Good News ! - Kampuni ya Precisionair kuingiza ndege saba mpya Tanzania

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
Ifuatayo ni habari njema kwa Watanzania, adha ya usafiri wa anga natumaini itapungua sasa..

Kampuni ya Precisionair kuingiza ndege saba mpya Tanzania

Na Andrew Msechu

KWA mara ya kwanza nchini, Kampuni ya Precision Airlines imeingiza ndege moja mpya kati ya saba aina ya ATR 72-500, ikiwa ni sehemu ya mkataba wa Dola za Kimarekani 129milioni (zaidi ya Sh150 bilioni).


Ndege hiyo ni sehemu ya mkataba ambao ulisainiwa hivi karibuni kati ya Precision na Kampuni ya ATR ya Toulouse, nchini Ufaransa kwa ajili ya kuingiza ndege saba mpya na vifaa vya ndege za ATR kwa nchi zote za Afrika.


Akizindua ndege hiyo kwa niaba ya Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge jana, Kaimu Mkurugenzi wa Usafirishaji katika wizara hiyo, Kirenga Ndomino alisema hatua hiyo ya Precision, ni changamoto mpya katika sekta ya usafiri wa anga nchini, hasa katika kuimarisha sekta ya uzalishaji na utalii wa ndani.


Ndomino alisema uamuzi wa Precision kuingia mkataba huo mkubwa zaidi kati ya Precision na ATR ambao haujawahi kusainiwa na kampuni yoyote binafsi ya ndege nchini, hasa kwa ajili ya kuingiza ndege mpya saba ndani ya miaka mitatu, ni mfano wa kuigwa katika juhudi za kuboresha sekta ya usafirishaji wa anga nchini.


"Hii si ndege ya kwanza kuzinduliwa na Precision, lakini ukweli unabaki pale pale kuwa hii ni kampuni ya kwanza kuingiza ndege mpya nchini, pia imeweka historia ya kuwa kampuni ya kwanza Afrika Mashariki na kati kuagiza ndege mpya kutoka kiwandani baada ya kampuni ya Kenya Airways. Kampuni nyingine zimekuwa zikitumia ndege zilizokwishatumika," alisema Ndomino.


Aliongeza kuwa kwa kutambua mchango wa kampuni hiyo katika kuboresha sekta ya usafirishaji wa anga nchini, serikali inaendeleza juhudi za kufanya maboresho makubwa kwenye viwanja vya ndege nchini kwa kuanza kwa awamu ya pili ya ukarabati wa Uwanja wa Ndege wa Kiamataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam, kuanzia mwezi ujao kwa gharama ya zaidi ya Euro25 milioni.


Kaimu Mkurugenzi huyo alisema ukarabati huo unaodhaminiwa na Benki ya Dunia, pia utaviwezesha viwanja vingine saba vya Arusha, Mafia, Bukoba, Shinyanga, Tabora, Kigoma na Sumbawanga kufanyiwa ukarabati mkubwa, mradi ambao tayari umeshaanza.


Mkurugenzi wa kampuni ya Precision, Alphonse Kioko alisema uamuzi wa kuwapo kwa sasa usafiri wa anga nchini unaweza kuwa rahisi zaidi kutokana na uamuzi wao wa kuingiza ndege mpya kutoka kiwandani, ambazo zitahakikisha usalama na mazingira mazuri zaidi kwa wateja na wao.


"Siku hii ya leo si ya kawaida kwetu, ni siku mpya katika utaratibu mzima wa utoaji wa huduma kwa wananchi wa Tanzania, tuna uhakika wa kuwahakikishia huduma bora zaidi, kwa haraka na raha zaidi, tunawashukuru wadau wetu wote waliotuwezesha kufika hapa tulipo leo" alisema Kioko.


Akizungumza katika makabidhiano ya ndege hiyo yenye uwezo wa kubeba abiria 70, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Precision, Michael Shirima alisema ndege hiyo inaungana na ndege nyingine nne za Precision ambazo zinaendelea kufanya kazi nchini.


"Tunaamini kuwa kutokana na uhusiano mzuri uliopo baina ya Precision na serikali na wateja wake ni moja ya sababu kubwa ya kutufanya tuwepo hapa leo, pia uthabiti wa ndege hizi za ATR unatufanya tujisikie fahari ya kuwakaribisha na kuwahakikishia usalama na raha kila mnaposafiri na sisi," alisema Shirima.


