Godbless Lema: CHADEMA imepata baraka kuondokewa na Lowassa

Na mapungufu yote uliyosema bado mkataka awe rais na amiri jeshi mkuu kweli? Hapa sio bure lazima bangi inahusika
 
Mlisubiri aondoke yeye awape baraka😂😂😂 Mlipaswa kujitafutia Baraka kwa kumuondoa na sio yeye awatafutie Baraka. Lakini muache akazamie alipovukia😎😎😎
 
ktk makosa ambayo CDM watayajutia vizazi hata vizazi........ni kumpokea lowassa.....litadumu milele.....hakupaswa kabisa....mliowapokea wote wamerudi nyumbani kwao.......Slaa na Lipumba walikuwa sahihi kukaa pembeni.....mstari mmeupindisha wenyewe nani wa kuunyoosha tena.......2020 hiyoooo.....
 
siasa mbaya sana pole pole naye alimponda lowasa sasa amerudi kwao amefurahi sana had anacheza kiduku, Kweli Nimegundua wanaotucheleweshea maendeleo ni Vyama vya siasa hasa Chadema na Ccm
 
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amefunguka kuhusu uamuzi wa aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa kurejea CCM.

Lema amedai kuwa uamuzi wa Lowassa unadhihirisha kuwa ameweka mbele maslahi yake binafsi kuliko mabadiliko aliyokuwa anayahubiri alipoingia Chadema.

Alidai kuwa Lowassa alifikia uamuzi huo ili kulinusuru shamba lake linaloshikiliwa Mkoani Tanga, shamba lake la mifugo linaloshikiliwa Dodoma pamoja na kumnusuru mkwewe Sioi Sumari na kifungo dhidi ya kesi inayomkabili.

Sumari anatuhumiwa kwa kula njama ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu, kughushi pamoja na utakatishaji wa fedha.

“Mtu huyu alitaka kuwa Rais, hali ya kisiasa ilivyo sasa watu wapo magerezani, wanapata misukosuko ya kibiashara, hawana cha kuipa CCM ili wapate ahueni, lakini kwa sababu yeye anacho cha kuwapa CCM ilia pate amani. Hajaona gharama ya kufanya hivyo,” Lema amekaririwa na Gazeti la Mwananchi

“Chadema imepata baraka kuondokewa na mtu kama huyu. Alikuja kwa ajili ya kutaka urais na sio mabadiliko aliyokuwa akiyanadi. Nchi inataka demokrasia, katiba mpya, sheria mpya na inakabiliwa na ubanaji wa vyombo vya habari… mwanasiasa makini hawezi kuungana na CCM,” aliongeza.

Lowassa alijiunga na Chadema mwaka 2015 baada ya jina lake kuondolewa kwenye kinyang’anyiro cha watu waliokuwa wakiwania nafasi ya kugombea urais kwa tiketi ya CCM. Aligombea urais na kuleta ushindani mkubwa dhidi ya Dkt. John Magufuli wa CCM.

Juzi alipokewa na Dkt. Magufuli, Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Lowassa alieleza kwa ufupi kuwa amerejea nyumbani. Alipokewa katika Ofisi ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam.
Lema kama kinyongaa,pia Lema kama sunguraa,sizitaki mbichi hizi.Kwa kifupi Lema asitufanye mazuzu ,yeye ndiye zuzu,hayoyite angesema wakati ule Lowassa yupo Chadema na sio baada ya kutoka,mbona alifyata mkia kama mbwa koko.
 
Ni kweli kabisa, unajua hata kibaka ama jambazi anaweza kuingia nyumba ya ibada na hutaweza kumjua kabisa; ila kadri ibada inavyoendelea na maombi yanavyopamba moto aisee ni lazima atachomoka tu...hawezi kumaliza ibada trust me lazima achomoke arudi alikitoka!!
 
Mimi huwa na mshangaa sana huyu bwana anajifanya ana DNA ya Chadema yani mtu akihama toka chadema kwenda chama kingine anamuona kama mkosaji sana na ni adui wa Chadema. Mbona wewe mwenyewe ulitoka TLP ukahamia Chadema. The problem is unaiona Chadema ndo baba yako na mama yako kwani kila ulichonacho sasa hivi ni hizi ruzuku za chadema mnazogawana otherwise ungekuwa bado unauza magodoro pale mianzini Arusha na ile gari yako Honda mbovu. So usiwe una panic sana mtu akitoka Chadema those are normaal things in politics brother
 
Mimi huwa na mshangaa sana huyu bwana anajifanya ana DNA ya Chadema yani mtu akihama toka chadema kwenda chama kingine anamuona kama mkosaji sana na ni adui wa Chadema. Mbona wewe mwenyewe ulitoka TLP ukahamia Chadema. The problem is unaiona Chadema ndo baba yako na mama yako kwani kila ulichonacho sasa hivi ni hizi ruzuku za chadema mnazogawana otherwise ungekuwa bado unauza magodoro pale mianzini Arusha na ile gari yako Honda mbovu. So usiwe una panic sana mtu akitoka Chadema those are normaal things in politics brother
Unateseka na nini! wewe CCM ni baba yako, au mama yako?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom