Good news: Diamond athibitisha Wasafi Tower kukamilika 95%

Mkuu namkubali diamond ila apo kusema kwamba ndo mwanamuziki anamiliki radio na television afrika sio kweli kuna mwanamuziki anaitwa salif keita yupo mali uko ana media house tangu miaka ya 90 na ana mpunga mrefu tu.
huyo hajulikani hata buza sawa dogo
 
Kazi kweli kweli, kwanza walidai pale wasafi mbezi b kwake, baadaye wakadai amekodi kwa miaka kadhaa, sasa yaja hii ya tower?! Ni shida..
 
huyo hajulikani hata buza sawa dogo
Mkuu hajulikani? Huyo jamaa ni maarufu sana ni moja kati ya wanamziki wenye hesima Afrika sema mziki wake si wa kizazi chetu cha akina dimaond na davido. Halafu ni albino. Utajiri wake unakadiliwa kuwa wa kiasi cha dollar milion 47, hiyo ni zaidi ya bilioni 90 za Kibongo.
Mimi mwenyewe miziki yake siielewagi naonaga kama anapiga mayowe nadhani kutokana na lugha anayotumia ila ni kati ya wasanii wakubwa toka Afrika na wanaoheshimika sana mpaka kwa wazungu.
 
haya masystem ya kutanguliza watu maharufu kwenye miradi mikubwa wanatumia sana wanasiasa na Mafia groups duniani kote!!
mifano ipo Mingi...hapa Tanzania unashangaa mfano Masanja Mkandamizaji in few years anamiliki mali zenye thamani ya mabilioni,wakati kina marehem Majuto,mzee Small n.k wamekufa hoeae masikini wa kutupwa japo wamechekesha jamii ya kitanzania for decades!! Erick Omond,Churchil ,Klint the drunkard wa Nigeria anafanya show nyingi na ni maharufu na Nigeria ina watu wengi wanaoangalia comedy lakini yeye na hawa wa Kenya wana utajiri wa kawaida!! Joti au Mpoki wana wapenzi wengi na wanafanya vizuri kuliko Masanja!! ila Masanja kawapita kwa mali...je ni mchele wa Ubaruku tu???na Kulala juu ya mafyover
Wanamziki kama Wale Wa Njenje,Sikinde,Kila late Remy Ongala,Moshi William Hamza Kalala na Wengine wameimba mziki ndani na nje ya Tanzania..Wengi wao wamefariki ata nyumba ya chumba kimoja awana.Diamond Baba ake mzazi mpaka leo hii anauza viatu vya mtumba anavyonunua pale Karume! aingii akikini mtu mwenye background kama yake na ukizingatia piracy ya music/movie za Kitanzania awe na pesa na mali ambazo anaonyesha kwenye social media...Ila ata last akuna siri chini ya jua...ipo siku all will be revealed
Maharufu_ maarufu, kumsaidia mzazi wake ni maamuzi yake binafsi,kwanini kama mzazi hakupigania kumsomesha au kumpatia mahitaji yake tangu utoto wake
 
Kweli ambaye amepewa kapewa tuu, na huu msemo umejidhihirisha mbele yaDiamond Platinumz kuwa ndo msanii ana yejituma kwa bidii zote kuliko msanii yeyote hapa bongo.

Pia ndo msanii ambaye anamiliki TV na radio Africa nzima pekeake.

Pia ndo msanii ambaye Tv na radio yake kwa Mara ya kwanza vitakuwa vinapatikana kwenye miliki yake, na sio kama radiona Tv Kama clouds, efm na nyingine zinazotegemea leasing area ili kuoperate.

HAIL TO DIAMOND PLATINUMZ THE G. O. A. T
Ndege Binafsi aliyonunua mwaka 2014 bado haijafika?
 
Back
Top Bottom