kmbwembwe
JF-Expert Member
- Aug 16, 2012
- 10,369
- 7,140
Nchi jirani ya uganda kwa wenye diploma kuanzia gpa 2.7 wanaweza kuomba kujiunga na vyuo vikuu lakini tanzania tumeweka gpa 3.0. Hata nchi za ng'ambo kama malaysia china na zingine wanakubali kuanzia gpa 2.7 kwa wenye diploma kama hizi zetu za nacte.
Ingefaa kiwango cha tanzania nacho kishuke ili vijana wanaotaka kujiendeleza kwa elimu waendelee kusoma badala ya kupoteza muda vijiweni huku wazazi wao wana uwezo kuwaendeleza.
Wazazi wengi wamekua wanagharamika kuwapeleka nje vijana wao vyuo vikuu vya nje huku baadhi ya vyuo nchini vikishindwa kupata wanafunzi kulingana na uwezo wao kwa kuwekwa kiwango cha kujiunga juu bila sababu za kimsingi.
Yapo masoma ambayo yanahitaji viwango vya gpa kubwa kama vile udaktari uhandisi na kadhalika. Lakini kuna masomo mengi tu vyuo vikuu nchi nyingi kiwango cha cini gpa ni chini ya 3.0.
Nashauri jambo hili liangaliwe ili kupatia vijana wenye kupenda kujiendelesa nafasi vyuo vikuu na pia kuweza kuchukua fulsa za uwezo kwa nafasi katika vyuo vikuu.
Ingefaa kiwango cha tanzania nacho kishuke ili vijana wanaotaka kujiendeleza kwa elimu waendelee kusoma badala ya kupoteza muda vijiweni huku wazazi wao wana uwezo kuwaendeleza.
Wazazi wengi wamekua wanagharamika kuwapeleka nje vijana wao vyuo vikuu vya nje huku baadhi ya vyuo nchini vikishindwa kupata wanafunzi kulingana na uwezo wao kwa kuwekwa kiwango cha kujiunga juu bila sababu za kimsingi.
Yapo masoma ambayo yanahitaji viwango vya gpa kubwa kama vile udaktari uhandisi na kadhalika. Lakini kuna masomo mengi tu vyuo vikuu nchi nyingi kiwango cha cini gpa ni chini ya 3.0.
Nashauri jambo hili liangaliwe ili kupatia vijana wenye kupenda kujiendelesa nafasi vyuo vikuu na pia kuweza kuchukua fulsa za uwezo kwa nafasi katika vyuo vikuu.