Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,348
- 217,388
Aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini (Chadema),Godbless Lema ametangaza nia ya kugombea nafasi ya ubunge ndani ya chama hicho baada ya kuchukua fomu makao makuu ya chama hicho na kuahidi ushindi was kishindo.
Akikabidhi fomu hiyo kwa mke wa Lema,Neema Lema baada ya Lema kuwa safarini, katibu wa chadema wilaya ya Arusha ,Mosses Nanyaro alisema kuwa chama hicho kimejipanga kutoa mgombea aliyebora ili kulirejesha jimbo hilo kwa kishindo kwa kuwa anaamini bado chadema inakubalika Arusha Mjini.
Nanyaro alisema kuwa utaratibu wa chama hicho katika nafasi ya ubunge ni kuwa na wagombea wapatao watano watakaotia nia ila hadi sasa waliojitokeza ni wanne akiwemo Lema aliyeamua kujitangaza huku wengine majina yao yakibaki siri.
Akiongea kwa niaba ya Lema ,Neema alisema kuwa ameamua yeye na watoto wake kumchukulia fomu mume wake kwa kuwa familia inaunga mkono jitihada zake za kisiasa .
"Ninauhakika iwapo chama kitampitisha Lema, chadema itashinda ubunge Arusha mjini asubuhi na mapema ,kwani mambo yaliyofanywa na baraza la madiwani wa chadema katika jiji la Arusha ni kielelezo tosha cha ushindi" Alisema Neema.
Hii ndiyo Taarifa zinazozunguka kwenye vijiwe vyote vya Arusha
Taarifa hii inazima kabisa uvumi wa Mh Lema kwenda kwenye majimbo Mengine
Pichani : Mwakilishi wa Mh Lema akichukua fomu kwa niaba yake
=====
Godbless Jonathan Lema alizaliwa Octoba 26, 1976. Ni mwanachama wa Chadem, aliekuwa mbunge wa Arusha Mjini tangu 2010 hadi 2020
Akikabidhi fomu hiyo kwa mke wa Lema,Neema Lema baada ya Lema kuwa safarini, katibu wa chadema wilaya ya Arusha ,Mosses Nanyaro alisema kuwa chama hicho kimejipanga kutoa mgombea aliyebora ili kulirejesha jimbo hilo kwa kishindo kwa kuwa anaamini bado chadema inakubalika Arusha Mjini.
Nanyaro alisema kuwa utaratibu wa chama hicho katika nafasi ya ubunge ni kuwa na wagombea wapatao watano watakaotia nia ila hadi sasa waliojitokeza ni wanne akiwemo Lema aliyeamua kujitangaza huku wengine majina yao yakibaki siri.
Akiongea kwa niaba ya Lema ,Neema alisema kuwa ameamua yeye na watoto wake kumchukulia fomu mume wake kwa kuwa familia inaunga mkono jitihada zake za kisiasa .
"Ninauhakika iwapo chama kitampitisha Lema, chadema itashinda ubunge Arusha mjini asubuhi na mapema ,kwani mambo yaliyofanywa na baraza la madiwani wa chadema katika jiji la Arusha ni kielelezo tosha cha ushindi" Alisema Neema.
Hii ndiyo Taarifa zinazozunguka kwenye vijiwe vyote vya Arusha
Taarifa hii inazima kabisa uvumi wa Mh Lema kwenda kwenye majimbo Mengine
Pichani : Mwakilishi wa Mh Lema akichukua fomu kwa niaba yake
Godbless Jonathan Lema alizaliwa Octoba 26, 1976. Ni mwanachama wa Chadem, aliekuwa mbunge wa Arusha Mjini tangu 2010 hadi 2020