Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,939
- 20,398
Google wapo katika mpango wa kuchukua picha za barabara zote katika nchi nzima ya Uingereza, katika kujaribu kutengeneza tovuti (website) iitwayo kwa kiingereza Street View mapping.
Gari la Google likipita kupiga picha
Lakini walipofika karibu na kijiji nnachoishi cha Cyber, gari ya watu wa Google aina ya Opel Astra ilianza kuchukua picha kwenye kijiji jirani kiitwacho Broughton, ndipo wananchi waishio katika kijiji hicho waliposimama katikati ya barabara na kuzuia njia ili gari hio isipite na isifanye kazi yake ya kuchukua picha.
Ndipo wananchi wote tuishio vijiji vya jirani tulipopata taarifa na kuunga mkono mgomo huo na baadae dereva wa gari hi alipogeuza na kurudi alipotoka. Mmoja wa wanakijiji akaita polisi na baada ya dakika chache polisi walifika eneo la tukio na kusikiliza madai yetu.
Kwamba Google wanaingilia uhuru wetu wa faragha kiasi cha kuchukua picha za mitaa yetu bila ridhaa yetu wananchi na kuanika katika hio tovuti yao.
Pili watu wa google wanarahisisha kazi kwa wezi kungamua ni wapi wanaweza kwenda kuiba kwa urahisi kwa kufuata hio Street View mapping.
Tatu watu wa google wanasaidia kitendo cha wizi.
Polisi waliposikiliza madai hayo wakaona kuna sense na wakamshauri mhandishi na dereva wa gari hilo aondoke katika eneo hilo.
Hapo kabla kumekuwa matukio matatu ya wizi ambapo wezi wamevunja nyumba za watu na kukwiba na kuwepo kwa usaidizi wa tovuti hii kutasaidia wizi huo kuongezeka.
Gari hilo la google lina mkonga ambao umeninginizwa camera ambayo ina uwezo wa kuzunguka nyuzi 360 na picha zinakuwa zikichukuliwa kila baada ya sekunde mbili chache kutoka kila eneo. Hii inawasaidia watu popote pale walipo duniani kuandika anuani ya sehemu yoyote ile katika tovuti ya Google kwa minajili ya kutafuta na kupewa majibu ndani ya sekunde chache tu. Pia picha za nyumba, bustani, majengo na vitu vingine muhimu vitaweza kuoneshwa.
Kwa hio mtindo huu umekuwa ni maarufu kwa watalii na watu wengine lakini kwa sasa umezua mabalaa kwa kuonesha picha za waume za watu wakiwa wanatoka nje ya nyumba za vimada wao au kwa wake pia kuonekana hivyo hivyo kutoka kwa mabwana zao, wengine kuonekana wakiwa wanaumwa barabarani na hali hii imeonekana kuingilia uhuru wa faragha kwa wananchi.
Kibaya zaidi ni kesi ya kuachana (divorce) ambapo mama anadai gari aina ya Range Rover la baba lilionekana limepaki nje ya nyumba ya rafiki yake wa kike wakati baba alisema amekwenda kwenye safari ya kibiashara.
Watu wa Google wamejitetea kwa kusema kwamba picha zote huondolewa pale mtu anapohitaji hivyo.
Mkuu Steve D na wengine mnaonaje kuja kwa Google latitude?
Gari la Google likipita kupiga picha
Lakini walipofika karibu na kijiji nnachoishi cha Cyber, gari ya watu wa Google aina ya Opel Astra ilianza kuchukua picha kwenye kijiji jirani kiitwacho Broughton, ndipo wananchi waishio katika kijiji hicho waliposimama katikati ya barabara na kuzuia njia ili gari hio isipite na isifanye kazi yake ya kuchukua picha.
Ndipo wananchi wote tuishio vijiji vya jirani tulipopata taarifa na kuunga mkono mgomo huo na baadae dereva wa gari hi alipogeuza na kurudi alipotoka. Mmoja wa wanakijiji akaita polisi na baada ya dakika chache polisi walifika eneo la tukio na kusikiliza madai yetu.
Kwamba Google wanaingilia uhuru wetu wa faragha kiasi cha kuchukua picha za mitaa yetu bila ridhaa yetu wananchi na kuanika katika hio tovuti yao.
Pili watu wa google wanarahisisha kazi kwa wezi kungamua ni wapi wanaweza kwenda kuiba kwa urahisi kwa kufuata hio Street View mapping.
Tatu watu wa google wanasaidia kitendo cha wizi.
Polisi waliposikiliza madai hayo wakaona kuna sense na wakamshauri mhandishi na dereva wa gari hilo aondoke katika eneo hilo.
Hapo kabla kumekuwa matukio matatu ya wizi ambapo wezi wamevunja nyumba za watu na kukwiba na kuwepo kwa usaidizi wa tovuti hii kutasaidia wizi huo kuongezeka.
Gari hilo la google lina mkonga ambao umeninginizwa camera ambayo ina uwezo wa kuzunguka nyuzi 360 na picha zinakuwa zikichukuliwa kila baada ya sekunde mbili chache kutoka kila eneo. Hii inawasaidia watu popote pale walipo duniani kuandika anuani ya sehemu yoyote ile katika tovuti ya Google kwa minajili ya kutafuta na kupewa majibu ndani ya sekunde chache tu. Pia picha za nyumba, bustani, majengo na vitu vingine muhimu vitaweza kuoneshwa.
Kwa hio mtindo huu umekuwa ni maarufu kwa watalii na watu wengine lakini kwa sasa umezua mabalaa kwa kuonesha picha za waume za watu wakiwa wanatoka nje ya nyumba za vimada wao au kwa wake pia kuonekana hivyo hivyo kutoka kwa mabwana zao, wengine kuonekana wakiwa wanaumwa barabarani na hali hii imeonekana kuingilia uhuru wa faragha kwa wananchi.
Kibaya zaidi ni kesi ya kuachana (divorce) ambapo mama anadai gari aina ya Range Rover la baba lilionekana limepaki nje ya nyumba ya rafiki yake wa kike wakati baba alisema amekwenda kwenye safari ya kibiashara.
Watu wa Google wamejitetea kwa kusema kwamba picha zote huondolewa pale mtu anapohitaji hivyo.
Mkuu Steve D na wengine mnaonaje kuja kwa Google latitude?