Kampuni hiyo iliyoanzishwa mwaka 1996 pia inatarajia kuingiza ndege nyingine aina ya Boeing 737-300 mwishoni mwa mwezi huu, pia imethibitishwa na Shirika la Viwango vya Usalama wa Anga Duniani na kuwa mwanachama wa IOSA.


Source: Mwananchi.co.tz

SteveD.
 
Nadhani itapendeza sana kuwa na ndege nyingi, huenda na nauli zikashuka. Inabidi jamaa wajikongoje, wawe kama Easy Jet, ama Sterling, kwa kutoa huduma kwa bei rahisi.
 
Nadhani itapendeza sana kuwa na ndege nyingi, huenda na nauli zikashuka. Inabidi jamaa wajikongoje, wawe kama Easy Jet, ama Sterling, kwa kutoa huduma kwa bei rahisi.


kazi kweli. hii itakuwa changamoto kweli.
 
Hizi ni habari nzuri!

Naskia sasa Hili shirika ni la pili kwa umaarufu na ukubwa ktk E and C Afrika baada ya Kenya Airways!

Hii ni poa tu.. nawapongeza!
 
Hongera Precision Air! Huduma bora ya kiwango cha juu inaonyesha kumjali mteja. keep it up!
 
Wakuu hii ndo ya kwanza ATR-72-500 Brand New hiyo. Ndo ilitua tarehe 3 March mida ya sa 3 unusu asubuhi DIA kutoka Ufaransa. Hongereni Precision ila nauli mpunguze
 

Attachments

  • Precision New ATR 72.jpg
    Precision New ATR 72.jpg
    33.7 KB · Views: 70
Wakuu hii ndo ya kwanza ATR-72-500 Brand New hiyo. Ndo ilitua tarehe 3 March mida ya sa 3 unusu asubuhi DIA kutoka Ufaransa. Hongereni Precision ila nauli mpunguze

Mbona ukiangalia imeandikwa Rombo Ubavuni??? Kwani Rombo ni nembo ya bishara ya hii kampuni?
 
Heshima mbele wakuu!
Nivigumu sana kununua ndege mpya,na nivigumu saana kushikilia soko lako,kuliko kupata jipya,nawapongeza hawa pw(precision)kwa mafanikio hayo yao,mind you wanaingiza boing nyingine end of this moon,lakini pia,wanaingiza ndege nyingine mpya kabisaa yaani brand new ATR72-500,
Nahapa ndipo kwenye somo kwa hawa ATCL,kuna advantage za kutumia hizi ndege za kifaransa,kuliko boing ama air bus,katika fuel consumption,ntakupa mfano rahisi kidogo,safari moja ya atr72,kutoka dar kwenda kigoma kupitia shy na tabora,na kurudi ni sawa na safari ya boing kuto dar kwenda mwanza pekee,bila kurudi,pia ukiangalia na idadi ya wasafiri wetu watumiao ndege,unaona atr ni bora kwetu kuliko ma airbus na hizo boing,haina maana kwamba pw walishindwa kupata boing,ama airbus,lakini waliangalia mbali zaidi kuliko wakina mataka,na dialo,ni matumaini yangu kua wamejifunza somo muhimu toka precision,
Once again,bravo kwa management ya PW na Wafanyakazi wote wa PW maana bila wao kusingekua na hayo muyaonayo mafanikio,one more thing,Nauli jamaani,punguzeni japo kiduuchu,tujimwayemwaye nasie kina yakhe,
LONG LIVE JF!
 
nasikia atc nao wameshusha kitu aina ya dash8 toka canada, chakushangaza imeenda sauz kupigwa chata! sasa kama ni mpya singepigwa chata kiwandani? au nisekandihendi? isijetuua bure!
 
nasikia atc nao wameshusha kitu aina ya dash8 toka canada, chakushangaza imeenda sauz kupigwa chata! sasa kama ni mpya singepigwa chata kiwandani? au nisekandihendi? isijetuua bure!

hapana Eddy,ile ndege dash 8,sio mpya,na ilishawahi kufanya kazi hapahapa bongo,nahaohao atcl,lakini ikaprove wrong,kwenye viwanja vya changarawe,wameirudisha tena tuone kitakachojiri maana,viwanja nivilevile,hakuna kuilichobadilika,yawezekana ni sehemu ya ufisadi,maana ni ndege cheap kwa kukodi.
 
