Godbless Lema aazimia kuondoa kazi za Diamond YouTube/Facebook

Koma kabisa hebu toa huu ushuzi tangu lini Mondi akawa zaidi ya chadema? ccm yenyewe pamoja na kukomaa na kuota mvi huko johanesburg lakini inaugwaya mtiti wa chadema hadi ikimbiliea polisi na usalama wa taifa ili kushinda wakisaidiwa na magari ya deraya na washawasha acha kuonesha upumbavu wako.

Ukome kuifananisha cdm na upuuzi wa aina yoyote tena nisije sikia unarudia maana waweza jikuta umepasukiwa yai maeneo ya kinyume cha mdomo chunga sana usije jikuta umezoa laana hadi kizazi cha nne, ina maana huna hoja? kwa hiyo mondi akigombea na Lema Arusha kwa akili zako za kukopa Mondi atashinda? hivi unawajua vijana wa ARACHUGA?
Diamond asingekuwa mkubwa kuzidi chadema viongozi wako wasihangaika kupambana nae.

Chadema ni fungu la kukosa
 
Mbowe ana wakati mgumu sana aisee... huyu ni mjumbe wa kamati kuu pamoja na huu uozo wake. DIAMOND ataiangusha CHADEMA.
 
Huku ni kuingilia uhuru wa mtu.
Mondi ana haki ya kushabikia chama chochote cha siasa na pia kumshabikia mwanasiasa yeyote aliyewekwa na chama chochote cha siasa.

Kushambulia kazi yake kisa tu ni mshabiki wa chama ambacho Lema hakubaliani nacho sio haki hata kidogo.

Huu mtindo mpya wa kuhusisha maisha ya mtu na ushabiki wake wa kisiasa utatuvuruga sana watanzania.
Ajabu wanaofanya hivi, ni watu wanajitanabaisha kuipigania demokrasia, hivi demokrasia nini.
Nilitegemea wao kuwa mdomo wa kumlainisha huyo kijana kubadili msimamo wake, badala ya kumkwamisha shuguri zake.

Haya ndiyo wanayoyalalamikia wao, kufanyiwa na serikali iliyopo madarakani, kumbe wanalalamika tu sababu wako nje.
 
Mwenye kipande cha track ya Diamond akiimba "wapinzani tunawapiga risasi" tafadhalini,naomba akiweke hapa.
 
Sifurahii mtu afeli mambo yake, ila katika hali ya kawaida kama ni mimi nipo ndani ya familia, vipigo na manyanyaso lakini ndugu yangu hanitetei wala kunitafutia msaada, ila anawasemea na kuwatetea majirani, siwezi kumuelewa.

Japo kua alichofanya ndugu Diamond si uungwana, kama binadamu namuelewa, alikaa kimya kulinda mkate wake, wengi tunafumbia macho madhaifu ya serikalini humu tunakofanyia kazi hata mtaani, maana ukiropoka tutakuokota baharini.

Ila kwa mwenzetu ni tofauti, yupo kwenye spotlight, he had to choose between the people or the government. He made his choice, the price has to be paid. Ni ngumu kuelewa hasira na maumivu ya kina Kigogo na wengineo kama wewe sio victim wa yaliyotokea ndani ya kipindi cha Jiwe.

Mungu atusaidie
Shida siyo kufanya kampeni Ccm.

Kipindi Naija watu wanauawa Diamond aliweka tweet kupinga yale mauaji. Aisee watu wamnanga sidhani kama huwa anatamani kuangalia ile tweet mara mbilimbili. Unajua ni kwanini?

Wasanii wa Bongo ni wanafiki sana. Matukio yakitokea Bongo wanakaa kimya. Wanalamba matako serikali. Yakitokea huko nje ndio wanajifanya kupiga kelele.



Pitia hiyo Tweet, kama ukishindwa kuelewa watu wanacholalamika sitakuwa na cha kukusaidia.
Screenshot_20210612-231619_Twitter.jpg
 
Hivi tumeishiwa maadui wa kupambana nao ?

Na katika hao maadui simaanishi CCM, bali Ujinga, Maradhi na Umasikini..., nadhani tuwekeze nguvu zaidi huko

Diamond tumpime kwa kazi zake na sio choice yake..., ikiwa hivyo mbona hatupigi kelele kwa Mama Samia Kuwa Rais wakati na yeye alikaa kimya ?
 
Back
Top Bottom