Godbless Lema: Rais Samia na Makamba wanatafuta mbinu za kumbebesha lawama hayati Magufuli

Etwege

JF-Expert Member
Jul 4, 2018
5,352
14,629
Mbunge wa zamani wa Arusha mjini aliyetimkia Ulaya baada ya maisha kumpiga kwa kuzidiwa na madeni Godbless Lema amefichua mbinu chafu za kutaka kumsingizia kila kitu na kumtafutia lawama aliyekuwa Rais wa awamu ya tano hayati Magufuli.

Lema amefunguka zaidi kwa kusema Rais Samia na waziri wake wa nishati January Makamba wanatafuta kila mbinu ili chanzo cha matatizo ya umeme na maji iwe Magufuli wakati hayupo na wakati Magufuli akiwepo hayo matatizo hayakuwepo kabisa nchini.

Lema amewataka watanzania kuamka na kuibana serikali yao ifanye kazi badala ya kuja na visingizio kila siku huku maisha ya watanzania yakiendelea kuwa magumu.
 
41 Reactions
Reply
Back
Top Bottom