Hivi kuna mtu anajua bei ya hii ndege mpya ya PW? Je wamechukua mkopo Benki au ni faida ya kukua kwa biashara?

Hivi nini kifanyike nayo ATC ifufuke iwe ktk chart kama PW?

Hivi kuna ndege zinaenda Mbeya kwa sasa? Hivi ule uwanja utakamilika lini?
 
Thamani ya ndege mpya ya pw ni dola m17.4,na nisehemu ya faida na mkopo wa citibank,ambayo itaiwezesha pw kupata ndege saba mpya,mbili kila mwaka,kuanzia mwaka huu,pia ni ubunifu wa management ya pw,determinations,na vision yao,nawajua viongozi wa pw,nawale wa ATCL,lakini hata kwa mazungumzo yao tu utaona tofauti zao,kusema ukweli atcl ya mataka,inasafari ndefu saana,time will prove me wrong!
 
Mbona ukiangalia imeandikwa Rombo Ubavuni??? Kwani Rombo ni nembo ya bishara ya hii kampuni?

Ahh, unajua Mzee wa Rombo (Shirima) alikuwa initial owner, baadae ikaja kuwa-acquired, lakini bado ana-own majority share ya Precision, ndio maana anatukuza kwao eti, wouldn't you?
 
Sidhani kama hizo ndege zilikuja zote.

Thanks Magezi kwa kufufua mada.... Labda tuwaulize walio karibu na jikoni,

A few days ago tulikuwa Mwanza tukiugulia jinsi ya kupanda ile Dash-8 ya ndege yetu ya Taifa, lakini hatukuwa na cha kufanya kwani nege mbadala kwa siku ile ilikuwa ATR42 ile isiyo na AC bomba....

On a positive note, ATR 72 iko poa sana na kwakweli ni ndege iliyotulia, pia wana boeing inayosaidia japo huenda mwanza mara tatu kwa wiki kama sikosei
 
Hizi ni habari nzuri!

Naskia sasa Hili shirika ni la pili kwa umaarufu na ukubwa ktk E and C Afrika baada ya Kenya Airways!

Hii ni poa tu.. nawapongeza!

Mkuu nakuunga mkono kuwapongeza Precisionair; lakini hebu tusiongeze chumvi kusema wao ni maarufu zaidi ya Ethiopia Airlines katika E & C Africa.

 
Wakuu hii ndo ya kwanza ATR-72-500 Brand New hiyo. Ndo ilitua tarehe 3 March mida ya sa 3 unusu asubuhi DIA kutoka Ufaransa. Hongereni Precision ila nauli mpunguze


Nadhani itapendeza sana kuwa na ndege nyingi, huenda na nauli zikashuka. Inabidi jamaa wajikongoje, wawe kama Easy Jet, ama Sterling, kwa kutoa huduma kwa bei rahisi.


Wakuu,

Kweli hili la kutaka wapunguze nauli ni kama mnawaonea tu. I am just thinking aloud here....watapunguzaje nauli wakati

1. Ndege hizi wamekopa na wanatakiwa kulipa mikopo, riba na wapate faida.

2. Viwanja vya ndege Tanzania vingi ni vibovu na hivyo kuongeza gharama za service na matengenezo mengine ya mara kwa mara kwenye ndege zao.

3. "Karibu" kila aina ya spare part ya hizi ndege inaagizwa nje ya nchi kwa kutumia USD.

4 Gharama za kufundisha rubani, mafundi na wahudumu wengine ziko juu (nje ya Tanzania - mara nyingi South Africa) na iko siku itawalazimu kutoa "experts" ng'ambo.

5. Precisionair wamejitosa kiume kupanua biashara ingawaje soko la kujaza kujaza ndege zao kila trip halipo hivyo hao abiria wachache waliopo ndio wanaendesha biashara...

6. Sasa hivi ni kama wana-monopoly kwenye hii biashara ndani ya Tanzania...ni mfanyabiashara gani ambaye hatatumia mwanya wa monopoly kujiongezea faida kwa kadri awezavyo.

Kwa kumalizia, hii changamoto kwa Watanzania; siku tukiamua kufanyakazi kwa bidii, nidhamu na maarifa tunaweza kuendesha biashara kubwa na kujenga uchumi wetu bila kutegemea kuomba omba kwa nchi yoyote.

Hongera sana Shirima na Timu nzima ya Precisionair; you make us proud.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom