeanza Kufunuka Macho na Kuona Ni Nani Wanamtumikia na CCM Sio Chama ni Miongoni mwa Udikteta Policies Zinanomaliza Afrika. Wengi Tulielimika na Kuona Maovu na Kujua Solutions za Inchi Yetu Teendelee Jitihada za Kuelimisha Wananchi na Chadema Lazima Waweke Efforts Kubwa Kuwaelimisha Wananchi ili Swala la Katiba Lijulikane kwa Wananchi Wote. Ni Kweli Kuna Wananchi Vipofu ila Idadi Yao Sasa ni Ndogo na Matokeo ya Uchaguzi 2010 Yamedhihilisha Hivyo. Uchaguzi Huu Umekuwa wa Mafanikio Sana na Tujipongeze.
 
Mbaya zaidi tunapojenga vyuo vikuu vya propaganda. What a shame, can we teach medicine and politics in one class. My hopeless "wasomi pori" njaa inauma lakini haionyong'onyezi fikra sahihi. Plz we need a change, a big change... Cant go on with this. Why dont wasomi take time to research and or atleast reflect before exposing ignorance in public.
 
Anayeshabikia ccm lazima atakua na akili punguani!mjerumani miundo mbinu reli bandari,mashamba makubwa ya kahawa katani karanga chai etc aliyoacha tanganyika ccm watueleze yapo wapi?
 
ninawasikitikia sana vijana wa tanzania. Vijana wanaotokea familia masikini, mafukara ambao wazazi wao wanaishi kwenye nyumba za tembe na kulala kwenye vitanda vya ngozi za ng'ombe.

Vijana wamejaaliwa vipaji vya elimu. Wazazi wao (wanaoshabikia ccm kwa sababu wanafikiri nyerere bado yupo hai) wamejikamua kuuza mifugo na mazao wapate elimu. Baadhi ya vijana hawa wamepata bahati ya kufika vyuo vikuu na kupata shahada na stashahada. Wapo mijini. Hawataki kurudi vijijini kwa sababu vijijini hakuna umeme. Vijijini hakuna zahanati na hospitali. Vijijini hakuna lami. Vijijini hakuna daladala wala taxi. Wala vijijini hakuna warembo kama huku mjini. Vijini kupata ‘netweki' ya simu ni ishu. Vijijini kuchaji simu mpaka ulipie sh. 500 kwa mtu mwenye jenereta.

Mmmh! Vijana. Wasomi. Wanafanya mambo ya aibu. Wanakula takrima za ccm na kufanywa makamanda wa green guard. Wanafanya kazi ya kuratibu ugawaji wa fulana na kofia za ccm. Wanasafirishwa kwa malori na wengine kupoteza maisha kwenye ajali kwa ajili ya kuwatumikia mafisadi, wakati watoto wa mafisadi wako upanga wanagombania rimoti za tv na kupunguza/kuongeza ubaridi wa viyoyozi.

Vijana masikini wa tanzania wamesahau shida walizonazo wazazi wao. Wamesahau kuwa ccm na watawala wake wanaokula rushwa ndiyo chanzo cha matatizo yote ya nchi hii.

Tanzania inawalilia enyi vijana kutoka familia masikini za tanzania. Jitengeni na ccm. Waacheni watoto na ndugu zao ndiyo wawe wapambe wao kwenye mikutano yao. Jiungeni na kundi la ukombozi.

Wakati ni huu. 2015 ni kesho tu.

watakula matapishi yao
 
wakati watoto wa mafisadi wako Upanga wanagombania rimoti za TV na kupunguza/kuongeza ubaridi wa viyoyozi.

hapa inaonyesha wazi wewe batch ya ndui yako ilikuwa imeshapitwa na wakati,umeona upanga ndio wanapoishi mafisadi tu...hatari kweli kweli:wacko:
 
Unapotoa lawama kulaumu society, students, kwanza ilibidi utoe maelezo yako binafsi kwamba umesadia jamii ktk mazingira gani. Toa mfano kwanza, kabla ya kulaumu.
 
Me nshasema kuendelea tz hadi ccm watoke madarakani vinginevyo akili za wanaodhaniwa kuwa ni wasomi zitaendelea kudumaa tu!

