kwa wakristo huwa inakubalika kushirikisha watu wengine ktk maombi anayokuwa nayo mtu ili nao wamsaidie muhusika kuyapeleka mbele za Mwenyezi Mungu. hata hivyo kwa mujibu wa maandiko matakatifu yatupasa kuomba Mungu kwa shukrani na si kumuomba alipize kisasi. Haki mbinguni, duniani sheria. ni vema CDM wakaendelea na tamko lao la kukata rufaa, kwa utaratibu wa kawaida uliowekwa kwa mujibu wa sheria ili kupata haki yao kwa mujibu wa sheria.
Nadhani kuna kuteleza kidogo. Tunatakiwa tumuombe mungu ili mapenzi yake yatimie (na sio kulipiza kisasi). Kama mungu ataona inafaa sasa kuwazuia wale wote wanaosababisha maisha ya watanzania kuwa magumu basi kupitia sala tunatakiwa tumuombe aingilie kati kulingana na mapenzi. (baba yetu ...... utakalo lifanyike duniani kama mbinguni...)