Je wananchi wa Mbozi wanaujua huu ukweli? Lakini ni kwa vipi yule mgombea wa CHADEMA hakuamua kufungua kesi ya kupinga matokeo?
G. Zambi anatokea Tarafa ya Igamba na ndo kwa wazazi wake, ukitaka kujuwa hakushinda panda gari kutokea Mlowo kama unaelekea Ziwa Rukwa kamsamba ni karibu tu ukaulize majirani kama anakubalika au la. Nijuavyo mimi kama mzaliwa wa Isansa tarafa ya Igamba ni kwamba , Zambi akienda Mbozi huwa anategemea zaidi ulinzi maana hata mkutano wa hadhara hawezi kuitisha tena tokea 2010. Wanyiha ni noumaaa!akikugeuzia shingo ndo basi tena. Zambi ni mbunge wa Ndisana(Mahenge) na wenzake ndo maana hata jamaa yake huyo Ndisana alitaka kuweka Bar kwenye geti la Shule ya msingi Haloli na watu walipopiga kelele akaibadili kuwa nyumba ya kuishi.
Baada ya kuona jina la Zambi katika list ya majina yanayopigiwa chapuo juu ya uwaziri, ilinibidi nifanye ufuatiliaji kidogo kwa wenyeji wa hapa Mbozi kwa kuwa nipo huku. Na majibu niliyopata ni kama haya:
Godfrey Zambi hatakiwi Mbozi kwa taarifa yako. Huyu jamaa ni corrupt sana tofauti na anavyojitambulisha bungeni. Zambi hupata ubunge kwa rushwa ya kusaidiwa na wafanyabiashara Wakinga wa Vwawa na Mloo. Wafanyabiashara hao humsaidia kwa imani kuwa atalinda interest za wakaazi wa Mbozi ambao si Wanyiha.
Na politics zinekuwa hivyo tangu wakati wa mbunge Halinga, ambaye hapo nyuma alionekana kuwanyanyasa wakaazi wa Mbozi ambao si Wanyiha. Zambi ndiye amekuwa kimbilio la hawa wakaazi kwa matumaini ya ulinzi.
Nakuhakikishia akipewa uwaziri yataanza kuibuka madudu ya rushwa yakitokea Mbozi mashariki. We subiri tu. Sana sana tukio hilo litamuongezea kijana Mwampamba wa chadema nguvu zaidi ya kushinda 2015. Nipo hapa.
My take: Sehemu kubwa ya wabunge wa CCM wanaojifanya kupiga kelele bungeni ni wanafiki. Kama Zambi anashinda kwa rushwa anawezaje kusimama kuipinga rushwa kwa dhati? Huyu akipewa kitu kidogo si anafunga mdomo au hata kugeuza mwelekeo kabisa? Na akipewa uwaziri je, anawezaje kujitenga na wizi na dhuluma ilhali na yeye ni uzao wa dhuluma?
wivu wa kike