Tatizo la TZ siyo chama, bali ni WTZ wenyewe. WTZ wanapenda kuzungumza, na kulaumu bila ya action yoyote.
 
Unapotoa lawama kulaumu society, students, kwanza ilibidi utoe maelezo yako binafsi kwamba umesadia jamii ktk mazingira gani. Toa mfano kwanza, kabla ya kulaumu.

Umeharibu mtililiko wa hoja nzima! Wakati mwingine ni busara kuacha kuchangia kuliko kuweka upupu!
 
Tatizo la TZ siyo chama, bali ni WTZ wenyewe. WTZ wanapenda kuzungumza, na kulaumu bila ya action yoyote.
Mkuu kuiteganisha mbumbumbu wa tz na ccm ni ngumu. Huwezi kuongelea ccm bila kugusia ujinga wa watz walo wengi!
 
Unapotoa lawama kulaumu society, students, kwanza ilibidi utoe maelezo yako binafsi kwamba umesadia jamii ktk mazingira gani. Toa mfano kwanza, kabla ya kulaumu.

Ulichoandika si kweli. Labda tu useme hukubaliani na hoja zilizotolewa. Hivi, mfano ukitaka kumkosoa kocha wa timu kwa kupanga kikosi kibaya utalazimika kusema wewe umesaidia vipi? Hapa imetolewa hoja, kama una majibu toa kama huna subiri wenzako wakusaidie. Hatuwezi kukaa kimya mambo yanaenda vibaya kwa sababu kuna watu watataka tuseme kwanza tumefanya nini! Hata hivyo kitendo cha ku-take time na kuweka thread kama hizi ambazo zinatoa nafasi kwa mjadala kwa vigezo vya hoja ni mchango mkubwa sana. Unaweza ukadhani "una busara" kuiga misemo ya "toa boriti kwanza kwenye jicho lako...." kumbe unanakili vitu vila kufahamu matumizi na muktadha. Anyway, mtu mmoja alisema "Commonsense is not common."
 
Ulichoandika si kweli. Labda tu useme hukubaliani na hoja zilizotolewa. Hivi, mfano ukitaka kumkosoa kocha wa timu kwa kupanga kikosi kibaya utalazimika kusema wewe umesaidia vipi? Hapa imetolewa hoja, kama una majibu toa kama huna subiri wenzako wakusaidie. Hatuwezi kukaa kimya mambo yanaenda vibaya kwa sababu kuna watu watataka tuseme kwanza tumefanya nini! Hata hivyo kitendo cha ku-take time na kuweka thread kama hizi ambazo zinatoa nafasi kwa mjadala kwa vigezo vya hoja ni mchango mkubwa sana. Unaweza ukadhani "una busara" kuiga misemo ya "toa boriti kwanza kwenye jicho lako...." kumbe unanakili vitu vila kufahamu matumizi na muktadha. Anyway, mtu mmoja alisema "Commonsense is not common."

Mwandishi aliendika hii article hamlaumu mtu mmoja, analalamikia kuhusu Graduate StudentS, StudentS. Huwezi kulaumu Society nzima kwa sababu hawafuati vile anavyoamini yeye.
 
mwenyewe ninao wadogo zangu watoto wa bamdogo ndo kazi walizokuwa wanadeal nazo wakati wa likizo m1 aliajiriwa kwa muda coz alimaliza UD syansi y siasa asa na mwenzie akipewa usimamizi wa TEMCO SINA HAKIKA KAMA NI FANS WA JF MAKE NAHISI WANGESHA BADILIKA NA KUWA NA MAWAZO MAPANA SI MBUMBUMBU NA KUWA WAFUASI TU WA CCM kwa vijirushwa hivi
 
Ninawasikitikia sana vijana wa Tanzania. Vijana wanaotokea familia masikini, mafukara ambao wazazi wao wanaishi kwenye nyumba za tembe na kulala kwenye vitanda vya ngozi za ng'ombe.

