Dua
JF-Expert Member
- Nov 14, 2006
- 3,229
- 662
GT said:Taarifa zinasema kwamba mradi huo wa fedha nyingi umekuwa ukigombewa na wakubwa: Mambo ya Ndani; Mambo ya Nje; Ofisi ya Waziri Mkuu na ulibuniwa na wajiriwa serikalini na kisha kampuni yao ya Gotham International ikapewa kazi ya upembuzi na hatimaye ikaandaa mchanganuo.
Kati ya waajiriwa hao wa serikali walikuwamo Jack Gotham mwenye uhusiano wa karibu na viongozi wengi serikalini na John Kyaruzi mwajiriwa wa Kituo cha Uwekezaji (TIC) ambaye ameelezwa kuwa ndiye aliyevuta kampuni moja ya Afrika Kusini, Business Connection (Bcx) kuunda timu ya Gotham International.
Vitambulisho hivyo vilikuwa vianze kutoka kabla ya mwaka ujao, lakini sasa baada ya utata huo baadhi ya wataalamu wa masuala hayo wanaona kuwa hakuna haja tena ya kuwa navyo kama havihusishi pamoja na mambo mengine, kama takwimu muhimu za wapiga kura.
Hicho kitambulisho kinachotafutwa kwanza ni ghali sana mpaka hata Benki ya Dunia ilihoji kama Tanzania inahitaji kitu ghali kama hicho.
Tanzania tunasifa ya kuwa na international companies hewa ambazo hazijafanya kazi kama hizo popote ulimwenguni.
Lakini pia sasa Tume ya Uchaguzi inapitia Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, ungetarajia kitambulisho hicho kiwe na taarifa zote hizo, lakini sasa Serikali inataka kuwa na utambulisho wake na Tume ya Uchaguzi nayo utambulisho wake, hii haileti maana, anasema mtaalamu mmoja wa takwimu.
Je, hii kampuni tayari imepewa uthibitisho wa kupata tenda ya kutengeneza vitambulisho?
Nani wamiliki halali wa hii kampuni?
Ilianza kufanya kazi Tanzania lini?
Ilisajiliwa lini?
Inafanya kazi gani South Afrika au mahali pengine popote duniani?
Je, wametengeneza smart cards za aina gani anywhere in the world.
Je, ni kweli Waziri Membe ana uhusiano wa karibu na hii kampuni?