Vijana wamejaaliwa vipaji vya elimu. Wazazi wao (wanaoshabikia CCM kwa sababu wanafikiri Nyerere bado yupo hai) wamejikamua kuuza mifugo na mazao wapate elimu. Baadhi ya vijana hawa wamepata bahati ya kufika vyuo vikuu na kupata shahada na stashahada. Wapo mijini. Hawataki kurudi vijijini kwa sababu vijijini hakuna umeme. Vijijini hakuna zahanati na hospitali. Vijijini hakuna lami. Vijijini hakuna daladala wala taxi. Wala vijijini hakuna warembo kama huku mjini. Vijini kupata ‘netweki' ya simu ni ishu. Vijijini kuchaji simu mpaka ulipie sh. 500 kwa mtu mwenye jenereta.

Mmmh! Vijana. Wasomi. Wanafanya mambo ya aibu. Wanakula takrima za CCM na kufanywa makamanda wa Green Guard. Wanafanya kazi ya kuratibu ugawaji wa fulana na kofia za CCM. Wanasafirishwa kwa malori na wengine kupoteza maisha kwenye ajali kwa ajili ya kuwatumikia mafisadi, wakati watoto wa mafisadi wako Upanga wanagombania rimoti za TV na kupunguza/kuongeza ubaridi wa viyoyozi.

Vijana masikini wa Tanzania wamesahau shida walizonazo wazazi wao. Wamesahau kuwa CCM na watawala wake wanaokula rushwa ndiyo chanzo cha matatizo yote ya nchi hii.

Tanzania inawalilia enyi vijana kutoka familia masikini za Tanzania. Jitengeni na CCM. Waacheni watoto na ndugu zao ndiyo wawe wapambe wao kwenye mikutano yao. Jiungeni na kundi la ukombozi.

Wakati ni huu. 2015 ni kesho tu.

Mtoa mada, kumbuka kuwa ukisha-graduate, wewe tayari uko nje ya kundi la maskini na fukara. Elimu uliyonayo inatosha kubadilisha familia yako na kuwa na uwezo wa kuishi kwa zaidi ya dola 10 kwa siku. Ukishagraduate, unatakiwa utumie akili yako uliyo-idaka kuweza kupambana na mazingira halisi yanayokuzunguka na kutegemeana na mwandamo wa mwezi wakati huo. Ukiamua kuitumia CCM au Chadema shauri yako; yote ni matokeo ya elimu uliyopata na inakuwezesha kupambanua kizuri na kibaya kipi. Haitatokea hapa Duniani watu wote wakawa wanafikiria kitu kimoja kwa wakati mmoja. Wa CUF mwache aende huko, wa Chadema mwache abakie Chadema na wale wa TLP au Chausta waache. Wako sawa sawa na wana uhalali wa kuwa hivyo walivyo.
Mtoa mada jaribu kubadilika na waelezee na wenzako kuwa Graduate siyo mtu wa kumburuza na kumpeleka peleka. Labda awe mjinga mjinga
 
Mwandishi aliendika hii article hamlaumu mtu mmoja, analalamikia kuhusu Graduate StudentS, StudentS. Huwezi kulaumu Society nzima kwa sababu hawafuati vile anavyoamini yeye.

Ni kweli kuwa mwandishi halaumu mtu mmoja. Hata hivyo ni vigumu kila utakachoandika utaweza kusema "baadhi ya......" Ni wazi kuwa akisema "Wasomi wanakula takrima...." haimaanishi ni wasomi wote hata kama hajasema neno baadhi. Hivi mtu akisema "Watanzania ni watu wanaopenda amani" ina maana ni wote? Au unadhani ni lazima aseme "Baadhi/Wengi wa Watanzania wanapenda amani"? Hauoni kuna baadhi ya generalization humaanisha specificity kwa ambao wanafall katika kundi la kulaumiwa au kusifiwa?

Bado lawama kwa wasomi haiwezi kuepukwa. Mimi ni msomi lakini sijachukua takrima ya CCM au CHADEMA na sina sababu ya kurusha ngumi eti kwa sababu mwandishi hajasema neno baadhi, tunahitaji kuangalia mazingira ya usemaji.

Bado wasomi tunaendelea kuwa watumwa wa wanasiasa hasa CCM jambo ambalo historia itatuhukumu.......
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom